Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Unaona basi, na wewe huelewi kabisa maana ya uraia pacha na hujui sifa za mtu kupewa uraia pacha.

Hebu niambie, huyo jaji wa USA anaelipwa milioni 45 kwa mwezi, atapewa uraia pacha waTanzania kwa vigezo gani?

Nahata kama ana vigezo (nakuaminisha hana), katika ncho zote zilizo na uraia pacha duniani, anasubiri tu Tanzania itakaporuhusu uraia pacha ndio aje anunue mashamba ya babu zako? Kwa lipi hasa tulilonalo ambalo nchi nyingine zote duniani ambazo zinaruhusu uraia pacha zmekosa?

Ndio maana nikasema wazi, mnaobisha juu ya uraia pacha wala hamuelewi maaana ya uraia pacha na hamjui vigezo vya mtu kupewa uraia pacha. Mnabisha tu kwa chuki na wivu, sio hoja za maana
 
Mifumo madhubuti yenye usimamizi thabiti, kama wanastahili kwanini wasipewe??
Uraia mtu hapewi tu kama cheti cha la 7. Tukifikia mifumo ikarekebishwa ni jambo la heri.

Mie naupenda uraia pacha, kwani diaspora hawajiamini kuwekeza nyumbani. Hela yote unamalizia kulipia permits.

Everyday is Saturday................................😎
 
wenye nchi hatutaki kama tu tulivyo msagia diamond kunguni huko BET.
 

Hata kama wamekwama wakija kupumzika nyumbani kuna tatizo? Sii ni ndugu zetu hawa.
 
Mkuu, tatizo kubwa hapa sio faida wala hasara. Angalia ramani ya uraia pacha katika Afrika, unaweza kweli kushuku faida za uraia pacha ikiwa umekumbatiwa kwa kiwango hicho? Hivi unadhani kwamba sisi na nchi tisa tu zilizobaki ndio tunaelewa hasara za uraia pacha kuliko wenzetu wote Afrika?

Labda la msingi ni kuwaelimisha wanaobisha juu ya uraia pacha kwa kuwa ni wazi kabisa hawaelewi kabisa maana ya uraia pacha na mtu anakuwaje raia pacha. Ukitaja uraia pacha wanadhani ni kuruhusu watu wa nje kuja kununua uraia wa Tanzania!
 
Hivi mtu yeyote mwenye akili na uwezo wa kufikiri, anapoangalia ramani hii, haoni kwamba kuna kitu hakiko sawa kuhusu sisi Watanzania, na hao wenzetu wengine tisa waliovaa dark blue kama sisi?

 
Hata kama wamekwama wakija kupumzika nyumbani kuna tatizo? Sii ni ndugu zetu hawa.
kupumzika wanakuja, mbona mange anaendaga huko kwao uchagani, amemjengea mama yake huko, ana biashara ila wabaki na uraia wao huko.
 
Wajinga wengi walitafsiri uzalendo ni kumpenda Magufuli na kukubakuana naye kwa kila jambo. Walimfanya Magufuli kuwa Mungu hivyo yeyote aliyetofautiana naye kwao hakuwa mzalendo.

Ndicho kilichomkuta Lissu na wengine waliopotezwa na kuokotwa kwenye viroba. Leo hii tumeambiwa makinukia yanasafirishwa nje ni halali.

Watu waliopiga EPA, MEREMETA, ESCROW, RICHMOND, KIVUKO nk hao walikuwa na uraia pacha?
 

Tunajaribu Mkuu, Nina uhakika Balozi Mulamula anaijua hii issue vizuri sana. Alikuwa Balozi Canada, USA, Mshauri mkubwa kuhusu haya mambo kwa Rais.

Naona kuna hofu kubwa sababu kutoelewa vizuri hii issue.
 
Mimi nasapoti Uraia pacha,hakuna cha Usalama wala nini,wauaji wote mfano wa Sabaya na wenzake hawana Uraia pacha lakini ni hatari kwa Tanzania.

Visingizio cha kijinga tuviache Uraia pacha ni Future.
 
kupumzika wanakuja, mbona mange anaendaga huko kwao uchagani, amemjengea mama yake huko, ana biashara ila wabaki na uraia wao huko.

Vipi kama angekuwa Kaka yako, mdogo wako, Baba yako, will you feel the same?

Kagame anawapa hadi viwanja wajenge ni nchi ndogo sana. China wanawaomba Diaspora wao warudi.

Ulaya, USA na nchi nyingi tu ukiwa na elimu (high skilled migrants) mtaji, kipaji (exceptional talent) wanakupa paper zao.

Unacheza soka vizuri, baskeball, athlete wanakupa. Wameanzisha hadi lottery kuwapa wati 50,000 makao ya kudumu baadaye uraia kila mwaka kutoka nchi nyingi duniani.

Ukiwa na Wazazi, Wazee kutoka nchi nyingi Ulaya wanakupa Uraia kupitia hiyo route (Ancestors).
 
Mkuu, kuna jamaa ilibidi aukane uraia wa Tanzania ili apate uraia wa Canada kwa kuwa aliishi kule muda mrefu na mazingira yalimlazimisha kuwa raia wa Canada. Huyu mtu kaoa M-Canada na ana watoto kule. Ndugu zake walilia alipowaambia analazimia kufanya vile utafikiri amekufa. Sasa kuja Tanzania lazima aombe visa, japo ndio nchi yake ya kuzaliwa, wazazi wake wapo hapa, makaburi ya babu zake yapo hapa..

Kwa hiyo kuna psychological issue pia kwa nini watu kama hao tuwaruhusu kuwa raia pacha, ili bado awe na attachment za roots zake. Sio suala la kuwekeza tu, kumnyima mtu haki zake za roots zake kwa kuwa ameoa raia wa nje na ili aishi huko bila matatizo kutunza familia yake inabidi achukue uraia wa nchi hiyo, ni kukiuka haki zake za binadamu. Canada wanasema wazi, sie hatuna tatizo na wewe, tatizo ni nchi yako, lakini ili uwe na haki ya mambo a,b,c,d lazima uwe raia wa Canada. Sasa kwa nini tumkwamishe mtu wa namna hiyo? Tukimruhusu awe na uraia pacha sisi tunapata hasara gani, ikiwa Canada wanasema hawana tatizo huyo mtu akiwa na uraia wa Canada na Tanzania?
 
Bernard Membe Jasusi mbobezi aliwahi kusema iwapo atashinda Uraisi wa Jamhuri ya Muungano basi Uraia Pacha utakua 'Rukhsa' sasa kama jasusi mbobezi anasema hivyo hawa makapuku wa if wanaosema kuhusu Usalama wa Taifa wamekula Maharage ya wapi?
 

Ni swala la muda soon or later itakuwa wazi kwa majority nini kifanyike. TZ sio kisiwa.

Hizi Assets (Rasilimali watu wetu wote ndani na nje) itafika mahali lazima tuzitumie zote.

Elimu mfano Undergraduate inaweza kuwa 36m hadi 50m kwa mwaka kwa wageni. Bado accomodation, chakula, usafiri.

Kwa mzawa labda 18m. Lakini unapewa grant na mkopo. Pesa za kujikimu (accomodation, food transport) unapewa unalipa tuition fee tuu. Hulipi kitu kutoka mfukoni kwako in advance.

Pia unaweza kutafuta kazi ikasaidia.

Post graduate hadi 90m.

Kwanini usichukue uraia kuepuka hizi gharama. Sio kwamba haupendi nchi yako ulipozaliwa. Hapana, unatumia opportunity iliyopo mbele yako.
 
Bernard Membe Jasusi mbobezi aliwahi kusema iwapo atashinda Uraisi wa Jamhuri ya Muungano basi Uraia Pacha utakua 'Rukhsa' sasa kama jasusi mbobezi anasema hivyo hawa makapuku wa if wanaosema kuhusu Usalama wa Taifa wamekula Maharage ya wapi?
Hewaaa! Mkuu hapo umemaliza kabisaaaa! Bernard Member, mtu wa TISS, anaejua espionage na counter espionage, anatoa kauli kwamba uraia pacha sio tatizo na akiwa raisi ataruhusu, hawa makapuku wanajifanya wanajua zaidi yake kuhusu usalama wa Tanzania!!!

Ndio maana nikasema wazi, ni wivu na chuki tu vimewajaa, wala hawajali usalama na uzalendo! Wape nafasi ya kula fedha za umma wataiba bila aibu huku wanajifanya eti wazalendo kuliko Diaspora
 
Ndio maana nikasema wazi, ni wivu na chuki tu vimewajaa, wala hawajali usalama na uzalendo! Wape nafasi ya kula fedha za umma wataiba bila aibu huku wanajifanya eti wazalendo kuliko Diaspora
Tena wacha Vichwa vya Diaspora virudi ili Wafanye kazi na Raisi Samia Suluhu wanachoogopa hao makapuku ni kuwa nafasi zao zitatwaliwa na Watanzania wenye Elimu ya kweli na Exposure kutoka Diaspora.

 
Hao walioko nje wamekwama unafikiri watawaza juu ya uraia pacha au kuupigia debe? Uwezo wako mdogo wa kufikiri hapa uko dhahiri kabisa. Wewe unaona ujiko kusema unaenda kunywa wine. Bila shaka utakuwa masikini aliyepata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…