Urusi yapeleka Manowari zake za kivita Cuba. Wamarekani wachanganyikiwa

Urusi yapeleka Manowari zake za kivita Cuba. Wamarekani wachanganyikiwa

Umewahi sikia kuna Taifa limewahi tupa hata unyoya ndani ya ardhi ya USA?.

Hicho kinachofanywa na Russia kinaitwa mikwala mbuzi.

Hoja ya msingi;
Tafuteni amani ya wenzetu weusi wa Sudan, Somalia, Dr Congo, Central Africa na kwingine kwenye shida ndani ya Africa maana hao ndio ndugu zetu, hao "red nose" mnaohangaika nao wala hawawatambui kama nyie ni binadamu kamili.
Mabepari wakitandikwa ndo amani ya hapo Congo itapatikana
 
Kama yamepelekwa, sioni yakitumiwa. Watayahifadhi tu.
Russia alibugi kuivamia Ukraine

Japan

Sioni cha ziada zaidi ya kuirjesha Cuba kwenye vikwazo vilivyoondolewa na Obama.
Kabugi ukraine...mbona hawajamtoa bado ,,,na mlisema kaishiwa silaha wakati ndo kwanza anataka kuzigawa......
 
Unajua mgunduzi wa NUKE ni nani hapa duniani?, unafahamu nani amewahi itumia hiyo NUKE kwenye vita?.

Tutafute amani na uhuru wa watu wetu wa Afrika kwanza.
Ndugu zetu huko Mozambique wanachinjwa kama kuku halafu dua na sala eti zinaelekezwa kwa wakoloni badala ya ndugu zetu halisia.

Huu ni ujuha tulio nao WaAfrica ambao tumekumbatia utumwa wa wakoloni wa Ulaya na Asia
Kwa hiyo AK47 haziwezi kuwadhuru warusi kwasababu aliyeigundua ni mrusi!?
Hizi akili za upinde.!!
 
Kwani umewahi sikia kuna taifa li.ewahi tupa hata unyoya Urusi? Ukiacha matendo machache ya kigaidi yanayoendelea saivi.
Wewe unahisi Urusi anampiga mkwara Marekani,Marekani mwenyewe anajitetea.
Ila bongo.
Ukraine alipiga mpka ikulu
 
Katika hali inayoelekea kuwachanganya wamarekani Urusi imetuma manowari zake zaidi ya 8 katika pwani ya marekani nchini Cuba sababu ikitajwq ni maandalizi ya mazoezi ya pamoja.

Hii ni mara ya kwanza kwa urusi kupeleka meli za kivita kwa kiwango hiki katika nchi ya Cuba. Wakati huo huo rais Putin anasema Urusi itaanza kutoa silaha za maangamizi kwa nchi zote ambazo ni maadui wa marekani hasa nchi za America ya kusini, North Africa , Iran na Far east.

Kwa mtazamo wa kiuchambuzi haya maandalizi ya Vita ya dunia ambayo kama marekani atalazimisha itokee basi safari hii tutashuhudia mabomu yakidondoka katika ardhi ya marekani.

urusi ana haki ya kujilinda na maadui,mazafaka USA akae mbali
 
Utakua umesahau au ni mtoto mdogo. Kiranja wa dunia alikua mrumi , akaja mwingereza akaitawala dunia lakini leo hayupo. Times count my friend
LEO NI USA 🇺🇸 Ndio Kiranja wa Dunia
@ Sir John Roberts acha kuvuta bangi wakati wa mchana
 
Umewahi sikia kuna Taifa limewahi tupa hata unyoya ndani ya ardhi ya USA?.

Hicho kinachofanywa na Russia kinaitwa mikwala mbuzi.
Kuna njia moja tu ya kujua kuwa ni mikwara ya mbuzi au la!
Biden afanye kweli ili mimi na wewe tujue zipi mbivu na zipi mbichi, au unasemaje mzee wa kazi!?
 
Eeeeh!
Kumbe!?
Kwahiyo wanaogopana, sio Russia anaiogopa USA!?
Vita na mkubwa mwenzio sio chai kila mmoja aililie.

Kwenye vita ktk dunia ya sasa, huwa hakuna mshindi, wote mnapoteza.
Inafikia hatua mnaamua kuridhiana mnashusha silaha chini maisha yanaendelea.

Hata kama umemzidi mabavu kidogo ukaamua kumkalia kinguvu mwenzio, tukifanya tathimini tutakuta pande zote zimedhurika pakubwa sana ikiwemo kupoteza raslimali watu, vitu, uchumi na miundombinu.

Kwa sasa hizo pande mbili lazima zizingatie ile kanuni isemayo "Njia bora ya kupigana vita, ni kuimaliza vita kabla ya kupigana".
 
Umewahi sikia kuna Taifa limewahi tupa hata unyoya ndani ya ardhi ya USA?.Hicho kinachofanywa na Russia kinaitwa mikwala mbuzi.

Kauli yako hii 👆🏽👆🏽 inapishana kabisa na kauli yako hii 👇🏽👇🏽
Vita na mkubwa mwenzio sio chai kila mmoja aililie.

Kwenye vita ktk dunia ya sasa, huwa hakuna mshindi, wote mnapoteza.
Inafikia hatua mnaamua kuridhiana mnashusha silaha chini maisha yanaendelea.

Hata kama umemzidi mabavu kidogo ukaamua kumkalia kinguvu mwenzio, tukifanya tathimini tutakuta pande zote zimedhurika pakubwa sana ikiwemo kupoteza raslimali watu, vitu, uchumi na miundombinu.

Kwa sasa hizo pande mbili lazima zizingatie ile kanuni isemayo "Njia bora ya kupigana vita, ni kuimaliza vita kabla ya kupigana".
 
Kauli yako hii 👆🏽👆🏽 inapishana kabisa na kauli yako hii 👇🏽👇🏽
Ukweli unabakia palepale, wote wanafanya mikwara tu lakini hakuna atakayerusha jiwe kwa mwenzake.

Ukimgusa mkubwa mwenzio umenunua matatizo, ndiyo maana nimekuambia hakuna vita hapo.

Russia ameenda kutalii tu huko, hawezi rusha hata unyoya kwenye ardhi ya USA maana atapelekea giza nene kutanda pande zote.
 
Back
Top Bottom