Ushauri: Nchi gani ya Ulaya ni rahisi kupata visa na kazi?

Ushauri: Nchi gani ya Ulaya ni rahisi kupata visa na kazi?

Wadau mimi nahitaji kwenda Ulaya kutafuta maisha, nauli ninayo hivo naombeni ushauri kwa anaefahamu nchi gani in Europe ina urahisi wa kupata kazi yoyote pia urahisi wa visa pia mahali pa kufikia ????? Wadau naombeni msaada wenu kwa anaefahamu.
Ila nikushauri kitu mkuu, kuwa makini sana maana humu wapo matapeli, wengi watajifanya ni mawakala na wengine wanajua kukuunganishia kazi mahali, watakupiga hela sana, mfano wa matapeli hao kuna katerlo, britannica na kuna mwingne jina limenitoka, ni matapeli hawa watu. So kuwa makini na bora ukakaa chini tuliza akili usikubali mtu wa hapa akuambie umtumie hela yeyote kwaajili ya ishu yako hii
 
Ulaya maisha nati sana kwa sasa mkuu.Kama unaweza nenda New Zealand,huko Kuna kazi za kumwaga but hakuna man power,baridi Ni kali Sana,but pia wanatoa offer ya kukusomesha kwa skill utakayokua unaifanyia kazi.But tatizo ni mpaka uwe card Fulani hivi ya kukutambulisha kwamba upo nchini kihalali.But kuipata huyo card hapo ni shida tupu.
Wamanisha settlement permit au?
 
Ndugu ngekuwa ni suala na nauli nafikiri wengi wangeenda kufanya kazi ulaya, ila nauli ni suala dogo sana. Cha msingi utapataje visa?? Visa rahisi unayoweza kupata kwako labda ni tourist visa mabayo kimsingi utatakiwa uwe na hela ya kutosha maana hizo nchi wako makini sana kwa watu wanaotoka nchi maskini, na hata ukipata hiyo visa ni ya muda mfupi na hutaweza kufanya kazi, unless uwe illegal immigrant. Na hata ukipata mwaliko kama ungekuwa na jamaa bado ni ngumu pia kupata hati ya ukaazi au work permit. Nakushauri hiyo hela ya nauli ifanyie jambo la maana hapa Tz
 
Kwa elimu ya kiafrica hupati kazi ulaya ila unaweza kupata foundation tu,ya kuanzia huko ulaya mfano we umesomea udereva lakin kwa ulaya huwezi endesha gari but huo uzoefu na vyeti vyako vitakusaidia kupunguza vigezo vya kupata leseni ya ulaya ndio utaruhusiwa kuendesha gari,lakin sio hizo degree zenu za kariakoo kule utasubiri sana mjomba.
 
USD 3000 Inakutosha kabisa kwenye nauli na kuomba visa ya utalii dubai and u can survive for atleast 3 months with a full accommodation.there after within that range of survuving inabidi uwe curious kuhusu hio nchi na ajira zake pamoja na namna ya kupata working permit.
Unaweza kuomba working visa ukiwa bado uko bongo whch is about 2.5M and kama utaipata basi utalipwa Mara mbili ya salary utakapo ajiliwa na compny kwq sabab ulitumia gharama zako kutafuta hio working visa.
So if you are serious and ready for it go for it.
 
Nakushauri kwa dhati ya moyo wangu. Jifunze udreva wa tax na mabasi kisha nenda Doha ama Dubai kafanye kazi ya udreva. Nafasi ni nyingi sana. Nchi hizo zimeendelea sana pia wageni ni wengi sana. Miaka ya hivi karibuni Ulaya pamekuwa si mahali pa kukimbilia. Nafasi za kazi hakuna na si kama zamani. Kwa zaidi njoo inbox nikushauri. Kuna jamaa zangu kadhaa wako huko watakupokea.
Hapo connection ya Doha mkuu imekaaje!
 
Njoo huku Brunei itatoboa, kumbuka kubeba nidhamu halisi vinginevyo utajuta. Mambo ya pambuchi za watu walioolewa kaa mbali nazo.
Mkuu nisaidie contact zako, nna mpango wa kuja huko kama ntafanikiwa
 
Back
Top Bottom