Usafiri wa Helkopta unaonekana siyo usafiri sahihi kwa viongozi wa kitaifa; nini maoni yako?

Usafiri wa Helkopta unaonekana siyo usafiri sahihi kwa viongozi wa kitaifa; nini maoni yako?

Tumeshuhudia usafiri wa helkopta ukiondoa nafsi za viongozi mbalimbali hasa katika kampeni za kisiasa au operesheni mbalimbali zikiwemo za kijeshi.

Ni usafiri ambao unafaha sana kuzunguka eneo kubwa kwa muda mfupi lakini ukumbana na changamoto kubwa ya hali ya hewa au hitilafu.

Akili yangu inanishawishi niwakumbushe viongozi kufanya uchunguzi maalum kuhusu usafiri huu kabla ya kuutumia. Tanzania ajali za helikopta ni nyingi kuliko ajali za ndege au wakati mwingine ajali za magari zinazohusisha viongozi.

Ndugu zangu wanasiasa kuweni makini sana na usafiri huu hasa tunapoelekea uchaguzi. Tuone namna yakukabiliana na ajali za usafiri huu ambao umeondoa viongozi wa Mataifa tajiri yenye ulinzi mkubwa Duniani.

Yawezekana chopa inalogeka kirahisi kuliko usafiri mwingine? Sizungumzii kulogeka kwa uchawi wa Ndumba bali kulogeka kiteknolojia au kulogeka kimedani za kivita.

Poleni wote mliowapoteza wapendwa wenu kwa chopa.
Ni usafiri mzuri lakini unahitaji proper maintenance. White house mpaka leo ana helicopter ya kumsafirisha rais. Matter of fact viongozi wengi wanazo.
Ila usaifir huo unategemea constant maintenance
 
Tuwataje wote maarufu walifariki Kwa ajali ya chopa
Kobe
Boss wa Wagner
Mbunge wa mbarali
Rais wa iran
Mkuu wa jeshi Kenya

Siyo kweli. Boss wa Wagner alifariki kwa ajali ya ndege.

Tanzania pia tuliwahi kushuhudia vifo vilivyotokana za ajali za ndege na magari, nyingi kuliko za chopa. Rais wa Msumbiji ajali ya ndege na wala siyo chopa.

Worldwide, viongozi waliofariki kwa ajali za ndege ni wengi kuliko chopa.
 
Tumeshuhudia usafiri wa helkopta ukiondoa nafsi za viongozi mbalimbali hasa katika kampeni za kisiasa au operesheni mbalimbali zikiwemo za kijeshi.

Ni usafiri ambao unafaha sana kuzunguka eneo kubwa kwa muda mfupi lakini ukumbana na changamoto kubwa ya hali ya hewa au hitilafu.

Akili yangu inanishawishi niwakumbushe viongozi kufanya uchunguzi maalum kuhusu usafiri huu kabla ya kuutumia. Tanzania ajali za helikopta ni nyingi kuliko ajali za ndege au wakati mwingine ajali za magari zinazohusisha viongozi.

Ndugu zangu wanasiasa kuweni makini sana na usafiri huu hasa tunapoelekea uchaguzi. Tuone namna yakukabiliana na ajali za usafiri huu ambao umeondoa viongozi wa Mataifa tajiri yenye ulinzi mkubwa Duniani.

Yawezekana chopa inalogeka kirahisi kuliko usafiri mwingine? Sizungumzii kulogeka kwa uchawi wa Ndumba bali kulogeka kiteknolojia au kulogeka kimedani za kivita.

Poleni wote mliowapoteza wapendwa wenu kwa chopa.
bado bodaboda itakua ndio usafiri hatari zaidi duniani, lakini usafiri wa anga utaendelea kua usafiri salama zaidi kuliko chombo kingine chochote cha usafirishaji licha ya kwamba athari zake ni mbaya zaidi kuliko chombo kingine chochote cha usafirishaji inapotokea ajali....

bodaboda anaweza baki na mguu moja akipata ajali, ila kwenye usafiri wa anga unaweza vunjika maeneo mbalimbali ,lakini hapo hapo bado ukaungua na moto tena dah, kupona ni nadra sana..

katika yote haya,
tahadhari za kiusalama na umakini ni jambo la maana na muhimu sana kuzingatiwa.

sio unaona kabisaa hali ya chombo au hali ya hewa na mazingira kiusalama si rafiki, kwa vipimo na hata kwa macho tu, eti kwakua wewe ni mwanajeshi unajipiga kifua aah hii mbona kawaida tu, pandeni Twendeni 🐒
 
Helicopter ajali zake zimekuwa nyingi kama bodabodaaa...!! Nadhani kuna poor service na maintanance yakeee kuanzia kina filikunjombe...kobe..mmiliki wa Leicester...general wa kenya now rais wa iran.. SIO USAFIRII SALAMA KABISA.

Wengi wenu inaonekana siyo wafuatiliaji kabisa wa matukio mbalimbali Duniani. Mnaona matukio mawili au matatu, mnakimbilia kwenye conclusion ambayo inakuwa siyo ya kweli.

Wakuu wa nchi waliokofa kwa ajali za ndege ni wengi maradufu ya wale waliokufa kwa chopa.

Wakuu wa nchi waliokufa kwa ajali za ndege ni 14:
Jose (Paraguay)
Ramon (Phillipine)
Nereu (Brazil)
Abdul (Iraq)
Humberto (Brazil)
Ahmed (Mauritania)
Jaeme (Ecuado)
Omar (Panama)
Samora (Mozambique)
Habyarimana (Rwanda)
Ciprian (Burundi)
Boris (Mecedonia)
Ryszard (Poland)
Lech (Poland)


Wakati, mpaka 2024, wakuu wa nchi waliokufa kwa ajali za chopa kwa Dunia nzima ni 3 tu.
 
Wengi wenu inaonekana siyo wafuatiliaji kabisa wa matukio mbalimbali Duniani. Mnaona matukio mawili au matatu, mnakimbilia kwenye conclusion ambayo inakuwa siyo ya kweli.

Wakuu wa nchi waliokofa kwa ajali za ndege ni wengi maradufu ya wale waliokufa kwa chopa.

Wakuu wa nchi waliokufa kwa ajali za ndege ni 14:
Jose (Paraguay)
Ramon (Phillipine)
Nereu (Brazil)
Abdul (Iraq)
Humberto (Brazil)
Ahmed (Mauritania)
Jaeme (Ecuado)
Omar (Panama)
Samora (Mozambique)
Habyarimana (Rwanda)
Ciprian (Burundi)
Boris (Mecedonia)
Ryszard (Poland)
Lech (Poland)


Wakati, mpaka 2024, wakuu wa nchi waliokufa kwa ajali za chopa kwa Dunia nzima ni 3 tu.
Tangu lini hii orodha?
 
Back
Top Bottom