Upinzani bila kubadili siasa mtapata hasara kubwa Kwa Samia..

Afoke asifoke hiyo siyo ISSUE kabisa. Watanzania tunataka KATIBA MPYA na Tume Huru ya uchaguzi na hivyo tayari vimeanza kumkosesha usingizi. Pia tunataka nchi iongozwe kwa kufuata na kuheshimu sheria za nchi mbali mbali, bunge, katiba na mahakama vitu ambavyo havikuwepo kwa muda mrefu sasa. Pia tunataka haki kwa Watanzania wote bila kujali itikadi zao. Siyo maccm yakivunja sheria za nchi hawaadhibiwi bali kulipa faini kidogo wakati wanaobambikiwa kesi FAKE huozea lupango au kuchajiwa faini kubwa sana na mifano iko mingi tu.
 
Ndio maana mleta Mada kaweka mada hapa mjielewe na kubadilika siasa za kizamani za kupinga kila kitu kwa jazba mpaka mnamuita Kiongozi dhaifu safari hii hakuzitoa
Huko Ujerumani, Amerika ya kina Baiden upinzani hawaropoki mfululizo wakati sio wake, subirini wakatiwa wa Chaguzi za serikali za mitaa 2024 na 2025
Leo tu mmeambiwa mtasikilizwa mnataka kwanza Covid 19 watolewe Bungeni
Mbeligiji arudishiwe V8 yake mafao yake na mishahara ya ubunge mwishowe na Ubunge au urais wake
Upinzani sio kila kitu kupinga hata mtu akienda chooni mnatafuta sababu
Mbona zitto hayupo hivyo au Lipumbasoma tena
 
Huyu ni mwepesi Sana mkuu...ila inahitajika timing ya kumchinja Kobe...uzuri anajijua ....ila NAMUOMBA TU ASIHARIBU..KAMA PALE TUNAPOTEGEMEA ATAHARIBU..,AKIPAGUSA AMEKWISHA..
 
Katiba Baba na Tume huru ya uchaguzi hivyo haviwezi KUKWEPEKA. Pia nchi kuendeshwa kwa haki na usawa. Unamuungaje mkono dikteta aliyekuwa akidharau katiba, mahakama, bunge na raia? Aliyefikia kujichotea trillions za walipa kodi kugharamia mambo ambayo hayana tija kwa Taifa na kuidhinishwa na Bunge kwa mfano ununuzi wa ndege kwa zaidi ya trillion 3 ambazo kwa miaka mitano zimeingiza hasara ya 154 billions? Unaungaje mkono ujenzi wa airport chato kijijini na majengo mengine muhimu pamoja na kuwa si tija kwa Taifa!?
CAG katoa ripoti hivi karibuni umemsikia Samia au Bunge wakizungumzia madudu chungu nzima kwenye ripoti ile? Wao ndiyo imeshatoka toka hiyo na baadhi ndani ya maccm wanataka kumuua CAG Kichere mama Samia KIMYAAAAA!!!


 
Taarifa za uhakika ni kwamba uwanja wa ndege wa Chato kwisha habari ! Mungu hataniwi
 
Siasa za miaka mitano iliyopita zilikuwa tofauti sana na za miaka mitano ijayo zitakuwa tofauti sana.

Nasema hivyo kwa sababu miaka mitano iliyopita Magufuli aliiua CCM badala yake yeye ndiyo akawa CCM hata uhai au nafasi za uongozi kwa mwanaccm yeyote zilitegemea Magufuli kaamkaje not on merits hivyo ilikuwa lazima upinzani upambane na Magufuli as a person kwa sababu yeye ndiye aligeuka kuwa ccm na ndiyo sera ya ccm kwa kipindi chake. Kingine Magufuli hakupambana na sera za upinzani alipambana na wapinzani individually.

Kwanini siasa za miaka mitano ijayo zitakuwa tofauti? Ni kwa sababu ccm italazimika kufufuka ili ikajitetee jukwaani tofauti na kusubiri Simon Sirro aitetee kwa maji ya washa washa na mabomu ya machozi kama wapinzani wataendelea kuwa vigilant nina hakika wataitesa sana hii ccm itakayokuwa inapambana kufufuka.

Matatizo yanayoikabili ccm ya sasa ni mawili 1. Haina hoja tena za kupeleka kwa wananchi 2. Haina watu wakuzipeleka hizo hoja kwa wananchi.

Ni jukumu sasa la upinzani kuamka kuacha kupambana na legacy choko ya marehemu warudi kwenye siasa halisi.
 
Uko sahihi. Ingawa kiuhalisia mlengwa hapo ni Chadema bila shaka, maana ndicho chama kikuu cha upinzani na chenye ushawishi kwa wapenda mabadiliko wengi, na hasa kwa upande wa Tanganyika.
Sawa sawa mkuu
 
Usijidanganye, Rais hajaenda ikulu kubembelezwa, ameenda ikulu kuwatumikia watanzania kwa kuwapa mahitaji yao ya msingi, ya kisiasa yakiwa miongoni mwao.

Wapinzani watabadilishwa na vitendo vyake, wakitaka Katiba mpya awape, wakitaka Tume huru awape, akifanya hivyo sio tu watamlegezea sauti kama mnavyotaka, bali watafunga midomo yao kabisa, lakini sio kumlegezea sauti kwasababu ya kupewa chai ikulu.

Nani mwenye uhakika kwamba Rais akilegezewa sauti ndio atatimiza matakwa ya wapinzani? au mnataka kuzubaisha watu muda uende halafu tena mje kusema walishindwa wenyewe.
 
Natamani wapinzani walione bandiko lako wajifunze kitu. Umeandika vema sana.
 
Umeongea ukweli ngoja tujipange sasa. Siasa ni nyakati
 
Ni kweli kabisa, wapinzani bila ya kushindana kwa hoja watakuwa na wakati mgumu sana
 
kwa sasa hawana chaguo.

kuchukia harakati za magufuli ni kupishana na watanzania wengi,kumfagilia mama samia ni kuungana na ccm.

lakini wa sababu walinyimwa busara,hawakuweza kujua hatari ya matokeo ya majibu watakayopewa baada ya kumwomba mungu wao.
leo hii magufuli amekufa,na chadema inaelekea kuzimu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…