Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Mimi niliomba scholarship sasa kimbembe passport kuanzia ofisi unayofanyia kazi ukimwambia HR niandikie barua ya kupata passport mtu anahisi unaenda Ulaya kesho
Ukienda ofisi za Uhamiaji nako mbinde ila thanks Lord nilimpata rafiki akanielekeza km unataka kuipata haraka passport.
Nimeipata tena passport kubwa ya miaka kumi kilichobaki ni ku apply scholarship mpaka usiku wa manane Halmashauri kumenichosha mwenzenu.
Ulitùmia njia ipi iliyo rahisi zaidi mkuu?
Na gharama ulitumia kama kiasi gani?
 
Mkuu, nchi zote za ulaya, Asia na America huendi bila kuwa na English proficiency test...kwa wale wanaoenda kwa ajili ya shule lazima uambatanishe cheti hicho ili uweze ku-qualify. Kuhusu hiyo mitihani, zamani walikuwepo jamaa wa British Council na walikuwa ndo wanatoa mitihani hiyo (TOEFL)...kama uko tz/Dar..jaribu kuwacheki hawo jamaa wa British Council wanaweza saidia kidogo....
British Council bado wanafanya hizo mishe iseee, mwaka jaña mwanzoni walitutembelea chuoni kutupa baadhi tu ya hizo mambo+scholarships za petroleum engineering. Kuna jamaa ninayo mawasiliano yake yuko pale anaitwa Mpoki.
 
Mkuu, nchi zote za ulaya, Asia na America huendi bila kuwa na English proficiency test...kwa wale wanaoenda kwa ajili ya shule lazima uambatanishe cheti hicho ili uweze ku-qualify. Kuhusu hiyo mitihani, zamani walikuwepo jamaa wa British Council na walikuwa ndo wanatoa mitihani hiyo (TOEFL)...kama uko tz/Dar..jaribu kuwacheki hawo jamaa wa British Council wanaweza saidia kidogo....
Hivi hata kwenda kwaajili ya kufanya kazi inabidi pia uwe umefanya huo English Proficiency Test?
 
Naombeni ushauri kuhusu SWEDEN ndugu zangu, mimi natarajia kwenda huko soon,vipi maisha ya Sweden na mazingira kwa ujumla?,nataka kwenda kuishi Stockholm
 
Naombeni ushauri kuhusu SWEDEN ndugu zangu, mimi natarajia kwenda huko soon,vipi maisha ya Sweden na mazingira kwa ujumla?,nataka kwenda kuishi Stockholm
Sweden kuzuri sana, maisha yako poa. Karibu Scandinavia.
 
Naomben kujua waungwana ivi kujaza fomu ya paspot pale kwenye taarifa za safar ni lazima kujaza maana mm sina mualiko wowte kwa sasa ila nahitaji paspot
 
Kaka Izzo shida yangu kubwa kupata mtu wa kunipa mwaliko kwenda usa kwani huko nina mwenyeji ambae awezi kunialika yeye mwenyewe kaniambia nitafute mtu wa kunipa mwaliko kisha nitafikia kwa mtu wangu msaada wa mwaliko kaka
 
Lusungo Siyo Danga Nakufanya baby dady kabisa
nani asiyetaka kuitwa mama ghorofa hapa mjini
 
Mbinu nyepesi sana ya kufanikisha ndoto zenu coz naona wengi mnatamani kuja au kwenda Ulaya na US lakini njia mnayotumia ni ndefu ikiwamo ya ndoa za usanii siku hz wanafatilia sana na njia hii siku hz ni ngumu kwa sasa hv kwani siasa za sasa ni siasa za utengano na kufunga mipaka dhidi ya wageni
Ok njia ya kwanza ni kuingia nchi ya Malta ,Malta ndio nchi inayomkaribisha mgeni yeyote na yenye sheria nyepesi sana za uhamiaji kwa wananchi wanaotoka nchi za Commonwealth ( British colonisation)
So ukishafika Malta ukiweza kukaa ndani ya Malta ndani ya mwaka mmoja bila ya kufanya jinai huna haki ya kuomba uraia so kama utakuwa umekwenda kusoma , kufanya kazi, kutembea au kwenda kufanya kazi ya kujitolea (kazi za bila ya malipo)
Ukishapata uraia wa Malta unakuwa na uwezo wa kwenda kufanya kazi nchi yeyote ya Ulaya kwani Malta ni nchi iliyo kwenye jumuhiya ya Ulaya
So kama unabahati unaweza kupata lakini nchi nying za ulaya au nchi za dunia ya kwanza kupata kazi kwa elimu uliyosomea Africa ni ngumu sana mpaka usome kwao ndio wanakuamini
Owk kama utakuwa uko vizuri kiafya unaweza kwenda Jeshini ,nchi nyingi za ulaya zinachukua raia wa nchi za ulaya kama wanajeshi au kama umetoka nje ya jumuhiya ya ulaya ni lazima upate parmanent resident kitu ambacho ni kigumu sana kukipata kwa nyinyi mnaokuja huku kiujanja janja
Nchi zinazochukua raia wa nchi nyingine kwenye majeshi yao nitakuja na list yao muda si mrefu
lakini ni nchi ambazo zipo kwenye kundi la A list duniani zikiwamo nchi zote za Scandinavian
Ushaingia jeshini ,majeshi mengi ya Ulaya wanapaga watu ambao si raia wa nchi hyo mkataba miaka mitano mitano ndani ya hyo miaka mitano unaruhusiwa kusoma chochote utakachopenda gharama ni za jeshi so utachagua cha kusoma kama umetoka bongo na ka degree chako utasoma masters kama umetoka manyoya utatafuta cha kusoma ndani ya miaka mitano ni mingi sana na unapata faida mbili moja kulipwa mshahara ,huduma za Afya na uhakika wa kupata uraia kama utaitaji
So ukimaliza miaka mitano tu usiongeze tena mkataba ongeza tena kama umeipenda kazi ya jeshi so kama umeona ni manyoya unaiacha so unalipwa mafao yako na unakwenda kuomba uraia na unapata hata bila ya kufanya mtihani wa kuomba uraia na hii kuna nchi hawataki uraia pacha kama Germany au Norway so kama nchi hawataki uraia pacha basi unachagua mmoja ukishamaliza kupata uraia wa nchi hyo uliyoichagua ww from there unatafuta kazi kwa vyeti ulivyosomea jeshini na tena wakijua ulikuwa mwanajeshi wanakuheshimu sana kwani unaonekana umejitoa kwa nchi so unapata kazi na maisha yanaendelea ndani ya miaka 6 tu mission inakuwa imekwisha ukipita Airport ukionyesha gamba la mzungu unapita tu hupekuliwi pekuliwi kama mwenye passport ya Bongo
Kuna website ambazo watu kutoka sehemu zote za dunia wanatafuta watu wa kuja kumfanyia kazi ya kujitolea ambapo yeye atakupa chakula na sehemu ya kukaa bure kipindi chote utakachokuwa pale kwake mwaka mmoja tu ndani ya Malta bhasi
Lakini leo kunambia sijui mnapanga kuondoka kwenda nchi ambayo huna mwenyeji naona mnacheza nyinyi na mnadanganyana Ulaya na US ya sasa si kama ya zamani utaishia jela au kufa tena na balozi zenu zilivyo ngumu kwa raia wake utakoma na kujuta kuja tena mkuu wenu amesema muachwe njia nyepesi kabsa ndani ya miaka 6 tu umefanikisha mwaka mmoja Malta miaka 5 jeshini mwaka wa sita unapassport ya mzungu
Na hii ni kwa wanawake na wanaume sehemu pekee ni kufika Malta tu mwaka mmoja tatizo nililogundua Waafrica wengi akili yetu tunawaza ulaya tena zile nchi tajiri tu lakini mmeshindwa kujua dunia nzima wanawaza hvyo hvyo njia hii ya malta bado wengi awajaijua then tafuta mtu wa malta kafanye kazi ya kujitolea kwa mwaka mmoja kwanza unapata pa kukaa kula na mwenyeji lakini kwenda sehemu kwa mipango mipango mtakuwa mnadanganyana tu wanawake hasa wa Tanganyika wamekuwa wanaogapa sana kuchukua maamuzi ya kuondoka lakini nataka kuwambia tena wanawake ndio njia nyepesi sana kwani wazungu wanawaheshimu sana wanawake cha kwanza kwa heshima kwa wazungu
1 Wanawake
2 Mbwa au wanyama
3 Mwanaume
So kwa dada zangu kwa njia hii ya Jeshi ni bora sana kwao tena sana naongea hv kwa kujua ninachosem

Ningependa kuwambia ndugu zangu Watanganyika kwamba dunia ya sasa maendeleo yamehama kutoka kwenye nchi zinazoongea kingereza na kuhamia kwenye nchi ambazo haziongei kingereza kwani dunia nzima robo tatu wanajifunza au wanajua kingereza na target yao ni kwenda kukaa nchi zinazoogea kingereza sasa utakuta nchi zinazoongea kingereza zimeshajaa wahamiaji kibao lakini niwape siri kubwa kuwa nchi zisizo ongea kingereza zinaitaji sana watu kwani watu wamekuwa wakienda kwenye nchi zinazoongea kingereza

MALCOM LUMUMBA
Kaka Izzo mimi nilikuwa naomba msaada nipate mtu wa kunipa barua ya mwaliko kwenda usa,kule nina mtu wangu ambae awezi kunipa mwaliko kwa sababu tofauti so kanipa nafasi nipate mtu wa kunipa mwaliko kisha nikienda nitafika kwa mtu wangu msaada wako plz
 
Naomben kujua waungwana ivi kujaza fomu ya paspot pale kwenye taarifa za safar ni lazima kujaza maana mm sina mualiko wowte kwa sasa ila nahitaji paspot
Ni lazima kujaza Mkuu!!.
IMG_20180514_184941.jpg
 
Daah sasa kama huna kwa kipindi hiki unafnyaje mkuu maana nahitaji kua nayo..safr inakuja muda wowote mbeleni
Unaweza kutafuta/kutumia sababu nyingine tu Mkuu, kama utalii,biashara,michezo,dini nk,ilimradi ukidhi vigezo katika category husika,ilimradi umepata tu!!.
IMG_20180514_193403.jpg
 
Back
Top Bottom