Joseverest
JF-Expert Member
- Sep 25, 2013
- 52,812
- 71,392
SUBSCRIBED
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata dereva imara pia maana kuna kusababishiwa majanga unafanyaje?usiku kuna so many reckless drivers na malori yanapaki hovyo sanaNakumbuka kuna siku tulikuwa tunawahi harusi kesho yake. Tukatoka Mwanza saa 12 jioni ili tuingie Dar saa 2 au 3 asubuhi.
Kwenye gari kila mtu alilala, tukabaki mi na dereva tu tunapiga story.
Tukafika maeneo ya tabora nadhani igunga sijui mida ya saa 5 usiku, kitu kimewaka moto.
Hamadi kuna lorry kama mita 50 limezima kati ya barabara na halijaweka alama yeyote. Uzoefu wa dereva ulituokoa lasivyo tusingekuwa duniani leo.
Tulivyofika manyoni mida ya saa 7 hivi tukaamua kulala tu. Hatukuona sababu ya kuwahi tena mjini.
Safari za usiku zinahitaji chombo na dereva imara.
Mkuu safari za usiku nimefanya Sana Ila hatari ya kufa IPO nje nje Sana, ndugu zangu wengi wameshauri Sana kuhusu safari za usikuUsiku ni risk sana, niliwah safiri mara moja niliapa sirudii tena huo ujinga, ni bora hata nitumie siku mbili njiani!
Sasa mbona Uzi wako una 'promote' watu wasafiri usiku na sio mchana ?Mkuu safari za usiku nimefanya Sana Ila hatari ya kufa IPO nje nje Sana, ndugu zangu wengi wameshauri Sana kuhusu safari za usiku
Kipindi napost huu Uzi nilikuwa nasafiri usiku Tu ila ndugu zangu wamenihusia Sana kutofanya safari za usiku kutokana na macho yangu kusumbuaSasa mbona Uzi wako una 'promote' watu wasafiri usiku na sio mchana ?
Mimi nikiwa naendesha gari hata mjini usiku huwa sipendelei sana. uoni unakuwa hafifu sana na vurugu zinakuwa nyingi hasa usiku mnene.Kipindi napost huu Uzi nilikuwa nasafiri usiku Tu ila ndugu zangu wamenihusia Sana kutofanya safari za usiku kutokana na macho yangu kusumbua
Starlet ni chuma cha pua,labda iwe ni mbovu tuNaogopa sana safari ndefu, Nina kistalet mwaka wa nne sass sijawah kwenda hata km200, December hii labda nijaribu!