Upanga, Dar: Yaliyojiri kutoka Ukumbi wa JWTZ, Mkutano na Waandishi wa Habari

Upanga, Dar: Yaliyojiri kutoka Ukumbi wa JWTZ, Mkutano na Waandishi wa Habari

Naamini itahusu habari za tishio la ugaidi kwasababu ya matukio yaliyotokea Uganda hivi katibuni, hapa kwetu hatuna shida na ugaidi tena inawezekana tuna hamu nao sana ndio maana tunawapa watu kesi za uongo.
Nilifikiri Jeshi wameamua kuchukua madaraka baada ya kuona mambo hayaendi vizuri kumbe ni huu unafiq wao tu.
 
What......!!!!!!!

Politicization of non political entities
Jeshi ni taasisi pana, ina kila fani na tasnia zote chini ya jua ndani yake. Rais ni mwanasiasa, ni askari namba moja (Amiri Jeshi Mkuu) hivyo Jeshi lina siasa ndani yake pia. Wagombea wote wa nafasi za Urais (ambao kimsingi ni Wanasiasa) lazima pia wafanyiwe vetting na Kamati ya Majeshi licha ya vetting za Chama na NEC. Lazima majeshi yamjuwe mtu ambaye wanaenda kufanya naye kazi (mtu anayeenda kuwacommand kama Amiri Jeshi Mkuu ana vigezo stahiki?). Jeshi linapotaka kushauriana na Rais kijeshi wanam-address kama #Afande-Amiri-Jeshi-Mkuu, linapotaka kuongea naye kiserikali wanam-address kama #Rais, hiyo ndiyo itifaki ya kijeshi.

Karibu Tarime.
 
Tunashukuru kwa maelezo yenu sasa wazazi na vijana wawe makini na matapeli.
 
Salaam Wakuu,

Leo Jeshi la Wananchi Tanzania, linafanya Mkutano na Waandishi wa habari. Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ) kutoa Tamko Maalumu 30 Novemba, 2021

Nipo Nimefika kwenye Ukumbi huu kuwajuza kila kitakachojiri.

=====

UPDATES: 1022hrs

======
View attachment 2027879
Waandishi wameshafika eneo la tukio

1034 hrs: Mkurugenzi wa Habari wa JWTZ, Luteni Kanali Gervas Ilonda
View attachment 2027914
Wengi tumekutana hapa kujua ni nini hasa tunataka kuzungumza. Siji kutoa tamko bali nimekuja kutoa ufafanuzi wa mambo ambayo jeshi limeona yanaendelea. Hatuwezi kuyafumbia macho.

Naomba nitoe ufafanuzi kwa Vijana wanaojiandikisha kujiunga na Jeshi.

Hapo nyuma Viongozi wamekuwa wakitembelea Miradi ya Kimkakati. Wakiwa kule, wamekuwa wakilizishwa na Vija wa kujenga taifa wanavyojituma na kuwa Wazalendo.

Viongozi baada ya kuona uzalendo na umahili wa hali ya Juu wamekuwa wakiwaahidi kwamba nafasi za jeshi zikitka watapata.

Hivi karibu zimetoka nafasi kwa vijana wa Makambi ya JKT sio wote. Zimetoka chache lakini si haba.

Nimelazimika kuongea na vyombo vya habari ili tufahamishe umma kwamba kwa sasa kumeanza kuibuka kwa vitendo cya baadhi ya watu kutumia hizi nafasi za hawa vijana kujinufaisha. Vitendo vya Rushwa na Udanganyifu katika nafasi hizi. Matapeli hao wamekwenda mbali zaidi kwa kusingizia viongozi kwamba wametumwa wamewe hela ili vijana waandikishwe. Wanadai Mkuu wa majeshi ndo amewatuma. Jambo hilo sio kweli. Hatiwezi kulifumbia macho kuona viongozi wetu wanasumbuliwa. Mbaya zaidi wanachukua nyumba za kulala wageni wanaingiza vijana na kuwaambia subiri tunaenda kuwatafutia kazi, matokeo yake wanaanza kuwafuata wakuu wa Majeshi kudai nafasi zao. Kupitia kwenu nawaomba muwapuuze na msidanganyike kutoa fesha kwa nafasi za kuingia jeshini.

Natoa rai kwa wanaofanya Vitendo hivyo kwamba sio vya busara wala kiungwana. Waache mara moja.

Baadhi ya Wazazi wameanza kuwafuata viongozi waliopo Jishini kwenye ngazi mbalimbali kuwaomba wawasaidie kuwaingiza vijana wao Jeshini. Jeshi la Tanzania, lina taratibu na kanuni za kuingiza Vijana Jeshini sio kwa fedha wala kuoneana huruma.

Kijana anatakiwa awe

1). Raia wa Tanzania wa kuzaliwa

2). Umri awe na miaka 18 hadi 28

3) Awe na afya njema ya mwili na akili

4). Lazima awe mwenye tabia njema na nidhamu nzuri, asiwe amepatikana na hatia ya kijinai

5) Awe na cheti halisi cha kuzaliwa, vya shule na chuo.

Kwa Upande wa Madaktari

Awe amemaliza mafunzo kwa vitendo na pamoja na kusaidiwa na bodi ya madaktari.

Hizi ndizo sifa zitatumika kuwachuja vijana Walioandikishwa kuingia Jeshi la wananchi wa Tanzania. Sio wote walioandikishwa watapita.

Kazi ya jeshi ni kazi ngumu, ukiingia kwa hela bila kuwa na utimu wa akili na mwili atapoteza uhai au atakuwa mlemavu

Kazi anayojiandikisha kufanya, wengi wanasema ni ajira. Hakuna mwanajeshi mwenye ajira. Wote wameandikishwa. Mwanajeshi halipwi Mshahara bali malipo. Huwezi kuajiriwa kutoa uhai wako bali unajiandikisha. Unatoa uhai kwa kulinda nchi. Ndo maana hatutoi ajira kwa upendeleo wala Rushwa.

Watanzania tuungane kupinga vitendo hivi viovu vya rushwa, udanganyifu Wizi, halafu akishakuibia analala mbele.

Nawaomba watanzania wote kwa moyo mmoja mkunjufu, tuungane kufichua vitendo hivi. Mkisikia mtu anataka apewe hela, toeni taarifa, jeshini, Polisi na TAKUKURU.

Watanzania tuendelee kuliunga mkono jeshi letu lililo imara. Tupo imara kuilinda katiba ya jamhuru ya Muungano wa Tanzania.

Asanteni sana
View attachment 2027914
View attachment 2027953
View attachment 2027959
View attachment 2027960

Yaani uchambuzi wote kuhusu taarifa hii ulifanywa na akina Yericko Nyerere matokeo ndio haya ⁉️ Wacha tule ..... 🇹🇿
DSC_0008.jpg
 
Yaani jeshi linaitisha press kulalamika! Hili nalo lilikuwa la press au ni kutoa Katazo la kawaida tu?
Tena wangefanya kwa maaandishi tu hilo katazo na ufafanuzi! ,kutisha na kushtuwa umma kumbe jambo la kawaida sana.
 
Kuwaweka watu hapo kumbe ni hilo tu wangesema wamewakamataa wahusika itakuwa bora.....jeshiiiiii buana naliheshimu lakina leo EMPTY kabisa
 
Wagombea wote wa nafasi za Urais (ambao kimsingi ni Wanasiasa) lazima pia wafanyiwe vetting na Kamati ya Majeshi licha ya vetting za Chama na NEC.
Sio kwa TZ otherwise JK au JPM wasingeigusa ikulu. Yaani JWTZ inajua Rais yupo unfit kiafya ikubali agombee?

TZ ni kwamba Nyerere alijaza CCM kwenye taasisi zote so ni viceversa, kabla hujawa promoted JWTZ, hao CCM nao wanataka uwahakikishie maslahi yao kwanza.

Kma JWTZ ipo na vetting JK alifaa kuliko Dr.Slaa??
 
SUKUMA GANG walidhani chizi pole pole anaenda kusimikwa na jeshi kuwa kiongozi was mpito,,,,, Wamepigwa za Chembeeeeee!!!
 
Nikajua wataongelea ishu za Mtwara huko.
Mtwara ni salama kuliko maelezo ya maneno matupu, ni salama kama Amboni na Kibiti zilivyo salama. Wiki iliyopita nilikuwa huko nikashuhudia malori makubwa kwa madogo yana cross mpaka kupitia daraja la Umoja zikiwa na shehena za korosho kuletwa bandari ya Mtwara ambayo ndiyo iko karibu na Cabo Delgado kuliko bandari ya Beira. Ilipo JWTZ huwa ni salama siku zote, aliye jirani na Tz yuko salama siku zote.

"Natamani ningekuwa Mjumbe kwenye mkutano wa Berlin wa kuligawa bara la Afrika ningewaomba Wakoloni waifanye Southern Rhodesia ipakane na Tanzania, Joshua Mqabuko Nyongolo Nkomo, akihutubia Kamati ya Ulinzi na Usalama ya ZAPU (siyo ZANU PF) enzi za vita ya uhuru" Nukuu isiyo rasmi.

Feel blessed to be Tanzanian.
 
Back
Top Bottom