Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa

Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa

Tozo ilivyojenga ofisi ya 11,000,000, unaambiwa ni ofisi ya kisasa zaidi.

-
Waziri Mkuu Majaliwa akiwa ziarani Wilayani Uyui, Tabora amekagua ujenzi wa Chuo kipya cha VETA na ameonesha kutoridhishwa na gharama za ujenzi wa kibanda cha Mlinzi ambacho ujenzi wake ni Tsh. Milioni 11 “TAKUKURU chunguzeni gharama za ujenzi wa kibanda hiki”

View attachment 2350408
PICHA: Kibanda cha Mlinzi kilichojengwa kwa Tsh Milioni 11
----
WALIOSIMAMIA UJENZI WA VETA UYUI WAKAMATWE- MAJALIWA


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Tabora, Musa Chaulo kuwakamata watu wote wanaohusika na usimamizi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) wilaya ya Uyui mkoani Tabora kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za mradi huo.

Amechukua hatua hiyo baada ya kukagua mradi huo na kuonesha kutoridhika na gharama za ujenzi wa baadhi ya majengo ikiwemo kibanda cha mlinzi ambacho ujenzi wake umegharimu shilingi milioni 11.
“Sitamvumilia yeyote atakayemuhujumu Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, watafutwe na wachukuliwe hatua.”

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Septemba 8, 2022) baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa chuo cha VETA wilaya ya Uyui mkoani Tabora ambapo amesema hajaridhishwa na ujenzi wa chuo hicho ambacho majengo yake yanejengwa kwa gharama kubwa tofauti na uhalisia kwa kutumia mfumo wa nguvu kazi ya ndani (force account).

Mbali na ujenzi wa kibanda cha mlinzi, pia Waziri Mkuu ameonesha kutoridhishwa na ujenzi wa nyumba za watumishi chuoni hapo ambapo nyumba moja yenye uwezo wa kuchukua familia mbili inajengwa kwa gharama ya shilingi milioni 114 na tayari wameshatumia zaidi ya shilingi milioni 70 na bado haijakamilika.

“Nyumba moja yenye uwezo wa kuchukua familia tatu Wizara ya Afya inajenga kwa shilingi milioni 90 na Ofisi ya Rais (TAMISEMI) wanajenga nyumba za walimu zenye uwezo wa kuchukua familia mbili kwa gharama ya shilingi milioni 57 na wanajenga kwa mfumo wa force account kama mnavyojenga hapa, hii haikubaliki.”

Kutokana na kutoridhishwa na ujenzi wa chuo hicho unaosimamiwa na VETA, Mheshimiwa Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Burian asimamie ujenzi wa chuo hicho ili uweze kukamilika kwa wakati. “Mkuu wa mkoa simamia vizuri ujenzi wa chuo hiki, tunataka ukamilike kwa wakati.”
Sasa hao mnaoita Wakuu wa Wilaya sijui Mikoa na Takukuru wenyewe huwa wanafanya Kazi gani Sasa kama vitu kama Hivi hata waje viongozi wa Kitaifa?

Kwani wanapoenda kukagua huwa unakagua nini sasa ikiwa huwezi fanya break through ya items husika?

Mpaka hapo wengine watakuwa wamestuliwa so wataingiza gharama kwenye items zingine..

Yaani sekretarieti za Mikoa zina wahandisi sasa Kazi zao huwa ni zipi hasa?
 
Yaani ukisikia kula kwa urefu wa kamba yako ndio huku. Ni kujipakulia tu kama unapakuwq ubwabwa.
20220908_181848.jpg
 
Itakuwa ni kweli.
Mimi nyumbani kwangu nimejenga choo na bafu ukubwa huo juu nimemwaga slab ya zege cement kali siyo hizo bati za Kiboko za kupauka tofali 6inch tena za kulala na imenigharimu 3,725,000/=.

Na ni Dar siyo huko porini huko wanatumia tofali za kuchoma moja Tsh 100,watu wanakula kwa urefu wa kamba zao usitetee ujinga
 
Kwa ujenzi wa kiserikali hiyo bei ni sahihi.
Kuna physibility study ya jengo kikao.
Kuna kunununa eneo kikao.
Kuna kupima udongo wa kiwanja kikao.
Kuna kumtafuta mkandarasi mshauri kikao.
Kuna kutangaza zabuni kikao.
Kuna kumchagua mzabuni kikao.

Vikao vyote vina posho.

Ikijumlisha na ujenzi imara wa hiyo ofisi hiyo gharama ni halari kabisa.
Boss upo kwenye chain hiyo nini?
 
Hivi TAKUKURU hadi waagizwe,wao hawaoni?wasipoagizwa hawafanyi kazi au wanachagua kazi za kufanya?
Hiyo wilaya ina mkuu wa wilaya,kamanda wa TAKUKURU,mkuu wa Usalama wa wilaya wote hawaoni hadi Waziri mkuu aagize?
 
Huyu PM anadharauliwa sana, amri zake huwa zinaishia magazetini. Hata kamati zake za kuchunguza huwa ni funika kombe
 
Tozo ilivyojenga ofisi ya 11,000,000, unaambiwa ni ofisi ya kisasa zaidi.

-
Waziri Mkuu Majaliwa akiwa ziarani Wilayani Uyui, Tabora amekagua ujenzi wa Chuo kipya cha VETA na ameonesha kutoridhishwa na gharama za ujenzi wa kibanda cha Mlinzi ambacho ujenzi wake ni Tsh. Milioni 11 “TAKUKURU chunguzeni gharama za ujenzi wa kibanda hiki”

View attachment 2350408
PICHA: Kibanda cha Mlinzi kilichojengwa kwa Tsh Milioni 11
----
WALIOSIMAMIA UJENZI WA VETA UYUI WAKAMATWE- MAJALIWA


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Tabora, Musa Chaulo kuwakamata watu wote wanaohusika na usimamizi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) wilaya ya Uyui mkoani Tabora kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za mradi huo.

Amechukua hatua hiyo baada ya kukagua mradi huo na kuonesha kutoridhika na gharama za ujenzi wa baadhi ya majengo ikiwemo kibanda cha mlinzi ambacho ujenzi wake umegharimu shilingi milioni 11.
“Sitamvumilia yeyote atakayemuhujumu Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, watafutwe na wachukuliwe hatua.”

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Septemba 8, 2022) baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa chuo cha VETA wilaya ya Uyui mkoani Tabora ambapo amesema hajaridhishwa na ujenzi wa chuo hicho ambacho majengo yake yanejengwa kwa gharama kubwa tofauti na uhalisia kwa kutumia mfumo wa nguvu kazi ya ndani (force account).

Mbali na ujenzi wa kibanda cha mlinzi, pia Waziri Mkuu ameonesha kutoridhishwa na ujenzi wa nyumba za watumishi chuoni hapo ambapo nyumba moja yenye uwezo wa kuchukua familia mbili inajengwa kwa gharama ya shilingi milioni 114 na tayari wameshatumia zaidi ya shilingi milioni 70 na bado haijakamilika.

“Nyumba moja yenye uwezo wa kuchukua familia tatu Wizara ya Afya inajenga kwa shilingi milioni 90 na Ofisi ya Rais (TAMISEMI) wanajenga nyumba za walimu zenye uwezo wa kuchukua familia mbili kwa gharama ya shilingi milioni 57 na wanajenga kwa mfumo wa force account kama mnavyojenga hapa, hii haikubaliki.”

Kutokana na kutoridhishwa na ujenzi wa chuo hicho unaosimamiwa na VETA, Mheshimiwa Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Burian asimamie ujenzi wa chuo hicho ili uweze kukamilika kwa wakati. “Mkuu wa mkoa simamia vizuri ujenzi wa chuo hiki, tunataka ukamilike kwa wakati.”
Waziri mkuu ni zaidi ya MANDONGA. Ameshaunda kamati nyingi sana za kufuatilia ubadhirifu lakini hakujawahi kuwa na mlejesho wowote ule.

CCM kwenye ubadhilifu huwa hawashugulikiani zaidi ya kulindana
 
Back
Top Bottom