Angalia usimponze Invisible kutakiwa kwa lazima kuwasilisha jina la mmiliki wa title ya Gavana humu jf , na kuliwasilishwa kunahusika ili kufanyiwa uchunguzi asije kuwa ni member wa vikosi vyetu, pia kutafutwa kwa kufanyiwa mahojiano marefu kuhusu posti aliyoipost jf kumtishia Magufuli kuwa asiringie majeshi , na kwamba kunauwezekano kumkuta kilichomkuta Karume Snr na Kabila Snr kwa kuondoshwa na anaowaamini!. Hivyo wakati tukisubiria wale 'jamaa zetu' kumjua Gavana ni nani, tunashauri rais Magufuli afanye pangua pangua ya mabadiliko ya haraka ya vile vikosi vyake vya ulinzi mapema, kwa kuwa weka pembeni walinzi wote waliopo, kama Gavana ni mmoja wao, au type ya hao Gavana aliyowazungumzia, kama wapo ili wasiweze kuleta madhara yoyote, na badala yake, sasa rais wetu alindwe na kikosi maalum cha sungusungu wa Ng'wana Ngosha kutoka Chato?!.
Pasco