Upotoshwaji unaoendelea kufanywa na baadhi ya Wafamasia kumpotosha Waziri wa Afya

Upotoshwaji unaoendelea kufanywa na baadhi ya Wafamasia kumpotosha Waziri wa Afya

Mkishakuaga na na vielimu uchwara ,mnavimba sana.


Sasa hiyo IV Gentamicin 80mg, na Mtoa mada wapi na wapi???.


Ulivyo Mpuuzi,Et 'Tena specialist ?!!.


KIHALISIA, KATIKA AFYA, DAKTARI ni Mfamasia, ni mtu wa Labo .


DAKTARI HAMHITAJI MFAMASIA...MFAMASIA LAZIMA AMUHITAJI DAKTARI.
Kwa hii nchi tunategemeana, Niwe muwazi kuna madaktari hawawezi bila manesi, wafamasia na hata wataalamu wa maabara,
Baadhi ya madaktari ni zerro brain

Kila mmoja ana umuhimu hata USA kuna Baraza la Phlebotomist kwa kua wanaheshimu kaz ya hao jamaa,

Tuwe na ushirikiano katika sector ya Afya Ili tufike mbali na SI maneno.
 
Muwe mnajitahidi kuficha ujinga wenu.


Kwa Maisha ya Watanzania walio wengi, ambao huishia kujitibia wenyewe Kwa kwenda kununua sawa bila kujua wanachoumwa.


Kumtoa Daktari , na kumwacha Mfamasia ,ni UJINGA ULIOPITILIZA.


Mimi hapa Kila siku lazima nipate SIMU za wafamasia wakinipa maelezo ya wateja wao na wakihitaji kujua Nidawa gani wawepe.


Mfamasia anajua Dawa, lkn Daktari anajua ni Dawa gan amwambie Mfamasia ampe Mgonjwa .
Blatant lie

Umesoma zaidi clinical management lakini mfamasia kasoma zaidi therapeutics

Sisi wauguzi tumesoma zaidi patient care

Stop lying
 
MAJIBU KWA MTU ANAYEJIITA JOSHUA GUYAHAMBI ANAVYOPOTOSHA UMMA WA WATANZANIA KUHUSU ADDO NA USIMAMIZI WA MADUKA YA DAWA NCHINI

Na Prof Patrick Kobono (MD, MMED, MPH, MBA, PhD in Human Anatomy)

Wasalaam!

Kwa kawaida hua sipendi kabisa kujibishana na wajinga wachache wanaopotosha umma ima kwa makusudi ili kukidhi tamaa na haja zake binafsi au kikundi fulani au ni ujinga unaotokana na yeye kutoelewa kwa sababu huenda hajui chochote au kuna tatizo mahali.

Kwanza amejiita Darasa la saba B, hii inadhihirisha ni jinsi gani alivyo na uelewa finyu kuhuhusu kozi ya famasia na utabibu au Uuguzi pamoja na huduma ya utoaji dawa nchini. Huwezi kua Darasa la saba halafu ukapata Moral authority ya kufanya simple analysis kumjibu profesa na mwalimu wa chuo kikuu. Kama wewe ni darasa la saba B ndio useme darasa la saba wanasomea wapi Famasia. Huu ni ujinga mtupu kutaka kupotosha umma wa watanzania bila kujali kua tunahangaika na afya zao. Unaleta porojo badala ya kuja na Details na majibu sahihi?

UKWELI NI HUU KUHUSU KOZI YA UDAKTARI, FAMASI NA UUGUZI NA NI NANI ANASTAHILI KUTOA DAWA?
Naomba kusema kwamba silengi kutweza taaluma za watu, ninaziheshimu sana lakini propaganda na upotoshaji unapozidi unatakiwa kujibiwa kwa hoja na ukweli kwani mwisho wa siku anayeumia ni mwananchi wa kawaida.

Kwa kuweka kumbukumbu sawa ni kwamba Famasia chanzo chake ilikua ni sehemu au tawi la kozi Mama ya udaktari baada ya kuona kwamba daktari atakua na kazi nyingi za kutafiti, kutengeza dawa na kutibu, ulitolewa uamuzi baadaye kua masuala ya dawa yajitegemee ndio likaibuka somo la Pharmacology as a branch of Medicine ambaye mwanzilishi wake alikua Mjerumani Oswald Schmiedeberg. Huyu alikua ni daktari wa binadamu na ndiye mwanzilishi wa kwanza wa kozi ya Famasia karne ya 18. Unapokuja na kujitutumua kutaka kupotosha umma wa watanzania na bila kujali unamjibu nani ni utovu wa nidhamu.

Mwanzilishi na mgunduzi wa dawa Duniani Hippocrates, alikua daktari wa binadamu. He was the father of medicine. Ndiye aliyesababisha leo kuwepo na kozi ya Famasia, ndiye aliyekuja kuwazalisha kina Dr Oswald Shmiedeberg. Huwezi kupotosha umma wa watanzania bila kujali kua ushauri wangu ulijikita zaidi katika kuishauri Serikali ispotoshwe na kikundi cha watu wachache wachumia tumbo kwa maslahi yao binafsi bila kujali unyeti wa eneo hili.

ANAYETAKIWA KUTOA DAWA KWA MGONJWA NI NANI?
Ninarudia tena, kuna kitu kinaitwa drugs Administration na dispensing. Hapa ndiko hawa wanaojiita wafamasia wanajichanganya huenda ndio matatizo haya .

Hivi mtu anaposema Mfamasia anafanya drugs Administration ana akili sawa sawa? Katika routes zote za drugs Administration ukitoa oral, ni route gani ambayo wafamaia wanafundishwa darasani na kufanya practises?

Wanafundishwa kutoa sindano kwa I.V au I.M? Mimi ninataka nijue pamoja na kua hizi njia huwezi kutolea kwenye pharmacy. Ukweli ni routes zote zinafanywa na madaktari au manesi.

Miaka 6 mtu anahangaika na magonjwa na dawa leo unasema hana uhalali wa kutoa dawa kwa mgonjwa kweli?

Mfamasia anachoweza kufanya ni ni dispensing kwa maelekezo au maagizo ya daktari. Drugs Administration is not Dispensing! Wafamasia muelewe, hii ndiyo ilikua maana yangu. 👇👇

Dispensing includes all of the steps necessary to translate a medication order (prescription) into an individualized medication supply that is both safe and appropriate.

SWALI: Kama wewe ni Mfamasia upo kwenye duka la dawa, amekuja mgonjwa hana cheti cha daktari utatoaje dawa wakati wewe siyo daktari? Ni nani aliyetufundisha kufanya History taking na kutoa Diagnosisi?

Ni Pharmacy ngapi Tanzania zinauzwa dawa kwa maelekezo ya Prescriptions za madaktari?

Unafikiri ni kwanini dawa kali zote zinatakiwa kuuzwa kwa vyeti vya madaktari na wakati huo huo unasema ili daktari huyo huyo auze dawa lazima awe na ADDO? Hii ni akili ya wapi?

Yaaani Daktari huyu huyu ambaye ndiye mwanzilishi na mwasisi wa kozi ya Famasia unasema awe na ADDO ndio afanye Dispensing?

Kwahiyo narudia maelezo yangu pale pale kwamba serikali kuondoa kozi ya ADDO ilifanya vizuri kuondoa ulaji wa kikundi cha watu wachache lakini ni KOSA KUBWA sana kuwaacha wafanasi wauze na kutoa dawa wao wenyewe, ni kosa la kitaalam. Ni lazima awepo na daktari au nesi ambaye ana utaalam wa kubaini magonjwa kama alivyofundishwa.

NI KOSA KUBWA SANA kusema huyu daktari ambaye ndiye mwasisi na mwanzilishi wa kozi ya famasia eti ili auze dawa kwa mgonjwa ni lazima awe na ADDO au si ruhusa yeye kuuza dawa. Ni kosa gani la kiufundi analoweza kufanya daktari ikiwa atatoa dawa aliyoandika yeye bila uwepo wa Mfamasia kama si ukiritimba na ukuaji wa baadhi ya watu kutaka kujipa uhalali na mamlaka ya kumiliki maduka ya madawa na kutaka kufanya kila kitu nje ya uwezo wao?

Hata viwandani kwenye zile karatasi wanazoweka maelezo mwisho hua wanaandika...as directed by Physician, who is physician? Why not Pharmacist?

NI UVIVU MKUBWA WA KUFIKIRI KUA MFAMASIA ANASOMA ILI BAADAYE CHETI CHAKE KITUMIKE KUSIMSMIA PHARMACY.
Wakati
wenzetu wanasoma Pharmacy ili kwenda kufanya tafiti na kutengeneza dawa mbalibali viwandani, Tanzania kijana anayesoma Pharmacy anawaza amalize ili cheti chake kikazimamie Pharmacy. Huu ni mfumo mbovu wa elimu na ndio unaozalisha hii migongano inayotokea mara ADDO leo usikie imesitishwa.Yote haya ni kwa sababu ya uvivu wa watu kujishughulisha kutaka akae akunje nne aweke cheti chake dukani alipwe milion moja kwa mwezi maisha yaendelee. Tuendelee kuhamasishwa serikali ilete na ivujitie wawekezaji wa viwanda vya kutengeneza dawa ili kelele na njaa hizi ziishe.

HITIMISHO: Mfamasia atengeneze dawa kiwandani, ahifadhi dawa,atoe na kusambaza dawa. Si kazi yake kuchukua history na kubaini ugonjwa kisha atoe dawa. Atoe dawa kwa maelekezo ya daktari kama taratibu zinavyosema, Pharmacies ziuze dawa kwa vyeti vya madaktari. Awepo daktari au nesi katika Pharmacy yeyote ile ili wasaidie kutoa dawa moja kwa moja kwa wagonjwa, huu ndio wajibu wao. Hakuna tatizo lolote nesi au daktari kuuza dawa maana hakuna hoja ya msingi ya kuzuia hili. Hata mahospitali za Wilaya nyingi tu na vituo vya Afya nchini Tanzania Nurse assistants ndio dispensers na hawana mafunzo ya ADDO.

Prof Patrick Kobono (MD, MMED, MPH, MBA, PhD in Human Anatomy)
NAENDELEA KUKUPONGEZA.UNAHOJA ZA MSINGI.
 
Sijui kama unajua tofauti kati ya kutoa ( administer ) na Ku dispense.tuanzie hapo kwanza.the doctor can dispense and administer the drug.
 
Muwe mnajitahidi kuficha ujinga wenu.


Kwa Maisha ya Watanzania walio wengi, ambao huishia kujitibia wenyewe Kwa kwenda kununua sawa bila kujua wanachoumwa.


Kumtoa Daktari , na kumwacha Mfamasia ,ni UJINGA ULIOPITILIZA.


Mimi hapa Kila siku lazima nipate SIMU za wafamasia wakinipa maelezo ya wateja wao na wakihitaji kujua Nidawa gani wawepe.


Mfamasia anajua Dawa, lkn Daktari anajua ni Dawa gan amwambie Mfamasia ampe Mgonjwa .
Unapigiwa simu na ADDO.. Unasema mfamasia....
Daktari anajua dawa... Mfamasia anajua dawa inafanyaje kazi ndani ya mwili na kwa muda gani mgonjwa anatakiwa awe amerespond kwa matibabu...
Mfamasia pia anatoa ushauri pia kwa daktari kuhusu dawa flani kama haitoi matokeo chanya...
 
Kwa wenzetu ishu kama hizi wangeandaa mjadala wa wazi tena kwenye media then sisi waitaji wa huduma zao tungeamua tumfuate nani
 
Unachekesha sana.yani daktari aende kusoma addo? Hahahaa!! Siku moja nilimfelisha interview mtu mmoja kwa kishindwa kujibu swali langu.Tena hawa wauza madawa wanaumiza watanzania kwa kutoa wrong dose kwa wateja wao.eg : azithromycin kwa magonjwa ya kawaida ni only for three days!! Siku mmoja nilibishana na hawa wanaojiita dispensors bila kujua kuwa Mimi ni daktari
Nasema wakasome Ufamasia namaanisha degree
 
Ninajivunia sana kuwa sehemu ya mtandao wa kijamii ambapo msomi kama huyu ni sehemu yake pia.

Umetumia lugha inayoeleweka sana na kwa umakini sana kuchambua na kushauri.

Heshima kwako sana Prof.
 
1.Kwanini cheti cha daktari kihitajike na sio cheti cha Mfamasia ambaye ndiye manasema mtaalamu wa dawa?
Dawa zinazotolewa kwa cheti cha daktari kwa sababu zinachukuliwa kuwa hatari ikiwa hazitatumiwa chini ya usimamizi wa mtaalamu wa afya aliyeidhinishwa.
Dawa hizo kwa ujumla zinakusudiwa kutibu matatizo makubwa zaidi ya kiafya. Hii inaweza kujumuisha kisukari, saratani,magojwa ya moyo,bakteria,virusi nk.

Baadhi ya nchi kama vile Uingereza wapo wafamasia na manesi ambao wameidhinishwa kutoa baadhi ya dawa hizo.

👇👇👇👇👇👇
 
HITIMISHO: Mfamasia atengeneze dawa kiwandani, ahifadhi dawa,atoe na kusambaza dawa. Si kazi yake kuchukua history na kubaini ugonjwa kisha atoe dawa. Atoe dawa kwa maelekezo ya daktari kama taratibu zinavyosema, Pharmacies ziuze dawa kwa vyeti vya madaktari. Awepo daktari au nesi katika Pharmacy yeyote ile ili wasaidie kutoa dawa moja kwa moja kwa wagonjwa, huu ndio wajibu wao. Hakuna tatizo lolote nesi au daktari kuuza dawa maana hakuna hoja ya msingi ya kuzuia hili. Hata mahospitali za Wilaya nyingi tu na vituo vya Afya nchini Tanzania Nurse assistants ndio dispensers na hawana mafunzo ya ADDO.
EeeeenHeeee Heeeee Heeeee!

Imenibidi leo nitoe kile kicheko changu cha kawaida baada ya kusoma kimakini hili andiko la huyu kijana ambaye bado ndio kaanza shughuli za kiutibabu. Bado ana ule msisimko wa sisi zaidi kuliko wao, kama vile Simba na yYanga; kumbe anayoyazungumzia ni maswala nyeti sana yanayohususu maisha ya mteja wao wote, ambaye kwa kweli ndiye BOSS wao wote, ambaye ni mgonjwa. Bila ya ushirikiano wa mgonjwa, huu usimba na uyanga kati yao hauna maana yoyote.

Baada ya kusoma, nimejiridhisha, hakuna mtu anayejiita "Profesa Patrick Koboro" mwenye 'credentials' za MD, MMED, MPH, MBA, PH.D., n.k..

Mtu huyo hayupo. Huyu anayeandika hapa ni kijana tu asiyekuwa na ufahamu wa muundo wa hizi taaluma za Udaktari na Ufamasia, na wala hajishughulishi kutaka kujua kwa nini muundo huo ulivyo kama ulivyo sasa, si kwa Tanzania pekee, bali duniani kote.

Tena, inawezekana sana hata asiwe mtu aliyehitimu na MD, inawezekana sana hata akawa ni clinical ofisa tu au mtu tu aliye na maslahi na hiyo ADDO, ambayo imemchanganya sana kiasi kwamba anasahau kuwa ADDO ni sehemu ndogo sana katika mpangilio wa huduma za afya hapa nchini.

Baada ya kugundua haya, sioni lazima ya kufafanua hatua kwa hatua yote aliyoyaandika, labda tu kwa ufupi nikazie haya yafuatayo.

Famasia na Udaktari ni taaluma mbili tofauti, lakini zinazotegemeana. Huwezi kusema Famasia inatokana na au ilikuwa tawi la utibabu, kwa hiyo ni lazima utegemee mzazi kwa uwepo wake.
Hao aliowataja kama waanzilishi wa taaluma hizo mbili, yeye kaamua kuwachukuwa wawe upande wake, lakini hataki kukubali kwamba walikuwa pande zote toka mwanzo kabla ya mgawanyo wa taaluma hizi.
Inafaa pia atambue kwamba tokea wakati huo, hadi sasa, pamekuwepo na mabadiliko makubwa sana, kiasi cha kwamba huwezi kuhusisha taaluma moja kuwa kisehemu cha taaluma nyingine, na mabadiliko ndiyo yanazidi kupamba moto wakati huu na haya maswala yanayojitokeza ya "individualized therapy" na maswala mazima ya Biotechnology inavyochukua nafasi yake. Hata huko kwenye utibabu kwenyewe, si swala tena la sisi ni madaktari. Watu wanajipambanua katika fani hiyo hiyo na kufanya vitu vya kipekee kabisa ambavyo wengine hawafanyi.
Kulilia kuwa sehemu ya kuuza madawa wakati huu, na kuacha kushughulikia kazi inayokuhusu ya kumhudumia mgonjwa katika utambuzi wa kinachomsibu mgonjwa, maana yake ni kwamba anatafuta kukimbia kazi anayotakiwa kuifanya kwa ufanisi na kwenda kufanya kazi ambayo hahusiani nayo kabisa.
Kama hapo mwanzo ilionekana kuwepo umuhimu wa kutenganisha majukumu ya udaktari na mambo ya kushughulika na dawa, iweje sasa wakati huu tena huyu kijana alilie kuongezewa majukumu zaidi, wakati hata yale aliyosomea bado hayamudu?

Weka 'focus' kwenye kazi yako uliyosomea, uifanye kwa ufanisi zaidi, hayo ya akina Famasia, himiza tu, na wao wafanye ya kwao kwa ufanisi

Ninakubaliana naye juu ya uozo mwingi uliopo huko ndani ya taaluma ya Famasia unaotakiwa kushughulikiwa na kunyooshwa, lakini siyo swala la kuleta tena tabaka jingine kwenye uozo huo huo. Hilo siyo suluhisho la tatizo hata kidogo.

2. Mara nyingi huwa sipendi kuandika magazeti marefu katika ukumbi huu. Kwa hiyo inanilazimu niishie hapa kwa sasa.

Ikilazimu, nitaweka bandiko jingine la mwendelezo wa hapa nilipoishia.
 
Unapigiwa simu na ADDO.. Unasema mfamasia....
Daktari anajua dawa... Mfamasia anajua dawa inafanyaje kazi ndani ya mwili na kwa muda gani mgonjwa anatakiwa awe amerespond kwa matibabu...
Mfamasia pia anatoa ushauri pia kwa daktari kuhusu dawa flani kama haitoi matokeo chanya...
na hapo ndipo penye palipojaa ujinga wenu wa kujiona Nyie na Madaktari ni sawa.


Kwahiyo ukishakua Mfamasia, wee una unauwezo wa kufanya Diagnosis na kutoa treatment ?.


ADDO?. unategemea Daktari ,ambaye alipitia Huu wizi wa ADDO, ... Anaweza nipigia simu Daktari mwenzie Et, Kuna Mgonjwa kaja, analalama hivi nahivi, nimpe dawa gan???.



Ifike Mahali, kubalini tu , nyinyi ni wasaidizi wa Madaktari.
 
Nafikiri wewe ndiye huna akili kabisaaa.yani mfalmacia atoe dawa kwa mgonjwa? How? Amesomea wapi anatomy? My dear friend ,dawa siyo maharage aisee!! lini mfamacia amesomea ABCD ? Yani airway, breathing, circulation and drug! Unaweza kutoa dawa kwa mgonjwa akakuzimikia !sasa unajua utamsaidiaje? Nurse na dakatari wanajua namna ya kumsaidia mgonjwa after any side effect from the admistered drug!! Addo na mfamacia wanavijulia wapi? Kitu ambacho daktari hawezi ni kutengeneza dawa na siyo kutoa dawa!! Full stop.so daktari haitaji kusoma Ado au au full pharmacy. Madakatari na manesi wanasoma pharmacology
Nina uhakika weee ni Clinical Officer au Mwanafunzi wa Utabibu

Mosi, haitwi Mfamacia bali ni Mfamasia

Pili, Kusomea ABC yaani Airways, Breathing and Circulation sio big deal. Hilo ni somo la kawaida hata Red Cross wanaliweza na linafundishwa katika First Aid tuu. Ni wajibu wa kila mtu kujua ABC kama ilivyo kuzima moto.

Tatu, Eti Madaktari na Manesi wamesoma Pharmacology. Huu ni uelewa duni ulionao juu ya Kozi ya Famasi. Naomba nikuambie Mfamasia anasoma Dawa zaidi ya kitu kingine chochote. Anaijua dawa ndani na nje kuliko Mtu yeyote chini ya jua

Nakutajia Masomo makuu ( core subjects) za Kozi ya Famasi ambazo husomwa throughout miaka 4 ya Shahada yake

1. Pharmaceutics hii ni science of dosage forms and design. Hii ndio shule ya dawa zinatengenezwaje, kwa nini dawa iwe ya kidonge, ya maji au kupakaa n.k. Kwa nini dawa hii itolewe mara moja, mbili au tatu kwa siku. Nini kinaenda kutokea kwenye mwili wa mwanadamu akipewa dawa hii. Dawa hii ihifadhiwe wapi na vipi.

Pharmacology. Mfamasia anasoma Basic Pharmacology ( pamoja na Madaktari) lakini huendelea kusoma Clinical Pharmacology and Therapeutics ( pekke yao Madaktari hawasomi hii). Hii ndio shule hasa ya magonjwa kwa nini dawa fulani hutolewa kwa Wagonjwa fulani. Daktari anasoma tuu Ugonjwa fulani hutibiwa kwa dawa fulani.

Pharmaceutical ( Medicinal ) Chemistry. Hii ni sayansi/kemia ya dawa. Kwa nini dawa hii hutolewa kwenye ugonjwa huu. Nini kipo katika dawa hii ambacho aidha kinaua wadudu wanaosababisha magonjwa au kipo katika dawa kinachofanya correction ya physiological abnormalities. Katika somo hilo Wafamaisa hujifunza ni kwa nini dawa fulani haiwezi kutengenezwa katika hali fulani mfano huwezi kuta Benzyl Penicillin maarufu kama Cristapen haiwezi kuwa ya vidonge au hakuna Aspirin ya maji. Kwa nini baadhi ya wadudu huuwawa na dawa fulani na dawa fulani haziwaui kulingana na Structure Activity Relationship

Pharmacognosy hii ni sayansi ya kupata dawa kutoka vyanzo vya asili kama mimea, madini n.k

Pharmaceutical Microbiology hii haina tofauti na Microbiology ya Madaktari lakini huenda mbali zaidi ku include aseptic techniques katika uzalishaji wa dawa na vaccines

Pharmacy Practice hii sasa ni somo la utendaji kila siku unapofanya kazi. Ni kuhusu Sheria, Miiko na taratibu za Taaluma ya Famasi ikiwemo management ya magonjwa mbalimbali
 
Umesema vyema kwamba Wafamasia wanachoweza ni drug dispensing. Basi hilo ndilo Taaluma yao. Daktari hajui drug dispensing ndiyo maana ni lazima asome ADDO.

Hayo mengine ni mbwembwe tuu.
Mfamasia hajui chochote zaidi ya kukaa stoo ya daw
 

Wazee wa copy na kupaste nimeichukua sehemu kama ilivyo....​

What is a pharmacist vs. a doctor?​

Pharmacists commonly work in drugstores and retail environments where they fill prescription medications and address customer needs. Some pharmacists work in hospitals where they support physicians and medical teams in treating patient symptoms and conditions with pharmaceuticals. While pharmacists provide one type of healthcare service, doctors are the medical professionals responsible for diagnosing and treating patients, including writing prescriptions that pharmacists fill for purchase.

Another distinction between pharmacists and doctors is that doctors work directly with their patients, whereas pharmacists work in a laboratory setting and away from patients and customers. However, pharmacists sometimes advise patients and educate customers in retail settings about prescription and over-the-counter medications.
same as Prof Koboko's post!
 
MAJIBU KWA MTU ANAYEJIITA JOSHUA GUYAHAMBI ANAVYOPOTOSHA UMMA WA WATANZANIA KUHUSU ADDO NA USIMAMIZI WA MADUKA YA DAWA NCHINI

Na Prof Patrick Kobono (MD, MMED, MPH, MBA, PhD in Human Anatomy)

Wasalaam!

Kwa kawaida hua sipendi kabisa kujibishana na wajinga wachache wanaopotosha umma ima kwa makusudi ili kukidhi tamaa na haja zake binafsi au kikundi fulani au ni ujinga unaotokana na yeye kutoelewa kwa sababu huenda hajui chochote au kuna tatizo mahali.

Kwanza amejiita Darasa la saba B, hii inadhihirisha ni jinsi gani alivyo na uelewa finyu kuhuhusu kozi ya famasia na utabibu au Uuguzi pamoja na huduma ya utoaji dawa nchini. Huwezi kua Darasa la saba halafu ukapata Moral authority ya kufanya simple analysis kumjibu profesa na mwalimu wa chuo kikuu. Kama wewe ni darasa la saba B ndio useme darasa la saba wanasomea wapi Famasia. Huu ni ujinga mtupu kutaka kupotosha umma wa watanzania bila kujali kua tunahangaika na afya zao. Unaleta porojo badala ya kuja na Details na majibu sahihi?

UKWELI NI HUU KUHUSU KOZI YA UDAKTARI, FAMASI NA UUGUZI NA NI NANI ANASTAHILI KUTOA DAWA?
Naomba kusema kwamba silengi kutweza taaluma za watu, ninaziheshimu sana lakini propaganda na upotoshaji unapozidi unatakiwa kujibiwa kwa hoja na ukweli kwani mwisho wa siku anayeumia ni mwananchi wa kawaida.

Kwa kuweka kumbukumbu sawa ni kwamba Famasia chanzo chake ilikua ni sehemu au tawi la kozi Mama ya udaktari baada ya kuona kwamba daktari atakua na kazi nyingi za kutafiti, kutengeza dawa na kutibu, ulitolewa uamuzi baadaye kua masuala ya dawa yajitegemee ndio likaibuka somo la Pharmacology as a branch of Medicine ambaye mwanzilishi wake alikua Mjerumani Oswald Schmiedeberg. Huyu alikua ni daktari wa binadamu na ndiye mwanzilishi wa kwanza wa kozi ya Famasia karne ya 18. Unapokuja na kujitutumua kutaka kupotosha umma wa watanzania na bila kujali unamjibu nani ni utovu wa nidhamu.

Mwanzilishi na mgunduzi wa dawa Duniani Hippocrates, alikua daktari wa binadamu. He was the father of medicine. Ndiye aliyesababisha leo kuwepo na kozi ya Famasia, ndiye aliyekuja kuwazalisha kina Dr Oswald Shmiedeberg. Huwezi kupotosha umma wa watanzania bila kujali kua ushauri wangu ulijikita zaidi katika kuishauri Serikali ispotoshwe na kikundi cha watu wachache wachumia tumbo kwa maslahi yao binafsi bila kujali unyeti wa eneo hili.

ANAYETAKIWA KUTOA DAWA KWA MGONJWA NI NANI?
Ninarudia tena, kuna kitu kinaitwa drugs Administration na dispensing. Hapa ndiko hawa wanaojiita wafamasia wanajichanganya huenda ndio matatizo haya .

Hivi mtu anaposema Mfamasia anafanya drugs Administration ana akili sawa sawa? Katika routes zote za drugs Administration ukitoa oral, ni route gani ambayo wafamaia wanafundishwa darasani na kufanya practises?

Wanafundishwa kutoa sindano kwa I.V au I.M? Mimi ninataka nijue pamoja na kua hizi njia huwezi kutolea kwenye pharmacy. Ukweli ni routes zote zinafanywa na madaktari au manesi.

Miaka 6 mtu anahangaika na magonjwa na dawa leo unasema hana uhalali wa kutoa dawa kwa mgonjwa kweli?

Mfamasia anachoweza kufanya ni ni dispensing kwa maelekezo au maagizo ya daktari. Drugs Administration is not Dispensing! Wafamasia muelewe, hii ndiyo ilikua maana yangu. 👇👇

Dispensing includes all of the steps necessary to translate a medication order (prescription) into an individualized medication supply that is both safe and appropriate.

SWALI: Kama wewe ni Mfamasia upo kwenye duka la dawa, amekuja mgonjwa hana cheti cha daktari utatoaje dawa wakati wewe siyo daktari? Ni nani aliyetufundisha kufanya History taking na kutoa Diagnosisi?

Ni Pharmacy ngapi Tanzania zinauzwa dawa kwa maelekezo ya Prescriptions za madaktari?

Unafikiri ni kwanini dawa kali zote zinatakiwa kuuzwa kwa vyeti vya madaktari na wakati huo huo unasema ili daktari huyo huyo auze dawa lazima awe na ADDO? Hii ni akili ya wapi?

Yaaani Daktari huyu huyu ambaye ndiye mwanzilishi na mwasisi wa kozi ya Famasia unasema awe na ADDO ndio afanye Dispensing?

Kwahiyo narudia maelezo yangu pale pale kwamba serikali kuondoa kozi ya ADDO ilifanya vizuri kuondoa ulaji wa kikundi cha watu wachache lakini ni KOSA KUBWA sana kuwaacha wafanasi wauze na kutoa dawa wao wenyewe, ni kosa la kitaalam. Ni lazima awepo na daktari au nesi ambaye ana utaalam wa kubaini magonjwa kama alivyofundishwa.

NI KOSA KUBWA SANA kusema huyu daktari ambaye ndiye mwasisi na mwanzilishi wa kozi ya famasia eti ili auze dawa kwa mgonjwa ni lazima awe na ADDO au si ruhusa yeye kuuza dawa. Ni kosa gani la kiufundi analoweza kufanya daktari ikiwa atatoa dawa aliyoandika yeye bila uwepo wa Mfamasia kama si ukiritimba na ukuaji wa baadhi ya watu kutaka kujipa uhalali na mamlaka ya kumiliki maduka ya madawa na kutaka kufanya kila kitu nje ya uwezo wao?

Hata viwandani kwenye zile karatasi wanazoweka maelezo mwisho hua wanaandika...as directed by Physician, who is physician? Why not Pharmacist?

NI UVIVU MKUBWA WA KUFIKIRI KUA MFAMASIA ANASOMA ILI BAADAYE CHETI CHAKE KITUMIKE KUSIMSMIA PHARMACY.
Wakati
wenzetu wanasoma Pharmacy ili kwenda kufanya tafiti na kutengeneza dawa mbalibali viwandani, Tanzania kijana anayesoma Pharmacy anawaza amalize ili cheti chake kikazimamie Pharmacy. Huu ni mfumo mbovu wa elimu na ndio unaozalisha hii migongano inayotokea mara ADDO leo usikie imesitishwa.Yote haya ni kwa sababu ya uvivu wa watu kujishughulisha kutaka akae akunje nne aweke cheti chake dukani alipwe milion moja kwa mwezi maisha yaendelee. Tuendelee kuhamasishwa serikali ilete na ivujitie wawekezaji wa viwanda vya kutengeneza dawa ili kelele na njaa hizi ziishe.

HITIMISHO: Mfamasia atengeneze dawa kiwandani, ahifadhi dawa,atoe na kusambaza dawa. Si kazi yake kuchukua history na kubaini ugonjwa kisha atoe dawa. Atoe dawa kwa maelekezo ya daktari kama taratibu zinavyosema, Pharmacies ziuze dawa kwa vyeti vya madaktari. Awepo daktari au nesi katika Pharmacy yeyote ile ili wasaidie kutoa dawa moja kwa moja kwa wagonjwa, huu ndio wajibu wao. Hakuna tatizo lolote nesi au daktari kuuza dawa maana hakuna hoja ya msingi ya kuzuia hili. Hata mahospitali za Wilaya nyingi tu na vituo vya Afya nchini Tanzania Nurse assistants ndio dispensers na hawana mafunzo ya ADDO.

Prof Patrick Kobono (MD, MMED, MPH, MBA, PhD in Human Anatomy)
well said prof maana naona huku mtaani kika mvaa koti jeupe anajitutumua kuwa daktari
 
Mfamasia hajui chochote zaidi ya kukaa stoo ya daw
Angekuwa hajui chochote huyo Profesa Uchwara asingeanzisha thread kwa thread kulia lia hapa.

Jua na uelewe, hakuna mtu anajua dawa chini ya jua kama Mfamasia. Anaijua nje ( kiwandani) anaijua ndani ( ndani ya mwili)

Nyie wengine kaeni kwa kutulia. A Pharmacist is the master and the owner of medicines.
 
Wamempotosha hadi Hospitali ya MLOGANZILA, badala arudishe MUHAS yeye anafanya tofauti.
 
Back
Top Bottom