LGE2024 Ushauri kwa CHADEMA: Susieni uchaguzi wa serikali za mitaa

LGE2024 Ushauri kwa CHADEMA: Susieni uchaguzi wa serikali za mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Kutokana na Hali iliyojitokeza jana , nashauri ya kwamba CHADEMA watangaze kususia uchaguzi Mkuu ujao na uchaguzi wa Serikali za mitaa. Hii ni kutokana kwamba Serikali kupitia polisi imeshaonesha biasness na kwamba uhalifu wowote dhidi ya CHADEMA polisi hawatashughulika nao.

Itakuwa ni aibu kwa CHADEMA kuaminika kwamba TAMISEMI chini ya mkwe wa Rais ambaye ana mamlaka juu ya polisi atakuwa na haki kwa CHADEMA kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Nashauri ya kwamba kwa jinsi polisi walivyojipanga Jana dhidi ya CHADEMA ni onyo kwa CHADEMA kwamba haitaruhusiwa kukaribia madaraka ya Rais na kwamba polisi wapo tayari hata kuua ili tu CCM ibaki madarakani.

CHADEMA ijiulize Kama Mzee Ally Kibao kauawa kikatili na hakuna yeyote aliyewajibishwa, Soka kapotea mazima, hakuna wakuwajibishwa. Kama uhai wa mtu haupewi thamani yake sembuse kura kwenye uchaguzi.

CHADEMA itangaze hadharani kwamba haitashiriki chaguzi zozote hapa Tanzania mpaka haki ya waliopotea na kuuawa inapatikana.
 
Hilo ni moja la kuzingatiwa. Mimi naamini tatizo la watanzania ni kila mmoja kujigeuza mchambuzi huku kazi kubwa ikiachwa kwa viongozi wa kisiasa pekee.

Fikiri Lema kakamatwa kwenye ndege, hakuna abiria au mfajyakazi aliyetoa taarifa hii. Lakini wakiingia humu watakwambia maandamano yameshindwa kwa sababu.
 
Kutokana na Hali iliyojitokeza jana , nashauri ya kwamba CHADEMA watangaze kususia uchaguzi Mkuu ujao na uchaguzi wa Serikali za mitaa. Hii ni kutokana kwamba Serikali kupitia polisi imeshaonesha biasness na kwamba uhalifu wowote dhidi ya CHADEMA polisi hawatashughulika nao.

Itakuwa ni aibu kwa CHADEMA kuaminika kwamba TAMISEMI chini ya mkwe wa Rais ambaye ana mamlaka juu ya polisi atakuwa na haki kwa CHADEMA kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Nashauri ya kwamba kwa jinsi polisi walivyojipanga Jana dhidi ya CHADEMA ni onyo kwa CHADEMA kwamba haitaruhusiwa kukaribia madaraka ya Rais na kwamba polisi wapo tayari hata kuua ili tu CCM ibaki madarakani. CHADEMA ijiulize Kama Mzee Ally Kibao kauawa kikatili na hakuna yeyote aliyewajibishwa, Soka kapotea mazima, hakuna wakuwajibishwa. Kama uhai wa mtu haupewi thamani yake sembuse kura kwenye uchaguzi.

CHADEMA itangaze hadharani kwamba haitashiriki chaguzi zozote hapa Tanzania mpaka haki ya waliopotea na kuuawa inapatikana.
Kwanza hapatakua na athari zozote za kikatiba, kisiasa au kidemokrasia nchini, ikawa ushauri huo utapokelewa na kutekelezwa vyema na Chadema, na kwahivyo vyama vingine vyenye uwezo vinaweza kushiriki uchaguzi huo bila mbambamba yoyote.

Infact, Tanzania kuna vyama vya kisiasa zaidi ya 22 vyenye usajili wa kudumu, na kwakweli hiyo itakua fursa ya kipekee sana kwa vyama hivyo vya siasa, kuvuna wanachama na kura za wanachadema waerevu, wenye fikra huru na wanaofahamu vyema haki na wajibu wao katika maamuzi ya uongozi wa nchi na uongozi wa maeneo wanakoishi.

Itakua ni fursa muafaka sana kwa wanachadema waliochoshwa na ngonjera za uongozi wa chama chao uliopo sasa , ambao umekosa kabisa mawazo mapya wala fikra mbdala, zenye kuwatia matumaini wanaChadema na wananchi kwa ujumla, bali daima wamekua wakiwavunja moyo na kuwakatisha tamaa wanachadema , kwa mipango na uelekeo wa kukurupuka na usio eleweka..

Hiyo itakua Fursa ya pekee sana na muafaka kwa viongozi waandamizi wa Chadema waliopo madarakani sasa, kuondoka uongozini mara moja, kwa kushindwa kwao kazi ya kusimamia misingi na malengo ya kuanzishwa kwa Chadema..

Hata hivyo, kuzira, kususaa, kuandamana au kugomea jambo lolote humu nchini, hakujawahi kuisaidia Chadema au wananchi kitu chochote, na hivyo huu utakua ni muendelezo wa ushauri au maamuzi ya hovyo na mabovu zaidi katika historia ya Chadema..

Naunga mkono hoja 🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Mambo ya kususa yamepitwa na wakati. Shiriki uchaguzi uhalisia uthihirike kuanzia mchakato hadi uchaguzi na matokeo ya uchaguzi. Hata hivyo hitaji la Katiba mpya ni muhimu na mazungumzo yaendelee kuhusu Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
 
Kutokana na Hali iliyojitokeza jana , nashauri ya kwamba CHADEMA watangaze kususia uchaguzi Mkuu ujao na uchaguzi wa Serikali za mitaa.
Hizi zitakuwa ni hasira za mkizi!, unamsusia ngedere shamba la mahindi...

Siasa zetu ni siasa kiti cha basi, unaposhuka, wanakaa wenzio, ukisusa, sie twala!.

P
 
Kususa sizani kama ni njia sahii kwa chama cha siasa,kwani hakuna, kinayempotezea nafasi na, ushawishi zaidi ya, wao wenyewe mm nazani wao hao chadema, lazima wakae waone wanafanyaje reformation ambayo inaweza zaa vijana wafia chama na vijana wenye mawazo mbadala.

labda tujiulizeswali saizi vpi chadema kwa sasa wanauwezo wa kuandaa vijana wenye uwezo wakujenga hoja kama zamani? Kama,yupo basi ni muda muafaka wa kubadilisha huyo mtu mana, ameshindwa, kuandaa vijana wanao weza, jua, falsfa, na itikadi vizri ya chama.

Jaribu kufatilia kunzia vyuoni vijana,wa TAHILISO wengi ni wasifiaji vp platform yao CHASO inafanya kazi zake kweli kila mkoa au limebki jina tu?
 
Hilo ni moja la kuzingatiwa.
Mimi naamini tatizo la watanzania ni kila mmoja kujigeuza mchambuzi huku kazi kubwa ikiachwa kwa viongozi wa kisiasa pekee.
Fikiri Lema kakamatwa kwenye ndege, hakuna abiria au mfajyakazi aliyetoa taarifa hii. Lakini wakiingia humu watakwambia maandamano yameshindwa kwa sababu....

Umeongea ukweli kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom