Ushauri wa bure: Madereva wa private cars tembeeni usiku kama unafanya Safari ndefu

Ushauri wa bure: Madereva wa private cars tembeeni usiku kama unafanya Safari ndefu

PureView zeiss

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2016
Posts
10,786
Reaction score
35,916
Imekuwa desturi na mazoea kwa madereva wengi wanaoendesha magari yao binafsi kufanya safari zao ndefu muda wa mchana ingawa ni jambo jema ila kwa mtazamo wangu mimi naona ni shida na usumbufu mwingi njiani.

Naongea hivyo kwasababu ndani ya mwezi Machi nilifanya safari ndefu ya kwenda Mwanza na gari yangu. Nakumbuka nilianza safari usiku saa 7 kutoka Dar ili kuepusha usumbufu kwenye kipande cha Dar-Moro (kwa wazoefu wa kipande hiki watakubaliana na mimi). Muda wa mchana nilipata shida na usumbufu na traffic pamoja mabus na fujo zao mpaka naingia Mwanza usiku saa 3.

Mpaka nimeamua kuandika ushauri huu ni kwa madereva wenzangu ni ushuhuda niliouona kwa macho yangu wiki hii.

Jumamosi iliyopita nimefanya safari tena nyingine ya kwenda Mwanza kwa kupanda bus hakika vituko vya madereva wa bus ni noma, hawa jamaa wanatumia barabara watakavyo,wanaovertake watakavyo tena sehemu yeyote ile ilimradi amekupita, yaani zile speed za miaka ile zimerudi tena na traffic hawana la kusema kwasababu jamaa alipigwa tochi mara 5 na bado hakupigwa cheti mpaka tunafika Mwanza.

Dereva wa bus alikuwa anaovertake mpaka malori matano hasa pale akiona mbele yake inakuja gari ndogo yaani utake usitake utasimama tu mpaka amalize kuovertake kumbe jamaa wanatudharau sana mpaka wanatuita wamama wa nyumbani (msemo huu alikuwa anautumia dereva wa bus akiwa anafanya fujo zake).

Nimeshuhudia kwenye vibao vya speed 50 magari madogo wanakatwa na traffic huku bus letu linapita tu tena na mwendo mdundo bila shida tena likiwa speed 102 hata ile alarm ya speed hakuna.

Nawashauri madereva wenzangu tembeeni usiku kuepusha majanga mchana haya mambo ya mchana tuwaachiwe wenye njia yao madereva wa mabus kwasabb kama kuna watu wanaenyoj barabaran ni watu wa mabus tu...Wale wenzangu na mm tusione tabu kuendesha usiku
 
Mabasi yanapeleka pesa kwa RTOs mwisho wa mwezi. Anaweza vunja sheria na asichukuliwe hatua.

Wewe endesha vile unakuwa comfortable.

Binafsi sipendi kuendesha usiku sana. Napenda niondoke alfajiri mpaka kuna kucha nimeshakata kama 250km.
 
pureView Zeiss

Kaka,

Unachosema ni kweli. Binafsi nimekua mtu wa kuendesha usiku mara kwa mara.

Na nimeenda mikoa mingi tu.

Ila changamoto kubwa ya usiku ni hawa watu wa malori na pia mambo ya uharifu zaidi sana iwapo utapata dharura.

Watu wa malory asilimia kubwa wengi wao hua hawazingatii sana sheria nyakati hizo za usiku.

Wamesha sababisha ajali nyingi mno barabarani (baadhi yao)

Kuhusiana na suala la mabus, hizo speed unazosema kaka ni speed zipi?
Mbona jamaa wanatembea vizuri tu, zaidi sana magari yote ya abiria sasa hivi yanaving'amuzi.

Sina hakika kama hakika kweli wanaenda rough hivyo.

Usiku ni raha, lakini ni hatari kubwa sana.
 
pureView Zeiss

Kaka,

Unachosema ni kweli. Binafsi nimekua mtu wa kuendesha usiku mara kwa mara.

Na nimeenda mikoa mingi tu....
Kuhusu speed aisee Kwenye haya Mabus niliyopanda hamna nilikaa mbele karibu na Dereva nimeona jamaa anapiga Hadi speed 127 km/h.....kama ujuavyo bus likiwa speed hiyo ni balaa yaani Ngoma inatembea balaa Hadi Mwanza nyegezi tumeingia saa 4:48 usiku
 
Kama u
Mabasi yanapeleka pesa kwa RTOs mwisho wa mwezi. Anaweza vunja sheria na asichukuliwe hatua.

Wewe endesha vile unakuwa comfortable.

Binafsi sipendi kuendesha usiku sana. Napenda niondoke alfajiri mpaka kuna kucha nimeshakata kama 250km.
Kama unaenda karibu haina shida Ila kama unaenda mbeya, songea,Mwanza na musoma lazima uanze Safar yako usiku
 
Kama u

Kama unaenda karibu haina shida Ila kama unaenda mbeya, songea,Mwanza na musoma lazima uanze Safar yako usiku
Safari kama ya Mwanza au Musoma either mnakuwa wawili au unalala njiani.

Kuondoka usiku sana kunafanya uchoke zaidi kuliko anaeondoka alfajiri.

Mf. Anaetoka saa 7 anachoka zaidi kuliko anaetoka saa 10 alfajiri.

Mkifika kati ya safari, wewe ulieondoka saa 7 upo likely kupata fatigue kuliko yule wa alfajiri.
 
Safari za usiku nzuri hujapatwa na janga kama breakdown nk

Nilikuwa nikisafiri usiku, siku moja porini kabisa hakuna watu bearing za nyuma zika jam. Sijawahi safiri tena usiku.

Pia niliwahi nusurika maeneo ya dakawa kupigwa na roli, nalipisha linajaa tu kwangu kesha vuka mstari wa kati unaotenganisha barabara.

Lakini pia usiku usisafiri kama gari yako haina beam ya kutosha taa za mbele. Barabara zetu ni mbovu sana hata za lami. Kukuta shimo katikati ya barabara ni kawaida sana

Mwaka 2013, baada ya kuvuka sekenke kutafuta vijiji vinavyofuata, almanusura na ingekuwa usiku pale na gari haina taa zenye mwanga, leo ningekuwa nishaihama Dunia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama u
Mabasi yanapeleka pesa kwa RTOs mwisho wa mwezi. Anaweza vunja sheria na asichukuliwe hatua.

Wewe endesha vile unakuwa comfortable.

Binafsi sipendi kuendesha usiku sana. Napenda niondoke alfajiri mpaka kuna kucha nimeshakata kama 250km.
Kama unaenda karibu haina shida Ila kama unaenda mbeya, songea,Mwanza na musoma lazima uanze Safar yako usiku
Safari kama ya Mwanza au Musoma either mnakuwa wawili au unalala njiani.

Kuondoka usiku sana kunafanya uchoke zaidi kuliko anaeondoka alfajiri.

Mf. Anaetoka saa 7 anachoka zaidi kuliko anaetoka saa 10 alfajiri.

Mkifika kati ya safari, wewe ulieondoka saa 7 upo likely kupata fatigue kuliko yule wa alfajiri.
Ni kweli kabisa hasa muda wa kuanzia saa 4 asubuh unakuwa Hoi Sana
 
Kama u

Kama unaenda karibu haina shida Ila kama unaenda mbeya, songea,Mwanza na musoma lazima uanze Safar yako usiku

Ni kweli kabisa hasa muda wa kuanzia saa 4 asubuh unakuwa Hoi Sana
Hapo itabidi utafute sehemu ulale kitu ambacho ungekifanya nyumbani kwako tu.

Safiri usiku kama una dharura kubwa, kinyume na hapo toka zako alfajiri ukaze.
 
Back
Top Bottom