Upinzani watangaza mapambano 2008

Upinzani watangaza mapambano 2008

Traitors ni wale Watanzania ambao wamekaa tu na kusubiri wengine wahangaike kuleta mageuzi. Ni wale wanaokaa bila mchango wowote katika mabadiliko ya kisiasa nchini petu. Ni wale wanaokaa na kulaumu wenzao na kusubiri wakosee wawaseme. Ni wale ambao wanadhani siasa ni tamu na hivyo wanasiasa tunafaidi ilihali tunarisk maisha na hata kutojiendeleza. Traitor sio Marando alieanzisha chama wakati ambao ilikuwa ngumu hata kuwaza kuanzisha chama. Traitor sio Marando ambae hata sasa anasaidia gazeti la mwanahalisi litoke kwa kutoa mchango wa hali na mali. Traitor si Marando alietukanwa na kila mtu bila kujali mchango wake katika mageuzi hapa nchini. Hawezi kuwa Marando traitor ambae wenzake wote wamerud CCM ila yeye na Ndimara bado wapo na chama chao! Traitor ni Mtanzania asietambua harubu tupatayo wanasiasa wa upinzani! Harubu tuipatayo tunapoenda vijijini kuongea na watanzania na kulala mahala ambapo mushi huwajahi lala.

Nakumbuka hadithi ya Prince Bagenda na Mabere Nyaucho Marando walipoenda Rufiji na kulala katika kitanda cha kamba. Watu wazima 2 kitanda kimoja. Kitanda kikakatika na wote kuanguka. Walikuwa katika kueneza vyama vingi. Wakati ambao ulikuwa ukihubiri vyama unaonekana kichaa na watu wanakaa kuleeeeeeeeeee! Hawa wanapswa kuenziwa na sio kuitwa majina yote mabaya. Wale waliopotea njia wanapswa kusikitikiwa kwa kuishia njiani. Lakini tukifika safarini tutawatambua mchango wao walioutoa. Tutafika siku chache zijazo.

Mzee Mtei husema mapambano ya kisiasa ni kama gari moshi liendalo Kigoma. Kuna abiria watashuka Pugu (chemponda etc) wengine morogoro (msabaha etc), wengine Kilosa (Lamwai etc), wengine Dodoma ( Tambwe Hiza etc), wengine Manyoni (Kabourou etc), wengine Kintinku (Akwilombe etc) na bado kuna wengine watashuka gari moshi linavyozidi kwenda. Ila kuna wengi watapandia Tabora, Urambo na Hata Luiche kuelekea kituoni Kigoma. Kuna wengine watajaribu kudandia tutakapokuwa tunatia breki Kigoma ili nao wawemo katika ushindi. Gari moshi hili linabadili madereva kila inapofaa.

Hekima hii ya Mtei ni muhimu sana. Gari moshi sasa linaenda kwa kasi, limekaribia Igalula. Siku si nyingi litafika Kigoma na Watanzania watapata uongozi unaostahili! Uongozi unaojali historia ya nchi na uongozi unaojua ni wapi nchi yapaswa kwenda. Uongozi utakaorevive Tanzanian Dream waliokuwa nayo akina Nyerere! Lakini kwa ushujaa wa akina Mkwawa, Isike, Mazengo, Kinjikitile na wengineo!

Nimeshukuru sana kwa maelezo yako!
Lakini nimeonelea niseme something..Especially hapo nilipo highlight!
Kwamba hayo maisha waliyokutana nayo kina Marando pamoja na nyie wanasiasa wa upinzani kwa ujumla ndio maisha wanayoishi watanzania walio wengi!

Hivyo basi si mbaya sana kwasababu hilo lita wasaidia kutokuwa out of touch.Litawasaidia kuyajua machungu ya wananchi walio wengi na shida na taabu wanazozipata! Si tu kwenye kulala bali chakula na matibabu pamoja na elimu!

Jingine ni hilo la kina Marando kuendelea na Siasa licha ya kwamba no body cares!
Na hapo ndio penyewe haswa! Kusema kuwa Mrema asingekuwa na mahali pa kwenda kama si Marando siyo kweli!

Kama angetaka na yeye kufungua chama chake angeweza..Ila bado ingemchukua muda zaidi na kwasababu hiyo aka consider watu amabo kimwonekano walikuwa kama wapinzani wa kweli na wazalendo!

Kumbe wao kina Marando walikuwa wakijua kuwa..MORE WANACHAMA=MORE MONEY! Which proved to be true!

Mrema hakujua kuwa hawa watu wanajali maslahi zaidi ya uzalendo!

Mimi niliwaona wakianza kunawiri mara baada ya kupata wanachama wengi na hivyo mapato ya chama kuongezeka! Sasa mara baada ya kupata umaarufu mkubwa na mipesa..Wakaanza urafiki na CCM na kujidai eti wanajali maslahi ya Taifa! WAPI BANA!

Mara nikaanza kusikia migogoro na Marando kuwa favored na CCM na Mkapa na Mrema kuendelea kuchukiwa na CCm huku akiitwa Kichaa!

Na marando kusapoti huo uoza!

Huku na yeye akiwapa CCM siri za Mrema na wapinzani na hivyo kumporomosha kisiasa!
Sasa yeye ni kipi kilichomfanya ageuze mawazo tofauti na wenzake kina Lamwai?

Hivi kweli Zitto...

CCM wamsapoti Marando,halafu waendelee kumwua mrema kisiasa..Hiyo sio maana sahihi ya kuwa "Traitor?

Ama kuna mengine tusiyoyajua?

NB: (kwenye red highlight) Nimeshawahi lala sehemu crazier ma man! Ila maybe in a diffrent situation and/or mission!
 
Mimi nisikufiche Zitto wananchi wanakuangalia kwa moyo wa matumaini makubwa mno!
Kuliko hata ya Mh Rais mwenyewe!
Ni kweli tunampa heshma zake zote lakini ikija kwa wananchi wa kawaida kama sisi..Ni wewe ndio tegemeo letu
!

mhm ! kama kweli, itabidi nianze kumuomba autograph mapema !
 
Nimshukuru sana kwa maelezo yako!
Lakini nimeonelea niseme something..Especially hapo nilipo highlight!
Kwamba hayo maisha waliyokutana nayo kina Marando ndio maisha wananoishi watanzania walio wengi!Hivyo basi di mbaya sana kwasababu hilo lita wasaidia kutokuwa out of touch.
Jingine ni hilo la kina Marando kuendelea na Siasa licha ya kwamba no body cares!
Na hapo ndio penyewe haswa! Kusema kuwa Mrema asingekuwa na mahali pa kwenda kama si Marando siyo kweli!
Mrema hakujua kuwa hawa watu wanajali maslahi zaidi ya uzalendo!
Mimi niliwaona wakianza kunawiri mara baada ya kupata wanacham,a wengi na hivyo mapato ya chama kuongezeka! Sasa mara baada ya kupata umaarufu mkubwa na mipesa..Wakaanza urafiki na CCM na kujidai eti wanajali maskahi ya Taifa! WAPI BANA!
Mara nikaanza kusikia mogogoro na Marando kuwa favored na CCM na Mrema kuendelea kuchukiwa na CCm huku akiitwa Kichaa!
Na marando kusapoti huo uoza!
Huku na yeye akiwapa CCM siri za Mrema na hivyo kumporomosha kisiasa!
Sasa yeye ni kipi kilichomfanya ageuze mawazo tofauti na wenzanke kina Lamwai?
Hivi kweli Zitto...CCM wamsapoti Marando,halafu waendelee kumwua mrema kisiasa..Hiyo sio maana sahihi ya kuwa "Traitor?
Ama kuna mengine tusiyoyajua?


Mrema ana nafasi kubwa sana katika siasa za vyama vingi na mageuzi ya kisiasa hapa nchini. Lakini naye pia ana makosa yake kama ilivyo kwa akina Marando. Wote wana makosa makubwa ambayo ipo siku watapaswa kuwaomba radhi watanzania. Mrema kanyanyaswa sana, kazuliwa mambo mengi sana. Lakini historia ya nchi itawalinda. Pale historia ya kweli ya nchi itakapoandikwa
 
...Harubu tuipatayo tunapoenda vijijini kuongea na watanzania na kulala mahala ambapo mushi huwajahi lala. Nakumbuka hadithi ya Prince Bagenda na Mabere Nyaucho Marando walipoenda Rufiji na kulala katika kitanda cha kamba. Watu wazima 2 kitanda kimoja. Kitanda kikakatika na wote kuanguka. Walikuwa katika kueneza vyama vingi...

Mheshimiwa Zitto, taadhima na shukrani siku zote kwa mchango wako.

Mheshima, hao kina Marando, Bagenda na wewe pia nadhani hamtakiwi kabisa kurudia hadharani hiyo hadithi ya kulala kwenye vitanda vya kamba kama kielelezo cha shuruba mnayo ipata. Inaonyesha mlivyo kuwa out of touch. Kama mnadhani ni harubu kuwa katika mazingira hayo wakati hivyo ndivyo wananchi wengi wanavyo ishi basi ujumbe wenu ni elitist.

Bonge la faux pas hilo.
 
Mheshimiwa Zitto, taadhima na shukrani siku zote kwa mchango wako.

Mheshima, hao kina Marando, Bagenda na wewe pia nadhani hamtakiwi kabisa kurudia hadharani hiyo hadithi ya kulala kwenye vitanda vya kamba kama kielelezo cha shuruba mnayo ipata. Inaonyesha mlivyo kuwa out of touch. Kama mnadhani ni harubu kuwa katika mazingira hayo wakati hivyo ndivyo wananchi wengi wanavyo ishi basi ujumbe wenu ni elitist.

Bonge la faux pas hilo.

Nadhani ni hadithi nzuri na inayofanya viongozi kuona hali ya maisha ya watanzania. Kuacha kusema ni unafiki kwani ukweli ni kwamba watu wengi hamuishi hivyo na wakati mwingine mnasahau kuwa kuna watanzania wanaishi hivyo. Nadhani ni hadithi nzuri na inafaa kuwa recited
 
Kuhani mkuu,
Kiongozi yeyote ni lazima afanane kimaisha na wananchi anaotaka kuwaongoza iwe kwa kifikra ama kimwili...
Kama ukionyesha hujalala ktk amka nikukaze ukazunguzia maisha ya Masaki na O'bay kwenye vyopo vya kuvuta, mkuu hao wakulima wetu huko vijijini watashindwa kukuelewa..Yaleyale ya The Gods must be crazy!
Ni muhimu uzungumze lugha wanayoifahamu na sio kuwaahidi Ndege kupaa wasifahamu unachojaribu kusema.
 
Kuhani mkuu,
Kiongozi yeyote ni lazima afanane kimaisha na wananchi anaotaka kuwaongoza iwe kwa kifikra ama kimwili...
Kama ukionyesha hujalala ktk amka nikukaze ukazunguzia maisha ya Masaki na O'bay kwenye vyopo vya kuvuta, mkuu hao wakulima wetu huko vijijini watashindwa kukuelewa..Yaleyale ya The Gods must be crazy!
Ni muhimu uzungumze lugha wanayoifahamu na sio kuwaahidi Ndege kupaa wasifahamu unachojaribu kusema.
Lakini haina maana kuwa wote wanaolala masaki ama osterbay hawajawahi kupitia suruba!
 
Tusisahau pia kujitolea siyo kujionyesha!
Kuna watu amabo ni matajiri lakini wamepitia mengi na bado wanakuwa concerned na watu masikini!
At the same time kuna wanaopitia maisha kama hayo na badae kuwadharau wengine kwasababu ya uchungu wa kule walikopitia!
 
Kuhani mkuu,
Kiongozi yeyote ni lazima afanane kimaisha na wananchi anaotaka kuwaongoza iwe kwa kifikra ama kimwili...
Kama ukionyesha hujalala ktk amka nikukaze ukazunguzia maisha ya Masaki na O'bay kwenye vyopo vya kuvuta, mkuu hao wakulima wetu huko vijijini watashindwa kukuelewa..Yaleyale ya The Gods must be crazy!
Ni muhimu uzungumze lugha wanayoifahamu na sio kuwaahidi Ndege kupaa wasifahamu unachojaribu kusema.

Mkandara ahsante.

Hujanielewa hata kidogo.

Pointi ya Mh. Zitto, mtanisahihisha kama naikosea, ni kwamba moja ya mfano wa shuruba wanazozipata ni kama vile walivyo lala kwenye vitanda vya kamba wakati wa uchaguzi. Pointi yangu mimi ni kwamba hicho kitu kukisema kama nembo ya heshima ni elitist kwa sababu sio cha ajabu hicho kwa wengi. Ndugu zangu wengi kijijijini ndivyo wanavyo lala, tena wengine hawana hata hivyo vya kamba.

Kwa hiyo kiongozi akisema nimepata shuruba kwa kulala kwenye kitanda cha kamba huyo mtu yuko out of touch.
 
Mimi naomba tu Mungu aisadie nchi yetu na wapinzani wasigawanyike tena jamani!
I am deeply concerned!
 
Niliwahi kuona tangazo katika mtandao wakati Fulani , mmoja wa wabunge wa upinzani Tanzania ameacha namba yake ya simu atakayotumia atakapofika marekani , kwa wale ambao hawako busy wanapenda kuonana nae na vijana wengine wengi wenye muelekeo wa kipinzani .

Sitaki kubisha inaonekana wapinzani wamewashika sana vijana wa kitanzania walio nchi za nje haswa marekani kiasi kwamba zitto anapokanyaga huko wanaona mwokozi wao kafika watu wanasongamana wanataka kumwona kupiga nae picha na vitu kama hivyo .

Pamoja na kuacha hizo namba za simu na watanzania kujitokeza kuonana nae , sera na mambo anayoongea katika mikutano hii ni zile zile , za ufisadi ambazo sasa hivi ni zilipendwa , yale yale ya epa na mambo mengine ambayo kwa hakika sio ya kujenga upinzani sio ya kujenga nchi ni ya kupasua hadhi ya nchi na watu wake nje ya mipaka yake .

Namheshimu Nyepesi na Wenzake wengi kama watanzania lakini siwezi kuheshimu na kuendelea kusikiliza watu wenye mawazo ya kuvuruga wananchi wakiwa nje ya mipaka yao huwa nashangaa kama hawana masuala mengine ya kuongea zaidi ya haya .

Hao ni chadema ndio wameshikilia Epa , Ufisadi na Usalama wa Taifa , ukirudi kwa upande wa baba zako chama cha wananchi CUF , ningekuwa mimi ni mwanachama wa CUF ningehoji kwanini hao viongozi wawili wa CUF wako pale walipo mpaka sasa hivi

Tangia upinzani umeanzishwa ni viongozi wale wale wa CUF wanaowashika masikio baadhi ya wanachama wao , ni viongozi wale wale wakorofi wako madarakani katika chama hicho mpaka sasa hivi , sijui CUF hawana viongozi wengine ni lazima wawe hawa hwaw ?

Mtihani wao wa kwanza wameshaushindwa wa kuleta maelewano huko visiwani , kwa sababu wameshashindwa jaribio hilo , sioni sababu ya kwanini wasiache nafasi hizo wazi waje watu wengine wenye utashi zaidi yao , watu wanaopenda kukaa mezani na kumaliza tofauti zao .

Niliangalia hata wakati wa maandamano ya CUF visiwani wiki iliyopita mmoja wa washairi aliposema kwamba anaweza kujilipua kama mambo yataendelea kuwa hivyo , wengine wakawaambia wenzao wasipeleka bidhaa katika kisiwa kingine wakipeleka basi wao ni halali yao .

Yote hayo yanasemwa viongozi wa CUF wamekaa katika viti wanasinzia wengine wanacheka na kufurahia kwa madaha kama vile ile ni halali yao kusema vile na hakuna chochote kile mbele yake .

Nilitegemea mmoja wa viongozi hawa au msemaji wa CUF aje mbele na kusema kile kilichosomwa na yule mshairi sio msimamo wa CUF lakini hakikutokea kitu kama hicho kwahiyo tuchukulie basi kuanzia sasa hivi na mpaka hapo viongozi wa CUF watakapoamua baadaye

Kwamba sera za CUF kuanzia sasa hivi ni KUJILIPUA , KUKATAZA BIASHARA NA UNGUJA NA KUPUNGUZA UNDUGU WAO kwa sababu hawa wengine sio wanachama wao , wao ni CCM.

51eDX%2BHzLoL._SS500_.jpg
 
Traitors ni wale Watanzania ambao wamekaa tu na kusubiri wengine wahangaike kuleta mageuzi. Ni wale wanaokaa bila mchango wowote katika mabadiliko ya kisiasa nchini petu. Ni wale wanaokaa na kulaumu wenzao na kusubiri wakosee wawaseme. Ni wale ambao wanadhani siasa ni tamu na hivyo wanasiasa tunafaidi ilihali tunarisk maisha na hata kutojiendeleza. Traitor sio Marando alieanzisha chama wakati ambao ilikuwa ngumu hata kuwaza kuanzisha chama. Traitor sio Marando ambae hata sasa anasaidia gazeti la mwanahalisi litoke kwa kutoa mchango wa hali na mali. Traitor si Marando alietukanwa na kila mtu bila kujali mchango wake katika mageuzi hapa nchini. Hawezi kuwa Marando traitor ambae wenzake wote wamerud CCM ila yeye na Ndimara bado wapo na chama chao! Traitor ni Mtanzania asietambua harubu tupatayo wanasiasa wa upinzani! Harubu tuipatayo tunapoenda vijijini kuongea na watanzania na kulala mahala ambapo mushi huwajahi lala.

Nakumbuka hadithi ya Prince Bagenda na Mabere Nyaucho Marando walipoenda Rufiji na kulala katika kitanda cha kamba. Watu wazima 2 kitanda kimoja. Kitanda kikakatika na wote kuanguka. Walikuwa katika kueneza vyama vingi. Wakati ambao ulikuwa ukihubiri vyama unaonekana kichaa na watu wanakaa kuleeeeeeeeeee! Hawa wanapswa kuenziwa na sio kuitwa majina yote mabaya. Wale waliopotea njia wanapswa kusikitikiwa kwa kuishia njiani. Lakini tukifika safarini tutawatambua mchango wao walioutoa. Tutafika siku chache zijazo.

Mzee Mtei husema mapambano ya kisiasa ni kama gari moshi liendalo Kigoma. Kuna abiria watashuka Pugu (chemponda etc) wengine morogoro (msabaha etc), wengine Kilosa (Lamwai etc), wengine Dodoma ( Tambwe Hiza etc), wengine Manyoni (Kabourou etc), wengine Kintinku (Akwilombe etc) na bado kuna wengine watashuka gari moshi linavyozidi kwenda. Ila kuna wengi watapandia Tabora, Urambo na Hata Luiche kuelekea kituoni Kigoma. Kuna wengine watajaribu kudandia tutakapokuwa tunatia breki Kigoma ili nao wawemo katika ushindi. Gari moshi hili linabadili madereva kila inapofaa.

Hekima hii ya Mtei ni muhimu sana. Gari moshi sasa linaenda kwa kasi, limekaribia Igalula. Siku si nyingi litafika Kigoma na Watanzania watapata uongozi unaostahili! Uongozi unaojali historia ya nchi na uongozi unaojua ni wapi nchi yapaswa kwenda. Uongozi utakaorevive Tanzanian Dream waliokuwa nayo akina Nyerere! Lakini kwa ushujaa wa akina Mkwawa, Isike, Mazengo, Kinjikitile na wengineo
!

Kweli kabisa Zitto,

Nakubaliana nawe kuwa matraitors ni kama kina Mushi hawa ambao wao wamekaa Marekani kwenye confort na kuanza kutukuna wenzao ambao wako msitari wa mbele.

Kwa nini wewe Mushi usiende Tanzania kuanzisha chama ambacho hakina wasaliti?
 
Kweli kabisa Zitto,

Nakubaliana nawe kuwa matraitors ni kama kina Mushi hawa ambao wao wamekaa Marekani kwenye confort na kuanza kutukuna wenzao ambao wako msitari wa mbele.

Kwa nini wewe Mushi usiende Tanzania kuanzisha chama ambacho hakina wasaliti?
Sasa kila mtu akianzisha chama kuna usalama?
Eti matraitor ni kina Jmushi waliokaa marekani!
Nani aliye kiongozi ambaye hakuwahi kukaa marekani?
Mwalimu?
Nani? Taja
Si wote waliokaa marekani lakini asilimia kubwa wamekaa marekani!
Na mimi niko hapa kimasomo na usishangae nikiwa kwenye kampeni 2010! Kuwapigia kampeni wazalendo!
Sasa kukaa marekani kunahusiana nini na mimi kutoa mchango wangu na kuuliza when mafisadi watakamatwa?
Wewe si ndio umemwambia mchafuzi akamtafute Balali?
Lugha chafu chafu tu na kujikomba komba!
 
Sasa kila mtu akianzisha chama kuna usalama?
Eti matraitor ni kina Jmushi waliokaa marekani!
Nani aliye kiongozi ambaye hakuwahi kukaa marekani?
Mwalimu?
Nani? Taja
Si wote waliokaa marekani lakini asilimia kubwa wamekaa marekani!
Na mimi niko hapa kimasomo na usishangae nikiwa kwenye kampeni 2010!
Sasa kukaa marekani kunahusiana nini na mimi kutoa mchango wangu na kuuliza when mafisadi watakamatwa?
Wewe si ndio umemwambia mchafuzi akamtafute Balali?
Lugha chafu chafu tu na kujikomba komba!

Wakati ukiwa marekani unategemea nani akuendeshee upinzani kule Tanzania?
 
Wakati ukiwa marekani unategemea nani akuendeshee upinzani kule Tanzania?
Nimeshakwambia nipo hapa kimasomo!Tena najisomesha elimu kama waliyosomeshwa mafisadi na wananchi!Si baba si mama si serikali! MAN ALONE!
Na kama ni kupigika nimepigika kama wengine tu!
Kwani marekani ndo mbinguni?
Nani kakwambia sirudi bongo?
 
Kuna moja nilliliacha lipite lakini naona watetezi kama kina Mgaya wanaliamsha bila kujua madhara yake.

Mheshimiwa Zitto angekuwa kwenye jamii iliyo iva kisiasa halafu akaita wananchi wasaliti angekuwa amejinywesha sumu ya panya. Angekufa kisiasa!
 
Lengo hapa ni kuibadilisha nchi yetu!
Bado na mimi nitatoa mchango wangu kama wengine!
Ila usifikiri kuwa mimi ni mgeni wa Tanzanian Politics!
Na therefore this time nasympathize na watu wanaopitia yale ambayo niliyapitia mimi!
Siwezi kukaa tu!
Nikitaka kufanya hivyo naweza! Ila kuna msukumo ambao siwezi kuuzuia na i dont know why!
Sio msukumo mbaya! Bali ni msukumo wa kutotaka kuona yale mabaya yaliyotokea kwenye upinzani yakiwa hayarudiwi tena!
 
Kuna moja nilliliacha lipite lakini naona watetezi kama kina Mgaya wanaliamsha bila kujua madhara yake.

Mheshimiwa Zitto angekuwa kwenye jamii iliyo iva kisiasa halafu akaita wananchi wasaliti angekuwa amejinywesha sumu ya panya. Angekufa kisiasa!

Kama watu ni wasaliti basi wanaitwa kwa jina lao - wasaliti. La sivyo watajua vipi kama wao ni wasaliti?
 
Nimeshakwambia nipo hapa kimasomo!Tena najisomesha elimu kama waliyosomeshwa mafisadi na wananchi!Si baba si mama si serikali! MAN ALONE!
Na kama ni kupigika nimepigika kama wengine tu!
Kwani marekani ndo mbinguni?
Nani kakwambia sirudi bongo?

Wakati ukiwa marekani, nani anakuendeshea hicho chama ambacho hakina wasaliti kama kina marando (kwa msimamo wako)?
 
Lengo hapa ni kuibadilisha nchi yetu!
Bado na mimi nitatoa mchango wangu kama wengine!
Ila usifikiri kuwa mimi ni mgeni wa Tanzanian Politics!
Na therefore this time nasympathize na watu wanaopitia yale ambayo niliyapitia mimi!
Siwezi kukaa tu!
Nikitaka kufanya hivyo naweza! Ila kuna msukumo ambao siwezi kuuzuia na i dont know why!
Sio msukumo mbaya! Bali ni msukumo wa kutotaka kuona yale mabaya yaliyotokea kwenye upinzani yakiwa hayarudiwi tena!

Ungekuwa na nia ya kuhakikisha yaliyotokea kwenye upinzani hayarudiwi basi ungekuwa msitari wa mbele kule Tanzania kupigania watanzania na wapinzani.

Mengine yote hapa ni kelele tu na kupondea wenzako ambao wanafanya kila wanachoweza kujenga demokrasia nchini.
 
Back
Top Bottom