Ms Billionaire
JF-Expert Member
- Jul 18, 2020
- 2,452
- 4,955
Tusihalalishe upumbavu kwa kigezo cha maamuzi binafsi.Na kama mtu hayupo tayari kuzungumza ya nyuma kwanini alazimishwe??? Kila binaadam ana siri yake na maamuzi yake yanapaswa kuheshimiwa, huwezi jua hilo tukio lilimuumiza vipi akaamua kulifukia na kuanza upya.
Nakupongeza kwa moyo ulionao mkuu, wewe ni zaidi ya malaika aiseee....😊Kwanini nisimuamini?
Jamani kila Mtu ana siri yake kama ameamua kuitunza as long as haikuwahi kuniletea madhara yoyote si basiiiii,
Tena haya mambo ya Mwanamke kuondoka mahali na kuacha mtoto kisha akaja kuolewa sehemu nyingine na kuzaa, mara nyingi huwasahau wale watoto wa mwanzo na kufocus na family mpya, hadi mtoto aje amtafute na hii sio kwa Mwanamke tu hata kwa Wanaume hutokea,
Mimi naona mnakuza vitu ambavyo kimsingi havina mashiko.
Trust ikivunjika, haiwezi kurudishwa. Suluhisho ni kuachana tu ili kuepusha maafa mengine.Kibongo bongo hutaeleweka
.......ohooo!! we unasema jambo kubwa wakati kuna komenti huko zinadai kwamba ni jambo dogo, yaani kumficha mwenzi wako kwamba unamiliki mwanadamu kwa miaka zaidi ya kumi ni jambo dogo sana.........Mwanaume yuko sahihi...Mwanamke anayeweza kuficha jambo kubwa hivyo ana roho ngumu mnoo
Usichokijua: saikolojia ya mwanaume ni tofauti kabisa na ya mwanamke.Ila wanaume huwa mnanishangaza jambo moja. Nyinyi mnazaa na michepuko yenu ilhali mpo kwenye ndoa, wake zenu wanakuja kujua mkishakufa. Mbona hawa vimbi mashavu kama mnavyovimba nyinyi??? Wengine mnawaletea kabisa nyumbani, na wanawapokea maisha yanaenda. Sasa huyu wa zamani kabla ya ndoa mnaumia nini. Wanafki nyinyi muwe mnatunza energy mnayoyafanya yakirudi kwenu mvumilie
Na mioyo ni tofauti? Mwanaume ana wa damu na nyama, mwanamke ana wa makaratasi?Usichokijua: saikolojia ya mwanaume ni tofauti kabisa na ya mwanamke.
Tatizo siyo kuzaa, ila uongo.Wakati mwingine tusiongozwe na hisia bali utashi wetu.
Kwani ni kosa mtu kuzaa, ni heri huyo amezaa maana kuna wengine wametoa zaidi ya mimba 7 hadi kuolewa kwao.
Ningekuwa Mimi huyo mtoto ningempokea na kumfanya mmoja ya watoto wangu, kwanza kwa mujibu wa mila zetu mtoto wa mkeo nao ni watoto wako
Umeanza mihemko isiyo na sababu.
Pili tusijadili mambo kimazoea ya kiswahili.
Mwanzo wa mahusiano una mambo mengi.
Kuna mwanamke mkianza mahusiano anakutaka uwe wazi kwake kama umewahi kuoa au kuzaa nje.
Kwa moyo mkunjufu unamweleza ukweli.
Naye anakwambia hajawahi kuolewa wala kuzaa, baada ya miska 15 ukagundua alizaa na alikuficha kwanini udimwache?
Mwanzoni ukiniambia hata una watoto wawili kwa uwazi huo mimi nitakuoa.
Napendezwa na mwanamke muwazi, makosa kila mtu hufanya.
Lakini kitendo cha kumficha binadamu aliyetoka kiunoni mwako, si unaweza kumficha mmeo jambo lingine kubwa?
Ongea uhalisia uache hasira
Ndiyo. Hisia za mwanamke na mwanaume ni tofauti kabisa.Na mioyo ni tofauti? Mwanaume ana wa damu na nyama, mwanamke ana wa makaratasi?
Hisia za kiume na kike ni tofauti kabisa.Ila wanaume huwa mnanishangaza jambo moja. Nyinyi mnazaa na michepuko yenu ilhali mpo kwenye ndoa, wake zenu wanakuja kujua mkishakufa. Mbona hawa vimbi mashavu kama mnavyovimba nyinyi??? Wengine mnawaletea kabisa nyumbani, na wanawapokea maisha yanaenda. Sasa huyu wa zamani kabla ya ndoa mnaumia nini. Wanafki nyinyi muwe mnatunza energy mnayoyafanya yakirudi kwenu mvumilie
Shangaa na wewe, mijanaume ya Kiafrika hua ni mibinafsi sanaaa, hii habari ingekua ni mwanaume ndie kaleta mtoto na Mwanamke ndie kataka talaka ungeona vile wanamshambulia Mwanamke na kumuita majina yote ya ajabu,Ila wanaume huwa mnanishangaza jambo moja. Nyinyi mnazaa na michepuko yenu ilhali mpo kwenye ndoa, wake zenu wanakuja kujua mkishakufa. Mbona hawa vimbi mashavu kama mnavyovimba nyinyi??? Wengine mnawaletea kabisa nyumbani, na wanawapokea maisha yanaenda. Sasa huyu wa zamani kabla ya ndoa mnaumia nini. Wanafki nyinyi muwe mnatunza energy mnayoyafanya yakirudi kwenu mvumilie
Wamechokana tu hao hamna lolote, jamaa alikua amechoka akapata pa kutokea! Yaani 4-1 si ni fare kabisa!Habari wana JF.
Kuna Ndoa imevunjika hapa ndoa ya miaka 15.
Mke alizaa kabla ya ndoa, sasa mama huyu alimficha mtoto,
Huyu mtoto alikuwa anaishi na Baba yake.
Mume alijua kwa mawasiliano ya simu.
Mama alipokuwa anaongea na mwanae.
Na mtoto anaumri wa miaka 20.
Mume wa ndoa kazaa nae watoto 4.
Dawati la suruhisho walijaribu kuweka sawa ili wasiachana ila ilishindika. Hata wachungaji walishauri kuwa asamee tuu kwani hata mtoto kashakuwa mkubwa hakuna shida yoyote lkn ndo hivyo ndoa imevunjwa jana na mahakama.
Huyu mama alizaa kipindi anaumri wa miaka 21.
Sasa wanajamii hivi vitu vinatokana na nini mpk mmoja anaamua kuficha mtoto?
NI NINI CHA KUFANYA BAADA YA KUJUA HATA KWA MUME KAMA ALIFICHA KUWA ALIKUWA ANAMTOTO.
Huyo ni Mwanaume suruali, halijui jando, hajafundishwa chochote kuhusu ndoa walizoana zoana tu wakaapa basi,Tusihalalishe upumbavu kwa kigezo cha maamuzi binafsi.
Kutotaka kuongelea umelala na wanaume wangapi hiyo ni hiari yako ila sio kuwa na mtoto na kuficha.
Unapoingia katika ndoa kuna baadhi ya haki unazipoteza na moja wapo ni uwazi wa uzao wako kabla ya ndoa.
Mtoto sio kijipu kusema utakificha mwisho kipotee.
Kuna watu wanawake kwa wanaume hawapo tayari kuingia kwenye mahusiano na mtu mwenye mtoto/watoto kabla. Sasa hapo haki iko wapi kwa mwanaume endapo ilikuwa hana azma ya kuoa mwanamke mwenye mtoto na mwanaume mwingine.
Haijalishi unaitazama kwa jicho gani, kuficha kuwa una mtoto kabla ya ndoa ni jinai kubwa katika mahusiano na mwanaume kuamua kutoa talaka ni ndani ya haki yake kwa jinsi alivyolichukulia.
Kwenye ubinafsi ndio point kubwa, naweka sawa WANAUME WA KIAFRIKA NI WABINAFSI WENYE ROHO MBAYA,Nakupongeza kwa moyo ulionao mkuu, wewe ni zaidi ya malaika aiseee....[emoji4]
Lakini ngoja nikugusie kidogo kuhusu sisi wanaume..... kwanza sisi ni wabinafsi kiasili, pia tunatabia ya kunyamaza lakini niwagumu sana kusamehe. Tofauti na ninyi hua mnaongea sana na kutoa maneno, lakini kesi zenu hua zinaisha na mnasamehe. Na hapa ndipo nimalizie tu kwakusema kwamba wewe ndie usirahisishe mambo kwasababu ungekua mwanaume pengine unge elewa hiki ninacho kizungumza na kilicho mkuta huyu mbwana kwenye hii mada.