Ushauri: Niende Serikalini au nibaki private sector

Ushauri: Niende Serikalini au nibaki private sector

Huwa ninamshangaa sana kijana wa kisasa aliyesoma mpaka chuo kikuu anapigania mambo ya job security, job security waongelee wazee wa miaka 60+, kuishi kwa kuteseka na laki nane miaka ishirini mwanaume unayetakiwa kujenga familia wakati una option ya kufanya kazi nzuri na ku grow huo ni ukosefu wa akili.
Huu uoga ndio unaiweka CCM madarakani mpaka leo
 
Nenda serikalini mzee wakati unaomba ulitarajia usipate??
Mwenye jibu ni wewe mwenyewe.Kwa sababu ni wewe uliyeomba hiyo kazi huko serikalini huku ukiwa muajiriwa wa private sector.Je ulilenga nini kuomba kazi wakati una kazi?mbona umezuia nafasi za wenzako.
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.
Usipime sana kazi kwa kiwango cha malipo unacholipwa bali angalia factors nyingine nyingi. Mf hapo ulipo kama hicho unachikipata ndani ya mkataba mmoja unaweza kutimiza malengo yako ya muda mrefu baki, mf. Unaweza kujenga ndani ya muda mfupi na kuanzisha uwekezaji mwingine ambao hata mkataba wako ukiisha au kusitishwa huwezi kuanza kuhangaika hangaika na kulia huku na kule.

Pili jikite kwenye faida za muda mrefu sio muda mfupi hasa juu yako mwenyewe baada ya miaka 10,15,20....,familia yako hasa watoto kuwasomesha mpaka mwisho bila kukwama njiani.
Mkeo, wazazi na wategemezi wengine.

Tatu angalia umri wako je bado kijana sana una future ndefu au tayari una majukumu ya familia au wategemezi.

Mwisho kitu chochote chenye ushindani mkubwa jua kinathamani kubwa hata kama haionekani kwa macho leo.

NB. Swali kwa nini watoto wa vigogo na viongozi wakubwa haijalishi wamesoma wapi, wana mitaji mikubwa ya kuweza kuwekeza au kuanzisha miradi au business kubwa kubwa.... Lakini wazazi wao wanahakikisha wanapata ajira selikarini???? Why????? Kwenye maisha fikiria miaka 20 ijayo au zaidi sio fikra za 2025 na 2027.
 
Kila jambo huja kwa kusudi maalum mkuu! Kumbuka kiroho wasemapo kuna amani ndipo uharibifu huja ghafula! Mungu anakusudi na hilo jambo usilichukulie kwa kuangalia tamaa zako! Yamkini huko serikalini ulikopelekwa ndipo kwenye usalama wako, Mungu anataka kukuokoa kwa kukutoa huko hata kama ni kwa maumivu lakini ndo usalama wako! Jiiulize maswali yafuatayo kabla haujafanya maamuzi
1: kwa nini Mungu aruhusu kipindi hiki ambacho mshahara wako ni mkubwa ndo utolewe database??? Kwa nini wewe sio mwingine???

2: je hapo ulipo leo ukipata ulemavu, au ukipata tatizo la kukaa home hata miezi 3 wataendelea kukuitaji????

3: wajuaje kuwa Mungu anakuepusha na ajali kazini au lolote mbaya kipindi hiki cha amani???

Note: Mungu anakusudi na kila jambo mkuu usiangalie mshahara hata kama ukilipwa mara 20 mshahara hautoshi! Kati ya watu kumi waliowahi kukataa nafasi kama hizi serikalini 9 wanajuta ni wachache sana ambao wanaendelea kuenjoy! Private unaweza kuamka ukakutana na barua mezani ya kufukuzwa kazini!


Amani ya moyo iamue moyoni mwako! Serikalini hatutegemei mishahara peke yake mkuu! Kuna vikao, semina, safari za hapa na pale! Nk
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.
Usipoenda Sahau kupata Ajira serikalini nakushaur nenda tu serikalin posho nyingi kuliko mshahara unakuta mtu ana mshahara mdogo lkn posho anapata hata Mara 5 YA mshahara wake.....jiulize siku mkikataliwa kurenew mkataba itakuaje
 
Kila jambo huja kwa kusudi maalum mkuu! Kumbuka kiroho wasemapo kuna amani ndipo uharibifu huja ghafula! Mungu anakusudi na hilo jambo usilichukulie kwa kuangalia tamaa zako! Yamkini huko serikalini ulikopelekwa ndipo kwenye usalama wako, Mungu anataka kukuokoa kwa kukutoa huko hata kama ni kwa maumivu lakini ndo usalama wako! Jiiulize maswali yafuatayo kabla haujafanya maamuzi
1: kwa nini Mungu aruhusu kipindi hiki ambacho mshahara wako ni mkubwa ndo utolewe database??? Kwa nini wewe sio mwingine???

2: je hapo ulipo leo ukipata ulemavu, au ukipata tatizo la kukaa home hata miezi 3 wataendelea kukuitaji????

3: wajuaje kuwa Mungu anakuepusha na ajali kazini au lolote mbaya kipindi hiki cha amani???

Note: Mungu anakusudi na kila jambo mkuu usiangalie mshahara hata kama ukilipwa mara 20 mshahara hautoshi! Kati ya watu kumi waliowahi kukataa nafasi kama hizi serikalini 9 wanajuta ni wachache sana ambao wanaendelea kuenjoy! Private unaweza kuamka ukakutana na barua mezani ya kufukuzwa kazini!


Amani ya moyo iamue moyoni mwako! Serikalini hatutegemei mishahara peke yake mkuu! Kuna vikao, semina, safari za hapa na pale! Nk
Posho za kumwaga
 
Usipime sana kazi kwa kiwango cha malipo unacholipwa bali angalia factors nyingine nyingi. Mf hapo ulipo kama hicho unachikipata ndani ya mkataba mmoja unaweza kutimiza malengo yako ya muda mrefu baki, mf. Unaweza kujenga ndani ya muda mfupi na kuanzisha uwekezaji mwingine ambao hata mkataba wako ukiisha au kusitishwa huwezi kuanza kuhangaika hangaika na kulia huku na kule.

Pili jikite kwenye faida za muda mrefu sio muda mfupi hasa juu yako mwenyewe baada ya miaka 10,15,20....,familia yako hasa watoto kuwasomesha mpaka mwisho bila kukwama njiani.
Mkeo, wazazi na wategemezi wengine.

Tatu angalia umri wako je bado kijana sana una future ndefu au tayari una majukumu ya familia au wategemezi.

Mwisho kitu chochote chenye ushindani mkubwa jua kinathamani kubwa hata kama haionekani kwa macho leo.

NB. Swali kwa nini watoto wa vigogo na viongozi wakubwa haijalishi wamesoma wapi, wana mitaji mikubwa ya kuweza kuwekeza au kuanzisha miradi au business kubwa kubwa.... Lakini wazazi wao wanahakikisha wanapata ajira selikarini???? Why????? Kwenye maisha fikiria miaka 20 ijayo au zaidi sio fikra za 2025 na 2027.
Una hoja Mkuu
 
Karibu tabora mkuu,sijui wilaya gani,privet sectors kuna mambo mengi mno licha ya mishahara minono,na kufukuzwa ni kugusa tu, huku halmashauri kuna pesa nyingi mno za dili mshahara ni geresha tu, karibu tabora, nitumie namba yako pm tuzungumze.
Mkuu nyie ndio wahujumu wa miradi yetu? 😀😀😀
 
Mwenye jibu ni wewe mwenyewe.Kwa sababu ni wewe uliyeomba hiyo kazi huko serikalini huku ukiwa muajiriwa wa private sector.Je ulilenga nini kuomba kazi wakati una kazi?mbona umezuia nafasi za wenzako.
Niliomba taasisi kubwa ya serikali mzee na ningepata huko nisingejishauri kwa chochote ningeenda sema nilikosa nafasi jina likabaki kwenye database ndio wamenipangia huko halmashauri sahv ambapo sikuombea ajira nimepangiwa tu
 
Kila jambo huja kwa kusudi maalum mkuu! Kumbuka kiroho wasemapo kuna amani ndipo uharibifu huja ghafula! Mungu anakusudi na hilo jambo usilichukulie kwa kuangalia tamaa zako! Yamkini huko serikalini ulikopelekwa ndipo kwenye usalama wako, Mungu anataka kukuokoa kwa kukutoa huko hata kama ni kwa maumivu lakini ndo usalama wako! Jiiulize maswali yafuatayo kabla haujafanya maamuzi
1: kwa nini Mungu aruhusu kipindi hiki ambacho mshahara wako ni mkubwa ndo utolewe database??? Kwa nini wewe sio mwingine???

2: je hapo ulipo leo ukipata ulemavu, au ukipata tatizo la kukaa home hata miezi 3 wataendelea kukuitaji????

3: wajuaje kuwa Mungu anakuepusha na ajali kazini au lolote mbaya kipindi hiki cha amani???

Note: Mungu anakusudi na kila jambo mkuu usiangalie mshahara hata kama ukilipwa mara 20 mshahara hautoshi! Kati ya watu kumi waliowahi kukataa nafasi kama hizi serikalini 9 wanajuta ni wachache sana ambao wanaendelea kuenjoy! Private unaweza kuamka ukakutana na barua mezani ya kufukuzwa kazini!


Amani ya moyo iamue moyoni mwako! Serikalini hatutegemei mishahara peke yake mkuu! Kuna vikao, semina, safari za hapa na pale! Nk
Una hoja nzito sana
Mfano Yusufu mtoto wa Yakobo

Ukiangalia Ile story kwenye Biblia unatambuwa kuwa siku zote mahali Mungu alipokukusudia ukutane mafanikio yako Huwa hapavutiii sana!

Na kwenye kuitwa katika kutekeleza kusudi la ki Mungu mara nyingi Huwa si pepesi!

Mwalimu Mwakasegeke Kipindi anafundisha somo la Mifumo! Aliongelea swala la ubinafsi kuwa kikwazo Cha mafanikio.
Ko
Umetoa hoja nzuri sana ! Sasa mdau kazi yake ni kujipima.

Je analitambua kusudi la Kuumbwa kwake? Mahali alipo Sasa! Anaishi Hilo kusudi?

Yamkini Mungu alipomkusudia si hapo ni serikalini! Je yupo tayari kuacha mshahara mkubwa na kwenda kwenye mshahara mdogo kwa ajili ya kuupa Kipaumbele UFALME wa MUNGU kwanza?


Amani ya Kristo na ifanye maamuzi ndani yake na si tamaa wala chochote!

Roho Mtakatifu amsaidie sana
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.
Bwana mkubwa:
1. Umesema uliomba kazi. Kwa nini uliomba i.e. ulisumbua watu halafu sasa unajishauri eti uende au usiende.
2. Qualification Professional ww ni nani au ndo Utumish i.e. Human Resources Officer? Hili ni muhimu sana niwekee wazi ili nikupe ushauri muafaka.
3. Umeshajiuliza ni kwa nini Private Sector (almost all private Sectors) uliyopo imeweka 3 yrs Contract but Renewable?????
4. Ni vizuri ukatoka nje ya box na ili upate exposure ya huko kwingine.
5. Dar itakuponza mkuu. Take it from me.
 
Niliomba taasisi kubwa ya serikali mzee na ningepata huko nisingejishauri kwa chochote ningeenda sema nilikosa nafasi jina likabaki kwenye database ndio wamenipangia huko halmashauri sahv ambapo sikuombea ajira nimepangiwa tu
Samahani lakini. Taasisi kubwa ya Serikali manake nini au ndo nini??. Kumbuka Serikali ni moja tu hapa Tanzania. Iwe ni Serikali za mitaa au Halmashauri au Serikali kuu. Tofauti iliyopo hapo ni katika utendaji tuu.
 
Huwa ninamshangaa sana kijana wa kisasa aliyesoma mpaka chuo kikuu anapigania mambo ya job security, job security waongelee wazee wa miaka 60+, kuishi kwa kuteseka na laki nane miaka ishirini mwanaume unayetakiwa kujenga familia wakati una option ya kufanya kazi nzuri na ku grow huo ni ukosefu wa akili.
Huu uoga ndio unaiweka CCM madarakani mpaka leo
Mkuu; hao unaosema ndo wanatakiwa waongelee job security i.e. wazee wa 60+ unadhani walizuka tu from nowhere ndo wakajikuta 60+?? Wahenga walisema: "Ukiona nyani kazeeka ujue amekwepa mishale mingi" Manake hao wazee wana uzoefu mkubwa na wamepitia mapito mengi hadi wakafika hiyo miaka 60+ Zingatia sana hili- Usiwadharau, just wape tu hashima yao. Kusoma hadi chuo kikuu hakumfanyi au hakumwondolei mhusika option ya kujipangia malengo ya muda mrefu e.g. atakavyoishi kama akibahatika kuufikia umri wa uzee.
Kijana wa kisasa ndo mzee wa kesho au soon atakuwa ni kijana wa zamani.
 
Mkuu; hao unaosema ndo wanatakiwa waongelee job security i.e. wazee wa 60+ unadhani walizuka tu from nowhere ndo wakajikuta 60+?? Wahenga walisema: "Ukiona nyani kazeeka ujue amekwepa mishale mingi" Manake hao wazee wana uzoefu mkubwa na wamepitia mapito mengi hadi wakafika hiyo miaka 60+ Zingatia sana hili- Usiwadharau, just wape tu hashima yao. Kusoma hadi chuo kikuu hakumfanyi au hakumwondolei mhusika option ya kujipangia malengo ya muda mrefu e.g. atakavyoishi kama akibahatika kuufikia umri wa uzee.
Kijana wa kisasa ndo mzee wa kesho au soon atakuwa ni kijana wa zamani.
Mkuu sijamaanisha kudharau hata kidogo, nimemaanisha kwamba kwa era ya maisha yao ilikua ni haki kupambania job security za serikali kipindi wanakua, hivyo mzee wangu akinishauri kuhusu job security siwezi kumshangaa hata kidogo,
Ila kwa kijana sio sawa, tuna factors nyingi sana za kuangalia kwa mtazamo wa kisasa
 
Kwanini usifanye kazi zote mbili sababu wewe ni 2in1
Anyway sijawahi fanya kazi serikalini na suitokuja kufanya japo niliwahi pata nafasi ya kwenda kufundisha DIT nikaamua kubaki zangu private sector
 
Mkuu sijamaanisha kudharau hata kidogo, nimemaanisha kwamba kwa era ya maisha yao ilikua ni haki kupambania job security za serikali kipindi wanakua, hivyo mzee wangu akinishauri kuhusu job security siwezi kumshangaa hata kidogo,
Ila kwa kijana sio sawa, tuna factors nyingi sana za kuangalia kwa mtazamo wa kisasa
Yeah uko sawa. kama ni kwa mtizamo wa kisasa. Lakini Je, itakuwaje utakapofikia umri wa uzee? i.e. Huwezi tena kukimbia-kimbia kama vijana watakaokuwepo wakati huo ww umeshakuwa ni kijana wa zamani. Future yako inatakiwa kuandaliwa sasa yan Utakapo kuwa ni mzee uweze bado kupata walau maokoto endelevu japokuwa ni kidogo. Kufanya kazi Serikalini japokuwa sio sekta zote; mshahara unayo makandokando mengi a.k.a maokoto mengine (allowances), kuna fursa ya kufanya mambo ya kwako ya ziada e.g. kuanzisha na kuendesha vijimiradi vidogo-vidogo na pia kwa hiyo job security mhusika anaaminika na anaweza kupata mkopo benki (sijui huko private sector inakuwaje)halafu serikalini unakuwa na health Insurance ya kudumu hata ukistaafu(Cjui huko private sector inakuwaje) mpaka umauti ukukute. Ninachelea kwamba Mshahara mkubwa wa sasa wenye Mkataba tena Mkataba wa muda mfupi e.g. 3 - 5yrs sio sustainable. Chief/Director akikuamkia vibaya kwako unatimuliwa fasta au anaweza kukataa Renewal ya Mkataba. Private Sectors mara nyingi unakuta zina mwelekeo wa ukanda/ukabila (egoism) au hata wakati mwingine udini unaweza kuwepo vitu ambavyo Serikalini havipo kivile. Private sector huwezi kuhama kirahisi kama mambo yakikuendea ndivyo sivyo au huridhishwi na mazingira ya kazi - Inakubidi ukomae hapo hapo. Serikalini unaweza kuomba kuhama utajihamisha au kubadilishana na mwenzako kituo cha kazi.
 
Back
Top Bottom