US yazionya nchi za Afrika kutonunua nafaka kutoka Urusi

US yazionya nchi za Afrika kutonunua nafaka kutoka Urusi

Tanzania hatuwezi kufa hatuna njaa na hatushoboki kwa Russia
Wewe unaongea mambo usiyo yajua kishabiki kama siasa za CCM.

Mwaka huu 2022 kuna njaa kali sana inakuja Tanzania. Mavuno ya mazao ya chakula yalikuwa duni sana sababu ya hali ya hewa na bei kubwa za mbolea au ukosefu kabisa wa mbolea nchini kipindi cha kilimo.

Save this comment and come back here December 2022 up to February 2023.
 
Mkuu unaandika haya ukiwa bar gani? (Samahani lakini)

Wakati Marekani anaivamia Iraq, Afghanistan, na mataifa kadhaa ya kiarabu na kuua maelfu ya raia wasiokua na hatia wanawake na watoto huku ndege zao zikihusika moja kwa moja kubeba mamilioni ya pipa za mafuta ghafi walikua sahihi?

Wameungana na washirka wao kumuondoa Gadafi na kumuua kokatili nani aliwanyooshea kidole?

Marekani anamsapoti Israel kuua mamia ya wapalestine kila wiki halafu sisi tuendelee kutumia mitambo yake ya kufua umeme ya songas pale ubungo kwa kia yeye ni nani?

Kwa haya yote marekani kapata wapi ukiranja wa kutuambia waafrika hiki tufanye na kile tusifanye....kwa kua anatupenda sana?

Hii dunia haiko fare..pengine ile hukumu ya "HAKI" atakayoitoa Mungu kwa walmwengu wote siku ya siku ndiyo itakayo tafsiri kila kinachotendeka sasa hivi na kila mtu atapata ujira wake.......

Ee mola tujaalie tupokee kitabu chetu kwa mkono wa kuloa siku hiyo Aamin!
Nashukuru jinsi unavyouchukia udhalimu. Mimi ninaandika pia kwa machungu ya kuuchukia udhalimu. Lakini kosa moja halihalalishi kosa jingine.
US kavamia, kaua na Kuunga mkono Israeli kuua Wapalestina kama ulivyoandika hapo juu na nakubali hilo SIO HALALI na pia Tukubali kwamba kumwuunga mkono Mrusi aliyevamia,kuua, kuunga mkono makundi ya wapiganaji dhidi ya Taifa la Ukraine, na kupora Nafaka katika Maghala (Hifadhi za Taifa) SIO HALALI.
Ukiranja wa Marekani mm siujui sawasawa kivile, nnachojua ni kwamba ni mbabe na mpenda vita.
Mimi nafikiri Tusiangalie kauli katoa nani bali tuangalie Mantiki na Uzito wa hiyo kauli.
 
Hawa jamaa wanataka Waafrika tufe kwa njaa kwa sababu ya manufaa yao? Ni wakati Africa kufanya mambo yetu bila kupangiwa wala kushinikizwa na mataifa mengine

👇🏻👇🏻👇🏻👇🏻👇🏻👇🏻👇🏻👇🏻
========

U.S. officials are cautioning African countries against buying grains plundered from Ukraine as some nations draw closer to Russia to slow surging food prices and stave off hunger.

The U.S. sent out a warning in mid-May to 14 countries, primarily in Africa, that Russian cargo ships were selling "stolen Ukrainian grain," The New York Times reported Monday. The report comes as humanitarian agencies warn of dire consequences from food supply lines disrupted by the conflict in Ukraine and days after African leaders met with Russian President Vladimir Putin to discuss exporting needed grains.

Putin met on Friday with Macky Sall, president of Senegal and chairman of the African Union, as well as African Union Commission chairperson Moussa Faki Mahamat, at the Russian leader's residence in the Black Sea resort city of Sochi.

After the meeting, Mahamat said on Twitter that the leaders called for the suspension of Western-imposed sanctions on Russia to allow the export of grains he said were needed to mitigate a growing food and energy crisis.

"Russia is ready to ensure the export of its wheat and fertilizer," Sall said in a Tweet, adding that he was willing to meet with Ukrainian President Volodymyr Zelensky as well.
Walete wao.
 
Wewe unaongea mambo usiyo yajua kishabiki kama siasa za CCM.

Mwaka huu 2022 kuna njaa kali sana inakuja Tanzania. Mavuno ya mazao ya chakula yalikuwa duni sana sababu ya hali ya hewa na bei kubwa za mbolea au ukosefu kabisa wa mbolea nchini kipindi cha kilimo.

Save this comment and come back here December 2022 up to February 2023.
Acha kukariri ,licha ya mavuno duni,kilichopungua ni kiwango cha ziada ila hakuna upungufu wala njaa..

Na usikariri kwamba chakula ni mahindi na mpunga tuu na kuthibisha hilo Serikali imesema kamwe haizuii mipaka kwa hiyo watakaoamua kuuza wauze..👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220606-214800.png
    Screenshot_20220606-214800.png
    89.4 KB · Views: 10
Wizi/Uporaji kwenye hiyo vita umeripotiwa sana sema tu labda kama hutaki kukubali kwamba kuna "Looting" sio nafaka tu bali na vitu vingine vingi.
Mkuu, labda niseme tu kwamba Waafrika wanajipiga (Wanajipigisha) wenyewe linapokuja swala la Resources zao.
e.g. Juzi tulisikia imeruhusiwa kusafirisha wanyama hai. Kufumba na kufumbua Ikawekwa Ban. Je, nani aliyekuwa anatupiga? Muda kati ya NI Ruksa na hakuna Ruksa Wameondoka wanyama hai wangapi?
Sasa hapo tunapiga kelele na kulalamika "tunapigwa" bila kumpin point mpigaji. Jamani asitudanganye mtu tunajipiga wenyewe bro.
Sawa mkuu
 
Wasituweke kati bwana...
Wazungu wanatuona waafrika kama vile ni wake zao, wanataka kutupangia mpaka bikini za kuvaa.
Ila kwa kua waafrika wenyewe tumekubali inabidi tuvae tu hizo bikini za nyota na mistari mistari ili bwana wetu asitukasirikie.
 
Hapa duniani kuna nchi nyingi za kijinga na kipuuzi! Ila Marekani na Israel naona zimepitiliza aisee.
Uko sawa; lakini wanapaswa wajue kwamba nyakati hubadilika; hawawezi kuwa walivyo siku zote, mambo yanaenda yakibadilika.
Zile amri za kiimla za wamarekani ambazo zilikuwa hazibishiwi enzi hizo, sasa zinajibiwa kwa namna mbalimbali; hata kwa kuviziwa kama walivyoviziwa na Osama na kuumizwa vibaya japo wanadai wamemuua.
Nchi zingine kama Korea Kaskazini na Iran, zamani zilikuwa zinaufyata; lakini siku hizi zinaweza kujibizana na U.S; hata kama hazijawahi kumpiga, lakini ana hofu nazo kwa sababu anajua kwamba zina teknolojia ya kivita (nuclear) ambayo inaweza kupiga ndani ya U.S; hata kama ana mifumo ya kukinga mashambulizi hayo, lakini hathubutu ku-risk kuruhusu mashambulizi hayo yafanyike, maana hana uhakika nini kitatokea!!
U.S ataendele kutupelekesha sisi waafrika na nchi zingine duniani ambazo hazina teknolojia ya nuclear.
Tutaendelea kudeki barabara zetu anapokuja Rais wa U.S kama ilivyofanyika kwa Obama na Bush Jr; lakini siyo kwa Russia, Iran, Korea Kaskazini na China.
 
Back
Top Bottom