Uchaguzi 2020 Upinzani ukimweka Membe itakuwa tofauti kubwa na ilivyokuwa kwa Lowassa! Watashinda

Uchaguzi 2020 Upinzani ukimweka Membe itakuwa tofauti kubwa na ilivyokuwa kwa Lowassa! Watashinda

Tatizo kubwa ambalo upinzani wanalo ni kuhusu ruzuku maana watapata kidogo sana kipindi hiki kwa sababu ya yaliyofanyika na ambayo Watanzania wanategemea kufanyika na kukamilika chini ya JPM na CCM.

View attachment 1485424

Hapa kazi tu!
Hao vijana naona wamekosa elimu. Bango lenye maneno machache kama hilo, lina makosa kibao ya kiuandishi.

Kiongozi usiwategemee sana wajinga, wategemee watu werevu. Mjinga akieleweshwa na akaelewa hawezi kuendelea kuunga mkono alichokuwa akikiunga mkono wakati wa ujinga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu lowasa alikuwa ni national figure yule nje na hapo alikuwa na majority suport ya mikoa mitatu [kama unaakili utanielewa] hata kabla ya kampeni

Kiufupi itahitaji miaka mingine hamsini upinzani kupata mgombea mwenye ushawishi kama mzee lowasa
Kuna siku hata magufuli mtaanza kumponda wanafiki bhana
 
Kuna rafiki yangu mmoja hupendelea kusema "Mungu (ni) fundi" akimaanisha "never say never". Mambo yanaweza kubadilika kwa namna ambavyo wengi hatukutarajia. Tumuachie Mungu tu.

By the way, najaribu kufikia kauli za Membe za hivi karibuni kuhusu kukiukwa taratibu za kufukuzwa ccm na uwezekano wa yeye kugombea ......amechagua maneno sana, ametumia sana nafsi ya "wingi"....."Sisi......!" Wapo yeye na nani?
 
Ni kweli BM anaweza kuitikisa sana CCM, hili hata wao wanalijua! .....Anaifahamu CCM na anaujuwa udhaifu wake lakini zaidi ya yote ana ushujaa na ujasiri ambao wana CCM wengi hawana, Tena anaweza kuongea bila kumung'unya maneno!
Vuta picha kwa mfano katika kampeni zake akataja mauzauza kibao ndani ya ccm yakiwemo mipango ovu ya kununua wapinzani n.k. Akaja kwa wanafunzi vyuo vikuu awambie anapunguza makato ya Bodi ya mikopo toka 15% hadi 5%, na pia mwanachuo ukimaliza chuo utapewa 2miln za kuanzia ujasiriamali na makato yake yanajuishwa hapohapo kwenye hiyo 5%! Je hapa si wanafunzi wote na wanufaika watamuunga mkono! Vuta picha awaambie watumishi atawalipa nyongeza zote za mishahara ya miaka 5 waliyodhulumiwa na serikali ya jiwe na kuanzia hapo nyongeza ya mshahara itakuwa kama kawa! Unazani wafanyakazi watamuangusha? Hebu vuta picha aje na ajenda ya kuhakikisha wafanyabiashara wote walionyanyaswa na serikali wanapata haki zao, hivi mfanyabiashara gani atamtupa! Hebu vuta picha aje na ishu ya kuwalipa fidia wananchi wote Tanzania nzima waliokwishabomolewa nyumba zao bila kulipwa chochote, Je hapa wananchi watamuacha? Aje na ishu ya kukomboa wakulima wa korosho, Pamba, ufuta na mazao mengine, Je hapa wakulima watamtosa kweli?.....Kwa hakika BM anaweza kuleta upinzani mkali sana na hata kuiondosha CCM madarakani na watu wasishangae!
 
Mbona anaogopa watu kumu challenge?

Hakuna mtu wa kutoa challenge hapo, kwa mafanikio haya ..... ...

1592832102786.png


Wengine wanawewesekaweweseka tu.
 
Mkimweka mamluki kutoka ccm tena aje agombee kupitia vyama vya upinzani ndio itakuwa mwisho wangu kuamini upinzani,sio kwa usaliti alioufanya lowasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli BM anaweza kuitikisa sana CCM, hili hata wao wanalijua! .....Anaifahamu CCM na anaujuwa udhaifu wake lakini zaidi ya yote ana ushujaa na ujasiri ambao wana CCM wengi hawana, Tena anaweza kuongea bila kumung'unya maneno!
Vuta picha kwa mfano katika kampeni zake akataja mauzauza kibao ndani ya ccm yakiwemo mipango ovu ya kununua wapinzani n.k. Akaja kwa wanafunzi vyuo vikuu awambie anapunguza makato ya Bodi ya mikopo toka 15% hadi 5%, na pia mwanachuo ukimaliza chuo utapewa 2miln za kuanzia ujasiriamali na makato yake yanajuishwa hapohapo kwenye hiyo 5%! Je hapa si wanafunzi wote na wanufaika watamuunga mkono! Vuta picha awaambie watumishi atawalipa nyongeza zote za mishahara ya miaka 5 waliyodhulumiwa na serikali ya jiwe na kuanzia hapo nyongeza ya mshahara itakuwa kama kawa! Unazani wafanyakazi watamuangusha? Hebu vuta picha aje na ajenda ya kuhakikisha wafanyabiashara wote walionyanyaswa na serikali wanapata haki zao, hivi mfanyabiashara gani atamtupa! Hebu vuta picha aje na ishu ya kuwalipa fidia wananchi wote Tanzania nzima waliokwishabomolewa nyumba zao bila kulipwa chochote, Je hapa wananchi watamuacha? Aje na ishu ya kukomboa wakulima wa korosho, Pamba, ufuta na mazao mengine, Je hapa wakulima watamtosa kweli?.....Kwa hakika BM anaweza kuleta upinzani mkali sana na hata kuiondosha CCM madarakani na watu wasishangae!
Good!
 
Mkuu lowasa alikuwa ni national figure yule nje na hapo alikuwa na majority suport ya mikoa mitatu [kama unaakili utanielewa] hata kabla ya kampeni

Kiufupi itahitaji miaka mingine hamsini upinzani kupata mgombea mwenye ushawishi kama mzee lowasa
Ujinga kabisa na upuuzi. Miaka hamsini ya kumpata mtu kama Lowassa? Kwa kitu gani special alichokuwa nacho? Sidhani na siamini kabisa kuwa kama taifa tumeishiwa kiasi hicho. Lowassa alikuwa wa kawaida tu na tena kawaida sana na kilichompandisha ni promo tu za Team Lowassa. Hakuwa presidential material kiivo kama unavyotushawishi. Na kwangu binafsi naona hakufikia upepo wa Dkt Slaa alipogombea urais.
 
Membe huyuhuyu au mwingine? unafikiri CCM ni wajinga kumvua uanachama? hana impact yoyote kabisa kwa CCM ndiyo maana wakamvua uanachama. Wapinzani wakimuchukua Membe basi watakuwa wamesaidia wenyewe kuufuta upinzani afadhali waendelee na wagombea wao akina Lissu,Mbowe na Zitto.
Si ndiyo Mimi nashangaa yani Jambo dogo Kama hilo mpaka tutumie nguvu kubwa kulielezea? Hana impact yoyote ile ni bora wakomae wenyewe inaweza leta mashiko wakimchukua tu wameharibu tena zaidi
 
Ujinga kabisa na upuuzi. Miaka hamsini ya kumpata mtu kama Lowassa? Kwa kitu gani special alichokuwa nacho? Sidhani na siamini kabisa kuwa kama taifa tumeishiwa kiasi hicho. Lowassa alikuwa wa kawaida tu na tena kawaida sana na kilichompandisha ni promo tu za Team Lowassa. Hakuwa presidential material kiivo kama unavyotushawishi. Na kwangu binafsi naona hakufikia upepo wa Dkt Slaa alipogombea urais.
Wewe unazijua siasa. Ni kweli ulio dhahiri kuwa Lowasa hakuwa presidential materia kama walivyo akina Tundu Lissu, Membe na Zitto kwa sasa!
 
Lowassa pamoja na kupendwa sana kwa kweli alikuwa dhaifu mno 2015. Tena mno, kimawazo (hakuwa na mvuto wa hoja) na hata kiafya (enzi za siha njema zilishampita). Kwangu mie hata JK kuhakikisha Lowassa hawi Rais ilikuwa ni kumsaidia rafiki yake ambaye alikuwa anajua undani wake. Lowassa asingeweza kuongoza vizuri na pengine hata afya yake ingetetereka zaidi na zaidi iwapo angekuwa Rais. Ni afadhali anavyoenenda kwa namana hii.

Ninawahakikishia Membe akibahatika kugombea kupitia upinzani - kuna uwezekano mkubwa sana wa upinzani kushinda uchaguzi ama kupata asilimia zaidi ya 40 za kura zote kwa Mwaka huu. Mwembe anakuja na approach nzuri, yaani analenga kupata msimamo wa kimataifa kuhusu chaguzi bora na zilizo huru (Fair and Free Election). Membe ameshaanza kuieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tume ya Uchaguzi ya Chama sio huru. Yaani ni MCCM halafu anajisema kuwa chombo cha kumpa ushindi yeye mwenyewe iwapo akipitishwa na CCM kugombea hakipo huru.

Ajabu sana kwani amekuwa akisema hili kwa muda tu na sio jana tu. Inawezekana kabisa huko huko Tume wanamtonya kuwa "Mkuu hatuko huru!". Sasa ukushaanza kuongelea kuwa Tume sio huru na kuvuta Jumuiya ya Kimataifa kwa jambo hilo ujue kuna watu unawaeleza siri zako za ndani na unawakaribisha waingilie. Kwa vyovyote vile iwapo Uchaguzi huu yatatokea maafa sio mbaya utawala huu kuja kuwajibishwa na vyombo va kimataifa hata kwa mauaji ya kimbari. Membe amelenga mbali sana - naamini akipata nafasi akaanza kuongea kwenye Kampeni atabadilisha sana upepo.

Membe akiongea kwa kukosoa Chama Chake kuhusu ujenzi wa mamiundo mbinu bila kujali hali za kipato kwa wananchi na kutamka wazi wazi wafanyakazi wamenyanyasika ni nani hatamsikia. Membe akitoa hadi njema kwa wananchi dhidi ya habari za kujenga mamiundombinu za awamu hii nani atasikiliza mambo ya mamiundo mbinu. Membe akieleza kwa ufasaha kuhusu zao la korosho lilivyodukuliwa na kuwasababishia wananchi wake ni nani hatamwelewa?

Membe akiongelea kupotea kwa akina Ben Saa Nane kwa kutoa siri anayoijua kuhusu hilo nani hatavutiwa naye? Membe akiongelea na kuwataja walimtwanga Tundu Lissu mirisasis kibao, ni nani hatamwelewa? Kumbukeni unaweza kutenda mema mengi lkn ukatenda baya moja tu likakuangusha katika maisha yako yote ya kutenda mema. hebu mchuku askofu aliyeponya wat na watu, siku ikatokea bahati mbaya tu akambaka muumini si na uaskofu wake anaweza kuukosa?

Mie ninaamini kabisa sasa CCM inaelekea kudondoka kwa kishindo kikubwa sana. Iwapo CCM itashinda mwaka huu basi itakuwa imeshinda kwa mbinde sana. Na isiposhinda itakuwa imejitakia yenyewe kwani asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Wananchi walikuwa wana mengi ya kusikilizwa na awamu hii - yamepuuzwa kwa kiburi cha kufikiri ni awamu inayopendwa kumbe ni hovyo kabisa na imejawa na udikiteta lukuki.
Duh!
Hii story INACHEKESHA!
 
2015 Lowassa alikuwa puppet wa CCM
Hapo ndipo ninapoiheshimu CCM.
Waliisoma CHADEMA wakajua pale wakufanya nao biashara ni MBOWE na LISSU tu. Wengine wote ni misukule, itafuata chochote kitakachoamliwa.
Wakapiga dili, dili likatiki wakaacha MISUKULE ikikunja ngumi na kuzungusha. GAME OVER!
 
Amin nakuambia,
wako watu wenigi ndani ya CCM hufuata maslahi tuu kwa vile wamelazimishwa ili wapate ajira.
Kiukweli idadi yao inaongezeka kila uchao na siku ya kuizamisha CCM ikifika ,hao ndio watakao kididimiza kichwa cha CCM ndani ya maji makuu isiibuke tena.
Hata wana CCM wenyewe wamekichoka chama chao ,kila siku wimbo ni ule ule wa ulaghai,
Hatimae Maisha yao yanazidi kuwa magumu
Hebu fikiria ! ni CCM wangapi walivunjiw nyumba zao pale jangwani,kimara,kibamba na kwengineko bila malipo hata kupewa kiwanja?
Hivi leo hakuna mtumishi hata mmoja wa umma aliye na amani, Hata hao wakuu wa mikowa au mawaziri wakijua wazi kuwa muda wowote ule wanaweza kutumbuliwa bila ya huruma na kuvunjiwa heshima zao hadharani.Pengine kwa makosa madogo na yasiyowahusu wao moja kwa moja.
Hivi unadhani U ccm wa Membe, Kinana, Nape na wengineo ni uleule wa zamani? ujuwe lazima wapo pale kimaslahi tuu.
Muda ukifika , na muda ndio huu CCM inakwenda zake KUZIMU bila kurudi, Kiburi cha CCM na Makufuru yao yamezidi mno.
Si dhani kama Mungu atawapa tena Upendeleo.
Kujigamba kuwa Utakuwepo Milele hii ni kufuru
Kujiita wewe Nabii, Chaguo la Mungu n.k hizi zote ni kufuru .
SUPRISE iko karibu wana CCM jiandaeni kiskolojia ,na wengi wataihama nchi, maana wanajua Madhambi waliyowafanyia watanzania.
Ndani ya vyombo vya dola pia wapo watu tofauti, wengi waoni wale wasioridhishwa na mfumo kandamizi ,ila wafanyije?
Siku ikifika Hao ndio watakuwa muhimilimkubwa wa mageuzi.
Naihurumia Tanzania yangu, Maana CCM wametengeneza bomu la kutega, siku likitumbuka hali itakuwa mbaya sana.
Si jui nani ataituliza hali.
Chuki zimepandikizwa nyingi mno.
Hali ya Ubaguzi ,na Maonevu , ya visasi
Sikuhiyo hali siui itakuwaje
 
Back
Top Bottom