USHAURI: Rais Samia suluhisho pekee kwa Bandari Tanzania ni hili

USHAURI: Rais Samia suluhisho pekee kwa Bandari Tanzania ni hili

Serekali ndio kikwazo cha bandari zetu kufeli angalia bandari kama Durbun inavyofanya kazi vizuri nimefika pale mazingira yake ni kama hii ya Dar wametenga eneo kama kigamboni wafanya biashara wamejengewa yard za kuzia biashara zao wanakodishwa wakiagiza mizigo meli zinashusha kwenye eno walilotengewa kwajili bila kulipia ushuru,wakiuza bidhaa moja nfano godoro wanalipia bidhaa iliyonunuliwa watu wa custom wako kwenye mageti ya kutokea mixigo bila kukilipia ushuru mizigo upitishi pake sio kama hapa kwetu ujuaji mwingi tungefanya kama wenzetu bandari zetu zingetengeneza ajira nyingi sana nchi jirani wasinge agiza mizigo kutoka nje wangenunulia hapa kwetu ukiwa na mtaji kidigo wa kununua mzigo unafanya biashara bila tatizo lakini hapa kwetu kizungumkuti nfanya biashara anaumiza kichwa gharama za manunuzi kusafirisha mzigo kulipia gharama za bandari kulipia ushuru storege akichekewa kidogo mnada unamuhsu akifika mtaani parchising power zero shida tupu tunapelekana mperapera sana nakukomoana ndiomana umasikini ningumu kuisha mwisho utasikia CAG riport yake anakuambia pesa zilizokusanywa zimeibiwa
Leo hii Serikali inataka kufanya hivi watu wanaleta mijadala uchwara humu.

Ujinga ni kipaji
 
Ndugu zanguni, kwanza kabisa tuelewe inaposemwa bandari hafanyi kazi kwa kasi inayotakiwa maana yake ni nini.
Kuna vigezo kadhaa vya kimataifa vinavyopima jambo hili lakini kikubwa kabisa ni kasi ya uingiaji wa meli nchini na kupata gati, kupakua kupakia na kuondoka. Ndio maana kitendo cha meli kukaa nje baharini kusubiria gati linapaka sana matope bandari yetu kimataifa.
Vigezo vingine lakini vyote ni vya kussuport hili la meli.
Sasa jambo la kujiuliza kabla kufikiria Bagamoyo je. Bandari yetu imetekeleza yote yenye kuongeza kasi ya meli kuingia na kutoka??
1. Je shughuli zote za bandari au zihusuzo mizigo zinafanyika masaa 24?? Watanzania bado tunapenda sana kupumzika. Hebu jiulizeni kama huduma za vitengo vyote vihusuzo mizigo kama kweli zipo masaa 24 kama hutakuta ni kule kwenye maji tuu
2. Je, urasimu wa vibali tokea custom, bandarini, TBS... Nk. Imekwisha??
3. Tecnohama inatumika ipasavyo kila kitengo?
4. Kwa nini hadi leo mizigo hazitoki bandarini kutoka kwenye meli moja kwa moja kwenye lorry la mwenye mzigo.. Under hook direct delivery
5. Kwa nini full swing use of Icds haufanyiki. Bandari sio mahali Pa kulundika mizigo
6. Je vifaa bandarini ni vya kisasa na vinatumika effectively

Nadiriki kusema PPP ni mhimu baada ya mageuzi makubwa kuonyeshwa na TICTS jambo ambalo halipashwi kusubiri kwenda gati zingine hata kwa mwekwzaji mwingine ikibidi ili ashindane na Ticts. Pia hadi General cargo vessels hadi kwenye magari

Tunaweza kufungua gati nyingine nyingi lakini mind set zetu zokabaki kufanya kazi kwa mazoea. Bandari na associated partners lazima ziwe kazini masaa 24.
Hakuna haja kufoleni maofisini kutafuta vibali vya kutoa au kuingiza mizigo kupakia.. Let computer do the work
Mizigo inayoweza kubaki bandarini ni Ile maalum au yenye matatizo tuu. Mingine itoke siku inapakuliwa. Malipo yote kabla meli haijafika
Ushauri wako ndo unafanyiwa kazi na Serikali sasa ila kuna mijitu inaleta siasa iki mradi waonekane tu wanajua kuongea na kupinga

Nchi hii ujinga ni kipaji
 
Na watanzania tulivyo……tunashabikia viongozi dhaifu tulionao na hata kufikia kutetea kasi ndogo ya maendeleo yetu!
Mbaya zaidi viongozi wakichukua hatua ili twende na kasi inayotakiwa katika maendeleo tunaanza tena kupiga kelele eti nchi inauzwa.

Tanzania ujinga ni kipaji
 
Ushauri murua ulishatolewaga kwa Rais kupitia JF. Na hii ni mwaka jana na Rais ameufanyia kazi.

JF ni kisima.
 
Ushauri murua ulishatolewaga kwa Rais kupitia JF. Na hii ni mwaka jana na Rais ameufanyia kazi.

JF ni kisima.
Ushauri wako ulihusisha kubinafsisha bandari kwa muda usiojulikana na kwa masharti yanayomnufaisha mwekezaji kuliko nchi?
Au unaropoka tu ili kuonesha ushauri wako ni ushauri
 
Amani iwe nanyi
Leo Rais wa JMT amemtumbua Mkurugenzi wa Bandari Ndug Erick Hamis.

Pamoja na kumtumbua Rais Samia amelalamika juu ya efficiency ya Mamlaka yetu ya Bandari na kusema kuwa Mamlaka hii ingekuwa inafanya kazi vizuri ingeweza kuchangia hata nusu ya mapato ya Bajeti yetu. Ni kweli kabisa naungana na Rais Samia kwenye hili!

Mfupa wa Bandari ni mfupa uliowashinda Marais karibu wote waliowai kutawala Tanzania! Hii imekuwa kawaida kila Rais mpya akiingia au Waziri Mkuu mpya akiteuliwa sehemu ya kwanzq kwenda kulalamika na kutumbua imekuwa Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Kwa kumbukumbu zangu kuanzia kwa Mkapa, Kikwete, Magufuli hadi sasa Samia, Bandari hapajawai kupoa.

Hoja yangu kuu kwenye hili ni kwamba inawezekana sana bado hatujajua shida ni nini hasa pale Bandarini na kwa uelewa wangu mdogo napenda leo nimshauri Mhe Rais mambo ya kufanya na naamini kama nilivyoshauri kuhusu Ngorongoro na ikafanyika na sasa imefanikiwa basi nashauri juu ya hili la Bandari na naamini ikifanyika itafanikiwa

1. Lazima tukubali kuwa Bandari ya DSM haiwezi kuwa efficient kwa sababu imekuwa finyu kuhimili idadi ya mizigo, Meli na Magari kiushindani

2. Lazima tukubali kuwa Serikali haiwezi kuendesha bandari kwa ufanisi tunaoutaka katika dunia hii ya ushindani. Bandari kubwa zote duniani na zinazofanya vizuri kwenye soko la ushindani kuanzia Dubai, Hong Kong, Singapore, New York na nyinginezo, zinaendeshwa either kwa sehemu kubwa na private sector au kwa ubia baina ya Serikali na Private Sector

Hivyo ili kufanikiwa kupata ufanisi hapa Tanzania kwenye sekta ya Bandari , Lazima tutake tusitake, tufanye yafuatayo

a. Kwa haraka sana, Ijengwe Bandari ya Bagamoyo ambayo iwe na Gati zisizopungua 40. Bandari hii iendeshwe na Private sector with exception kwenye masuala ya Ulinzi, Usalama na Kodi

b. Sekta binafsi wapewe pia fursa ya kujenga Miundombinu ya Reli na barabara kuunganisha Bandari ya Bagamoyo na Jiji la Dar es Salaam ikiwemo reli ya kati SGR na TAZARA

c. Bandari za DSM, Tanga, Mwanza na Kigoma na Mtwara ziendeshwe kwa ubia na Private sector. Serikali isimamie masuala ya kodi , ulinzi na usalama tu!

d. Barabara ya Mandela Road( dsm) itanuliwe kuwekwa njia 8 kutokea Bandarini hadi Ubungo na utanuzi wa njia 6 uendelee kutoka Kimara hadi Ubungo. Hii ni ili kuleta ufanisi wa usafirishaji mizigo katika Jiji la Dsm. Ikiwezekana Private sector washirikishwe kwenye hili.

e. Kulikuwa na Mpango wa Kujenga Barabara ya Malori kutokea Bandarini hadi Chalinze. Mpango huu ufufuliwe na barabara hii ijengwe hata kwa kutumia Private sector! Fedha zitarudi haraka sana hata kwa toll tax!

Nchi kubwa duniani ziliona hili na wakaamua kufanya! Hata kwa Tanzania Serikali iking'ang'ania kuendesha bandari kila siku mtaishia kushikana uchawi na kutumbuana!

Ni suala la kuamua tu na wakati ni sasa
Tatixo kubwa sio mwekezaji tatizo ni mkataba wa kihuni
 
Ushauri wako ulihusisha kubinafsisha bandari kwa muda usiojulikana na kwa masharti yanayomnufaisha mwekezaji kuliko nchi?
Au unaropoka tu ili kuonesha ushauri wako ni ushauri
Wapi na lini Bandari imebinafsishwa kwa muda usiojulikana?
 
Kila mtu mwenye umri wa kuanzia miaka kumi na nane atoe at elfu kumi hela itakayo patikana wapewe T.P.A yote hayo yafanywe na mamlaka ya kitanzania kwa watanzania
 
Leo hii Serikali inataka kufanya hivi watu wanaleta mijadala uchwara humu.

Ujinga ni kipaji
Maaskofu wamejitoa mhanga kwamba lolote na liwe, kitu ambacho sio kizuri. Rais hafanyi kitu kwa maamuzi yake binafsi ni ushauri wa wataalam wengi tena wanachokiongea kinawekwa kwenye kitabu kimoja kinachoitwa ilani ya uchaguzi.

Wasidhani kuwa uwekezaji wa DP World ni maamuzi ya jana au juzi au kama inavyosemekana kwamba Dubai ni wajomba zake SSH, haya ni maamuzi ya miaka na miaka yaliyoanza na ujenzi wa SGR kwanza ambayo imekula matrilioni ya pesa mpaka kufika ilipofika muda huu.

SIdhani kama hao waliowashauri maaskofu walifuatilia masuala mazima ya muendelezo wa ilani ya CCM katika kutekeleza sera zake zaidi ya hoja zao kutegemea zile hisia za SSH kutaka kuwaridhisha jamaa zake wa Dubai.

Walichokifanya ni kutaka kutunishiana misuli na mamlaka ya rais kwa kutumia ukongwe wa kanisa kwa kutumia kuungwa mkono kwa hoja zao, wameamua kujilipua lakini maisha yanaendelea siku zote.
 
Back
Top Bottom