Ushauri wa Bure: Ukijikwaa ukaanguka, usiangalie tu pale ulipoangukia, bali angalia pale ulipojikwaa

Pale hamna Case ndugu, Zittow alijua hatoshinda akaachana na case, wamama Hawa pia hawatoboi.

Achana na hii issue inaondoa CREDIBILITY Yako. Kuna kesho ujue.
 
Hujawahi kuwa na nia njema na Chadema hata siku moja,utabakia kuwa adui wa Chadema kama alivyokuwa yule dhalim aliyetumia mabilioni ya kodi zetu na mitutu ya bunduki kuiangamiza Chadema matokeo yake kaangamia yeye.
 
Huwa unakuja na thread zako kuonesha kama vile una jambo jipya, lakini kwa msomaji aliyekuzoea, na anayejitambua upstairs, ataona bado unazunguka pale pale.
Mkuu denooJ , there is nothing new under the sun, hivyo hakuna kipya chini ya jua.
Sisi kwenye tasnia ya habari, kuna stories ambazo ni completing stories, tukio linatokea, linaisha na likiripotiwa the story ends up there.

Lakini kuna matukio yanaitwa a developing stories, yaani ni tukio muendelezo, tukio limetokea na kila siku new things vina unfold, hivyo the story goes on and on.
Hivyo hili saga la wabunge 19 wa Chadema, ni a developing story, hii ngoma bado ni mbichi, hivyo kila siku there is something new.
Thread zako nyingi kuizungumzia Chadema na hao covid huwa unakuja na allegations pekee, unatoa shutuma lakini kwa makusudi huwataji kwa majina unaowalaumu, ili tu uwalinde rafiki zako wasaliti waliowahi kufukuzwa Chadema.
Ma great thinkers huwa hawajadili watu, tunajadili ideas. It's true nawajua kwa majina ila sina sababu ya kutaja majina mfano namjua huyu Voices From Within: Unaweza usiamini! Aliyetoa A Go ahead kwa Mdee na Wenzake ni Kigogo wa Chadema!. Alikuwepo Ukumbini na Vikaoni! Je, ni nani? lakini simtaji, au najua CHADEMA Kuna Kirusi! Je, Unajua kirusi hiki ni Nani?! Na The Motive Behind?
Nikwambie kitu, kama kweli unakiamini unachoandika kuhusu kuwatetea hao unaodai wameonewa, wataje kwa majina wale waliowaonea, na uoneshe kwa ushahidi ni kwa vipi walihusika kwenye huo uonevu, lakini kinyume na hapo, wacha kuchezea akili za watu bro.
Bandiko hili ni kuhusu haki bin haki, nimeonyesha jinsi Zitto Kabwe alivyohunumiwa kwa uonevu na kuzungumzia bakora za karma zilivyo watandika wahusika. Mtu ukikumbwa na janga lolote, kama una jicho la ndani ndio utagundua ni karma, it's very unfortunately Chadema hawana hilo jicho la ndani, nilichofanya kwenye uzi huu ni kuwaazima Chadema jicho langu la ndani ili kuzuia majanga zaidi.
Jina la Mwandishi wa ule Waraka doesn't matter much but the contents, jee we wewe mwenzetu uliusoma ule Waraka wa Mabadiliko?. Ningekuwa CC ya CHADEMA ningemsamehe Kitila Mkumbo
Hiki ndicho hiki nilichosema hapa, Chadema ina katiba sheria taratibu na kanuni, kwanini hazifuatwi?. Mmezoea vya kunyonga hamviwezi vya kuchinja. Hongera sana Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji

Na hapa Ni Ubatili Mtupu Mpaka Basi!. CC ya CHADEMA ilipata wapi mamlaka?. Baraza Kuu halina mamlaka hiyo!. Je, inawezekana CHADEMA ni chama majanga ila?

Na Chadema pia tumewashauri Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi
P.
 
Hapo kwenye kureport polisi, kwa jeshi lipi la polisi lingewasaidia chadema zama za Bwana yule!?

Chadema wanapitia magumu , hata uhai wa chama chao wanastahil pongezi za dhat
 
Pascal Mayalla
1) Policcm hawawezi kuchunguza chochote kwa weledi kitakacho inufaisha Chadema (rejea mwenendo wao kwenye kesi ya Mbowe)
Mkuu Babu Ochu , kuna kitu kinaitwa hisia Vs realty, katika kufanya baadhi ya mambo ni lazima Chadema wajifunze kuachana na hisia na and do the right thing.

There is no any other way Chadema wanaweza kuiona barua ya uteuzi kutoka Chadema kwenda NEC, nje ya uchunguzi wa kijinai.

Jeshi la polisi ndio maana rasmi ya uchunguzi, hata kama Chadema wanaweza kutumia njia yoyote kuipata barua ya uteuzi kutoka Chadema kwenda NEC iliyopitisha majina hayo 19, na ikajiridhisha ni forgery, mamlaka pekee ya kuwaeleza NEC it's forgery ni Jeshi la polisi. Tuweke hisia pembeni, lets face the reality.
2)Vivyo hivyo kwa mahakimu ambao Lissu anaowaita majaji wa Magufuli na kesi hii (mark my words) haitasha hadi 2025
Kwenye hii issue ya forgery, ni kesi ya jinai na sio kesi ya Chadema!. Hapa Chadema ni Shahidi number 1. Kama Chadema wange ripoti polisi na kuuthibisha forgery, saa hizi saa nyingi NEC ingeisha watengua.
P
 
Acha njaa zilizopitiliza nafahamu unajipendekeza ili upate vitenda vya kufanya PA sabasaba kutoka Kwenye taasisi za ccm.
Unafahamu kabisa pasipo shaka kwamba hakuna kikao chochote cha chadema kilichokaa na kupitisha majina Yale kama katiba inavyoeleza unajifanya huoni hilo.
Yule nusrat alikuwa mahabusu wakatolewa Bila kufata tararibu za kimahakama wala za kipolisi akasafiri usiku kwenda dodoma kuapishwa kesho yake.. Sijawahi kushuhudia toka nijielewe wabunge kuapishwa kihuni namna ile alivyofanya ndugai nje ya utaratibu wa kuapishwa Kwa wabunge
Wewe jamaa unajishushia hadhi Kwa mabandiko yako ya kinafki.
Watu wote wanaojielewa wanajua suala la kina covid 19 limeshakwisha sio tena wana chadema na Kwa mujibu wa katiba hawastahili kuwa wabunge
Na kama kwenda polisi Kwa nini NEC baada ya malalamiko ya chadema wao NEC wasiripoti polisi ili waichunguze hiyo barua kama ni ya kweli au sio kwani wao ndio wamedanganywa
 
We kada na hii ni"MASLAHI MAPANA KWA TAIFA" ama?
 
Paskali mimi ni fan wa liver kwahiyo maisha yangu yote ni kuiombea mabaya man u sasa wewe kutoa ushauri kwa cdm wakati ni kada mtiifu huo ni uongo wa dhahiri, kuhusu kovid 19 kuwa bungeni wewe mwenyewe nafsi yako inafahamu nini kilitokea, ndiomaana watu wanashindwa kujadili mada wanakujadili wewe. CDM inafanya hatua zake ili mwisho wa siku ibaki kwenye kumbukumbu walichukua hatua chamani, wakina mdee hawatatoka mule hadi waliowaingiza waamue kuwatoa
 
Naona Naona
Chadema wapo sahihi. Chama lazima kiheshimiwe hata Kama mtu ana ushawishi kiasi gani.
 
Kama
Kwa hivyo waliandika barua halafu wakaja kuwafukuza?. Yani chama kinakuteua halafu kinakufukuza , huoni unadanganya.
 

Please, Zitto hakufukuzwa Bali alijifukuzisha baada ya kwenda mahakamani na akabwagwa.
 

Deep state ndio Nini? Acheni kutukuza watu as if Wana akili kuliko malaika wakaita Ni wakawaida. Ingekuwa anachoongea ni kweli nguvu isingetumika dhidi ya CHADEMA. Ukiona risasi na kesi za ajabu zinatumika na serikali ujue uwezo wa serikali wa kufikiri umefikia
 
Bado unazunguka tu, kusema GT huwa hawajadili watu ndiko unakutumia kama kichaka cha kujifichia, ili uendelee kuja na hizi thread zako zinazoelea siku za mbeleni.

Unataka Kitila Mkumbo asamehewe kwasababu ipi? wale watu walileta ujuaji mwingi wakati ule, na adhabu waliyoipata waliistahili, walipewa nafasi ya kujitetea hawakuomba msamaha, walijaa viburi kama hawa Covid wa sasa, nipe ushahidi kuonesha waliomba msamaha kama unao, vinginevyo huwezi kuwasamehe wasiokiri kosa.

Kama mpaka leo bado unaamini ule uamuzi wa Spika Tulia kuwaacha kina Mdee wakae bungeni sababu wana kesi mahakamani ulikuwa sahihi, hapa ndipo unapodhihirisha nia yako ovu kila unapokuja na hili suala.

Chadema imewafukuza uanachama wakina Mdee, sheria inataka mbunge awe anawakilisha chama cha siasa bungeni, wakina Mdee baada ya kufukuzwa wanapoteza sifa ya kuwa wawakilishi kupitia Chadema.

Kama wanataka kurudi bungeni sharti washinde kesi yao mahakamani ndipo warudishiwe uanachama wao wa Chadema ili wawe na sifa ya kuwa wabunge.

Hapa sheria imevunjwa na Spika ambaye ni "gwiji wa sheria" nawe mjuvi wa sheria mwenye "banda" la "constitutional law" unatetea huu uvunjifu wa sheria, halafu ajabu unawalaumu Chadema kila siku hawatendi haki, wakati walifuata sheria na taratibu zao kuwaadhibu wale wanawake, hueleweki bro.

Ukiondoa zile makala zako unazoandika kwa "maslahi ya taifa", hizi zinazoizungumzia Chadema kuhusu wale Covid huwa unaziandika kwa "maslahi ya CCM" yako, nothing more.
 

Polisi gani? Hawa waliopo kuididimiza CHADEMA ?. Acha unafiki, Lissu alipigwa risasi hakuna uchunguzi wanadai Lissu aje atoe ushahidi je angekufa?
 
Bado unazunguka tu, kusema GT huwa hawajadili watu ndiko unakutumia kama kichaka cha kujifichia, ili uendelee kuja na hizi thread zako zinazoelea siku za mbeleni.
Hii issue ya hawa mashujaa Wabunge 19 wa Chadema walioipigania Chadema kwa machozi jasho na damu, ni a developing story na a continuous story, inaendelea natunaendelea nayo mpaka iishe, hivyo Mkuu denooJ have popcorns za kutosha, sit and watch, it's not over until it's over!
Unataka Kitila Mkumbo asamehewe kwasababu ipi?
Kiukweli nataka Kitila asamehewe kwasababu Chadema wote waliopo mpaka leo mpaka kesho, haina mtu wa kalibre ya Kitila, kwa 2025, Kitila hatapitishwa popote CCM kwa sababu fulani, lakini akigombea popote kupitia chama chochote atashinda, hivyo Kitila ni fursa, anaweza kurudia kulamba matapishi yake akarejea ACT, au Chadema mkimhitaji Chadema ndio imuombe msamaha, lakini kwa vile yeye ni academician anaweza kuamua kustaafu siasi na kurejea kwenye academia pale pale UDSM au chuo chochote tena sasa ni kwa level ya kamsela!.
No sio walileta ujuaji mwingi, ni wajuaji kiukweli, hebu niambia baada ya kumtimua Kitila, Chadema ina think tank gani?. Watu walioona madhaifu ya Chadema, wakafanya study ya jinsi ya kuiokoa Chadema, wakaandiko andiko "Waraka wa Mabadiliko", Chadema baada ya kuupata waraka ule, badala ya kuzifanyia kazi hoja za waraka ule, wao wakajikita kwenye dhana ya usaliti, waombe msamaha wa nini?, wewe unaombwa usaidiwe unakataa msaada anayetaka kukusaidia ndio akuombe msamaha, what for? kwa kosa lipi?. Kitila ni mtaji ambao umekalia kuti kavu CCM.
Kama mpaka leo bado unaamini ule uamuzi wa Spika Tulia kuwaacha kina Mdee wakae bungeni sababu wana kesi mahakamani ulikuwa sahihi, hapa ndipo unapodhihirisha nia yako ovu kila unapokuja na hili suala.
Haya sio mambo ya imani kusema ninaamini, haya ni mambo ya facts, rules and regulations hili nimelisemea vizuri kabisa hapa Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi
Hapa ndipo mahali ambapo watu kama akina sisi tunahitajika sana, kuielimisha jamii na umma. Vyama vya siasa viko kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, na uanachama wa chama cha siasa ni kwa mijibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, vivyo hivyo kwenye kufutwa uanachama, uanachama pia unafutwa kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni. Kichadema imewafuta uanachama wao, hao sii wanachama wake, lakini kwa sababu ufutaja wa uanachama wao, umefanywa kihuni huni tuu, kiukweli na kiuhalisiana kikatiba, hao bado ni wanachama halali wa Chadema ndio maana bado ni wabunge!. Kunapotokea mgongano wowote kati ya katiba na sheria au taasisi yoyote, katiba will prevail. Hili pia ni somo nililiendesha humu Je, wajua Vyama vya Siasa TZ ni Public Parties? Maamuzi yake lazima yazingatie Public Interest na siyo kufuata ujinga na ubinafsi wa viongozi insane!
Hapa sheria imevunjwa na Spika ambaye ni "gwiji wa sheria" nawe mjuvi wa sheria mwenye "banda" la "constitutional law"
Mkuu denooJ kwanza asante kwa your recognition ya lile "banda" la "constitutional law" nililolipata rasmi 2007 baada ya kugraduate LL.B, UDSM, more than 15 years ago!, kwa vile I have always been a journalist, nimerealize kuwa na "banda" la "constitutional law" ambalo hulifanyii kitu chochote zaidi ya kuandika humu jf, kuwa nina "banda" la "constitutional law", haisaidii kitu, hivyo nimeamua kuanzia mwezi ujao, nitaanza ku run both concurrently as a journalist and as a lawyer ili hilo banda nikalifanyie kazi kuisaidia jamii, hivyo nitalitendea haki banda langu kwa kutoa elimu ya katiba kwa umma kupitia TV series.

unatetea huu uvunjifu wa sheria, halafu ajabu unawalaumu Chadema kila siku hawatendi haki, wakati walifuata sheria na taratibu zao kuwaadhibu wale wanawake, hueleweki bro.
Hapa Mkuu denooJ nakuomba sana be honest kwasababu hapa ndipo karma inapolalia, Chadema walifuata sheria na taratibu zao kuwaadhibu, naomba unielimishe walifuata vipi?. Ikikupendeza anzisha uzi wa jinsi Chadema inavyofuata katiba yake, sheria, taratibu na kanuni katika kuwaadhibu watovu mbalimbali wa nidhamu ndani ya chama.
Vinginevyo ukipata muda, pitia nyuzi hizi, humu ujibu Chadema ilifanyagaje
Anza na
Hapa Uamuzi wa CHADEMA dhidi ya madiwani: "A Big Mistake!"
Kisha hapa Wito: CHADEMA Watendeeni Haki Wanachama Wenu Ili Kuwatendea Haki Watanzania 2015!
Kisha Opinion: Kung'atuka Kwa Zitto, CHADEMA, Msishangilie, Mkajisahau, Jiandaeni kwa "Karma!"
Na sasa Mmezoea vya kunyonga hamviwezi vya kuchinja. Hongera sana Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji
Ukiondoa zile makala zako unazoandika kwa "maslahi ya taifa", hizi zinazoizungumzia Chadema kuhusu wale Covid huwa unaziandika kwa "maslahi ya CCM" yako, nothing more.
Hapa tena Mkuu denooJ naomba nikupe big up, kwasababu "you have the powers from within!". Kwanza nasema asante kwa kuzikubali makala zangu za kwa kwa maslahi ya taifa na makala ya leo ni HII HAPA YA FUPA LILIWASHINDA WATANGULIZI,
Nimekupa big up na kukupongeza kuwa you have the powers za jicho la ndani la kubaini kina ninachoandika kuwatetea hao wabunge 19, huwa naandika kwa maslahi ya CCM and nothing more!. Yaani unanifanya nijione kama mwanga aliyebambwa akiwanga barazani kwa watu alfajiri akiwa kama alivyozaliwa!. Hiki ninachofanya kwenye bandiko hili ni kuisaidia Chadema, kwa Zitto ilijikwaa, ikaanguka, na ikala kichapo cha bakora za karma za kutosha, kwa hili la Halima Mdee, Chadema imejikwaa tena!, hivi karma wenzetu hamzioni?, mbona hamuisaidii Chadema kuziepuka?. Unamjua aliyebeba the heaviest load ya karma ya Zitto ni nani and how hard it hits na the consequences, mimi namjua atakayebaba karma ya kina Mdee, mimi sio Chadema, naogopa, kumbe kuna watu mnamacho, mbona hamuisaidii Chadema?. Isipotenda haki this time, take it from from me, the consequences will be devastating!.

P.
 
Na siku watakayo thibitishwa kufurushwa kwao, sina shaka UTAPOTEZA FAHAMU kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…