Urais wa Tanzania hautafutwi kwa nguvu ya pesa wala upendeleo

Urais wa Tanzania hautafutwi kwa nguvu ya pesa wala upendeleo

Salaam, Shalom!!

Tangu uhuru, wote walioutamani Urais, Urais uliwakimbia. Kwa kadri unavyozidi kuutamani Urais wa Nchi hii ambayo Nyerere alikuwa mwasisi wa mifumo ya uongozi na utawala, Kwa spidi hiyo hiyo ya kuutafuta, utateleza mikononi mwako usiamini kilichotokea.

1. Rais Mwinyi, hakuwahi kuutafuta Urais, Urais ulimtafuta.

2. Rais Mkapa hakujulikana, Wala hakuwahi kuutafuta Urais, Urais Ulimtafuta.

3. Rais KIKWETE hakutumia pesa kuusaka Urais, Urais ulimtafuta.

4. Kadhalika, Rais Magufuli pia hakuwahi kuota ndoto za Urais na kuzianika hadharani, Urais ulimtafuta Hadi Chato.

Hizi kelele za kuwa Marehemu Lowassa alisalitiwa na Rais KIKWETE ni unafiki tu, Urais hautafutwi Kwa pesa, na Urais haugaiwi kiurafiki Wala kindugu kwamba ukimaliza kula niachie nami zamu yangu!!


Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿.

Amen
Huo ndio uhalisia
 
Vipi JM Junior 2025 huenda akawa wa kwanza kuupata kwa kuwa natamaa tangu 2015 na hatimaye atapewa na BT, maana Godfather wa siasa ndani ya kampuni ni BT kwa sasa.
 
Vipi JM Junior huenda akawa wa kwanza kuutaka na akapewa na BT, maana Godfather wa siasa ndani ya kampuni ni BT
Historia ya nchi hii inaonyesha, wote walioumezea mate, Urais uligeuka kambale, ukateleza mikononi mwao😀😀

Ngoja tusubiri.

Muda ni mwalimu.
 
Acha ukorofi,

Urais haugaiwi kama nyama mnazikula hapo msibani!!

Kwamba, nikatie Ile yenye mafuta iliyonona😀

..Kikwete alikuwa genge moja na Lowassa.

..walitumia fedha nyingi kutafuta Uraisi na kuchafua wenzao na kukigawa chama.

..umesahau walivyokuwa wakimuandama Waziri Mkuu Sumaye?

..umesahau walivyomchafua Mzee John Malecela?

..umesahau fitina na ubaguzi dhidi ya Salim Ahmed Salim?

..Kikwete na Lowassa lao lilikuwa moja wamekuja kusalitiana wakati wa Richmond.
 
..Kikwete alikuwa genge moja na Lowassa.

..walitumia fedha nyingi kutafuta Uraisi na kuchafua wenzao na kukigawa chama.

..umesahau walivyokuwa wakimuandama Waziri Mkuu Sumaye?

..umesahau walivyomchafua Mzee John Malecela?

..umesahau fitina na ubaguzi dhidi ya Salim Ahmed Salim?

..Kikwete na Lowassa lao lilikuwa moja wamekuja kusalitiana wakati wa Richmond.
Usaliti wa Lowassa vs KIKWETE ni dhana tu na michezo ya wakubwa ya kufikirika.

Rais KIKWETE hakuutafuta Urais Kwa pesa.

Ingekuwa pesa inanunua Urais, Membe, Malecela, Lowassa wangeukwaa Urais.
 
Usaliti wa Lowassa vs KIKWETE ni dhana tu na michezo ya wakubwa ya kufikirika.

Rais KIKWETE hakuutafuta Urais Kwa pesa.

Ingekuwa pesa inanunua Urais, Membe, Malecela, Lowassa wangeukwaa Urais.

..nimekwambia Jk na El walikuwa genge moja.

..makubaliano yao ilikuwa atangulie Jk kupata Uraisi halafu afuatie El.

..walitumia pesa na mbinu nyingine chafu dhidi ya wenzao.

..tatizo lilikuwa Jk kutokutimiza abadi kwa mwenzake.
 
..nimekwambia Jk na El walikuwa genge moja.

..makubaliano yao ilikuwa atangulie Jk kupata Uraisi halafu afuatie El.

..walitumia pesa na mbinu nyingine chafu dhidi ya wenzao.

..tatizo lilikuwa Jk kutokutimiza abadi kwa mwenzake.
Ndo nakwambia,

Pesa za Lowassa hazikumpa KIKWETE Urais, ni zaidi ya hapo.

KIKWETE hawezi kulaumiwa kushindwa kumkabidhi KITI Lowassa sababu Yeye hakuwa final say juu ya nani arithi KITI chake.

Acheni hizo basi,

Yaani wewe JokaKuu unaamini Kweli kuwa KIKWETE angeweza kuamua Membe awe Rais, akawa?
 
Ndo nakwambia,

Pesa za Lowassa hazikumpa KIKWETE Urais, ni zaidi ya hapo.

KIKWETE hawezi kulaumiwa kushindwa kumkabidhi KITI Lowassa sababu Yeye hakuwa final say juu ya nani arithi KITI chake.

Acheni hizo basi,

Yaani wewe JokaKuu unaamini Kweli kuwa KIKWETE angeweza kuamua Membe awe Rais, akawa?

..Pesa za Kikwete na Lowassa ndizo zilizompa Kikwete Uraisi.

..Kinachofanyika ni ku-eliminate mgombea kikwazo ili mgombea aliyepangwa spite.

..Kikwete alimuengua Lowassa ili kumpendelea Membe lakini mambo yakaharibika kwenye kura.
 
Salaam, Shalom!!

Tangu uhuru, wote walioutamani Urais, Urais uliwakimbia. Kwa kadri unavyozidi kuutamani Urais wa Nchi hii ambayo Nyerere alikuwa mwasisi wa mifumo ya uongozi na utawala, Kwa spidi hiyo hiyo ya kuutafuta, utateleza mikononi mwako usiamini kilichotokea.

1. Rais Mwinyi, hakuwahi kuutafuta Urais, Urais ulimtafuta.

2. Rais Mkapa hakujulikana, Wala hakuwahi kuutafuta Urais, Urais Ulimtafuta.

3. Rais KIKWETE hakutumia pesa kuusaka Urais, Urais ulimtafuta.

4. Kadhalika, Rais Magufuli pia hakuwahi kuota ndoto za Urais na kuzianika hadharani, Urais ulimtafuta Hadi Chato.

Hizi kelele za kuwa Marehemu Lowassa alisalitiwa na Rais KIKWETE ni unafiki tu, Urais hautafutwi Kwa pesa, na Urais haugaiwi kiurafiki Wala kindugu kwamba ukimaliza kula niachie nami zamu yangu!!


Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA [emoji1241].

Amen
tawire tawire
 
..Pesa za Kikwete na Lowassa ndizo zilizompa Kikwete Uraisi.

..Kinachofanyika ni ku-eliminate mgombea kikwazo ili mgombea aliyepangwa spite.

..Kikwete alimuengua Lowassa ili kumpendelea Membe lakini mambo yakaharibika kwenye kura.
Si Kweli,

Ni zaidi ya hapo.

Magu hakuzuka kama uyoga,

Urais wa Magu hakuwa Bahati mbaya kama wengi tunavyodhani.

Funzo muhimu hapo, ni kuwa ,Urais Nchi hii haupatikani Kwa lobbying.

Wanasiasa wasihangaike kuifisadi Nchi kuusaka Urais,

Wataishia kuusikia tu😀
 
Si Kweli,

Ni zaidi ya hapo.

Magu hakuzuka kama uyoga,

Urais wa Magu hakuwa Bahati mbaya kama wengi tunavyodhani.

Funzo muhimu hapo, ni kuwa ,Urais Nchi hii haupatikani Kwa lobbying.

Wanasiasa wasihangaike kuifisadi Nchi kuusaka Urais,

Wataishia kuusikia tu😀😀

..genge la Lowassa liliamua kumpigia kura Magufuli dhidi ya wagombea walioonekana kuungwa mkono na Kikwete.

..Magufuli alishinda kwasababu Kikwete hakucheza karata zake vizuri.

..Kikwete alitakiwa awakate wagombea wote strong ambakishe Membe na wagombea dhaifu.
 
..genge la Lowassa liliamua kumpigia kura Magufuli dhidi ya wagombea walioonekana kuungwa mkono na Kikwete.

..Magufuli alishinda kwasababu Kikwete hakucheza karata zake vizuri.

..Kikwete alitakiwa awakate wagombea wote strong ambakishe Membe na wagombea dhaifu.
Kwamba CCM Huwa wanasheshimu Sanduku la kura!!

Ngoja ninyamaze!!!😀😀
 
Back
Top Bottom