Urusi kupeleka majeshi yake na silaha nzito nchini Cuba na Venezuela kama Marekani itaendelea na kujiingiza Ukraine

Urusi kupeleka majeshi yake na silaha nzito nchini Cuba na Venezuela kama Marekani itaendelea na kujiingiza Ukraine

Mwanzoni mwa vita zote ujerumani alikuwa anaelekea kushinda vita , Marekani kudandia vita ndo kuliwaokoa hao warusi , waingereza , wafaransa nk so vita zote aliyebadili upepo ni Marekani na ndo aliwapa morali hao waungwaba kuamka na kuanza kupambana upya na ujerumani
Urusi hupewa mpaka sifa za uongo, ila ushindi katika vita vyote vya dunia, yani WWI na WW2 vilitegemea kwa kiasi kikubwa mchango wa US.
 
Bongo
Sio kwamba US walimuogopa Mrusi kule Syria. Strategically, hata kwa Raisi kichaa kama Trump, isingekuwa busara kuipeleka nchi kwenye vita nyingine katika kipindi kile. Kasheshe kule Iraq na Afghanistan zilikuwa bado zimepamba moto. Ndugu yetu Omera (Obama) aliahidi kwamba atamaliza vita hizo mbili. Na bado hakuweza kuimaliza mpaka alivyomaliza muda wake.

Wakati huo huo, yule dogo kule Korea (Kim) na yeye alikuwa anahitaji attention. Korean peninsula watu walitegemea vita wakati wowote. Kule Iran [emoji1130] ndio usiseme. Ma Ayatollah walikuwa wanampiga mkwara Israel kila siku. Kwa hiyo, Strategically, haikuwa busara kwa US kwenda kuvimbanusha misule na vishoka. Na hiyo ndii ikawa baraka kwa Russia na Putin mpaka leo.

Hii dunia inawenyewe. Na US [emoji631] ndio kinara wa wenyenayo.
Malekani anachokoza ugonvi kwasababu anategemea NATO. Hakuna vita aliyokwenda peke yake
 
Iran ni sawa na mafahali wanapigana afu kuna mtetea anataka kuingilia ugomvi. Hakuna uwezekano wa vita na Korea Kaskazini. Urusi anarusha rusha mateke kutokana na ukweli kuwa ameona US kupitia NATO wanataka kumzunguka hapo nyumbani kwake, na wasiwasi wa Kremlin ni kuwa, Ukraine akijiunga basi itachochea mataifa mengine yaliyomeguka kutoka USSR kujiunga na NATO hivyo kuweka rehani usalama wa Urusi. Mchina kawekewa India na Japan ili waendelee kupekuwa utovu wake wa nidhamu.
Iki ndicho ninachokijua hata mimi
 
Mkuu kasome some historia vizuri Kati ya hao washirika wa NATO na USA wao enzi za Hitler nani aliweza kumtwanga Hitler kwa Ulaya,kama sio mrusi!!

All in all USA anamuogopa mrusi na amejaribu miaka mingi kujaribu kuua uimara wake ikiwemo kuua dude la USSR Ila bado Moscow ni mbabe pekee dhidi ya USA!!

USA peke yake hawezi kuingia vitani na Urusi.
Hata USA na washirika wake wakiungana dhidi ya Urusi-bottom line is:
 
Mkuu kasome some historia vizuri Kati ya hao washirika wa NATO na USA wao enzi za Hitler nani aliweza kumtwanga Hitler kwa Ulaya,kama sio mrusi!!

All in all USA anamuogopa mrusi na amejaribu miaka mingi kujaribu kuua uimara wake ikiwemo kuua dude la USSR Ila bado Moscow ni mbabe pekee dhidi ya USA!!

USA peke yake hawezi kuingia vitani na Urusi.
Kwa hiyo Russia wao wahaiogopi marekani sio?,wanaichukulia kama Tanzania tu eti?..Ila wanazi wa JF bana 😀 😀
 
Urusi alipelekaga silaha zake kwenye nchi jirani na marekani mpaka marekani wakaomba mazungumzo.hawa wakipigana ujue ni vita ya 3 ya dunia ndo maana marekani hawewezi kumzuia urusi ukraine.
Nchi jirani ipi??
 
Aaaargh tumechoka kutishana tishana.

Wapigane, wauane sisi tusonge mbele
 
Urusi hupewa mpaka sifa za uongo, ila ushindi katika vita vyote vya dunia, yani WWI na WW2 vilitegemea kwa kiasi kikubwa mchango wa US.
Marekani walishawahi kumpa silaha na pesa Joseph Stalin kupambana na Hitler kabla USA hawajaingia moja kwa moja vitani ila watu humu hawasomi vitu wanafata mihemko tu....
 
Itakuwa ulikuwa unatafiti ujinga.
Hamna vita Marekani hawezi Vita na urusi na hawana la kuwafanya urusi ukraine
Screenshot_20220203-135329.jpg
 
Huenda dunia ikarudi tulikotoka 1962,baada ya uoga wa Marekani dhidi ya USSR na kuamua kupeleka silaha za nyukilia nchini uturuki ili kuivizia USSR,nayo USSR haikua mvivu,ikapeleka silaha zake nzito nchini Cuba ili kuidhibiti Marekani.
Leo Tena Marekani na mpango wake wa kutaka kuikaribia Urusi Kijeshi Tena nje ya mlango wa Urusi yaani Ukraine,kwa kulazimisha Ukraine ijiunge na NATO ili iwe rahisi kuikabili Urusi pale itakapohitajika kufanya hivyo,nayo Urusi Tena sio mvivu,Bali inafikiria kupeleka majeshi nchi jirani na Marekani Cuba na Venezuela ili iwe rahisi kuikabili Marekani pindi kitakaponuka huko Ukraine.


Ifahamike kwamba Urusi hawashindwi kufanya hivyo,"ukimwaga ugali namwaga mboga".

Russia Suggests Military Deployment to Venezuela, Cuba if Tensions With U.S.​

Russia’s deputy foreign minister said talks with the U.S. over the security situation in Ukraine had stalled and suggested that Moscow could dispatch a military deployment to Venezuela and Cuba, as the Kremlin seeks to pressure Washington to meet its demands to halt Western military activity that Russia claims
Hawana hiyo budget Marekani mziki mwingine..
China na Urus watapata tabu sana.
 
Hawana hiyo budget Marekani mziki mwingine..
China na Urus watapata tabu sana.
Uwezo wanao hao wanauza gesi ulaya.jamaa ni matajiri Sana alafu washawahi kupelekea huko silaha zao.burget kubwa ya marekani sio lolote.
 
Back
Top Bottom