Urusi ni super power ya mdomoni, jana nilitaka kusafiri nikakumbana na haya ndani ya ndege za Urusi

Urusi ni super power ya mdomoni, jana nilitaka kusafiri nikakumbana na haya ndani ya ndege za Urusi

Umeiweka kitaalamu sana.
Ni lini iliwahi kuwa superpower?

Superpower ni uwe umeenea - kiuchumi, kisiasa, kijeshi, kidiplomasia, kisayansi na kiuongozi - vyote kwa pamoja.

Ndio maana sio nchi zote tajiri (first world) ni superpower au zenye watu wengi (mfano India) ni superpower.
Russia hajawahi kujitosheleza katika hayo; ila kidogo labda kijeshi na kisayansi. Kiuchumi yuko hoi tangu kale.
Russia imekuwa ikipokea misaada na mikopo na toka USA, World Bank na IMF toka 1950's! Tafuteni data ziko lukuki.

'Kutajwa tajwa hapa na pale' ni ktk ku certify ego yake. Ni kama wana msanifu tu.

Na hakuna superpower wengi, huwa ni mmoja....halafu wengine wanajiita au kujitutumua tu
 
Naongea nachokiishi siyo nachosimuliwa, kabla mrusi wa buza hujaanza kunibishia shiba sana kwanza vitumbua kwa mama willy hapo Tandale, nakusisitiza kabisa ichaji techno ya shangazi yako unayotumia kwa kujiiba ku comment JF, nasisitiza hakikisha una pitia notice ulizokalili kuhusu uchumi kwa mkandawile na vibatu vyenye harufu ya bamia.

Bwana last week nikawa na kazi sehemu kama kawida yangu, nikatafta booking ya ndege nilikuwa naenda Nchi fulan kwa ajili ya kazi (inside job) nikapitia kurasa kadhaa za kutangaza safari za ndege za shirika la urusi maarufu kama Russia airline, na wajanja sana wao wanachofanya wanakwambia kwamba ndege hii inasafiri hadi uingereza au kokote dunian ila wanachofanya wanakukatia kufaulisha maana hawawezi toboa dunian kulingana na mzozo wake na Dunia, nchi pekee ambazo ndege za urusi zina access ya kuingia ni Iran, Turkmenistan, North Korea, Nicaragua, na hapo kwa north korea bado kuna matatizo kulingana na wateja kukosa huko hivo wanalazimika kuacha route hiyo iwe dominated na air koryo tu ya nk,

Ndege zina hitlafu sana hazifunction inavyotakiwa na wahudumu au raia mnakuwa strictly prohibited kupiga picha na kusambaza, nje ya hapo utakipata cha mtema kuni.

Ratiba zao za ndege Magumashi kama Air Tanzania kwa sasa, muda wa kuondoka mnaandikiwa saa 4 lakin mnachelewa mpaka masaa 2 mbele bila sababu za msingi, kichekesho zaidi yan Urusi yangu hii ina matatizo ndege inasukumwa na mikono kuingia kwenye run way nikajiuliza hivi vile vi gari vya kusukuma havipo au wana sababu zao nyingine za kiusalama?

Kwakweli huduma zao ni za hovyo sana kabisa kwa karne hii ya 21 na technology waliyo nayo urusi tunayoaminishwa wanayo, nimejiuliza mengi ni ama urusi ni majigambo kama mtu fulan hapo Tanzania au ni shida ya vita ndo imemlegeza hivi?

Maana hata wapiganaji wa kuendeleza vita baada ya bajeti na nguvu kazi kukata nimeona juzi wanalazimisha watu wa kada kadhaa kwenda mapiganoni ilihali hawana ujuzi na si hiari yao, naona wameleta makundi yaliyokuwa ya Islamic states ndo yasaidie pia katika kupigana na dubwana liitwalo Ukraine.

Nataman hii vita waimalize watu waishi kwa raha kama zamani, tunaambia thamani ya sarafu ya urusi imeimarika lakin kwenye makaratasi, ila tulioko ground kazi ni ngumu na mambo ni Magumu sana, ingekuwa ni hiari yangu bila kushinikizwa na kazi ni bora nikahamia nchi nyingine kuliko Urusi.

Wameanzisha mfuko maalumu wa kuwalazimisha wafany biashara kutozwa tozo ya 12% extra ya mapato yao ku supplement matumizi ya serikali ya Putin, GTI9-0, Wafanya biashara wakilalamika ndo inakula kwao ni ama wapotezwe au biashara yote inachukuliwa kimafia.

Kwa sasa wapinzani wameanza kumpa joto Putin kwakuwa uchaguzi unakaribia, ila kapiga marufuku hakuna mikutano kisiasa hali haija kaa sawa kiusalama wa nchi.

Je, hii ndo Superpower?

Britanicca
Kama unapanda Aeroflot it’s going to take off but don’t expect it to land you do that at your own risk good luck
 
Najua wewe lazima utakuwa ni mfuatliaji wa matukio mbalimbali, japo sina uhakika kama lile tamko la mkuu wa Nato ulilisikia.

Mwakajana NATO walisema kuwa uwezo wa kivita wa Urusi, ulikuwa exagerated. Kumbuka Urusi walipoivamia Ukraine, na kudai ile operation itachukua siku 3, hakuna nchi yoyote iliyoipa Ukraine msaada wowote, kwa sababu nchi zote, kwa kile walichokiamini nguvu ya kijeshi ya Urusi, kisingekuwa na maana yoyote. Baada ya Ukraine kumfurusha mrusi Kyiv, na mrusi kukimbilia ile mikoa ya Mashariki, ndipo Dunia ilipoona kuwa kumve uwezo wa Urusi wa kivita ni wa kawaida sana. Nguvu pekee kubwa ya mrusi anayoitegemea nibmakombora ya nuklia, sawa na ilivyo North Korea.

Kumbuka, hata katika kipindi cha kawaida, uchumi wa Urusi ni mdogo sana. GDP yake ni ya chini kupindukia ukilinganishia na mataifa kama US, Germany, France, n.k. Uchumi wa Urusi ni mdogo kuliko wa South Korea.

Sarafu ya Urusi iliporomoka ghafla baada ya ule uvamizi kutokana na hofu. Baadaye ikaimarika kutokana na mauzo ya mafuta. Lakini mwaka huu imekuwa ikiporomoka, na haitegemewi kunyanyuka tena, labda vita ikome. Ikumbukwe kuwa sarafu ya Urusi ilipanda kutokana na kupanda sana kwa bei ya mafuta, na wakati huo huo mataifa hayo ya Magjaribi yalikuwa hayajapata mbadala wa mafuta na gas ya Urusi. Kwa sasa mataifa hayo yamepata alternative sources, na yanazaidi kufuta mahusianobya kibiashara wajati tayari kulikuwa na miundombinu iliyokuwa imejengwa toka Urusi kwenda Ulaya kwaajili ya gas na mafuta. Miundombinu hiyo haina kazi tena, na kujenga mingine kwenda mataifa kama ya China au India, siyo kazi ya muda mfupi.

Mnunuzi mkubwa wa mafuta ya Urusi ni India, lakini India imekuwa inafanya processing ya hayo mafuta kwaajili ya kutoa products mbalimbali kama vile mafuta ya jet engines, soko kuu likiwa Ulaya. Lakini sasa tayari India imekwishatangaziwa tishio kuwa kwa vile zile products zinatokana na mafuta ya Urusi, hazitaruhusiwa kuingia Ulaya. Hiyo ina maana kuna uwezekano wa India kuacha kununua mafuta toka Urusi ili kuokoa soko lake la bidhaa zitokanazo na mafuta.

Ikumbukwe pia, ndege na zana mbalimbali, vipuli vyake vilikuwa vinatoka Ulaya, na Urusi haina uwezo wa ndani. Kwa sasa Urusi inaitegemea China kuziba hilo pengo, lakini China nayo ina mapungufu mengi kwenye ubora. Makampuni yanayotengeneza bidhaa zenye ubora yaliyopo China, ni makampuni ya Ulaya yaliyowekeza China ambayo yanalazimiki ku-comply na masharti ya mataifa yao ambako ndikobyaliko makao makuubya makampuni yao.

Vijana wengi wasomi na wenye uwezo wa kifedha, wanafanya kila namna kuondoka Urusi. Na hao ndio wazalishaji na wataalam ambao wangekuwa na mchango kwa Urusi, sasa wanaondoka.

Pole sana. Lakini utegemee mabaya zaidi kadiri siku ziendavyo. Labda vita isimame. Mataifa ya Magharibi, kama alivyosema Biden, yataendelea kuisaidia Ukraine mpaka watakapohakikisha Urusi siyo tishio kwa nchi yoyote Duniani. Wanataka wammalize mrusi kiuchumi na kitekinolojia na katika nguvu za kivita. Baada ya hapo wataijenga Ukraine kama walivyofanya kwa Korea Kusini, na warusi wengi watahangaika sana kutaka kuhamia Ukraine kwa sababu huko kutakuwa na maisha bora zaidi ukilinganisha na Urusi, nchi ambayo kwa muda mrefu imeishi kwenye uchumi duni na udikteta.
Mkuu amka utajikojolea!
 
Ni Leo ndo umefahamu kwamba mashirika ya ndege Huwa yanafaulisha abiria..ujui kwamba unaweza Kata KQ ukapandishwa precision au ni mara ya kwanza kupanda ndege.
 
We jamaa huendi mbinguni yani unasikiliza story za empty minded kipanya afu unatuletea humu
 
Najua wewe lazima utakuwa ni mfuatliaji wa matukio mbalimbali, japo sina uhakika kama lile tamko la mkuu wa Nato ulilisikia.

Mwakajana NATO walisema kuwa uwezo wa kivita wa Urusi, ulikuwa exagerated. Kumbuka Urusi walipoivamia Ukraine, na kudai ile operation itachukua siku 3, hakuna nchi yoyote iliyoipa Ukraine msaada wowote, kwa sababu nchi zote, kwa kile walichokiamini nguvu ya kijeshi ya Urusi, kisingekuwa na maana yoyote. Baada ya Ukraine kumfurusha mrusi Kyiv, na mrusi kukimbilia ile mikoa ya Mashariki, ndipo Dunia ilipoona kuwa kumve uwezo wa Urusi wa kivita ni wa kawaida sana. Nguvu pekee kubwa ya mrusi anayoitegemea nibmakombora ya nuklia, sawa na ilivyo North Korea.

Kumbuka, hata katika kipindi cha kawaida, uchumi wa Urusi ni mdogo sana. GDP yake ni ya chini kupindukia ukilinganishia na mataifa kama US, Germany, France, n.k. Uchumi wa Urusi ni mdogo kuliko wa South Korea.

Sarafu ya Urusi iliporomoka ghafla baada ya ule uvamizi kutokana na hofu. Baadaye ikaimarika kutokana na mauzo ya mafuta. Lakini mwaka huu imekuwa ikiporomoka, na haitegemewi kunyanyuka tena, labda vita ikome. Ikumbukwe kuwa sarafu ya Urusi ilipanda kutokana na kupanda sana kwa bei ya mafuta, na wakati huo huo mataifa hayo ya Magjaribi yalikuwa hayajapata mbadala wa mafuta na gas ya Urusi. Kwa sasa mataifa hayo yamepata alternative sources, na yanazaidi kufuta mahusianobya kibiashara wajati tayari kulikuwa na miundombinu iliyokuwa imejengwa toka Urusi kwenda Ulaya kwaajili ya gas na mafuta. Miundombinu hiyo haina kazi tena, na kujenga mingine kwenda mataifa kama ya China au India, siyo kazi ya muda mfupi.

Mnunuzi mkubwa wa mafuta ya Urusi ni India, lakini India imekuwa inafanya processing ya hayo mafuta kwaajili ya kutoa products mbalimbali kama vile mafuta ya jet engines, soko kuu likiwa Ulaya. Lakini sasa tayari India imekwishatangaziwa tishio kuwa kwa vile zile products zinatokana na mafuta ya Urusi, hazitaruhusiwa kuingia Ulaya. Hiyo ina maana kuna uwezekano wa India kuacha kununua mafuta toka Urusi ili kuokoa soko lake la bidhaa zitokanazo na mafuta.

Ikumbukwe pia, ndege na zana mbalimbali, vipuli vyake vilikuwa vinatoka Ulaya, na Urusi haina uwezo wa ndani. Kwa sasa Urusi inaitegemea China kuziba hilo pengo, lakini China nayo ina mapungufu mengi kwenye ubora. Makampuni yanayotengeneza bidhaa zenye ubora yaliyopo China, ni makampuni ya Ulaya yaliyowekeza China ambayo yanalazimiki ku-comply na masharti ya mataifa yao ambako ndikobyaliko makao makuubya makampuni yao.

Vijana wengi wasomi na wenye uwezo wa kifedha, wanafanya kila namna kuondoka Urusi. Na hao ndio wazalishaji na wataalam ambao wangekuwa na mchango kwa Urusi, sasa wanaondoka.

Pole sana. Lakini utegemee mabaya zaidi kadiri siku ziendavyo. Labda vita isimame. Mataifa ya Magharibi, kama alivyosema Biden, yataendelea kuisaidia Ukraine mpaka watakapohakikisha Urusi siyo tishio kwa nchi yoyote Duniani. Wanataka wammalize mrusi kiuchumi na kitekinolojia na katika nguvu za kivita. Baada ya hapo wataijenga Ukraine kama walivyofanya kwa Korea Kusini, na warusi wengi watahangaika sana kutaka kuhamia Ukraine kwa sababu huko kutakuwa na maisha bora zaidi ukilinganisha na Urusi, nchi ambayo kwa muda mrefu imeishi kwenye uchumi duni na udikteta.
Uchambuzi wako kuhusu mgogoro wa ukraine na urusi umeegemea zaidi kwa propaganda ya marekani na washirika wake na upotoshaji wa historia na siasa za kimataifa. Chimbuko la mgogoro huu ni 1) Ubabe na ubeberu wa marekani na 2) ukiukwaji wa utekelezaji wa makubaliano ya Minsk. Tangu kusambaratika Usoviet ilikubalika taifa la Urusi wasizingilwe na majeshi wala silaha za maangamizi ya wamarekani. Kilichofata ni kwa marekani na mataifa ya nato siyo tu kuizingila nchi ya urusi kwa majeshi bali pia kuzidisha silaha za maangamizi jirani na kujitoa ktk makubaliano ya kudhibiti silaha kali. Sasa Ukraine ikajizatiti kwa chuki na jeuli zaidi dhidi ya urusi na warusi kwa niaba ya narekani (proxy). Wakaendesha mauaji (genocide) kwa raia wa kirusi maeneo ya mashariki ya donesk n.k. kwa miaka mingi na hata kupiga marufuku lugha na utamaduni wao. Nia ya marekani ni kuifanya ukraine koloni lake na hatimaye kuwaigiza nato tyr kuisambaritisha urusi. Pengine bado unayo kumbukumbu kwa kilichotokea urusi ilipo peleka makombora yake cuba miaka ya 60 - leo makombora makali zaidi ya marekani yanaendelea kusambazwa kilomita chache kuizingira urusi. Kuhusu mwenendo wa kivita na ukubwa wa uchumi, warusi wanapigana na mataifa ya nato (27) siyo ukraine. Matrillion ya pesa na silaha kali zimemwagwa. Ni wazi taifa lenye uchumi dhaifu kwa vigezo duni vya gdp kuilinganisha urusi na s/korea lisingehimili vikwazo na vita kali kama urusi inavyoonyesha. Taarifa za hivi karibuni za Kamanda mkuu wa nato hulo ulaya ni kwamba urusi bado iko imara mno na uwezo wao kijeshi na kiuchumi haujateteleka kama mataifa ya magharibi walivyotarajia. Hata hivyo ni kweli pia warusi waliboronga kwa ku underestimate uwezo wa ukraine kivita ambao walikuwa wanajitayarisha kwa msaada wa marekani na hatimaye kutupilia mbali mkataba wa minsk. Tusisahau pia hata marekani majuzi wamefurushwa na taifa maskini la afghanistani. Jiulize ni kwanini hawa Marekani wamesambaza majeshi yao na silaha kila kona ya dunia. Kwanini kila vita imechochewa na Marekani - vietnam, korea, iraq, afghanistan, libya, cuba, chile, iran, syria, hiroshima/nagasaki, n.k...... jiulize!
 
Back
Top Bottom