Upatikanaji wa Sukari na utulivu wa Bei ya sukari umeimarika sana Chini ya Bashe!

Upatikanaji wa Sukari na utulivu wa Bei ya sukari umeimarika sana Chini ya Bashe!

Inaelekea hujui hata unachotetea .
Hoja ni ukiukwaji wa utaratibu wa kutoa vibali vya uagizwaji wa sukari nje pindi kunapokuwa na uhaba wa sukari viwanda vinapositisha uzalishaji wa sukari.
Utaratibu huo upo na waziri bashe aliukiuka na hilo alikiri bungeni kwamba alilazimika kutokufuata utaratibu huo ili kuwaokoa wananchi baada ya sukari kuadimika.
Mpina ndio akaibuka na hoja zake kwamba waziri kadanganya na amekituka taratibu na kuboronga kabisa hadi kuzipa vibali kampuni za kijanja ambazo hazikuwa na sifa wala vigezo vya kuagiza sukari nje.
Hizo kampuni ambazo nyaraka zake brela zinaonyesha zina hisa ndogo zimetoa wapi fedha za kuagiza sukari za kiasi kikubwa hivyo kama sio hapo tayari kuna suala la utakatishaji wa fedha na ukwepaji wa kodi mkubwa sana umefanyika?
Kwamba ukiwa na hisa ndogo, ukapata tenda kubwa huwezi kukopa ukadeliver?
Yani mtu mwenye mtaji mdogo hapaswi kukua?
 
Wakuu wote salaam!
Kwa wanaonisomaga humu watashangaa Sana nikisimama na Bashe leo kwenye sakata la sukari!

Ila Leo ntasimama nae tena kwa hoja na sio vihoja!

Kwanza kabisa Bashe ni moja ya mawaziri vijana ambaye utendaji wake unapaswa kutufariji vijana na kutupa motisha kuwa tunaweza kugeuza mawazo na matamaanio yetu kuwa vitendo.

Bashe anatuhumiwa kuzipa tenda kampuni ambazo zinasemekana kutokuwa na sifa...
Kwa ufupi kabisa hizo ndio tuhuma.

Sasa maswali ya msingi!
1. Je kampuni hizo zimedeliver? Yani zimetekeleza makubaliano zilizoingia.
JIBU; Ni ndio tena kwa 100%

2. Je kuna wizi wowote ulioonyeshwa na yeyeto anayetuhumu ukianzia na Mpina?
JIBU; Hakuna wizi wa hata senti tano moja mbovu

SASA HIZI KELELE NI ZA NINI?
Kelele ni juu ya rangi ya paka na sio ufanisi wa paka.

Ukiangalia Upande wa Sukari, na hapa ukweli tu Usemwe...kabla ya Bashe hali ilikuwa mbaya Sana!
Nani hakumbuki kilichotokea wakati wa Mwendazake?
Hayo yanayoonekana ni makampuni yenye sifa yalifanya nini?
Kuna sehemu kilo iliuzwa elfu 8 na sukari ikawa haipatikani.
Viongozi wote wa serikali wakaingia mtaani kutafuta sukari na tochi mchana.
Hili hatulikumbuki?

Mnyonge mnyongini ila haki yake mpeni!
Sometimes, na hili mimi naliafiki, Kuna haja ya kuachana na mazoea...Hawa wanaoitwa wakongwe na wenye sifa.. wana-practice za kimazoea. Ndio walafi kupitiliza na ndio shida kubwa ambayo hata mwendazake ilimtoa jasho.
Wanaingiza sukari kweli ila hawajawahi kutosheka na faida. Hata sukari ikiwa hapa bado wanatengeneza 'uhaba/ scarcity' ili tu faida iwe mara dufu.

Sasa Kama Kuna paka mweusi na anakamata panya, shida iko wapi!
Unang'ang'ana na paka mwenye rangi nzuri ili ajisaidie ndani halafu wapeane tano na panya?
Mwezi wa ngapi huu?

Subiri februari uupandihse Tena huu uzi
 
Utadhibitisha umaiti wako. Mwenzako katoa tuhuma za sukari na ukiukaji wa taratibu alioufanya Waziri Bashe. Wewe unaleta hadithi za kumsema mke wa mtu. Kweli uchawa ni ujinga.
Mimi sijaongelea mke wa mtu!
Hizo tuhuma hazina maana
 
Kwamba ukiwa na hisa ndogo, ukapata tenda kubwa huwezi kukopa ukadeliver?
Yani mtu mwenye mtaji mdogo hapaswi kukua?
Naona hili swala limeshikiliwa kiushabiki wa kibiashara na kisiasa kuliko uhalisia.


( Labda ni kweli Bashe amevunja kanuni ya uingizaji bidhaa nchini, SIJUI) Lakini wanufaika ni nani ?
Binafsi mnufaika wa kwanza ni Bashe mwenyewe iwe kisiasa ama kiuchumi..
Mnufaika wa pili ni hao waliopewa vibali..
Mnufaika wa tatu ni mimi (sisi wanunuzi wa mwisho) hatimae tunanunua sukari kwa 2,800 - 3,500 /kg.

Wakereketwa ni wazalishaji wa ndani (HAWAAMINIKI NYAKATI NYINGINE)..
Wanafata wenye uchu wa kisiasa..
Kisha wenzangu na mie kila tukisikia wizi/kujipambania roho zinatuuma tunatamani tungeiba sie mali.


NB: Kama mtapita na hukumu ama uwajibishwaji wa Bashe kwa kuvunja kanuni ni sawa ,ILA bei ya sukari ibaki hii hii ya sasa 2,800-3,500.
 
Habari wakuu Mimi Nina certificate ya laboratory technician pia Nina experience ya miaka 3 kuhusu laboratory technician, laboratory analysis, QC,QA pia blending oparetor au syrup oparetor pia naweza kufanya kazi popote pale penye maabara au panapozalishwa bidhaa .yeyote atakaye nisaidia kupata connection ya job nipo tayari kumpa % kadhaa katika mshahara kama shukurani
 
Kwamba ukiwa na hisa ndogo, ukapata tenda kubwa huwezi kukopa ukadeliver?
Yani mtu mwenye mtaji mdogo hapaswi kukua?
Unaweza kukopa kama ukienda kuongeza shareholding.
Sasa hadi mpina amekwenda brella kufanya official searching hisa za kampuni zilikuwa ndogo.
Sio rahisi benk kukopesha kampuni yenye hisa ndogo fedha nyingi jaribu kufikirisha ubongo ndugu acha kutetea uovu
 
Unaweza kukopa kama ukienda kuongeza shareholding.
Sasa hadi mpina amekwenda brella kufanya official searching hisa za kampuni zilikuwa ndogo.
Sio rahisi benk kukopesha kampuni yenye hisa ndogo fedha nyingi jaribu kufikirisha ubongo ndugu acha kutetea uovu
Kwa lazima wakope bank?
Kwani akishirikiana na rafiki mwenye fedha kufanya hiyo biashara Kuna shida gani? Hivi nyie mnataka watu wenye mitaji midogo waamkeje?
 
Wakuu wote salaam!
Kwa wanaonisomaga humu watashangaa Sana nikisimama na Bashe leo kwenye sakata la sukari!

Ila Leo ntasimama nae tena kwa hoja na sio vihoja!

Kwanza kabisa Bashe ni moja ya mawaziri vijana ambaye utendaji wake unapaswa kutufariji vijana na kutupa motisha kuwa tunaweza kugeuza mawazo na matamaanio yetu kuwa vitendo.

Bashe anatuhumiwa kuzipa tenda kampuni ambazo zinasemekana kutokuwa na sifa...
Kwa ufupi kabisa hizo ndio tuhuma.

Sasa maswali ya msingi!
1. Je kampuni hizo zimedeliver? Yani zimetekeleza makubaliano zilizoingia.
JIBU; Ni ndio tena kwa 100%

2. Je kuna wizi wowote ulioonyeshwa na yeyeto anayetuhumu ukianzia na Mpina?
JIBU; Hakuna wizi wa hata senti tano moja mbovu

SASA HIZI KELELE NI ZA NINI?
Kelele ni juu ya rangi ya paka na sio ufanisi wa paka.

Ukiangalia Upande wa Sukari, na hapa ukweli tu Usemwe...kabla ya Bashe hali ilikuwa mbaya Sana!
Nani hakumbuki kilichotokea wakati wa Mwendazake?
Hayo yanayoonekana ni makampuni yenye sifa yalifanya nini?
Kuna sehemu kilo iliuzwa elfu 8 na sukari ikawa haipatikani.
Viongozi wote wa serikali wakaingia mtaani kutafuta sukari na tochi mchana.
Hili hatulikumbuki?

Mnyonge mnyongini ila haki yake mpeni!
Sometimes, na hili mimi naliafiki, Kuna haja ya kuachana na mazoea...Hawa wanaoitwa wakongwe na wenye sifa.. wana-practice za kimazoea. Ndio walafi kupitiliza na ndio shida kubwa ambayo hata mwendazake ilimtoa jasho.
Wanaingiza sukari kweli ila hawajawahi kutosheka na faida. Hata sukari ikiwa hapa bado wanatengeneza 'uhaba/ scarcity' ili tu faida iwe mara dufu.

Sasa Kama Kuna paka mweusi na anakamata panya, shida iko wapi!
Unang'ang'ana na paka mwenye rangi nzuri ili ajisaidie ndani halafu wapeane tano na panya?
Kelele ni za wagalatia wazee wa mauaji, na sukuma gang
 
Kwa lazima wakope bank?
Kwani akishirikiana na rafiki mwenye fedha kufanya hiyo biashara Kuna shida gani? Hivi nyie mnataka watu wenye mitaji midogo waamkeje?
Kwa nini uipe kazi kampuni isiyo na vigezo vya kifedha bila kufata taratibu.
Hivi huoni kabisa ni tatizo
 
Watu washakula hela za wale matajiri 7 eti bashe anaua viwanda vya ndani walitaka sukari iendelee kuwa adimu..

Mama ikimpendeza bashe awe naibu waziri mkuu kabisa
Kweli kabisa,sasaivi hamna tena uadimu wa sukari
 
Kwa nini uipe kazi kampuni isiyo na vigezo vya kifedha bila kufata taratibu.
Hivi huoni kabisa ni tatizo
Wewe umeangalia data za Brela..
Je, wakati wa kupewa tenda, bank statement zao zilikuwa zinasomaje..??
Kama walisajiliwa wakiwa na mitaji midogo inamaana hawakupaswa kukua...

Late Mengi alianza biashara kwa kuuza kalamu tena analala nazo kitandani.. je leo, kampuni zake haziwezi kupewa kazi kubwa kwa bases ya mtaji wake wa mwanzo tu?
 
Huyo Msomali asipoangaliwa atakuja kuvuruga kila kitu
 
Mimi hapo sioni hoja..
Kampuni isiyo na sifa according to who?
Wewe kwanini unahisi haina sifa wakati imeleta sukari? Kinachotakiwa si sukari? Na si imeletwa? Wewe ulitaka wawe na sifa gani zaidi?

Suala la kampuni moja kuwa supplier na kampuni nyingine kuwa distributor mbona ni kawaida Sana kwenye logistics... Wewe unataka kampuni moja ipambane kwenye chain yote ya supply?
Kwanini kwanza!
Kwani Richmond ambayo ilikuwa ya Godfather wa huyo Bashe ilikuwa haizalishi umeme??
 
Kwani Richmond ambayo ilikuwa ya Godfather wa huyo Bashe ilikuwa haizalishi umeme??
Tuache mambo ya kusadikika, Kama Kuna ushahidi wa wizi uwekwe..ila sio mambo ya kudhania. Kwamba itakuwa ameiba..tusiharibu sifa za watu, career za watu kwa chuki tu na husuda.
 
Wewe umeangalia data za Brela..
Je, wakati wa kupewa tenda, bank statement zao zilikuwa zinasomaje..??
Kama walisajiliwa wakiwa na mitaji midogo inamaana hawakupaswa kukua...

Late Mengi alianza biashara kwa kuuza kalamu tena analala nazo kitandani.. je leo, kampuni zake haziwezi kupewa kazi kubwa kwa bases ya mtaji wake wa mwanzo tu?
Mkubwa kampuni mtaji ukiongezeka si taarifa inapelekwa brella ili wafanye mabadiliko.
Ishu ni kwamba wakati wanapewa hiyo tenda mtaji wao ulikuwa unasoma hivyo milioni 1
 
Mkubwa kampuni mtaji ukiongezeka si taarifa inapelekwa brella ili wafanye mabadiliko.
Ishu ni kwamba wakati wanapewa hiyo tenda mtaji wao ulikuwa unasoma hivyo milioni 1
Huu mwingine ni uchawi tu!
Kwani mtaji ukisoma milioni moja hauruhusiwi kufanya biashara kubwa?
 
Back
Top Bottom