Upoteaji wa majina ya asili ya Waafrika

Upoteaji wa majina ya asili ya Waafrika

Mambo mengi ya asili yanaendana na uchawi.Majina ya asili yapo connected na mizimu na matambiko. Mizimu na matambiko ndo chanzo jinsi waafrika tulivyo, matatizo, umasikini, magonjwa chanzo ni mizimu. Mizimu haitaki maendeleo, hofu watu wakiwa na maendeleo wataelimika wataacha kutambika mizimu.
Wewe umepumbazwa(brainwashed).
Ebu nipe tofauti ya mzimu na mtakatifu? Hayo Majina yenu ni ya mizimu ya kiarabu na ya kizungu.
Nitafitie mzungu anayeitwa abdulaziz au mwarabu anayeitwa Johnson.

Jina linapaswa kutokana na lugha yako unayoongea na siyo dini.
 
Wewe umepumbazwa(brainwashed).
Ebu nipe tofauti ya mzimu na mtakatifu? Hayo Majina yenu ni ya mizimu ya kiarabu na ya kizungu.
Nitafitie mzungu anayeitwa abdulaziz au mwarabu anayeitwa Johnson.

Jina linapaswa kutokana na lugha yako unayoongea na siyo dini.
Mzimu ni shetani aliyevaa roho za watu wa familia,kabila,au ukoo wa Jamii fulani,akijifanya still yupo hai na uhitaji tambiko la kafara ya damu ya mtu, wanyama,nk,mzimu unashikilia miongozo yote ya maisha ya jamii husika.
Mizimu haitaki maendeleo na unazuia mafanikio ya jamii inayoabudu mizimu hofu ya kwamba watu wakipata maendeleo wataacha kuabudu mizimu.
Mtakatifu ni mtu aliyeishi maisha ya uadilifu na utakatifu mbele ya jamii na Mungu pia. Waafrika watakatifu wapo wengi.
Haya ni kwa ushahidi wa Quran, Biblia na Elimu ya uchawi pia imethibitisha ninayoyasema.
 
Watu wa West Africa wametuzidi sana. Kuanzia majina, mavazi na lugha. Sisi huku kusini mwa jangwa la Sahara tumekuwa kama misukule ya wazungu. Yaani unakuta mtu majina yote matatu ya kizungu, hadi unashangaa huyu ni mdudu gani wa kizungu?!!
 
hongera sana kwa uzi huu mzuri. Hili jambo huwa nalifikiria sana aisee. Yaani tumepoteza identity yetu kabisa. Na hili kwa kiasi kikubwa linachagizwa na dini za kigeni tulizoletewa. Mfano, Kwa wakristo wanakwambia kabisa mtoto wakati wa kubatizwa apewe jina la kikristo, hapa wanakuwa washakulimit kutumia jina lako la asili kwa kisingizio cha dini. Kwani tujiulize, huwezi kuwa mkristo au muislam na ukatumia jina lako la asili.? Je jina lako ndo tiketi ya kuiona pepo?
Mbona west africans ni waumini wa hizi dini tulizoletewa na wengi wao wanatumia majina yao ya asili?

Pili, haya majina yanachagizwa na ulimbukeni wa wazazi ambao wanadhani jina la kizungu ni superior kwa jina kiafrica. Wapo radhi kulikejeli na kulicheka jina la asili na kulitukuza jina la kigeni. Huu ni upotokaji wa kiwango kikubwa sana. Yaani mtu yuko proud kuitwa jina la muarabu au mzungu ila asiitwe jina ala asili yake!

Hivi wazungu/ waarabu tuliwa jiuliza huwa wanatufikiriaje wakisikia tunajiita majina yao?

Ukikataa majina yao, mkatae na Mungu wao pia.
 
Hiki kizazi cha nyoka hakitauelewa huu uzi kwa sasa. Ila siku zaja ambapo wajukuu, vitukuu na vilembwe vyetu vitaitafuta asili yao (utamaduni na mila) maana watajikuta majina yao ni kama ya wazungu lakini asili yao ni tofauti na wazungu.
Umenena vyema sana
 
Ongezea pia mtu mweusi anaitwa Abdoul razack majid au fatma masoud
Hao wazanzibar ndio wana majina ya kitumwa kabisa;
Khalifa Hamis Seif
Suleiman Aboubakar Khatib
Mahmoud Salim Mahboub
Khalid Said Khalid
Khadija Maalim Juma
Yaani ni vichekesho vitupu!!! Waarabu weusi wasiojua walitoka wapi na asili yao ni nini. Hakuna utumwa mkubwa kama kupoteza identity yako!
 
Mi najiulizaga wale wavaa kobazi hawana makabila? maana karibia wote wana majina ya kiarabu
 
Ukweli usemwe, hizi dini za kuletewa zimetutoa kwenye asili yetu. Wakristo wamechukua majina ya kizungu, waislamu wamechukua majina ya kiarabu.
 
Mzimu ni shetani aliyevaa roho za watu wa familia,kabila,au ukoo wa Jamii fulani,akijifanya still yupo hai na uhitaji tambiko la kafara ya damu ya mtu, wanyama,nk,mzimu unashikilia miongozo yote ya maisha ya jamii husika.
Mizimu haitaki maendeleo na unazuia mafanikio ya jamii inayoabudu mizimu hofu ya kwamba watu wakipata maendeleo wataacha kuabudu mizimu.
Mtakatifu ni mtu aliyeishi maisha ya uadilifu na utakatifu mbele ya jamii na Mungu pia. Waafrika watakatifu wapo wengi.
Hizo ni tafsiri za jamii iliyopumbazwa. Kwanini jamii zetu ndo zipewe maana mbovu ya mizimu? Na mizimu ya wazungu ipewe maana nzuri ya mizimu?

Inshort babu yako aliyekufa anaitwa mzimu, babu wa kizungu aliyekufa anaitwa mtakatifu kama ujui.
Kuna jamaa yangu ana watoto 8 na watoto 7 wana majina ya asili sasa hawa watoto wote hakuna aliyemzima ni mwendo wa kuumwa kila wakati hebu tazama kuna kipindi watoto 3 walilazwa kwa pamoja kuna aliyekuwa bugando, Sekwao Toure (Seketule) na Mhimbili na wengine nyumbani baadhi wanalipuka mapepo n.k ila huyu mwingine 1 asiye na hayo majina hana shida yoyote akaja gundua baba yake na mama yake dada zake shangazi zake wengi ni wachawi wa kutupwa hivyo wanachezea watoto tangu nilipoona hili tukio la huyu bwana tena kwa macho yangu na wala si kusimuliwa HAKUNA MWANANGU ATAITWA HAYO MAJINA

Tatizo africa ktk koo zetu kuna mambo machafu na ya ajabu ila hatupendi hata kuyajadili unaweza jikuta unateseka ktk maisha yako yoote ya hapa duniani kisa majina ambayo kwa hakika hatujui hao wahenga wetu walikuaje. Mfano kuna jamaa alimaliza form 6 1992 PCB kutoka shule kubwa flani hapa nchini alipata division 1.5 yaani alikuwa BBA kabla ya kujiunga na MUHAS aliumwa miaka 3 yupo home na baadae akajiunga MUHAS akaumwa tena mwisho akaambiwa ili apone inabidi awe mganga wa kienyeji na kweli alipokubali akapona sasa hivi anatibu watu huko kijijini ana manywele mareefu kama jini lililofufuka hana mbele wala nyuma.
Huo ndo upumbavu wenu na akili ya kupumbazwa. Yaan inaingia akilini mtoto kuumwa kwa sababu umempa jina la asili.

Acheni ujinga ndo maana watoto wenu mnawapa Majina ya mashoga na wasagaji. Mwisho wa siku mtaua kizazi chenu.
 
Tambiko lina faida gani, waafrika wameanza kutambika hata kabla ya ujio wa wageni,nini wamepata.Wenzetu weupe wapo vile sababu hawana connection na upumbavu.
Unajua maana ya matambiko? Kanisa katoliki ambalo ndo kiongozi wa makanisa yote inafanya matambiko.

Tatizo lenu mnadhani wazungu Wana maisha mazuri kuliko sisi, yaan kwa Hawana shida hata kidogo.

Connection na upumbavu kivp wakati upumbavu wao unausoma na kuufuata kwenye dini na elimu zao.

Penda vya kwenu kama vibovu, vifanyie maboresho.
 
Ni Nchi gani hiyo ambayo institutional racism imetamaraki hivyo? Nchi nyingi za ulaya na America hata kusema Black man ni kosa. Utasikia wakisema coloured man, nk
Hapo ndo ujinga wetu ulipo, yaaan unajisikia vibaya kuitwa black man. Hawa jamaa wanajua kucheza na akili zetu ndo maana tunakataa asili zetu, Majina yetu, rangi zetu na lugha zetu ila tunajisikia vizuri tukitumia Majina yao, lugha zao, asili zao na rangi zao.

Tukiwa comfortable na asili zetu, hata ukibaguliwa utaona sawa. Na anayekubagua akikuona uko comfortable na asili yako hatakubagua kwa sababu atajua unajua thamani yako.
 
Unajua maana ya matambiko? Kanisa katoliki ambalo ndo kiongozi wa makanisa yote inafanya matambiko.

Tatizo lenu mnadhani wazungu Wana maisha mazuri kuliko sisi, yaan kwa Hawana shida hata kidogo.

Connection na upumbavu kivp wakati upumbavu wao unausoma na kuufuata kwenye dini na elimu zao.

Penda vya kwenu kama vibovu, vifanyie maboresho.
Mifumo yao ya maisha Ina nafuu sana ongelea maisha bora basic needs sizungumzii utajiri,hata nchi za kiislamu za kiafrica Wananchi wao awaisomi Sana number. Katoliki na matambiko wapi na wapi.
Kutambika ni ushirikina.Na ushirikina ni ibada ya shetani.
 
Kwahiyo hayo majina ya wazungu wenye nayo wapo hawajafa si ndio? Hawakuwahi kugombana na koo zao si ndio? Walikuwa wako karibu sana na familia zao si ndio?

Hakuna watoto wa kizungu wasio na akili? Nawao hii inasababishwa nanini? Wamelogwa?

Hakuna wazungu ambao hawaolewi? Wamelogwa?
Hakuna wazungu ambao hawazai? Wamelogwa?
Ndugu yangu kuna watu hapa duniani utadhani wanatumia makalio kuwaza/kufikiri. Usipate tabu sana maana miafrika mingine ndivyo ilivyo!
 
Majina ya kitamaduni za Kiarabu nayo ndio balaa, mtu anajiona wa maana sana kujiita au kumpa mwanae jina kama Farhiya, Masoud, Mohammed, Juma, Abdulmalik n.k anajiona kama kaisha fika mbinguni!

Upande mwingine sasa kuna jina watoto wa kike sasa hivi wanapewa kabla hata hawajazaliwa Precious "Preshaz"!!

Ni ujinga unaoenda kwenye upumbavu!

Tumeiga kila kitu cha wageni, nguo, majina, nyumba, pombe, majina, miungu n.k
 
Hapa babu ameamua bora ajiite Maghayo badala ya Copenhagen 😂


Halafu ninyi wadada wa dar najua mpo hapa, kwanini mnapenda kujiita majina ya precious, Conscious, diva n.k?
 
Hizo ni tafsiri za jamii iliyopumbazwa. Kwanini jamii zetu ndo zipewe maana mbovu ya mizimu? Na mizimu ya wazungu ipewe maana nzuri ya mizimu?

Inshort babu yako aliyekufa anaitwa mzimu, babu wa kizungu aliyekufa anaitwa mtakatifu kama ujui.

Huo ndo upumbavu wenu na akili ya kupumbazwa. Yaan inaingia akilini mtoto kuumwa kwa sababu umempa jina la asili.

Acheni ujinga ndo maana watoto wenu mnawapa Majina ya mashoga na wasagaji. Mwisho wa siku mtaua kizazi chenu.
Mtu akishakufa roho yake urudi kwa Muumba wake kusubiria hukumu na mwili unarudi udongoni.Hio nadharia ya mzimu ni babu aliyekufa inatoka wapi.Hata ukisoma vitabu vya elimu ya wachawi au mambo ya giza elimu yao inadhibitisha Hakuna roho inayobaki hai mtu akifa,sasa wewe hio Elimu ya mzimu ni babu umeipata wapi?
 
Back
Top Bottom