Ushauri: Nifanyeje juu ya hali hii ya maisha yangu?

Ushauri: Nifanyeje juu ya hali hii ya maisha yangu?

Kusema kweli naona makelele tu ,sioni solution ya kumsaidia mtoa mada
 
Wakubwa kwangu shikamoni, wadogo kwangu habari zenu ?

Hongereni kwa majukumu na afya njema, poleni mnaoumwa Mungu akawajaalie mpone.

Ndugu, Nilizaliwa miaka 31 iliyopita. nilipenda sana kuwa mwanajeshi wa jeshi la wananchi, sikufanikiwa kutokana na umri wangu kupita ule unaotakiwa, kukosa fani zinazotakiwa huko, na kutokuwa na mtu wa kunishika mkono kuingia huko. Nina shahada ya sayansi.

Kuna mahala serikalini nimejitolea kwa miaka minne sasa, walivyotoa ajira kupitia utumishi nimebwagwa kwenye usahili nikashindwa ! wakaajiriwa vijana wengine ambao hawakuwa wakijitolea pale. Nimefanya saili nyingi za kuomba kazi utumishi na kwingineko lakini sijafanikiwa kupata kazi.

Hapo Kibaruani wanatoa sh. 15000 kwa siku mtu atakayofanya kazi, (300,000 na kidogo kwa mwezi maana ijumaa pili hatufanyi kazi) hicho kiasi cha fedha kwa mkoa wa Dar es salaam kinaishia kulipa kodi, nauli za kwenda kibaruani, kununua umeme, kula kwa mama ntilie (2000 msosi mmoja), kulipia taka, kulipia ulinzi mtaani, sadaka kanisani, VOCHA na matumizi mengine; sijafanikiwa kuweza kuweka akiba. Sina mchumba, mke wala mtoto maana sina hela za kuniwezesha kuwahudumia, Ukinunua napo magonjwa lukuki .... ila homoni za mwili zenyewe zinafanya kazi yake hazielewi hali yako kiuchumi kwa hiyo ni shida tupu.

Huwa ninatamani sana kwenda jeshini lakini umri, fani na konekisheni ni changamoto

Ninatamani kuoa lakini sina kazi, nikifikiria kurudi kijijini kulima, sawa lakini mtaji wa kulimia na mashamba sina. Nafikiria kusoma 'post graduate diploma in education' ili niwe na taaluma ya ualimu badae niombe kazi serikalini kama mwalimu wa fizikia n.k lakini hela ya kulipia ada (milioni mbili) sina. Huwa ninapenda pia kufanya biashara ya stationery lakini mtaji nao sina !

Ninawaza kurudi chuo kusoma kozi za afya kwa diploma, ada sina ! Nipo njia panda ndugu ninaombeni mnishauri nifanyeje ili kupata hela, niache kujitolea niende chuoni kusoma, niajiriwe serikalini au taasisi binafsi au nifanye miradi hiyo, n.k maisha mengine yaendelee.

Ninatanguliza shukrani kwa ushauri wenu, ninawatakia mda mwema.
Inasikitisha. Hii serikali badala ya kuendelea kunyonya nguvukazi ya vijana kama wewe ningeshauri waweke utaratibu wa kuwaajiri vijana waliyojitolea mfululizo japo kwa miaka minne. Hua navyojua wanatoa mikataba mifupifupi ili kuepa sheria inayosema mtu akiajiriwa kwa muda fulani mfululizo kama kibarua inabidi spewe ajira kwa kudumu. Sio vyema serikali kutumia mbinu za waajiri binafsi kunyonya nguvukazi ya vijana wake.
 
Kuwa na malengo mengi kwa wakati 1 it means unakimbiza vipepeo wengi kwa wakati mmoja mwisho wa siku wote wanaruka na kuwakosa ushauri wangu chagua jambo moja unaloliamini sana kukuvusha komaa nalo la sivyo ukitaka kukamaa na yote mwisho wa siku hautafanikiw hata moja tumia 10000 save 5000 walinzi wanalipwa laki 1.5 hadi laki mbili na wanabalance matumizi yao kwa mwezi
 
Inasikitisha. Hii serikali badala ya kuendelea kunyonya nguvukazi ya vijana kama wewe ningeshauri waweke utaratibu wa kuwaajiri vijana waliyojitolea mfululizo japo kwa miaka minne. Hua navyojua wanatoa mikataba mifupifupi ili kuepa sheria inayosema mtu akiajiriwa kwa muda fulani mfululizo kama kibarua inabidi spewe ajira kwa kudumu. Sio vyema serikali kutumia mbinu za waajiri binafsi kunyonya nguvukazi ya vijana wake.
Ajira ni ngumu sana siku hizi, unajitolea miaka kadhaa mahala na wakitoa ajira wanaajairi vijana wengine tuu maana wanachojali wao ni ufaulu wa kwenye usaili tuu. Mtihani utokane na kada yenu halafu wewe mwenyewe mwenye uzoefu na hapo, na mtihani umejibu vizuri ila unafeli, vijana wasiofanya kazi hapo wanafaulu kwa viwango vya juu, nadhani kuna suala la anakujua nani au rushwa huko juu. Mungu atusaidie sana vijana tunapitia wakati mgumu sana.
 
Kuwa na malengo mengi kwa wakati 1 it means unakimbiza vipepeo wengi kwa wakati mmoja mwisho wa siku wote wanaruka na kuwakosa ushauri wangu chagua jambo moja unaloliamini sana kukuvusha komaa nalo la sivyo ukitaka kukamaa na yote mwisho wa siku hautafanikiw hata moja tumia 10000 save 5000 walinzi wanalipwa laki 1.5 hadi laki mbili na wanabalance matumizi yao kwa mwezi
Sawa.
 
Ahaaah, ngoja ntajaribu nione. Tatizo huwa wanakataa kutupatia kazi ya ualimu maana hatujasoma masomo ya ualimu, na Wapo sahihi kwa kigezo chao cha kuhitaji mwalimu aliyesomea hiyo kazi. Japo ninaweza kufundisha na nimefundisha sana wanafunzi.
Nenda hapo ,uje ulete mrejesho
 
Back
Top Bottom