Ushauri: Kuelekea bima ya afya kwa wote, serikali iweke tozo maalum kwenye sigara, pombe, soda ili mama na mtoto watibiwe bure

Ushauri: Kuelekea bima ya afya kwa wote, serikali iweke tozo maalum kwenye sigara, pombe, soda ili mama na mtoto watibiwe bure

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Haina shaka kwamba pombe na sigara, soda na vinywaji aina yake, na pengine sekta ya madini, ndio visababishi vikubwa vya maradhi. Visababisha maradhi basi viwe na mchango katika tiba.

Serikali ikae ifanye tathmini ili kujua endapo itaongezwa shilingi 100 kwa kila kinywaji, itapatikana shilingi ngapi.

Halafu iangaliwe huduma ya mama na mtoto huwa inagharimu shilingi ngapi, zipelekwe huko. Mama mjamzito, mama aliyejifungua na mtoto, wapewe huduma bure. Pia mtoto yeyote anayelazwa apewe huduma bure pamoja na wazee.

Wataalamu wakae wafanye tathmini ya makadirio ya gharama hizo. Hii inaweza kugusa huduma maalum za matibabu ya moyo kwa watoto. Hii itampa nafuu Malisa kuchangisha watu huko mitandaoni, na pia ugonjwa hauna chama.

Wanaume tukisaidiwa gharama za kuwatibu mke na mtoto, sisi tutajitibu wenyewe
 
Viongozi wanapenda sana aina hii ya mindset kwa Raia wanaowaongoza.

Hatuongelei ma v8 ya 400 mil plus za viongozi wanazonunua kama pipi, gharama na matumizi mabaya ya puplic funds bali tunajibana sisi kwa sisis kwa vitu ambavyo tunaona havituhusu.
 
Viongozi wanapenda sana aina hii ya mindset kwa Raia wanaowaongoza.

Hatuongelei ma v8 ya 400 mil plus za viongozi wanazonunua kama pipi, gharama na matumizi mabaya ya puplic funds bali tunajibana sisi kwa sisis kwa vitu ambavyo tunaona havituhusu.
Nchi inajengwa kwa mifumo (systems)
 
Nchi inajengwa kwa mifumo (systems)
Umemsikia raisi wa Zambia? Amekataa kusaini new package ya presidential motorcade worth 1.8 million us dollars, ilhali kuna magari mazuri tu yapo kutoka utawala uluopita.

V8 vxr, moja manunuzi pamoja na matengenezo yake kwa mwaka linaweza lipia bima hao akima mama zaidi ya mia nane
 
Ufanye mapenzi mwenyewe kwa raha zako alafu unataka wengine wakulipie? acha kuzaa kama unaona huna uwezo
Umeona eeh! Mijitu bado inaishi life styles za akina Mkwawa kwa kuoa na kuzaa hovyo bila kuangalia changamoto za malezi zilizopo hivi sasa.

Halafu majitu hayo yanategemea tuyasaidie kulea. Kabla hujazaa jipange kwanza.
 
Umemsikia raisi wa zambia? Amekataa kusaini new package ya presidential motorcade worth 1.8 million us dollars , ilhali kuna magari mazuri tu yapo kutoka utawala uluopita.
V8 vxr , moja manunuzi pamoja na matengenezo yake kwa mwaka linaweza lipia bima hao akima mama zaidi ya mia nane

.
Huyo ni populist, ngoja alkaeda wamtungue ndio atajua umuhimu wa usalama wa kiongozi wa nchi
 
Naunga mkono hoja.

Katika Watoto laki moja wanaozaliwa nchini Tanzania watoto miatano hufariki , Hapo sijazungumzia kina mama wenyewe .


Ili Kuipa nguvu Jamii na kuimarisha huduma za bure KWA mama na mtoto Hatuna Budi kufanya kama ulivyoshauri mkuu...


Pia Matibabu ya mtoto chini ya miaka mitano yawe ni bure na yenye ubora
 
Haina shaka kwamba pombe na sigara, soda na vinywaji aina yake,na pengine sekta ya madini, ndio visababishi vikubwa vya maradhi. Visababisha maradhi basi viwe na mchango katika tiba.

Serikali ikae ifanye tathmini ili kujua endapo itaongezwa shilingi 100 kwa kila kinywaji, itapatikana shilingi ngapi.

Halafu iangaliwe huduma ya mama na mtoto huwa inagharimu shilingi ngapi, zipelekwe huko. Mama mjamzito, mama aliyejifungua na mtoto, wapewe huduma bure. Pia mtoto yeyote anayelazwa apewe huduma bure pamoja na wazee.

Wataalamu wakae wafanye tathmini ya makadirio ya gharama hizo. Hii inaweza kugusa huduma maalum za matibabu ya moyo kwa watoto. Hii itampa nafuu Malisa kuchangisha watu huko mitandaoni, na pia ugonjwa hauna chama
Bima ya Afya kwa wote itaenda kuondoa msamaha kwenye matibabu.
Wasiwasi wangu ni Je,shirika litakalohusu Bima ya Afya kwa wote litaweza ku_afford kulipa madeni ya huduma kwa wanachama ikiwa NHIF sasa inaenda kufa kwa sababu ya mzigo wa madeni?!
 
Bima ya Afya kwa wote itaenda kuondoa msamaha kwenye matibabu.
Wasiwasi wangu ni Je,shirika litakalohusu Bima ya Afya kwa wote litaweza ku_afford kulipa madeni ya huduma kwa wanachama ikiwa NHIF sasa inaenda kufa kwa sababu ya mzigo wa madeni?!
NHIF inadai serikali, serikali wanaikopa sana, ni kutunga sheria kuzuia serikali kukopa huko, michango yote iende moja kwa moja kwa mfuko
 
Ushafatilia makusanyo na matumizi ya tozo, badala ya kuiambia serikali yako iache matumizi ya kijinga kama kudhamini mashindano ya cecafa unawaza kuongeza tozo.

Inaelekea una.phd ya uchumi ya mchongo
 
Huyo ni populist, ngoja alkaeda wamtungue ndio atajua umuhimu wa usalama wa kiongozi wa nchi
Kwamba gari la gharama ndio usalama?

Yupo realistic, the lavish and luxurious life of leaders should not be at taxpayers burden ,kiongozi akitaka v8 anunue lake
 
Duh.! Mama na mtoto watibiwe bure tena? Tunarudi kwenye ujamaa kamili wa kukamua watafutaji kodi za damu ili wanaozaa bila kujiandaa wapewe kila kitu bure?
 
Raslimali tulizonazo zinatusaidiaje mpaka tuanze kukamuana mpaka kunguni kwa maskini
 
Ufanye mapenzi mwenyewe kwa raha zako alafu unataka wengine wakulipie? acha kuzaa kama unaona huna uwezo
Bima inapaswa kuwa swala la mtu mmoja mmoja sio si swala la kikundi flani , kila mtu apambane apte bima sio mimi nifannye kazi halafu halfu nikatwe pesa kwa ajili ya wahuni flani wanolaliana na kufanya mapenzi hiovyo
 
Back
Top Bottom