Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa

Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa

Km Level ya chini kabisa zinapigwa hivi na watu wapo confotable kabisa then huko juu itakua balaa...hawa wa chini wanajifunza na kupata confidense kutoka kwa walio juu yao.
 
Gharama za ujenzi ziko Juu jamani
Daah huku ni kutafuta sifa na kutrend.
Hicho kibanda ni cha serikali kingejengwa sh ngapi?

1. Posho za ma consultants
2. Site visiting za viongozi???
3. Milango 2 pamoja na finishing 700k
4. Tofali za serikali ni grade one
5. Cement ni grade one( 42.5 )
6. Bati na usafiri wake
7. Plasta
8. Rangi
9. Tiles
10. Malipo ya ufundi..khaa
Kama imepigwa ni 500,000
Takukuru itatumia kiasi gani kujilipa ufuatiliaji?. Hii ni kesi ya wizi wa kifaranga
 
Kuhusu Uyui na Tabora kwa ujumla kuhusu upigaji,upumbavu wa viongozi, rushwa nimeandika sana humu jukwaani!Lakini hakuna anaejali!

Uyui hapo upumbavu ni mwingi mno wanahujumu hadi tanesco huko vijijini wanapeleka umeme hawasambazi kwa wana chi hadi uhonge mapesa mengi ndio unapewa nguzo!

"Rasimu ya warioba irudi mezani sasa iwe katiba mpya"
 
Tozo ilivyojenga ofisi ya 11,000,000, unaambiwa ni ofisi ya kisasa zaidi.

-
Waziri Mkuu Majaliwa akiwa ziarani Wilayani Uyui, Tabora amekagua ujenzi wa Chuo kipya cha VETA na ameonesha kutoridhishwa na gharama za ujenzi wa kibanda cha Mlinzi ambacho ujenzi wake ni Tsh. Milioni 11 “TAKUKURU chunguzeni gharama za ujenzi wa kibanda hiki”

View attachment 2350408
PICHA: Kibanda cha Mlinzi kilichojengwa kwa Tsh Milioni 11​
Watu ambao hawajawahi kujenga ndio watashangaa mimi nikikiangalia hicho kibanda mbona pesa hiyo ni halali!.

  1. Kuchimba msingi vibarua 500,00
  2. Kujenga Msingi mawe zege 1,000,000
  3. Kuinua kuta 1,000,000
  4. Madirisha 3 ya PVC za Uturuki 3,000,000
  5. Milango miwili ya Mninga 1,000,00
  6. Bati ya South 1,000,000
  7. Tails za mable 1,000,000
  8. Scatting ya black granite 500,000
  9. Rangi ile washable 500,000
  10. Msimamizi 1,000,000
  11. 10% ya aliyetoa kazi 1,000,000 hapo kuna wizi gani?.
JIfunze kuangalia quality kabla hatujakimbilia kupigia kelele wizi na ufisadi, ujenzi wa majengo yoyote ya umma unatanguliwa na BOQ.
Kwa msio jua quality ya ujenzi, nendeni makaburi ya Kinondoni kuna kaburi pale limegharimu TZS 36.M!.

Mfano mimi natamani tomb stone yangu iwe kama ile ya ku roll, find out how much it costs, tusishabikie tuu ufisadi!.
P
 
Mleta mada tukupe laki tano utujengee kibanda kama hicho,???! japo Kuna upigaji hicho ni zaidi ya hiyo, dirisha la alluminium TU linafika au kukaribia laki tano, na yanaonekana mawili hapo...Bado tofali,cement,bati,tiles, rangi, umeme,ufundi nk nk
 
Eeh ni sahihi kimetulia...we ulitaka kiwe bei gani?...heheehe
 
Hakuna kitu cha kushangaza hapo. Upigaji wa kitaasisi upo tangu enzi za TASAF kwenye awamu ya Mkapa na Kikwete!. Gharama ya jengo hilo dogo ni sahihi kabisa ukiangalia bei ya vifaa vilivyotumika kujengea, ila kutakua na kiasi kama hicho au zaidi kimejenga jengo jingine la mkubwa mmoja mwenye mamlaka, mhasibu au hata dereva kwenye deal la namna hiyo.

Huko kwenye Halmashauri au Serikali kuu kwenye mikoa ya pembezoni ambako hawakaguliwi mara kwa mara ndio sehemu muafaka kupiga hela ya Serikali, kumejaa ukoo unaofanana na ule wa panya. Ukijifanya mlokole sana na uadirifu wa Zakayo, utaishia kuchekwa hata utakapokuwa mstaafu. Huo ndio utamaduni wetu wa hovyo!!.
 
Kwa wanaojua Ujenzi hio pesa ni sawa kabisa...

Msingi wa hiyo makitu inaweza fika 1m hadi 2m
Tofari hadi juu zikiwa zile za buku bei ya kitaa kama laki 5
Kenchi misumari n.k kama laki 7 bile ufundi
Bati kama laki 5 hadi 6
Rangi ndoo moja ya silk 140,000 MARA 2
Roller 2 na brush 2 = 16,000
Plaster cement mifuko 4
mchanga tipper 2 laki 4
Maji wale wamama kubeba elfu 30 hadi ujenzi unaisha
Kukodisha ngazi na mirunda elfu 60
tiles box 10 za kichina for 30,000 - laki 3
kupaua ufundi wake laki 4 hadi 5
Mkandarasi cost m2 hadi 3
VAT 18%
 
Inaonekana mtoa Mada hajawahi kujenga au alijenga miaka ya '90 wakati Bati inauzwa 1,250/-


Bei ya Bati 28G saivi ni 43,000 - 47,000
Bei ya Tiles ya 50x50 ni 39,000
Mlango huo unaweza kufika 850,000 pamoja na frame

Ikumbukwe hiyo kazi amefanya Mkandarasi, naye ameajiri na analipa watu Mishahara kwahiyo lazima aweke Faidi ambayo inaweza kuwa 10% ya gharama za Mradi.

Ingekuwa kinajengwa Kwa njia ya Force account walau gharama yake ingeshuka hadi 6.5M hivi kutokana na hadhi ya kibanda chenyewe.
 
Back
Top Bottom