Upotoshwaji unaoendelea kufanywa na baadhi ya Wafamasia kumpotosha Waziri wa Afya

Upotoshwaji unaoendelea kufanywa na baadhi ya Wafamasia kumpotosha Waziri wa Afya

Umetaja medical errors

Naomba nikueleze amount ya medical errors katika nchi hii ni nyingi sana. Najua medical errors zina stem kutoka maeneo mbalimbali. Lakini hebu pitia hii study kidogo tuzidi kujielimisha hawa Madaktari wanao claim wao ndio Watu sahihi wanaojua dawa ili tuone wanafanyaje kazi hapa nchini

I knew several cases of medical errors hata kwenye hizi mada mbili kuna wachangiaji wameongelea poor decision za medics which almost cost their lives.

If anything haya majibizano ya wataalamu ndio yamehalalisha the extent of the problem if this how they work.

Sasa medical error zinasababu nyingi main one ni ‘human factor’ kama wewe daktari unajifanya unajua kushinda mtu yeyote na professional mwenzako ana second opinion utaki kusikiliza kwa sababu wewe ni superior si unauwa mgonjwa.

Ni hivi hiyo wizara mifumo iliyopo tu kuheshimiwa shida ili huduma iwe na quality Dr Gwajima alionyesha madhaifu hayo; jumlisha na changamoto za kureview mifumo inayolea uzembe na kuja na mikakati mingine ya supervision kuboresha huduma.

Huyo waziri aliyepo hapo anatosha kweli.
 
Sijabishia hilo lakini pia aruhusiwi kutoa baadhi ya dawa bila ya prescription ya MD, sasa kama kuna mazingira ambayo watu awawezi kwenda hospitali (I don’t know how is that possible or just permitted kwa uzembe wa wasimamizi) ambayo yanaruhusu pharmacists kufanya diagnosis na kutoa dawa this is against evidence based medicine approach kwa sababu a pharmacist is not trained to that.
Hicho ndicho tukipige vita!! Wafamasia wana maadili yao ya kitaaluma na hawawezi kutoa dawa ambazo zinahitaji prescription ya daktari. Tuwaelimishe watu wasiwakwepe madaktari na kukimbilia pharmacy. Lakini hatuwezi kutatua tatizo la watu kuwakwepa madaktari kwa kuwaruhusu madaktari kukaa pharmacy moja kwa moja. Tukifanya hivyo watazigeuza pharmacy kuwa dispensary na hospitali kosa ambalo ni baya zaidi!! Tatizo tulitatue kwa kutoa elimu kwa jamii!!
 
Hii ni kosa kabisa kusema eti Pharmacist hawajui diagnosis 😃😃😃

Shule ya Mfamasia inamtosha kufanya a rational judgement ya magonjwa mengi tuu. Ndiyo maana kuna Pharmacy Only Medicines ambazo Mfamasia anaweza kuzitoa bila ya kuhitaji cheti cha Daktari
Ata daktari afanyi kila diagnosis mwenyewe kuna vipimo vya machine kama x-rays, scanners, laboratory and so forth; ndio anaamua matibabu na dawa.

Sasa ni upuuzi kusema pharmacists aliye pharmacy ambayo aina assitive technology wala maabara ya vipimo anaweza fanya diagnosis na kuamua dawa.

Ni hivi hiyo wizara inahitaji technocrat kuna so much ego amongst different professionals.
 
Mimi sio

Mimi sio Daktari hata hivyo nimesoma post zenu moja ya Dactari na hii ya kwako ya Pharmacist
Nilichokiona hapa ni kuwa kila mmoja amebobea kivyake na maanisha Dactari anajua dawa gani inatibu nini hata kama hajui composition ya hiyo dawa kitu ambacho ndicho kinafanywa kwenye drug dispensing
Na maanisha Pharmacy inamuhitaji Mfamasia kwa ajili ya kuangalia storage na zile dawa zinazo hitaji kuchanganywa nk hata hivyo sijui kwa nini Dactari asiweze kutoa dawa aliyo iandika mf: Oxycline 10mg 2x3/14days? ( sorry mimi sio dactari)
Ila naamini wafamacia ni watu muhimu sana hasa kwenye kuandaa/kutengeneza dawa nk
Nakuambia kitu sasa Daktari anakalili Sawa full stop..... STANDARD TREATMENT GUIDELINE hichi ni kitabu kinaelezea kila ugonjwa utibiwe na dawa gani

Hichi kitabu hata wewe unaweza download na ukajua

NB:Ndicho hutumia kukalili baada ya kumaliza miaka Yao 5 shule..... it's so simple


Jiulize sasa hakuna mfamasia ambae Hana hii soft copy, ila vitu vingi it's normal things kwenye management so mfamasia anaweza akafanya substitute ya dawa ila Daktari asijue,mana anajua kile Tu kilicho andikwa na kama hakipo anakufosi ukainunue


ila pharmacist anaangalia inaenda kutibu nini na hii dawa chemically ipoje, na inauwezo gani katika hili na Hali ya mgonjwa ipoje.... lastly unashangaa Anakupa m'badala ukatumie




Nawasilisha
 
Hicho ndicho tukipige vita!! Wafamasia wana maadili yao ya kitaaluma na hawawezi kutoa dawa ambazo zinahitaji prescription ya daktari. Tuwaelimishe watu wasiwakwepe madaktari na kukimbilia pharmacy. Lakini hatuwezi kutatua tatizo la watu kuwakwepa madaktari kwa kuwaruhusu madaktari kukaa pharmacy moja kwa moja. Tukifanya hivyo watazigeuza pharmacy kuwa dispensary na hospitali kosa ambalo ni baya zaidi!! Tatizo tulitatue kwa kutoa elimu kwa jamii!!
Issue sio kuelimisha watu ni wizara kutoa maelezo kipi kinaweza uzwa pharmacy na kipi lazima kitolewe kwa prescription only na kupiga ban kwenda tofauti; vinginevyo ukibainika sheria ichukuwe mkondo wake.

Sema sasa humu naona kuna arguments za sijui kuna watu wapo mbali na hospitali mara vituo vya afya ndio maana pharmacists wanaweza toa dawa bila ya prescription; hilo swala alikubaliki bila ya Dr kama kuna mazingira hayo.
 
Hii ni kosa kabisa kusema eti Pharmacist hawajui diagnosis 😃😃😃

Shule ya Mfamasia inamtosha kufanya a rational judgement ya magonjwa mengi tuu. Ndiyo maana kuna Pharmacy Only Medicines ambazo Mfamasia anaweza kuzitoa bila ya kuhitaji cheti cha Daktari
Mimi nimeshangaa huyu jamaa anajiita Koboko...
Eti Pharmacist hajui diagnosis...
Na unaweza kukuta huyu ni Medical officer wa kawaida.. Anataka akae Pharmacy...
Wanaenda huko Wizarani na kuandaa research hewa na kumdanganya waziri mambo mengi tuu kuhusu hii taaluma ya famasi..
 
NAENDELEA KUKUPONGEZA.UNAHOJA ZA MSINGI.
Unampongeza bure!! Hujajua hoja yake ya msingi!! Hoja yake ni kwamba, kwa kuwa yeye ni daktari basi afanye pia kwenye pharmacy kwa kuwa anazijua dawa anazohitaji mgonjwa na hahitaji msaada wa mfamasia. Anataka wafamasia waende viwandani kutengeneza dawa na kufanya tafiti za dawa! Dr KIoboko kimsingi anataka kuunganisha kamba yake kama daktari na ile ya mfamasia!! Hajaridhika kula kutokana na urefu wa kamba yake ya udaktari!! anataka na ile kamba ya ufamasia!! Huu ni uroho! Dr Koboko ningemwelewa kama angekuwa anasisitiza wagonjwa lazima wapate cheti cha daktari kwa baadhi ya dawa kwa mujibu wa sheria. Sasa yeye Koboko anataka mgonjwa hana haja ya kuwa na cheti cha daktari anapoenda pharmacy maana huko pharmacy atamkuta daktari pia!! Sasa hii ni dhana hatari na itavunja sheria, maana daktari akikaa pharmacy ataigeuza pharmacy kuwa dispensary au clinic au hospitali! Dr Koboko ridhika na jukumu la kumtibu mgonjwa kwa maana ya kumchunguza na kumwandikia dawa!! Sehemu iliyobaki kwa mgonjwa waachie taaluma nyingine za afya kama wauguzi na wafamasia!!
 
Nina uhakika weee ni Clinical Officer au Mwanafunzi wa Utabibu

Mosi, haitwi Mfamacia bali ni Mfamasia

Pili, Kusomea ABC yaani Airways, Breathing and Circulation sio big deal. Hilo ni somo la kawaida hata Red Cross wanaliweza na linafundishwa katika First Aid tuu. Ni wajibu wa kila mtu kujua ABC kama ilivyo kuzima moto.

Tatu, Eti Madaktari na Manesi wamesoma Pharmacology. Huu ni uelewa duni ulionao juu ya Kozi ya Famasi. Naomba nikuambie Mfamasia anasoma Dawa zaidi ya kitu kingine chochote. Anaijua dawa ndani na nje kuliko Mtu yeyote chini ya jua

Nakutajia Masomo makuu ( core subjects) za Kozi ya Famasi ambazo husomwa throughout miaka 4 ya Shahada yake

1. Pharmaceutics hii ni science of dosage forms and design. Hii ndio shule ya dawa zinatengenezwaje, kwa nini dawa iwe ya kidonge, ya maji au kupakaa n.k. Kwa nini dawa hii itolewe mara moja, mbili au tatu kwa siku. Nini kinaenda kutokea kwenye mwili wa mwanadamu akipewa dawa hii. Dawa hii ihifadhiwe wapi na vipi.

Pharmacology. Mfamasia anasoma Basic Pharmacology ( pamoja na Madaktari) lakini huendelea kusoma Clinical Pharmacology and Therapeutics ( pekke yao Madaktari hawasomi hii). Hii ndio shule hasa ya magonjwa kwa nini dawa fulani hutolewa kwa Wagonjwa fulani. Daktari anasoma tuu Ugonjwa fulani hutibiwa kwa dawa fulani.

Pharmaceutical ( Medicinal ) Chemistry. Hii ni sayansi/kemia ya dawa. Kwa nini dawa hii hutolewa kwenye ugonjwa huu. Nini kipo katika dawa hii ambacho aidha kinaua wadudu wanaosababisha magonjwa au kipo katika dawa kinachofanya correction ya physiological abnormalities. Katika somo hilo Wafamaisa hujifunza ni kwa nini dawa fulani haiwezi kutengenezwa katika hali fulani mfano huwezi kuta Benzyl Penicillin maarufu kama Cristapen haiwezi kuwa ya vidonge au hakuna Aspirin ya maji. Kwa nini baadhi ya wadudu huuwawa na dawa fulani na dawa fulani haziwaui kulingana na Structure Activity Relationship

Pharmacognosy hii ni sayansi ya kupata dawa kutoka vyanzo vya asili kama mimea, madini n.k

Pharmaceutical Microbiology hii haina tofauti na Microbiology ya Madaktari lakini huenda mbali zaidi ku include aseptic techniques katika uzalishaji wa dawa na vaccines

Pharmacy Practice hii sasa ni somo la utendaji kila siku unapofanya kazi. Ni kuhusu Sheria, Miiko na taratibu za Taaluma ya Famasi ikiwemo management ya magonjwa mbalimbali
Kwahiyo pharmacognosy ndio ikazaa bupiji sio? Tanzania nchi yangu nakupenda, mnavyobishana hapa utadhani nchi inatengeneza hata Panadol au hatupeleki wagonjwa India kutibiwa yaani
 
Basi MD & Nurse fanyeni kazi zote hospitalini wenyewe na kozi ya famasi waifute Tanzania mazimaa

Sijawahi kuona watu wenye gubu na wivu kama watz dah walio soma kitu fulani wanajiona special kuliko wengine.
 
Hoja yake sio kuingiliana majukumu
Hoja yake ni pale Daktari anapo onekana hawezi kutoa dawa ambazo yeye mwenyewe ndiye ameziandika.
Hakuna anayesema kuwa daktari hawezi kutoa dawa pale pharmacy, maana hata manesi wanaruhusiwa kutoa dawa pale pharmacy!! Ila Daktari anaweza kutoa dawa pale pharmacy kwa usimamizi wa mfamasia pale pharmacy! Dr Koboko anataka ajitawale pale pharmacy bila uwepo wa mfamasia. Anataka wafamasia waende viwandani kutengeneza madawa na kufanya tafiti zaq madawa!! Hilo hapana! Kitu ninachokubaliana naye ni ile bodi ya pharmacy ilikuwa inataka daktari au muuguzi kupata mafunzo ya ADDO ili kuweza kuhudumia duka la dawa. Huo ulikuwa ni upigaji!! Na tayari wizara ilishaliona hilo na kulizuia!!
Dr Koboko anataka kumiliki pharmacy na kuihudumia bila msaada wa mfamasia! Ukiruhusu hilo ataigeuza pharmacy kuwa dispensary!!
 
Issue sio kuelimisha watu ni wizara kutoa maelezo kipi kinaweza uzwa pharmacy na kipi lazima kitolewe kwa prescription only na kupiga ban kwenda tofauti; vinginevyo ukibainika sheria ichukuwe mkondo wake.

Sema sasa humu naona kuna arguments za sijui kuna watu wapo mbali na hospitali mara vituo vya afya ndio maana pharmacists wanaweza toa dawa bila ya prescription; hilo swala alikubaliki bila ya Dr kama kuna mazingira hayo.
Unachosema ndivyo ilivyo!! Kuna baadhi ya dawa pharmacist haruhusiwi kutoa bila prescription!! Sheria hairuhusu!! Watu wanavunja sheria kwa sababu ya ujinga na njaa!! Ndiyo maana ni muhimu kuwekeza pia kwenye elimu ya jamii!! Wazo la Dr Koboko ni la hatari!! Anataka daktari akae pharmacy ili kuondoa ulazima wa mgonjwa kwenda pharmacy akiwa na prescription kwa baadhi ya dawa! Ukifanya hivyo huyu daktari ataigeuza pharmacy kuwa dispensary. Sasa hao wenye dispensary wafanyeje?? Pointi yake kuhusu ADDO ni sahihi, ila hili la ADDO tayari wizara ilishalifanyia kazi na bodi ya pharmacy walikubali.
 
Mtoa mada yupo kwa ajili ya kuongea mambo ambayo hayajui..
Nani kakwambia mfamasia haruhusiwi kufanya drug administration?
Nenda nchi za Uganda / SA hata nje la bara letu..
Nani kakwambia Mfamasia hajui diagnosis..?
Ndio maana unaweza ukakutana na kituko cha daktari wa watoto wanaandika dose za ajabu kwa watoto na kuleta uharibifu kwenye figo.. Wao ni kuandika tuu dawa mchanganyiko zisizo endana..
Hivi wewe unajiita prof sijui kokoto..
Unaweza kumuandikia mtoto mchanga IV Gentamycin 80mg ...? Tena masiku ya kutosha?
Hao ni madaktari tena specialist?
Hivi hamuoni mnaaribu figo za watoto?
Mnakazana kuzunguka nchi nzima / Wizara ya Afya mnasema hakuna Malaria...
Juzi hapa Mtoto kaletwa Muhimbili kutoka Temeke Hospital na ambulance.. Just mnakazana na kusema hii sio malaria.. Ni degedege...
Hivi nyie mnataka kuuwa watu?
Mtoto temp ipo 38 haishuki.. Akila anatapika.. Anatetemeka.. Mnakazana na Carbamazepine na Paracetamol kisha mnamwambia mama yake akatafute huko nje dawa ya kuzuia kutapika...
Mnakimbilia kupima mRDT badala ya field stain kuprove parasite wa malaria...
...mRDT haiwezi kuonyesha malaria.. Na ikionyesha hiyo ni severe tena inaweza ikawa cerebral malaria. ...
Wewe prof.... Waambie wenzako.. Mtakuja kuendelea kuuwa watu kwa poor management.... Na kujidai nyie mnajua mambo wakati.. Au basi
Sio vizuri kudanganya au kuandika uongo hapa
 
Unachosema ndivyo ilivyo!! Kuna baadhi ya dawa pharmacist haruhusiwi kutoa bila prescription!! Sheria hairuhusu!! Watu wanavunja sheria kwa sababu ya ujinga na njaa!! Ndiyo maana ni muhimu kuwekeza pia kwenye elimu ya jamii!! Wazo la Dr Koboko ni la hatari!! Anataka daktari akae pharmacy ili kuondoa ulazima wa mgonjwa kwenda pharmacy akiwa na prescription kwa baadhi ya dawa! Ukifanya hivyo huyu daktari ataigeuza pharmacy kuwa dispensary. Sasa hao wenye dispensary wafanyeje?? Pointi yake kuhusu ADDO ni sahihi, ila hili la ADDO tayari wizara ilishalifanyia kazi na bodi ya pharmacy walikubali.
Dah sasa nimeelewa, huyu Dr tamaa.
 
1. Duniani kote utafiti unaonyesha, kwa wengi, mtu akiumwa mtu wa kwanza kwenda kumuona ni pharmacist. Kuna dawa nyingi sana anazoweza pewa na mfamasia bila kuhitaji cheti cha daktari. Anapata ushauri mwingi pia.

2. Daktari hajui kilichopo ndani ya dawa. Ni hatari kumuachia pharmacy. Mfano rahisi, kuna dawa kibao za kikohozi ambazo ni mchanganyiko wa mitishamba, hata kumi sometimes. Daktari anafahamu vile ni vitu gani? Anajua vinafanya nini mwilini? Wafamasia tunaziogopa sana dawa, tunajua vilivyopo ndani.

3. Sheria ya utoaji wa dawa zinazohitaji cheti cha daktari zinajulikana. Kutoifuata ni kosa. Lakini si kutumia kosa hilo kutaka wasiofahamu masuala ya dawa nao waruhusiwe kuzihandle.

4. Na historia. Mtu wa kwanza kuanza kuchanganya na kuponda mitishamba kwa lengo la kujitibu ndiye mfamasia wa kwanza. Si ajabu ufamasia ulianza kabla ya udaktari.
 
1. Duniani kote utafiti unaonyesha, kwa wengi, mtu akiumwa mtu wa kwanza kwenda kumuona ni pharmacist. Kuna dawa nyingi sana anazoweza pewa na mfamasia bila kuhitaji cheti cha daktari. Anapata ushauri mwingi pia.

2. Daktari hajui kilichopo ndani ya dawa. Ni hatari kumuachia pharmacy. Mfano rahisi, kuna dawa kibao za kikohozi ambazo ni mchanganyiko wa mitishamba, hata kumi sometimes. Daktari anafahamu vile ni vitu gani? Anajua vinafanya nini mwilini? Wafamasia tunaziogopa sana dawa, tunajua vilivyopo ndani.

3. Sheria ya utoaji wa dawa zinazohitaji cheti cha daktari zinajulikana. Kutoifuata ni kosa. Lakini si kutumia kosa hilo kutaka wasiofahamu masuala ya dawa nao waruhusiwe kuzihandle.

4. Na historia. Mtu wa kwanza kuanza kuchanganya na kuponda mitishamba kwa lengo la kujitibu ndiye mfamasia wa kwanza. Si ajabu ufamasia ulianza kabla ya udaktari.
Hata kama ni kweli kuwa watu wengi wakiumwa hupenda kwenda pharmacy, hayo mazoea ni mabaya! Ukweli utabaki kuwa pharmacy si mahali pa kutolea tiba!! Hayo ni makosa makubwa ambayo jamii inapaswa kuelimishwa!! Mahali pa kupata tiba ni hospitalini na mtu sahihi wa kutoa ushauri wa kitabibu ni daktari!! Pharmacy ni mahali pa kotolea dawa!! Japo si kila dawa inahitaji prescription ya daktari! Kama dawa unayotaka haihitaji prescription ya daktari hapo ni sahihi kwenda pharmacy moja kwa moja!! Watu wanataka urahisi, japo kuendekeza urahisi kwenye suala la afya yako kunaweza kukuingiza kwenye gharama kubwa sana!!
Tunawaomba hawa wataalamu wetu wa afya wazingatie maadili ya kazi zao na kutanguliza utu badala ya fedha! Mtu wa pharmacy anakuja mtu dukani kwako nanataka madawa ya moyo tena ya bei mbaya!! lakini hana cheti! usitamani hiyo pesa bali mwelekeze mgonjwa akamwone daktari kwanza!! Na madaktari wana hulka ya kudharau kazi za kada nyingine as if wao peke yao ndio wanaweza kila kitu! hapana!! Vinginevyo tuondoe wauguzi na wafamasia hospitalini wafanye wao peke yao!! Msiendekeze njaa!!
 
Nchi zingine Daktari hahusiki kabisa na pharmacy! Daktari hufungua Medical Consultation Office na kazi yake ni kutoa ushauri kwa wagonjwa na kuwaandikia wagonjwa cheti (prescription). Kazi yake inaishia hapo!! Halafu mgonjwa huenda pharmacy akiwa na cheti chake na huko atahudumiwa na mfamasia kwa mujibu wa prescription!!

Tatizo la huyu Dr ni kwamba yeye anaqtaka afanye vyote! Anataka awaandikie wagonjwa cheti kisha na huko pharmacy akae yeye ili awape dawa!! Kisa eti kwa sababu kazi ya kutoa dawa anaiweza kwa kuwa prescription ameandika mwenyewe!. Nimwulize huyu daktari, kwani yeye kama daktari hajui kuchoma sindano? je hawezi kumchukua mgonjwa wodini na kumhudumia wodini?? Basi adai kufanya na majukumu ya nurse/muuguzi maana anayaweza! Achome wagonjwa sindano, awatundikiea drip nk. Wagonjwa wakifa, awapeleke mochwari! kwana daktari si anajua namna ya kumpeleka maiti mochwari!! Afanye yeye!!

Ninachotaka kusema hapa ni magawanyo ya majukumu baina ya kada mbali mbali za tiba! Daktari baki hospitalini uandikie wagonjwa dawa! Mfamasia baki pharmacy ukihudumia wagonjwa kwa mujibu wa prescription ya daktari kwa dawa zinazohitaji prescription ya daktari. Tatizo la Maboko anataka kumfukuza mfamasia pale pharmacy halafu yeye afanye peke yake!! Huo ni ulafi!! Basi mfukuze na muuguzi wewe daktari uoshe vidonda na uchome sindano, si unaweza kuosha vidonda na kuchoma sindano kama unavyojua kutoa dawa??
Shida ya madaktari wengi huwa wanahisi wamesoma sna kuliko watu wengine
 
1. Duniani kote utafiti unaonyesha, kwa wengi, mtu akiumwa mtu wa kwanza kwenda kumuona ni pharmacist. Kuna dawa nyingi sana anazoweza pewa na mfamasia bila kuhitaji cheti cha daktari. Anapata ushauri mwingi pia.

2. Daktari hajui kilichopo ndani ya dawa. Ni hatari kumuachia pharmacy. Mfano rahisi, kuna dawa kibao za kikohozi ambazo ni mchanganyiko wa mitishamba, hata kumi sometimes. Daktari anafahamu vile ni vitu gani? Anajua vinafanya nini mwilini? Wafamasia tunaziogopa sana dawa, tunajua vilivyopo ndani.

3. Sheria ya utoaji wa dawa zinazohitaji cheti cha daktari zinajulikana. Kutoifuata ni kosa. Lakini si kutumia kosa hilo kutaka wasiofahamu masuala ya dawa nao waruhusiwe kuzihandle.

4. Na historia. Mtu wa kwanza kuanza kuchanganya na kuponda mitishamba kwa lengo la kujitibu ndiye mfamasia wa kwanza. Si ajabu ufamasia ulianza kabla ya udaktari.
Madaktari wao huwa wanahisi wana akili kuliko watu wote
 
Wapo wengi mno wataalamu lakini MD wamekua wakiona kua wao ni muhim sana na wanaweza kila jambo.

KIKUBWA kaz zigawanywe kwa kila mwenye mamlaka husika na sio kujitoa ubeparii kwenye sector hii

Watu wa afya ttzo kubwa hatuelewani kabisaa,

Imani yangu wataalamu ni wengi ila ubepari ni mkubwa sana.
Lengo lao ni maslahi wala hawana lolote
 
Tatizo la Tanzania linakwenda deep na ni very complicated! Huu mgangano umetokea kwa sababu ya hali mbaya ya uchumi kwa madaktari na mafamasia. Ni kwamba daktari kazi yake tu haiwezi kukidhi mahitaji yake ya maisha. Na mfamasia hivyo hivyo. Matokeo yake wanagongana kwenye kutafuta namna ya kutosheleza kipato. Chanzo cha haya ni nini? Uongozi wa nchi mbovu! Listen, suala la mfumo mbovu wa uongozi wa nchi yetu lina athari nyingi sana katika maisha yetu. Hata wafanye nini kujaribu kurekebisha, ukweli ni kwamba bila ku-deal na kiini cha tatizo i.e. mfumo na uongozi mbovu, ni bure.
Shida ya nchi nyingi za Africa ni mfumo mbovu wa kiutawala
 
Back
Top Bottom