Pre GE2025 Upendo Peneza: Maandamano ya CHADEMA hayahusu Miswada, yanalenga kuangalia kama bado wana watu

Pre GE2025 Upendo Peneza: Maandamano ya CHADEMA hayahusu Miswada, yanalenga kuangalia kama bado wana watu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sijawahi kuamini mara moja chochote kinachotoka kinywani mwa mwanasiasa yeyote yule!... Hasa nyakati kama hizi...

Aelewe ya kwamba ni rahisi sana kuibomoa nyumba yako ya zamani!.... Lakini Kuna kazi kubwa zaidi! ... kuanza kuijenga nyumba mpya!
 
Ujinga wa waafrica ni siasa za kuletwa na wazungu eti democracy 😆😆😔....Wajinga ndio wanaamini siasa wakati ni porojo za kuwalisha watu wachache ...


Wajinga acheni siasa ndio mtego mliwekewa ili muibiwe .. Wanasiasa ndio wafanyabiashara hao haoa kama sio utapeli ..
 

Attachments

  • VID_24540627_150836_707.mp4
    33.7 MB
mbona haeleweki, tafuta kigogo mpe akupe ukumbukwe kwenye teuzi, ya chadema hayakuhusu maana umeshaondoka
Sema tena na tena. Tatizo anatumia ujanja wa kizamani sana. Haya mambo ya kutoka chama fulani leo halafu kesho yake unakuja na tuhuma za kuwashambulia kibao yamepitwa na wakati. Kwanza unajionyesha jinsi ulivyo mjinga na usiyeaminika. Wenzake walifanya hivyo wakaja juta baadae. Kama ni kuhama, wewe hama na usileta shutuma za kijinga.
 
Akitangaza kuhamia CCM jana January 22, Upendo Peneza amesema kuwa...

"Sasa tuna hoja nzuri sana mezani, Bungeni kuna Miswada mitatu ya Sheria ambayo inabidi ipitishwe na Bunge lakini mmesikia Mwenyekiti Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa) akitangaza maandamano jambo ambalo Mimi naliona (na haya ni mawazo yangu binafsi), Mimi nadhani Viongozi wapo kwenye mshtuko, wanataka kukagua kwa sababu wameshawafanya Wananchi na Wanachama wao ni bidhaa sasa wanataka kutumia maandanamano waangalie hivi tuna bidhaa ngapi na zipi zilizoondoka

Wameshapoteza uhalali wa Kisiasa sasa wanalazimisha uhalali wa Kisiasa wanataka kwenda kwenye maandanamano, wanatumia hoja nzuri sana, na hoja hii naomba niwashukuru sana Viongozi wa Dini na Watu wote ambao wameenda kutoa maoni

Hoja ni nzuri sana lakini inatajwa hoja nzuri ili kuwaaminisha Watu kwamba hiki ndicho wanachokipigania ili Watu kuwaingiza Barabarani lakini lengo ni kuangalia hivi hizo bidhaa bado tunazo au zimeshatukimbia?"

Hii ni hazina adimu ambayo Chadema wameipoteza!

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa viti Maalumu Chadema, Mheshimiwa Upendo Peneza, katika mkutano wa hadhara uliyofanyika Ruangwa Mjini, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi, Julai 12, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
View attachment 541840
images
images
images

MBUNGE wa Viti Maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Upendo Peneza amewaomba wananchi waliombee Taifa liendelee kuwa na amani pamoja na kuwaombea viongozi wa kisiasa, wawe na uvumilivu ili wazidi kusonga mbele kimaendeleo.

Alisema hayo juzi katika mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Shule ya Msingi Likangara wilayani Ruangwa wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mkoani Lindi.

“Wananchi wa Ruangwa nawatakia maisha mema ili mzidi kusonga mbele, tuombee amani ya nchi yetu na mtuombee viongozi tuwe na uvumilivu wa kisiasa,” alisema mbunge huyo kijana kutoka mkoani Geita, ambaye bungeni anaongoza Chama cha Wabunge Vijana.

Mbali na Peneza, pia mkutano huo ulihudhuriwa na wabunge wengine ambao ni Hassan Masala (Nachingwea – CCM), Zubery Kuchauka (Liwale - CUF), Hassan Kaunje (Lindi Mjini – CCM) na Hamida Abdallah (Viti Maalumu – CCM).

Kwa pamoja, wabunge hao walisema lengo la kushiriki kwenye ziara hiyo ni kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi aliwataka wananchi kuhakikisha wanaendelea kudumisha na kuilinda amani iliyopo kwa sababu ndiyo inayowawezesha kufanya shughuli zao za kimaendeleo.

Alisema licha ya kuwepo kwa matukio machache ya uhalifu yanayojitokeza katika baadhi ya maeneo, vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na mikoa jirani, limejizatiti kukabiliana na wahalifu wa aina yoyote kwa mtu mmoja mmoja au vikundi.
Masikini Chadema...!, lost this Gold in the rough! .
View: https://youtu.be/aHJGqYKrX5U?si=uX9m2pe3OIrHIHTX,
Nimemsikiliza, nimeguswa!.

Kiukweli I was very right about this beautiful queen, young and very energetic lovely lady ambaye ni beauty with brain!.

Nilimfahamia Upendo Peneza kupitia kwa Regia Mtema (RIP) Life After Life: Regia Mtema (RIP) Amerejea Bungeni Kiaina?

Angalieni niliwahi kusema nini kumhusu Upendo Furaha Peneza humu[/SIZE]
  1. Upendo Furaha Peneza (@UpendoPeneza) | Twitte
  2. Upendo Furaha Peneza: Gold in the rough. Vijana CHADEMA mpo?
  3. Upendo Peneza ni malkia Nzinga Mbandi wa BAVICHA
  4. Upendo Peneza: Nahitaji kushinda na nitashinda
  5. Upendo Peneza leo Bungeni; Huyu Dada ana uwezo mkubwa sana
  6. Upendo Peneza wa CHADEMA atoboa siri ya CHADEMA na Sabodo
  7. Mungu amenipa nafasi nyingine ya kumtumikia na kutumikia watu wake. Praise be to God!
  8. Upendo Peneza kapata ajali Geita akitokea kwenye Mikutano ya Kampeni (05 Dec 2014)
  9. Upendo Peneza ataja sifa za mwanaume wa kumuoa
  10. Upendo Peneza (CHADEMA) awalaumu Wabunge wanaohama vyama. Asema chaguzi za marudio ni kucheza pesa za wananchi!
  11. Mheshimiwa Upendo Peneza asisitiza amani akiwa ziarani na Waziri Mkuu
  12. Mbunge Upendo Peneza(CHADEMA) akamatwa Geita mjini, aachiwa kwa dhamana
  13. Je, Rais wetu, Magufuli anasoma JF? Rais, Please msikilize Binti huyu, ana hoja ya Msingi!

Nilikuja kumtafuta na nikaja kukutana nae View attachment 2879719
Hapo tulipokutana, yeye akiwa 20 something, mimi nilikuwa 50 something, nikiwa nimeisha oa na nina watoto 10!, hivyo sikuthubutu kumweleza lolote la moyoni mwangu, ila ningekuwa kijana... nakuapia... Haki ya ...!, nisinge kubali, .... naomba nisimalizie!.

Mungu ambariki sana Upendo Furaha Peneza!, hapa CCM imelamba dume!, naomba mimi ndio niwe mwana JF wa kwanza kuwatangazia Mbunge wa Geita 2025!.

P
 
Ujinga wa waafrica ni siasa za kuletwa na wazungu eti democracy 😆😆😔....Wajinga ndio wanaamini siasa wakati ni porojo za kuwalisha watu wachache ...


Wajinga acheni siasa ndio mtego mliwekewa ili muibiwe .. Wanasiasa ndio wafanyabiashara hao haoa kama sio utapeli ..
Hii kusingizia wazungu na demokrasia kwa kuwa na viongozi wabovu, wezi na mafisadi ni kujidanganya.

Tatizo la Waafrika ni ile hulka ya kuchagua na kuendekeza mafisadi wanaohodhi vyombo vya dola na kuvitumia kufisidi na kuhujumu uchumi bila kuhojiwa. Demokrasia inawapa uwezo wa kudhibiti viongozi. Nyinyi hamtaki kutumia akili mnakimbilia kujikomba, kuwa machawa wa viongozi halafu mnamlaumu “mzungu” kwa ujinga wenu.

Ukikataa demokrasia, mbadala sahihi ni upi? Udikteta?
 
Mkuu

Regardless motive of anything,Chadema ina power!

Na power ni exclusive haitaki umalaya malaya kuchanganya na Mwabukusi and shit.

Chadema ina power...sasa wewe kiutani ruhusu waandamane 24 watakuja wachache then 25 utaona vitu vya ajabu

Ni kesho actually

Nyie jamaa mnataka ku play down Chadema's power as if haina power
Mkuu!
.
Point yangu ni kwamba, Maandamano ya Mwambukusi yalikuwa yana maaana sana lakini chadena hawa kumuunga mkono.

Lakini hayo maandamano ya kesho utaona ni ya kutetea vyeo vya kina Mbowe zaidi alafu wanataka kila mtu awaunge mkono
 
Hakuna anayelazimishwa kuandamana kwenye hayo maandamano ya cdm, na Wala ww hutakiwi kwenye hayo maandamano maana utaishia kupora vitu vya watu. Cdm ni taasisi ina taratibu zake. Mwabukusi ni taasisi gani?
Hoja yake je?

Mngekuwa na akili mngeanzia pale pale pa Mwambukusi.

Lakini kwa kuwa haya kuwa maandamano ya kutetea vyeo mkaona mjinga.
 
Hii kusingizia wazungu na demokrasia kwa kuwa na viongozi wabovu, wezi na mafisadi ni kujidanganya.

Tatizo la Waafrika ni ile hulka ya kuchagua na kuendekeza mafisadi wanaohodhi vyombo vya dola na kuvitumia kufisidi na kuhujumu uchumi bila kuhojiwa. Demokrasia inawapa uwezo wa kudhibiti viongozi. Nyinyi hamtaki kutumia akili mnakimbilia kujikomba, kuwa machawa wa viongozi halafu mnamlaumu “mzungu” kwa ujinga wenu.

Ukikataa demokrasia, mbadala sahihi ni upi? Udikteta?
Kataa siasa ni utapeli kwa waafrica .
 
Back
Top Bottom