Ushauri: Anataka kuacha kazi Serikalini sababu ya maslahi madogo

Ushauri: Anataka kuacha kazi Serikalini sababu ya maslahi madogo

Huu uongo
Dr sehemu ina maduka mawili ya Mpesa, nauli 6k kuifikia benk hiyo ni sehemu ya kusema sijawahi kuona au kufika eneo kama hilo, u r kidding brother,
mimi niliwahi fika mahala huko Mbeya tukampa mzee lift kwenye escudo, baadae tunamshusha anauliza huyu mnamchinja akiwa na ukubwa gani? hapo ni full kinyaki anajua lile gari ni mnyama!
 
Mwanangu kasomea india udaktari wa moyo kafanya intership jakaya kaona wafanyakazi walivyo na roho mbaya humo jakaya na kujipendelea kaangalia mshahara kaona nayenyewe ovyo, kagoma kumalizia intership hataki kabisa anasema bora akafanye biashara yoyote ile tumebembeleza sana kagoma
Mwanao ni muongo,
1.baada ya super speciality in cardiology hakuna internship
2.Ili uwe cardiologist inachukua zaidi ya miaka 10,MD=5,MMED=3,MSc Cardiology =2,hakuna mtu aliyemaliza supercialist hapa bongo akakosa KAZI ya kufanya ama hajui cha kufanya
Muulize vizuri,alisoma nini huyo mwanao na kabla ya kwenda the so called India,alikua ana elimi gani
 
Lift za bodaboda ,by the way mwanamke akiwa kwenye umri wa tension yeyote yule anapita nae na ndio Huwa hivyo mwishowe.

Jifanyeni masista duu ila mkirogwa tuu mkapangiwa Vijijini mumekwisha mtakuwa wa huko huko.

Vijijini kuna Watendaji,Walimu,manesi ,MaCO,Polisi Kata,Extension officers,Maofisa maendeleo ya jamii kata na wale wengine wanaosimamia maji hapo ni kile Kijiji Kikubwa Makao Makuu ya kata.

Vijiji vingine utaishia kuona Walimu na manesi tuu na kulipwa na bodaboda au Dereva wa vihiace vya kuja mjini.

Maofisa wa Halmashauri ni WA kubahatisha maana Ukiwa na huyo unaweza hamia mjini
Hapa mdau umeongea ukweli mtupu aisee,🤣🤣
 
Ukiwa huna ajira utatamani nafasi ya huyu mwamba upewe wewe lakini kwa tuliotembea vijijini kuna maisha hata hiyo ajira haina maana yoyote.

Ifike wakati serikali iajili watu kutoka kwenye jamii husika wafanye kazi kwa moyo na mazingira ndio walikozaliwa hayawapi tabu
Kuajiri watu wanaotoka kwenye jamii husika kunadumaza eneo husika.

Angalia baadhi ya halmashauri kongwe haziendelei kwa tabia hiyo.
 
Ukiwa huna ajira utatamani nafasi ya huyu mwamba upewe wewe lakini kwa tuliotembea vijijini kuna maisha hata hiyo ajira haina maana yoyote.

Ifike wakati serikali iajili watu kutoka kwenye jamii husika wafanye kazi kwa moyo na mazingira ndio walikozaliwa hayawapi tabu
Kuna jamii sio za kutangamana nazo yaani yafaa waajiriwe wa kulekule
 
Afanyekazi kwa malengo, kumbuka kwamba ajira ni sehemu pia yakujipatia mtaji wakufanya biasha, hususani ajira za serikalini, kwanza angalee fursa kwenye maeneo yanaomzunguka.
 
Kuna jamii sio za kutangamana nazo yaani yafaa waajiriwe wa kulekule
Kuna sehemu inaitwa Nana iko mpakani na wilaya ya Kilosa na Gairo ila ni rahisi kufika Kidete Kilosa kwa pikipiki.

Pale nilinunuwa mgodi wa Moonstone na nikakaa kambini na timu yangu.

Kiasili sehemu zenye madini hakuna maji, maji na madini havikai pamoja.

Kuagiza maji mwanakijiji namtuma alfajiri na punda anarudi saa 10 jioni imagine na hayo maji si salama naweka water guard.

Katika kupelekeza hawa watu wanaishi vipi natafuta mihogo ya kuchemsha kunywea chai kwanza nikapata sehemu ya kuchaji simu kuna kilabu cha pombe.

Kuna kitu sikuelewa ilibidi niulize mbona kila anayekuja kunywa ana kibegi mgongoni? Ndio nikaambiwa huku watu hawana pesa wanaleta mahindi wanapewa pombe.

Hayo maeneo kwanza yana baridi kali halafu maji hakuna mtu kukaa wiki bila kuoga ni kawaida na mvua ikinyesha ni neema, sasa imagine mwalimu amekulia Dar unamtupa hapo ni mateso matupu, mimi nilirudi mjini mweusi tii.
 
Maisha ya kijijini mazuri sana nimezaliwa kijijini, nimesomea kijijini na mitikasi mingi nimefanyia kijijini napakubali kinoma huku mjini nililoea after chuo

Sio kila mtu atakuwa tajiri na concept ya mafanikio ni perception za mtu na malengo aliojiwekea

Wengi wenye malengo na mindoto mikubwa huishia kuwa masikini wa kutupwa na hopeless ni bora ukaishi uhalisia

Aache kazi asiache kazi uhalisia wa maisha yake utabaki vile vile hakuna kitakacho badilika
 
Niulize nini faida ya kufanya kazi serikalini, kama ualimu na daktari?

Kuna mwana ni mwalimu ajira mpya mwaka jana anatamani kuacha kazi mazima ila pa kuanzia sasa ndo haelewi. Anaomba ushauri sababu haoni challenge yoyote ya maisha ikiwa hamna marupurupu na take home ni finyu kidogo.

Mazingira sio poa ni kijiji ndani huko, maduka mawili tu ya mpesa, benki mpaka utoe nauli ya elfu 6 ndio unafika.

Soma Pia: USHAURI: Niliacha kazi Serikalini kutokana na mazingira magumu ya kazi miaka miwili imepita, baada ya mambo yangu kutengemaa nataka kurudi
Wazo zuri sana
 
Huku ndio hapawezi kabisa ataishia kuamini watu ni freemason, ndinga kubwa matumizi million kama buku tu halafu huoni watu wanafanyakazi gani na wala siyo majambazi

Huku mtaani ndio kwenye matumizi ya akili winner to stay

Kuna dogo mmoja alikuwa na akili nzuri za darasani lakini sasa hivi asubuhi anaamkia visungura keshadata na degree yake kabatinim
Hatari dogo ana degree ya nn?jaribu kumtia moyo mkuu ukimuacha hata potea.
 
Wakati nipo field Mwalimu mmoja alinambia kuwa

Upo willing kuwa Mwalimu ?

Nikamwambia yes

Akasema huku chakula, sehemu ya kulala uhakika Ila mambo makubwa makubwa haiwezekani kiyafikia kirahisi.

So na Kama UPO ndani ndani kijijini lazima uone hali IPO hivyo.


So fanya mahesabu vizuri ujue kipi hasa ukifanya kitakupeleka mbele na kipi hasa ukifanya kitakupa furaha.

All the best
 
Maisha ya kijijini mazuri sana nimezaliwa kijijini, nimesomea kijijini na mitikasi mingi nimefanyia kijijini napakubali kinoma huku mjini nililoea after chuo

Sio kila mtu atakuwa tajiri na concept ya mafanikio ni perception za mtu na malengo aliojiwekea

Wengi wenye malengo na mindoto mikubwa huishia kuwa masikini wa kutupwa na hopeless ni bora ukaishi uhalisia

Aache kazi asiache kazi uhalisia wa maisha yake utabaki vile vile hakuna kitakacho badilika
Wewe huelewi hata ulichokiandika, vijiji vya Tanzania vinafanana?

Kuna mwalimu anaweza kulalamika yupo Uchagani mazingira magumu? Vijiji vina umeme na maji tangu mkoloni na walimu na mapadre wanaheshimika sana.
 
Niulize nini faida ya kufanya kazi serikalini, kama ualimu na daktari?

Kuna mwana ni mwalimu ajira mpya mwaka jana anatamani kuacha kazi mazima ila pa kuanzia sasa ndo haelewi. Anaomba ushauri sababu haoni challenge yoyote ya maisha ikiwa hamna marupurupu na take home ni finyu kidogo.

Mazingira sio poa ni kijiji ndani huko, maduka mawili tu ya mpesa, benki mpaka utoe nauli ya elfu 6 ndio unafika.

Soma Pia: USHAURI: Niliacha kazi Serikalini kutokana na mazingira magumu ya kazi miaka miwili imepita, baada ya mambo yangu kutengemaa nataka kurudi
Katika hali hiyo,je hajaona fursa?
 
Back
Top Bottom