Urusi huenda imebakia na nguvu ya mashambulizi kutoka angani tu, ardhini pumzi imekata?

Urusi huenda imebakia na nguvu ya mashambulizi kutoka angani tu, ardhini pumzi imekata?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Mimi binafsi sipendi vita, na katika vita vya Ukraine sitaki kushabikia upande wowote kuhusu mauaji, japokuwa siungi mkono kabisa uvamizi wa kijeshi wa Russia katika nchi ya Ukraine kwa kuwa ilitosha mgogoro huu kumalizwa kidiplomasia.

Nilihisi na hata kutamani kuona Urusi ikimaliza tukio la kuivamia Ukraine ndani ya siku tatu tu ili kuepusha mauaji endelevu ambayo yangetokana na muendelezo wa kupigana vita kwa muda mrefu. Lakini hali imekuwa tofauti sana, mpaka leo hii, takribani mwezi mmoja tangu kuanza vita vya Ukraine hali bado tete huku Russia ikishindwa kumaliza shughuli za uvamizi kwa wakati.

Ukiachilia mashambulizi kutoka angani ambayo kutwa na usiku yamekuwa yakifanywa na Russia, tena yakilenga makazi ya watu, shule, hospitali, taasisi za uzalishaji nishati na maeneo mengine ya umma, hakuna kipya, kikubwa na cha zaidi ambacho Russia inaelekea kukifanya kupitia ardhini. Nguvu ya kupigana vita vya ardhini ni kama ndogo au inakumbana na upinzani mkali kutoka kwa wanajeshi wa Ukraine. Sehemu ya askari wa Russia waliofanikiwa kuingia na kukaa katika miji ya Ukraine ni kama wametelekezwa na Russia kiasi cha kukosa chakula au kuzingirwa upya na kisha kuangamizwa na askari wa Ukraine

Nawaza tu, mara ghafla anga la Ukraine na mataifa jirani yanayozunguka Ukraine likifungwa na kuzuiwa kwa Russia kukaribia ili kuishambulia Ukraine, nini kitafuata?
 
Hongera sana mtunzi wa somo hili leo hii. Urus kabla ya kuivamia Ukraine alionesha dalili za uchokozi hivyo nchi karibia zote za NATO ziliisha jiandaa jinsi gani ya kuisaidia Ukraine ili Urusi iporoke kiuchumi na kukosa dira.

kitakacho bakia sasa ni kona urusi imeshindwa vita na NATO hawatatoa Vikwazo vya kiuchumi mpaka mahakama kuu ya the hague iwashitaki watawala wa Urusi kwa makosa ya mauaji . Hitler alijinyonga sasa puttin sijui atafanyaje.

Nchi tajiri kama venezuela yenye mafuta mengi na uchumi azizi iliwekewa vikwazo vya kiuchumi na marekani na support ya EU ilihusika. Venezuela walisota raia zake mpaka watu milion sita wakakimbia nchi kama wakimbizi. yaani hata toilet paper walikuwa wananunua kwa folleni! wewe ngoja tuu athari ya vikwazo ikianza kufanya kazi Urusi, itakuja kutokea folleni hata za kununua mchicha na pilipili mbuzi!
 
Nilihisi na hata kutamani kuona Urusi ikimaliza tukio la kuivamia Ukraine ndani ya siku tatu tu ili kuepusha mauaji endelevu ambayo yangetokana na muendelezo wa kupigana vita kwa muda mrefu.
Hivi unaujua ukubwa wa eneo la Ukraine mpaka ufikiri operesheni ingeisha ndani ya siku tatu?

Pia ujue kuwa hii siyo vita halisi kama USA na Iraq, hii ni operations maalumu ambayo ililenga kuondoa nguvu za kijeshi za Ukraine ambazo marekeni walikuwa wamewajengea kwa lengo la kuweka makombora ya kuilenga Urusi.

Wakati Russia wanailalamikia Marekani na kutaka security assurance lengo hasa lilikuwa kutaka marekani aondoe maabara za biological weapons na aache kusuply makombora kwa Ukraine. Karibu 80% ya nguvu za kijeshi ya Ukraine imeteketezwa!
 
Sehemu ya askari wa Russia waliofanikiwa kuingia na kukaa katika miji ya Ukraine ni kama wametelekezwa na Russia kiasi cha kukosa chakula au kuzingirwa upya na kisha kuangamizwa na askari wa Ukraine
Hii sijui chanzo chako umetoa media gani.
Ogopa propaganda za vita.
Ukraine wanashambuliwa vibaya sana kutokea mbali.
Vita imechukua muda mrefu sababu Ukraine anasaidiwa na nchi nyingi za EU na NATO.
Mwisho wa siku nchi yao itamegwa vipande viwili na itakuwa masikini kwa muda wa miaka mingi kisha upande mmoja utapata nafuu.

Kosa walifanya wamarekani ni kumchagua Biden sababu utawala wake ndiyo ume engineer hii vita. Familia yake ina maslahi na biashara za silaha nchini Ukraine. Kijana wake wa kiume alikuwa na mradi wa silaha za kibaolojia Ukraine wakati baba yake akiwa makamu wa raisi.

Mwanzo zilipo ibuliwa tuhuma hizi na Russia ilionekana ni uzushi na propaganda lakini sasa vyombo vikubwa vya habari vya magharibi vimethibitisha mradi huo wa silaha hatari za kibaolojia.

Mtoto wa Biden aliacha /telekeza laptop yake kwa fundi siku nyingi. Humo ndipo zilikopatikana email za mawasiliano yanayo husu huo mradi.

Mradi huu ndio umemgharimu Tramp hadi akahojiwa kama ametumia madaraka yake vibaya na ndio umemuondoa.
 
Urusi wapo vizuri tuu, shida ni Ukraini wanajeshi kujichanganya na Raia, inaleta shida kwa Urusi kufanya upembuzi yakinifu kwa vita ya aridhini. Ndio maana Urusi ameona isiwe tabu ngoja atokee angani sasa.
Ndio mbinu za kivita sasa hizo
 
Urusi wapo vizuri tuu, shida ni Ukraini wanajeshi kujichanganya na Raia, inaleta shida kwa Urusi kufanya upembuzi yakinifu kwa vita ya aridhini. Ndio maana Urusi ameona isiwe tabu ngoja atokee angani sasa.

Siyo kweli, warusi wanajua kurusha makombora na kubomoa majumba tu, siyo kupigana vita. Wanavyofanya sasa hivi Ukraine ndivyo walivyofanya Aleppo Syria na pia walifanya hivyo Grozny Chechnya. Siku chache zijazo Ukraine itapata Patriot Air Defense System uone kama Urusi itaweza vita tena.
 
Mimi binafsi sipendi vita, na katika vita vya Ukraine sitaki kushabikia upande wowote kuhusu mauaji, japokuwa siungi mkono kabisa uvamizi wa kijeshi wa Russia katika nchi ya Ukraine kwa kuwa ilitosha mgogoro huu kumalizwa kidiplomasia...
Anga linafungwa na nini? Kufuli za Solex ama?

Kuna nchi za kufungia anga kama Libya ila sio Russia.

Unaifahamu Tu-160? Ka google usome, hio ni bomber ambayo supersonic inapiga mach 2.05 at altitude.

Inabeba ton 20 ya free falling body ikiwemo silaha za nuclear cause ni nuclear capable bomber.

Ndio ndege yenye kasi zaidi, kubwa zaidi ya kijeshi na nzito zaidi kuwahi kuruka ambayo ina sweep wing.

Nimesema hio ndege ni supersonic kwenye speed kali licha ya ukubwa wake, mbawa zake huwa zinarudi nyuma inakua kama Mig.
Ikiwa slow inapanua mbawa zake kama Boeing 787 au ndege ya abiria ya kawaida.

Hio ndege ina uwezo wa kuipiga Kiev kukabaki shimo baadae kizazi kijacho wakaja kudhani kuna kimondo kilitua kama kule Arizona. Tena inapiga nje kabisa ya anga umbali wa km 5500.

Kumbuka hizo wanazo zaidi ya 60.

Kuna kitu kinaitwa s500 kuna mdau mmoja amesema humu ina uwezo wa kuzuia hata punje ya mchele😂😂😂, mi namuunga mkono, kwa maana s500 inashusha satellite.

Kama radar inaona tone la mvua basi hata punje ya mchele ukiirusha tokea Kiev itaonekana tu ikiingia Russia.

Nato haina uwezo wa kuifungia Russia anga.

Ndio maana nikasema labda wafunge na kufuli.

Unaposikia Russia wanasema wanafanya operation ujue wanafanya operation.

Putin hataki kuichukua Ukraine iliyo vipande vipande anaitaka nzima nzima, na Ukraine.

Kwa hio mkuu Russia si nchi ya mchezo mchezo kwenye vita.

Halafu huwezi kumpangia mtu kushambulia vipi.
 
Warusi wataomba poo mda si mrefu.
Mahesabu ilikua watwange Ukraine siku kadhaa tu waiweke chini yao.
Imeshindikana,kuna vikosi vipo pale ndani sio NATO wala EU combat force wanapigana kwa kwenda mbele,hakuna utambulisho ila wapo.
Kuna mabus yanaondoka na nguo zana na wanajeshi every week.
Wanaenda huko.
Ukraine kama yeye mpaka leo angeshasurrender.
Pale ni battle field tu.
Mrusi anapigana na Mmarekani na watu wake.
Kinachoogopwa Putin anaweza kuanzisha libeneke nchi zote za Scandinavia anawamudu.
Yuko jirani tu nao.
Hapo ndo utaskia WW3.
HAWAwataungana na ndio exit ya Putin.
Kwa ubishi atajiua tu km Hitler.
 
Anga linafungwa na nini? Kufuli za Solex ama?

Kuna nchi za kufungia anga kama Libya ila sio Russia.

Unaifahamu Tu-160? Ka google usome, hio ni bomber ambayo supersonic inapiga mach 2.05 at altitude...
Kwanini operesheni imechukua muda?

Ninavyokwambia ndo kwanza jamaa wanajipanga kwenda huko.

Hii wiki yapili sasa washafika.

Midege yoote mikubwa ya Mrusi ni kubeba mizigo.

Supersonic unazosema hizo kabisaa zinaangushwa mapema tu.

Haziruhusiwi kuruka hata mail moja.

Kaa utulie hapo.

Mrusi kamaliza ila hawa ndio wanaanza.
 
Siyo kweli, warusi wanajua kurusha makombora na kubomoa majumba tu, siyo kupigana vita. Wanavyofanya sasa hivi Ukraine ndivyo walivyofanya Aleppo Syria na pia walifanya hivyo Grozny Chechnya. Siku chache zijazo Ukraine itapata Patriot Air Defense System uone kama Urusi itaweza vita tena.
Wamarekani wa kwa mtogole muwe na akili hata kwa 25% kuwa bila ya misaada ya silaha za kivita na wanajeshi toka EU kama Canada, hao Ukraine wangekuwa katika hali gani hivi sasa [emoji848]

Russia hajaomba msaada kwa Taifa lolote zaidi ya kupambana kiume na USA na EU hadi sasa, na mzidishe maombi China, North Korea, Iraq na Iran wasitie maguu kumsapoti RUSSIA kama USA anavyosapotiwa na EU katika hii vita, la sivyo WWIII ina-download wakati wowote itaitika ndipo tutapozidi kuendelea kukaza mafuvu kujua uwezo wa RUSSIA kiuchumi, kiujasusi, kivita, kiteknolojia, kibiashara na hata kirasilimali duniani [emoji847]
 
Warusi wataomba poo mda si mrefu.
Mahesabu ilikua watwange Ukraine siku kadhaa tu waiweke chini yao.
Imeshindikana,kuna vikosi vipo pale ndani sio NATO wala EU combat force wanapigana kwa kwenda mbele,hakuna utambulisho ila wapo.
Kuna mabus yanaondoka na nguo zana na wanajeshi every week.
Wanaenda huko.
Ukraine kama yeye mpaka leo angeshasurrender.
Pale ni battle field tu.
Mrusi anapigana na Mmarekani na watu wake.
Kinachoogopwa Putin anaweza kuanzisha libeneke nchi zote za Scandinavia anawamudu.
Yuko jirani tu nao.
Hapo ndo utaskia WW3.
HAWAwataungana na ndio exit ya Putin.
Kwa ubishi atajiua tu km Hitler.
Watwange Ukraine siku kadhaa kwani mnaongea kwa kutumia akili zipi [emoji848]

Inamaana nguvu za kijeshi za Ukraine na hata kilometers za miraba kwa eneo ni sawa na Iraq [emoji848]

Na hiyo misaada ya silaha za kivita na wanajeshi toka Canada [emoji848]

Kufanya kwenu kazi NGOs kusiwaondolee akili za kudadavua ukweli halisi kwa mahaba yenu juu ya USA na EU [emoji4]
 
Kwanini operesheni imechukua muda.?
Ninavyokwambia ndo kwanza jamaa wanajipanga kwenda huko.
Hii wiki yapili sasa washafika.
Midege yoote mikubwa ya Mrusi ni kubeba mizigo.
Supersonic unazosema hizo kabisaa zinaangushwa mapema tu.
Haziruhusiwi kuruka hata mail moja.
Kaa utulie hapo.
Mrusi kamaliza ila hawa ndio wanaanza.
Kauli tu ya Biden kumzunguza Putin ni muuaji na hafai kwenye uongozi, Nato wenzie wamempinga Biden akiwemo raisi wa France na Waziri mkuu wa UK .

Sasa kama porojo tu za midomoni wanaogopa, hizo hatua za kijeshi?
 
Kauli tu ya Biden kumzunguza Putin ni muuaji na hafai kwenye uongozi, Nato wenzie wamempinga Biden akiwemo raisi wa France na Waziri mkuu wa UK .

Sasa kama porojo tu za midomoni wanaogopa, hizo hatua za kijeshi?
Hizo mbinu tu za kidiplomasia kumdumaza huyo Putin.

Wako mstari wa mbele ku push vita.
Kwasasa Ukraine hamna kilichobaki ni rubble tu.
Kama mpaka anapiga maeneo ya wamama,wazee na watoto ndio kete ya mwisho.
Na ndio itatumika kumuondoa.
Hao wamarekani wanatafuta tik to go on.
Tuko nyuma yako EU.
Anaondoshwa tu.
 
Watwange Ukraine siku kadhaa kwani mnaongea kwa kutumia akili zipi [emoji848]

Inamaana nguvu za kijeshi za Ukraine na hata kilometers za miraba kwa eneo ni sawa na Iraq...
Mkuu hujui kitu ,hao wako hapo ndani si kutoka Canada wala wapi.
Washashushwa mi najua 2 weeks ago.
Na wanaongezeka,Mwingereza hayupo NATO wala EU alijitoa.
Kapeleka battalion ,silaha na misaada ya wamama ,watoto na wazee.
Fikiria tu anampelekea nani silaha huku hamna wapiganaji?
 
Anga linafungwa na nini? Kufuli za Solex ama?

Kuna nchi za kufungia anga kama Libya ila sio Russia...
Sitaki kuandika kishabiki, lakini kiuhalisi anga linaweza kufungwa kuzuia ndege za Russia kukatiza, na zikikatiza zitashushwa mara moja.

Narudi pale pale kwenye mada yangu, ukiondoa nguvu ya mashambulizi ya anga ya Russia, kwa mwenendo wa vita wa sasa ni kama Russia pumzi imekata ardhini?
 
Urusi wapo vizuri tuu, shida ni Ukraini wanajeshi kujichanganya na Raia, inaleta shida kwa Urusi kufanya upembuzi yakinifu kwa vita ya aridhini. Ndio maana Urusi ameona isiwe tabu ngoja atokee angani sasa.
Katika hili unakubaliana na mimi kuwa, mbinu na nguvu ya kijeshi ya Russia ya ardhini ni duni kiasi cha kushindwa kuwadhibiti wa Ukraine?
 
Back
Top Bottom