Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Mkuu Pasco nafikiri huu msemo wa "mwenye nguvu mpishe" hauna mashiko kwenye siasa. Na sio tu kwenye siasa hata ktk maisha ya kawaida. Mwenye nguvu kabiliana naye, pambana naye hata ufe ukipambana. Ni heri kufa ukipigania haki yako kuliko kuishi ukiwa mtumwa. Kama wenye nguvu tutakuwa tunawapisha wafanye wanavyotaka basi tukubali kuwa watumwa maisha yetu yote.
Mkuu Danny, nakubaliana na wewe, dawa ya adui sii kumkimbia au kumpisha bali kukabiliana nae, na hata kama utaangamia katika kukabiliana huko, na kupoteza maisha, jina lako ndilo litabaki kama shujaa, cha muhimu cha kujiuliza, ni nani muhimu zaidi kati ya shujaa mfu, au mfungwa hai aliye gerezani?!, au aliyejificha mwituni?!.

Kwa maoni yangu, kama unakiona kifo kile, halafu unakikimbilia na kufa tuu ili uonekane shujaa, wewe ni shujaa mjinga!. Kama unataka kushindana au kupigana na mtu mwenye nguvu zaidi yako, hivyo unaingia kwenye mapambano ili hali unajua utawawa, wewe pia ni shujaa mjinga!. Shujaa mwerevu ni yule ambaye hawezi kuingia kwenye vita ambayo anajua atashindwa!, bali atampisha huyo mwenye nguvu, huku yeye akijijenga mpaka awe na nguvu za kukabiliana na kushinda!.

Naomba take time kasome bandiko langu hili, utanielewa ninamaanisha nini
Tuko Vitani Tuna Wapiganaji Shupavu, Wapiganaji Makini na ...

Pasco
 
Mr Pasco, please hebu naomba nijuze kidogo, inawezekana mimi sielewi.

Hivi hizi "politics of development" ni zipi hizo na zinafanywaje mkubwa?

Na ukimaliza kueleza hebu dadavua na "politics of confrontation" ni zipi hizo na zinafanywaje eti?

Nimeona na kimsikia mkulu wetu mara nyingi naye akisema "watanzania wanataka siasa za maendeleo"... it is a little bit confuses me ninaposikia na kusoma vitu kama hivi!

It is either you and Mr president don't understand the meaning of politics in relationship with development or you purposely try to manipulate people with your own defenition of politics!

That's what I can comment about these fallaciuos statements from you guys!!

Namkumbuka sana Dr Wilbroad Peter Slaa katibu mkuu wa CHADEMA aliyepita aliyeongoza harakati kabambe wakati wa Kikwete hata kuiweka CHADEMA ktk chati ya juu na pengine kuifanya serikali iamke na kufanya kazi ya ziada ktk kutekeleza ahadi zake za kuwahudumia wananchi kwa kutekeleza miradi mingi ya maendeleo japo kasoro za hapa na pale haziwezi kukosekana.

Tell me. CHADEMA ya wakati wa Dr Slaa ilikuwa inafanya siasa za namna gani kati ya hizo ulizozitaja.....development or confrontation politics.........or both?
Mkuu Kitaturu, kuna siasa za aina tatu, siasa za maendeleo, (developmental politics), siasa za kujifurahisha (politics of politiking), na kuna siasa za migogoro, (politics of confrontation).

1. Siasa za Maendeleo.
Hizi ni siasa zenye malengo ya kuleta mabadiliko chanya, changing for the better. Kila political move unayofanya, ila malengo chanya ya kuleta mabadiliko, siasa hizi zimefundishwa sana na Mwalimu Nyerere katika kitabu chake cha Binadamu na Maendeleo. Siasa hizi ni siasa zenye sera, ilani, malengo, mikakati na time frame, hizi mimi naziita SMART Politics, ni siasa zenye
S - specific, significant, stretching
M - measurable, meaningful, motivational
A - agreed upon, attainable, achievable, acceptable, action-oriented
R - realistic, relevant, reasonable, rewarding, results-oriented
T - time-based, time-bound, timely, tangible, trackable

2. Siasa za Kujifurahisha.
Hizi ni kauli za kisiasa kwa ajili ya kujifurahisha tuu to gain political mileage lakini hakuna chochote kinachofanyika, hizi zinajumlisha ahadi zisizotekeleka, hizi ni politiking, mtu unazungumza ili tuu uonekane na wewe upo upo. Kwenye kundi hili, zile siasa za bendera fuata upepo pia zimo kwenye kundi hili. Hizi ni siasa ambazo hazina maana yoyote kwa maendeleo!, huku ndiko siasa za fitna, majungu, uongo, zengwe etc, etc.

3. Siasa na Migogoro
Hizi naziita ni siasa za attention seeking, yaani kupinga tuu kila kitu ili tuu kuonekana na kutafuta public sympathy, lakini hizo moves hazina faida yoyote wala manufaa yoyote ya maana!. Hapa ndio pale watu wanapinga kila kitu hata kile chenye manufaa kwao kwa lengo la kutafuta tuu mgogoro. Siasa hizi hufanywa sana kwa mikutano ya hadhaa na maandamano ambayo hayana manufaa yoyote!.

Mfano hai ni hii kampeni ya UKUTA!, Rais Magufuli ambaye kweli ni dikiteta, amevunja katiba kwa kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara kinyume cha katiba!. Chadema wanasema wao wataandamana na kufanya mikutano nchi nzima!. Lengo la mikutano hii na maandamano wameiita kupinga udikiteta nchini!. Sasa kitakachofanyika kwenye mikutano hiyo na maandamano ni mabango na kauli chonganishi kuupinga udikiteta ili wananchi waone Chadema inapinga udikiteta wa Magufuli!. Kupinga huku ni kwa kujifurahisha tuu, kwa sababu hakutabadilisha lolote wala chochote katika udikiteta wa Magufuli, sana sana Magufuli atawatandika tena kwa kutumia "za moto" japo taarifa ya polisi itasema ni rubber bullets, na miili ya baadhi ya wataotandikwa, itachukuliwa na polisi na ku vanish into thin air!, hakuna atakayejua nini kiliwasibu!.

SMART politics kwenye kuupinga udikiteta wa Magufuli, ni kwa kutumia katiba na sheria, imeeleza wazi nini kinachotakiwa kufanywa pale kiongozi aliyeapa kuilinda katiba, akawa ndie wa kwanza kuivunja hiyo katiba!. Mikutano ya hadharra na maandamano sio njia sahihi ya kudeal na udikiteta wa mkuu wa nchi, haswa ukizingatia dikiteta mwenyewe, ni dikiteta mzalendo!, hicho anachofanya rais Magufuli, ndicho wananchi wanachotaka na ndicho kinachoweza kufanyika kututoa hapa tulipo, na kutufikisha kule tunakotaka kwenda!.

Kama ulifuatilia ule mkutano wa Chadema wa Mwembe Yanga, ulioitangaza list of shame, Katibu Mkuu wa Chadema na viongozi wote walikuwa wakali sana kuhusu rushwa na ufisadi, huku wakiendesha siasa za uanaharakati. Miongoni mwa sala za wanahaakati ni kumuomba Mungu, atupatie rais dikiteta mwenye uwezo wa kudeal na rushwa na ufisadi!. Mungu katusikia sala zetu, katupatia rais dikitate kweli, John Pombe Magufuli!, sasa wale wale waliokuwa wakipinga rushwa na ufisadi, sasa ndio wamewakumbatia mafisadi wale wale wa kwenye list of shame na sasa ndio wanaopiga kelele kulaani rais dikiteta!.

Pasco
 
Chonde Chonde ndugu zetu wa Chadema, ili chama chenu kifanikiwe, ni lazima sana mjifunze kubadilika na wakati!, sasa tuko kwenye wakati tofauti, JK alikuwa ni mtu wa mchezo na kiukweli, tulimchezea sana!. Magufuli sio mtu wa mchezo mchezo, huyu ni mtu wa kazi tuu!, hataki mchezo!. Sasa Chadema pia ibadilike ifanye kazi ya siasa na sio kuendelea kucheza michezo ya siasa!, jamaa hataki mchezo!, nasisitiza wito wangu humu, msishindane na mwenye nguvu!, mwenye nguvu mpishe!.

Pasco
 
THEN KWA KIFUPI PASCO HAKUNA HAJA YA VYAMA VINGI UNTIL 2020
Vyama vingi ni wakati wa uchaguzi au uchaguzi mdogo, uchaguzi ukiishaisha sasa ni wakati wa kufanya kazi, kazi tuu!.

Pasco
 
Mkuu Danny, nakubaliana na wewe, dawa ya adui sii kumkimbia au kumpisha bali kukabiliana nae, na hata kama utaangamia katika kukabiliana huko, na kupoteza maisha, jina lako ndilo litabaki kama shujaa, cha muhimu cha kujiuliza, ni nani muhimu zaidi kati ya shujaa mfu, au mfungwa hai aliye gerezani?!, au aliyejificha mwituni?!.

Kwa maoni yangu, kama unakiona kifo kile, halafu unakikimbilia na kufa tuu ili uonekane shujaa, wewe ni shujaa mjinga!. Kama unataka kushindana au kupigana na mtu mwenye nguvu zaidi yako, hivyo unaingia kwenye mapambano ili hali unajua utawawa, wewe pia ni shujaa mjinga!. Shujaa mwerevu ni yule ambaye hawezi kuingia kwenye vita ambayo anajua atashindwa!, bali atampisha huyo mwenye nguvu, huku yeye akijijenga mpaka awe na nguvu za kukabiliana na kushinda!.

Naomba take time kasome bandiko langu hili, utanielewa ninamaanisha nini
Tuko Vitani Tuna Wapiganaji Shupavu, Wapiganaji Makini na ...

Pasco
Kwa maneno yako,nchi nyingi leo zisingekuwa huru!Kuna watu walienda kupigana Vita wakijua hawatapona lakini uhuru utapatikana!
 
Vyama vingi ni wakati wa uchaguzi au uchaguzi mdogo, uchaguzi ukiishaisha sasa ni wakati wa kufanya kazi, kazi tuu!.

Pasco
Pasco mwaka 2025 jamaa akiamua atagombea tena kwa mabavu na kuvunja katiba,tutulie tu!Akishindwa akajitangaza mshindi tutulie tu kisa mkubwa ana jeshi?
 
Ni kweli kabisa Pasco kuwa Rais wetu ni Dikteta!! Lakini ni dikteta ambaye hataki kuitwa dikteta!!.
Mengi sana tutayaona!!
Pasco unasema jamaa wasiandamane je wafanye nini ili uhuru huu na haki wanayopigania vipatikane!!!!!????
 
Pasco anatumika vibaya sana sijui ni kwa hicho kibarua anachopewa?
Mkuu , Pasco wa jf ni independent, hatumwi na mtu!, hivyo situmiki vibaya kwa sababu situmwi na yeyote!. Labda useme najitumia vibaya!.

Pasco
 
Ushauri umefika!!


Wanabodi,

Kama kawaida yangu kutoa ushauri wa bure, huu ni ushauri wa bure kwa Chadema, japo kuandamana na mikutano ya kisiasa ni haki iliyotolewa kihalali ndani ya katiba, nawashauri kwa dhati kabisa, tafadhalini sana msiandamane, na kusitisha hiyo Operesheni UKUTA, ili kuutumia ule msemo wa Kiswahili "Mwenye nguvu mpishe", hata kama una haki, usitake kujipima nguvu kwa kutunishiana misuli na mtu mwenye nguvu zaidi yako, na sio tuu ana nguvu zaidi yako, na tayari, umeishajua ni dikiteta, bali ndio mwenye nguvu ya dola mikononi mwake!.

Misingi ya Katiba na The Rule of Law
Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya katiba na sheria, (the rule of law) ambapo inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa matamko ya viongozi yanayokwenda kinyume cha katiba!.

The Separation of Powers & Check and Balance .
Nchi yetu ina mihimili mikuu mitatu, Serikali, (the executive), Bunge (The Legislature) na Mahakama (The Judiciary). Mihimili hii mitatu, ilipaswa kufanya kazi kwa kujitegemea bila mhimili mmoja kuingilia mhimili mwingine (independence), huki kila mhimili uki act as a watchdog wa muhimili mwingine usivuke mipaka ya madaraka au mamlaka yake yaani (The sepaation of powers check and balance).

Serikali yenye Nguvu, Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo!.
Mihimili hii, inaongozwa na viongozi ambao wana mamlaka kuu kuhusu mihimili yao. President ndio mkuu wa the executive, Spika ndio mkuu wa The Legistlatue, na Jaji Mkuu, ndie mkuu wa The Judiciary, lakini pamoja na nia njema kuwa mihimili yote inamamlaka na hakuna mhimili wowote uliokuwa unapaswa kuwa na mamlaka kuliko mhimili mwingine, lakini kiukweli, mhimili wa the executive ndio mhimili mkuu unaomiliki vyombo vya dola na kuitawala mihimili mingine yote!, hivyo mkuu wa the executive, yaani rais, ndio kila kitu!, akisema!, amesema!.

Rais Magufuli na Uvunjaji wa Katiba.
Tuambiane ukweli, tangu rais Magufuli ameingia madarakani, sio mara moja au mbili amekuwa akitoa kauli tata, zinazokwenda kinyume cha katiba, mhimili wa Bunge na Mahakama ilipaswa kuingilia kati kwa kumcheck mkuu wa the executive, lakini vyombo hivyo vimekaa kimya hivyo kumfanya rais ajisikie kuwa he is always right! kwa kanuni ya "the boss is always right!".

Udikiteta wa Magufuli.
Hoja kama Magufuli ni dikiteta au la, haina mjadala, Magufuli ni dikiteta wa ukweli ambaye hana msalie mtume, na alipoingia tuu madarakani, alianza kuonyesha udikiteta wake right away kwa kuliingilia bunge na mahakama kuziweka chini ya amri zake!. Lile katazo lake la watumishi wa umma hawaruhusiwi kusafiri safari za nje bila kibali chake kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, liliwahusu watumishi wote wa serikali, likiwemo bunge na mahakama!, just imagine Jaji Mkuu na Spika wa bunge wakapige magoti kwa rais kuomba kutimiza wajibu wao!.

Baada ya katazo lile, checks and balance zingepaswa kuanzia hapo kwa Jaji Mkuu kumweleza rais huko ni kuingilia uhuru wa mahakama (the independence of the judiciary) hivyo muhimili wa mahakama haukupaswa kujisubmit chini ya the executuve, bali mamlaka hayo ya kuzuia safari za nje, Spika alipaswa kuwa nayo kudhibiti safari za mhimili wa bunge, na Jaji Mkuu alipaswa kuwana nayo kudhibiti safari za mhimili wa mahakama, lakini mihimili hii ilikaa kimya kwa kujisubmit chini ya the executive, hivyo kumfanya rais ndio kila kitu!.

Hivyo sasa rais Magufuli ndio kila kitu, hakuna cha bunge, mahakama, wala katiba, amri ya rais ndio kila kitu na ndio sheria kuu!, hivyo nawashauri Chadema kwa dhati kabisa, wasitishe maandamano yao, wasifanye kabisa mchezo wa kumjaribu Ngosha, wataumia bure!.

Hili la udikiteta wa rais Magufuli, tumeisha lizungumza sana humu
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya ...
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote | Page ...
Nimetishwa, Kushitushwa na Kuogopeshwa na Kauli Hii ya Rais ...
Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ...
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...

Ila kitu kimoja kuzuri kuhusu udikiteta wa rais wetu, ni Rais Magufuli ni dikiteta mzalendo!, mwenye uchungu na umasikini wa nchi hii, mwenye nia njema ya kusafisha uozo wote wa uzembe, rushwa na ufisadi, na kulikomboa taifa letu toka kwenye lindi la umasikini uliotopea na kuwa nchi ya maziwa na asali kupitia uchumi wa gesi na viwanda.

Mungu mbariki Magufuli!.

Mungu ibariki Tanzania.

Wasalaam.

Pasco
Rejea za shauri za bure
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa ...
Ushauri wa Bure kwa CCM: Hope for the best but get prepared for ...
Ushauri wa Bure kwa Mhe. Lowassa: Ili kuilinda Heshima yako ...
Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep ...
Ushauri wa Bure Kwa Hon Dr. Harison Mwakyembe (Mb)-Kwa Hili la ...
Ushauri wa Bure Kwa Mhe. Zitto on Escrow Report: Please Keep Quite ...
Ushauri wa Bure kwa CHADEMA: Heri Nusu Shari Kuliko Shari Kamili ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Magufuli, Futilia Mbali Utawala wa Sheria ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Usikanyage Arumeru!, Atamponza Sioi!.
Ushauri wa Bure kwa Dr. Shein: Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ...
Ushauri wa Bure kwa Magufuli, DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es ...

[/QUOT

Nafikiri ndugu pasco mshauri anayekosea, ukawa waendelee na operesheni ya kumtoa nyoka
 
Ritz ni bora Ben ateswe mpaka kufa kuliko afe kwa ngoma alafu tuone aibu kusema marahemu hakuvaa condom
 
Mkuu Kitaturu, kuna siasa za aina tatu, siasa za maendeleo, (developmental politics), siasa za kujifurahisha (politics of politiking), na kuna siasa za migogoro, (politics of confrontation).

1. Siasa za Maendeleo.
Hizi ni siasa zenye malengo ya kuleta mabadiliko chanya, changing for the better. Kila political move unayofanya, ila malengo chanya ya kuleta mabadiliko, siasa hizi zimefundishwa sana na Mwalimu Nyerere katika kitabu chake cha Binadamu na Maendeleo. Siasa hizi ni siasa zenye sera, ilani, malengo, mikakati na time frame, hizi mimi naziita SMART Politics, ni siasa zenye
S - specific, significant, stretching
M - measurable, meaningful, motivational
A - agreed upon, attainable, achievable, acceptable, action-oriented
R - realistic, relevant, reasonable, rewarding, results-oriented
T - time-based, time-bound, timely, tangible, trackable

2. Siasa za Kujifurahisha.
Hizi ni kauli za kisiasa kwa ajili ya kujifurahisha tuu to gain political mileage lakini hakuna chochote kinachofanyika, hizi zinajumlisha ahadi zisizotekeleka, hizi ni politiking, mtu unazungumza ili tuu uonekane na wewe upo upo. Kwenye kundi hili, zile siasa za bendera fuata upepo pia zimo kwenye kundi hili. Hizi ni siasa ambazo hazina maana yoyote kwa maendeleo!, huku ndiko siasa za fitna, majungu, uongo, zengwe etc, etc.

3. Siasa na Migogoro
Hizi naziita ni siasa za attention seeking, yaani kupinga tuu kila kitu ili tuu kuonekana na kutafuta public sympathy, lakini hizo moves hazina faida yoyote wala manufaa yoyote ya maana!. Hapa ndio pale watu wanapinga kila kitu hata kile chenye manufaa kwao kwa lengo la kutafuta tuu mgogoro. Siasa hizi hufanywa sana kwa mikutano ya hadhaa na maandamano ambayo hayana manufaa yoyote!.

Mfano hai ni hii kampeni ya UKUTA!, Rais Magufuli ambaye kweli ni dikiteta, amevunja katiba kwa kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara kinyume cha katiba!. Chadema wanasema wao wataandamana na kufanya mikutano nchi nzima!. Lengo la mikutano hii na maandamano wameiita kupinga udikiteta nchini!. Sasa kitakachofanyika kwenye mikutano hiyo na maandamano ni mabango na kauli chonganishi kuupinga udikiteta ili wananchi waone Chadema inapinga udikiteta wa Magufuli!. Kupinga huku ni kwa kujifurahisha tuu, kwa sababu hakutabadilisha lolote wala chochote katika udikiteta wa Magufuli, sana sana Magufuli atawatandika tena kwa kutumia "za moto" japo taarifa ya polisi itasema ni rubber bullets, na miili ya baadhi ya wataotandikwa, itachukuliwa na polisi na ku vanish into thin air!, hakuna atakayejua nini kiliwasibu!.

SMART politics kwenye kuupinga udikiteta wa Magufuli, ni kwa kutumia katiba na sheria, imeeleza wazi nini kinachotakiwa kufanywa pale kiongozi aliyeapa kuilinda katiba, akawa ndie wa kwanza kuivunja hiyo katiba!. Mikutano ya hadharra na maandamano sio njia sahihi ya kudeal na udikiteta wa mkuu wa nchi, haswa ukizingatia dikiteta mwenyewe, ni dikiteta mzalendo!, hicho anachofanya rais Magufuli, ndicho wananchi wanachotaka na ndicho kinachoweza kufanyika kututoa hapa tulipo, na kutufikisha kule tunakotaka kwenda!.

Kama ulifuatilia ule mkutano wa Chadema wa Mwembe Yanga, ulioitangaza list of shame, Katibu Mkuu wa Chadema na viongozi wote walikuwa wakali sana kuhusu rushwa na ufisadi, huku wakiendesha siasa za uanaharakati. Miongoni mwa sala za wanahaakati ni kumuomba Mungu, atupatie rais dikiteta mwenye uwezo wa kudeal na rushwa na ufisadi!. Mungu katusikia sala zetu, katupatia rais dikitate kweli, John Pombe Magufuli!, sasa wale wale waliokuwa wakipinga rushwa na ufisadi, sasa ndio wamewakumbatia mafisadi wale wale wa kwenye list of shame na sasa ndio wanaopiga kelele kulaani rais dikiteta!.

Pasco
Naona Maelezo yako Pasco hayajakata kiu,umepita juu juu tu ukikwepa swali la msingi!Mpaka ikafikia wananchi wakataka mabadiliko hata wagombea wote wakaimba mabadiliko ni kutokana na mambo kwenda hovyo awamu ya 4!Wananchi walijua udhaifu huo wa serikali kupitia hasa kwa wapinzani hasa CDM ambao walifanya mikutano kuwaamsha wananchi!Nakumbuka Zitto aliingia matatizoni ikiwa kufungiwa ubunge kwa miezi 5 alipoibua sakata la buzwagi na mirahaba,Dr slaa alichachamaa kukosoa serikali hasa kwa ufisadi!Ni kwa mambo hayo wananchi wakaona wanahitaji mabadiliko!Kama JK angekuwa Dikteta kama JPM angeweza kuwazuia kina Dr slaa na wapinzani kwa kuzuia mikutano yao na kuwachapa risasi pale wanapokaidi!Na nina uhakika hilo lingefanyika wananchi wasingejua uovu wa serikali!Kwahiyo movement zile ziliwaamsha watanzania!Impact yake ikaonekana kwenye uchaguzi baada ya kuwa na mchuano mkali!
Siasa unayofanya Leo sio lazima ikupe matokeo papo kwa papo!Unaweza Fanya jambo leo lakini ukategemea results hapo baadaye kama mtawala hatojirekebisha!So unaposema Ukuta haina impact unajidanganya au huna uelewa wa kutosha!Movement hiyo itawapa awareness wananchi juu ya nini kinaendelea na kuwapa tahadhari ya kuwa na viongozi wa namna hiyo!Nkirunzinza alianza taratibu,akanogewa sasa anang'ang'ania madaraka!Hii inaweza kuwajenga kwa ajili ya uchaguzi ujao!
 
Pasco mwaka 2025 jamaa akiamua atagombea tena kwa mabavu na kuvunja katiba,tutulie tu!Akishindwa akajitangaza mshindi tutulie tu kisa mkubwa ana jeshi?
Mkuu Bomee, kama katiba yetu inasema mwisho ni vipindi viwili, mwisho ni vipindi viwili, ni kichaa tuu pekee anayeweza kuona mwisho ni vipindi viwili, akataka kugombea kipindia cha tatu!.

Ila pia katiba sio Biblia au Msahafu, inaweza kubadilishwa wakati wowote!, katiba ni yetu sisi Watanzania kwa ajili yetu, tukimuona Magufuli ni mzuri sana, na taifa bado linamuhitaji, tutaibadili katiba, kukiondoa hicho kipengele cha mwisho ni vipindi viwili vya miaka 5 mitano, na badala yake, tuweke mwisho vipindi viwili vya miaka 10 kumi!, tena kwa uzoefu hakuna rais amewahi kutumikia kipindi kimoja tuu, lazima vitimie viwili, then tunaweza kabisa kuamua 2020 hakuna haja ya uchaguzi wa rais, ni wastage of time, money na resources, Magufuli anatosha!, na baada ya hapo tukaamua endelee, kuna ubaya gani?!.

Nisome hapa
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020 ...

Pasco
 
Mkuu Bomee, kama katiba yetu inasema mwisho ni vipindi viwili, mwisho ni vipindi viwili, ni kichaa tuu pekee anayeweza kuona mwisho ni vipindi viwili, akataka kugombea kipindia cha tatu!.

Ila pia katiba sio Biblia au Msahafu, inaweza kubadilishwa wakati wowote!, katiba ni yetu sisi Watanzania kwa ajili yetu, tukimuona Magufuli ni mzuri sana, na taifa bado linamuhitaji, tutaibadili katiba, kukiondoa hicho kipengele cha mwisho ni vipindi viwili vya miaka 5 mitano, na badala yake, tuweke mwisho vipindi viwili vya miaka 10 kumi!, tena kwa uzoefu hakuna rais amewahi kutumikia kipindi kimoja tuu, lazima vitimie viwili, then tunaweza kabisa kuamua 2020 hakuna haja ya uchaguzi wa rais, ni wastage of time, money na resources, Magufuli anatosha!, na baada ya hapo tukaamua endelee, kuna ubaya gani?!.

Nisome hapa
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020 ...

Pasco
Kwa hali hii waandishi kuna haja ya kuangaliwa upya taaluma zenu au mfumo wa upatikanaji elimu yenu!Si bure,kuna tatizo sehemu!
 
Kwa hali hii waandishi kuna haja ya kuangaliwa upya taaluma zenu au mfumo wa upatikanaji elimu yenu!Si bure,kuna tatizo sehemu!
Hakuna tatizo lolote, sifa ya kuwa mwandishi ni kujua tuu kusoma na kuandika!, mimi elimu yangu ni daasa la saba la UPE na nilipasi ili sikuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari!. Kuwa mwandishi hukitaji elimu yoyote zaidi ya kujua kuandika!. Tatizo ni nini?!, niliposema katiba sio Msahafu, tuibadili kutoka vipindi 2 ya miaka 5 hadi vipindi 2 vya miaka 10?!.

Pasco
 
Mkuu Pasco!
Kwani itakuwa ni Kuandamana nchi nzima au Kuandamana kuelekea wapi na kwa nani alafu ili iweje?
Isije ikawa unafahamu/umeelezwa mbinu ya kuandamana, kumbe maana ikawa nyingine kabisa.
Binafsi nauona ufisadi unaofanywa na wanasiasa kuilazimisha serikali kutumia gharama kulinda Amani ya nchi.
Kwa muktada huo watu watapigwa kwa kodi zao na huku wengine wakilipwa kwa kodi zao na wengine kufurahia kuzidi kuaminiwa na wakubwa /wafadhili wao.
Siasa ni mchezo hatari unaotumia watu kama ngao dhidi ya wengine ili wachache wafurahi na wengi watakaofurahi ni lazima jasho liwatoke.
Aisee ni hatari sana!
 
Hakuna tatizo lolote, sifa ya kuwa mwandishi ni kujua tuu kusoma na kuandika!, mimi elimu yangu ni daasa la saba la UPE na nilipasi ili sikuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari!. Kuwa mwandishi hukitaji elimu yoyote zaidi ya kujua kuandika!. Tatizo ni nini?!, niliposema katiba sio Msahafu, tuibadili kutoka vipindi 2 ya miaka 5 hadi vipindi 2 vya miaka 10?!.

Pasco
Kama katiba inaweza badilishwa ili kukidhi. haja za mtu fulani aweze kuendelea kuongoza tutakuwa tunajenga picha gani kwa viongozi wa bàadaye?Huoni kuwa kuna risk ya kumwaga damu kama Burundi?Namaanisha siku tukipata Rais ambaye ameshaona hayo yanawezekana si anaweza tumia nguvu yake kijeshi na kupeleka katiba bungeni ibadilishwe!Hawezi shindwa hasa akiwa na wabunge wengi!Hata kura ya maoni atatumia power yake kubatilisha kama mambo yakienda kombo!Mambo haya sio yakufanyia mzaha Pasco,hasa kwa mtu wa taaluma yako!
 
Kama katiba inaweza badilishwa ili kukidhi. haja za mtu fulani aweze kuendelea kuongoza tutakuwa tunajenga picha gani kwa viongozi wa bàadaye?Huoni kuwa kuna risk ya kumwaga damu kama Burundi?Namaanisha siku tukipata Rais ambaye ameshaona hayo yanawezekana si anaweza tumia nguvu yake kijeshi na kupeleka katiba bungeni ibadilishwe!Hawezi shindwa hasa akiwa na wabunge wengi!Hata kura ya maoni atatumia power yake kubatilisha kama mambo yakienda kombo!Mambo haya sio yakufanyia mzaha Pasco,hasa kwa mtu wa taaluma yako!
Bomee, kwani kuna first and hard rules utawala uwe ni miaka mitano mitano? . Mbona Marekani ni miaka 4 tuu? na Uingereza ni miaka 6?. Nimekupa froof kuwa hakuna rais wa Tanzania aliyekaa miaka 5 tuu, hivyo tunaweza kuamua vipindi vyetu viwe ni miaka 10! .

Katiba ni yetu na sio Msahafu hivyo ni rucksa kuibatilisha wakati wowote wa hitaji la mabadiliko! .

Pasco
 
Unachembechembe za mwanamke sio bure....nmerudia kuusoma huu uzi kutokan na kuanzisha uzi mwingine unaosema utakwenda kuandaman nmebaki kushangaaa kama kweli wew wakiume sijapata jibu...wew na kubenea hamna tofauti
 
Unachembechembe za mwanamke sio bure....nmerudia kuusoma huu uzi kutokan na kuanzisha uzi mwingine unaosema utakwenda kuandaman nmebaki kushangaaa kama kweli wew wakiume sijapata jibu...wew na kubenea hamna tofauti
Dino, pole sana kwa kutokunielewa, tatizo ni uwezo na viwango vya uelewa!. Watu wa levels tofauti za uelewa wanahitaji times tofauti kusoma jambo na kulielewa, nenda kasome tena bandiko lile huku umetulia, ukijiona bado hujaelewa, then utakuwa hujafikia level ya uelewa wa bandiko lile !.

Pole tena.

Pasco
 
Back
Top Bottom