Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Juzi tu NMB Dodoma:

Jamaa flan kavaavaa tu afu na midevudevu hivi

Kaenda NMB ATM kakuta na wadada wa benki wameweka meza ya kutoa huduma kwa wateja pemben hapo. Akafika tu kauliza (bila hata kusalimia).....kwanini kadi yangu inakataa kuniunganisha NMB mkononi

Dada kamjia juu...."kwanza salimia;...vipi habari za huko,...haya tukusaidie nini??"

Jamaa hakupokea. Mie nawaangalia tu.

Dada karudia tena ...."vipi mzima mwenzetu?? Za ulikotoka??!.....mbona umekuja kasi sana??!"....

Jamaa anaeaangalia tu. Mara akauliza...."ivi ni lazima kusalimia/ au kupokea salam ya mhudumu ili nipewe huduma NMB???...

Wakaanza kumshangaa ..."unatokea wapi wewe, yani unakuja kuvamia tu bila kusalimia..." ....wamamzodoa flan.

Jamaa akaingia Benki ndani. Straight kwa Meneja. Nafkiri hakueleza shida aliyopata nje. Alimueleza tu kama kutaka kusaidiwa shida yake. Sijui ndani waliongea nini??

Wametoka na meneja...hadi pale ATM kwenye meza ya wale wadada....meneja akiwa kashika mkononi kadi ya yule mshua....akawambia wale wadada mmoja wao (sikumbuki jina)...

Meneja: .....hebu msaidie Katibu Mkuu hapa kumuunganisha na NMB Mkononi...(Meneja akaongeza:....mkuu hapa utahudumiwa)...mara meneja katuomba wote wa kwenye foleni ya ATM..."naomba ndugu tumpishe kiongozi anajambo kidogo kwenye ATM ...samahani"...wakaingia ATM meneja, mshua na yule dada.

Wakafanya mambo humo ...kidogo wakatoka. Tukaendelea.

Meneja akamsindikiza yule mshua hadi kwenye gari akaondoka meneja anapunga mkono.

Niliwaangalia wale akina dada mavi yalivyowagonga chupi. Walitoa macho sana wakawa na wasiwasi mkubwa....

Walimchukulia poa
Huyo katibu mkuu nae atakuwa siyo mstaarabu tu. Kusalimia watu kwake ni shida? Ni mmoja wa wale waliolewa madaraka.
 
hapana mkuu ,wakati mwingine wakuu zetu katika kazi huwa wanataka kujua kitu flani kupitia njia tofauti tofauti..mf
Mwaka 2013 huko kwetu ( ) kuna kiongozi mkubwa sana wa taifa hili alikuja sehemu kama mwananchi wa kawaida huku akiwa amevaa shuka za kimasai na kofia zile za pama..baadae sana baada ya kuondoka ndio ikajulikana kama ni boss wa taifa kaingia hapa.
Huyo katibu mkuu nae atakuwa siyo mstaarabu tu. Kusalimia watu kwake ni shida? Ni mmoja wa wale waliolewa madaraka.
 
Kuna siku niliazima gari nikaenda pale best bite kuchukua zaga.

Sasa nilivyoingia ndani nikakutana na pisi tatu za kwenda zinatoka ndani, nikazipa hi zikachuna full kunipandisha na kunishusha, nikaona POA tu nikafuata kilichonipeleka.

Sasa ile natoka nje nikazikuta ziko bize zinajisnap kwenye gari niliyokua nayo, hiiiiiiiiii bagoshaaa, mbona walikoma kunijua.

Nilianzisha zogo la maana makusudi kabisa, nikaita mpaka uongozi wa pale nikawaambia wawaambie wateja wao wafute picha zote walizopiga gari yangu otherwise niite Askari pale obey waniambie Wana lengo gani na picha za mkwaju wangu?
Jamani Mimi Nina mwili mdogo halafu ni mfupi dharau ninazopitia duniani hapa huwa naishia kucheka.siku moja naenda kazini niko kituoni daladala inakuja ile naanza kuingia konda akanisukuma akasema kwa sauti sipakii mwanafunzi.nikambembeleza akanipakia nikatoa 200 na miaka yangu 30
 
Jamani Mimi Nina mwili mdogo halafu ni mfupi dharau ninazopitia duniani hapa huwa naishia kucheka.siku moja naenda kazini niko kituoni daladala inakuja ile naanza kuingia konda akanisukuma akasema kwa sauti sipakii mwanafunzi.nikambembeleza akanipakia nikatoa 200 na miaka yangu 30
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Mimi kuna siku tena ni zaidi ya mara moja inanitokea, mara ya kwanza ilikuwa pale nje ya wizara ya ardhi niliegesha gari pembeni nikanunue gazeti narudi nakuta wale majamaa wamelifunga.
Nikaanza zozana nao wao jibu wanalonipa kamwite mwenye gari. Yani kila nalowambia wananiambia mwenye gari atalipa we unahangaika nini kamwite mwenye gari, dah ila mwisho nikampa 20,000 akalifungua nikasepa.
Mara nyingine nilikuwa pitiliza mataa wakati taa zimezuia, kumbe mbele kuna traffic, akandaka. Akaanza kunisngekuwa na boss wako usingefanya hivi na maneno mengi. Baadae, akaniomba leseni na kadi ya gari nikampatia akakuta kadi ya gari ina jina sawa na leseni. Akasema kumbe gari lako nikamjibu ndiyo, akaishia kucheka akasema yani watoto wa kishua bwana mnakula maisha kwa pesa ya baba zenu. Mimi nikacheka tu akaniandikia faini nikasepa huku nikiwaza ungejua mimi mpambanaji tu.
Mara nyingine niliacha gari lilikuwa na matatizo na mimi nina haraka nikalipaki pembeni ya barabara nikachukue boda boda, kumbe huku nyuma askari wakapita lipo, wakapita tena lipo ikabidi watanaze times ambaye katelekeza gari akalichukue mimi sikuwa na habari. Narudi baadae kulichukua nikiwa na fundi, gari silioni, namuuliza muuza matunda ndiye akaniambia wamelibeba wamelipeleka kituo cha polisi cha kawe. Kesho yake naenda kawe mkuu wa kituo akawa ananizngua kuwa nikamtafute mwenye gari, mpaka nilipofungua nikamwonyesha kitambulisho na kadi ya gari majina yana match. Aliniambia tu niwalipe waliolivuta nisepe tu.
Yani mimi nina mwili mdogo kama wa Mrehemu Ruge Mtahaba, nakutana ma mazarau sana maana hata nikivaa suti haikai ni kama imetundikwa tu.
Hahahahah pole mkuu nenepa kidogo
 
Kwanza naomba 'nidiclee' kwamba mm ni mmoja wa ME ambae si mtu wa fashion, yani mimi sijui kuvaa kabisa na sina hiyo passion ya pamba pamba. Nishawahi kusemwa sana na ma-ex wangu kuhusu uvaaji wangu lakini haikusaidia kitu.

Sasa weekend iliyopita nilienda sehemu moja flani hivi amazing, chimbo la uhakika haswaa, limejitenga na limetulia kweli. Nilipigilia kipensi changu na ka t-shirt flan hivi local nikachagua sehem nikakaa, kutizama vizuri nikaona kuna meza amekaa mdada mmoja hivi and of coz she is gud looking nikaamua kujitosa angalau kumpa hata hi 'coz tulikuwa wateja 2 tu, nikamfata nikamsalimu.

Yule dada kwanza alinishusha kuanzia juu mpaka chini then akaitikia salamu yangu ki-design kama namsumbua flani hivi. Nikaomba kujumuika nae kama asipojali. Jibu lake ndo lilinitoa confidence kabsa, alinambia: "Kwahiyo kaka unadhani kila msichana akikaa peke yake anahitaji kampani? Hapana sihitaji" Dah, mwanamme nikajizoazoa pale nikarudi nilipokaa. Nilikaa kama masaa ma3 hivi nikaamsha zangu. Sasa kilichotokea jana ndo kimenifanya niandike huu uzi.

Nilipokea maagizo kuanzia J3 ya wiki hii kuwa leo watakuja watu wa Taasisi flani ya kifedha kutoa semina kwa sisi wafanyakazi kwa ajili ya kutushawishi kujiunga na huduma za Taasisi yao, hivyo mimi nikapewa jukumu la kuwakaribisha na kuwapeleka sehemu ambapo semina itafanyika.

Asubuhi mida kama ya saa 3 hv ugeni ukafika, walikuwa watu kama 7 hivi, kati yao alikuwepo yule dada nilieonana naye weekend.

Wakaingia ofisini nikawakaribisha, wakati mkubwa wao anatoa introduction macho nikayakaza kwa yule dada, bahati nzuri tukagonganisha macho, akashtuka flani, nikajua kashanikumbuka.

Baada ya semina kuisha ikafika kipindi cha watu kujiunga sasa kwa walioshawishika. Nikamfata yule dada nikamuomba aje anielekeze namna ya ujazaji fomu. Alivyofika tu, nikamuuliza "Unanikumbuka?" Akachekaaa, akaniambia "Yani wewe, sikutarajia kama unaweza kuwa unafanya kazi huku", nikamuuliza ulitarajia niwe nafanya kazi wapi? Akaishia kucheka tu. Mawasiliano yake kanipa; fresh bila shida kabisa.

Sasa naomba kuuliza wadau, mshawahi kukutana na situation ya namna hii?

Mimi kuna 'Wajeda' Wawili hivi nakumbuka Siku moja nilikumbana nao 'Kichochoroni' wakiwa 'wamemkwida' Dada Mmoja hivi wa 'Kitaani' huku wakiwa 'Wanampiga' na Yule Dada akiwa 'anawatukana' Matusi makubwa makubwa tu. Na huyu Dada nakumbuka amekuwa 'akinipuuza' mno tu pengine kutokana na 'Ukapuku / Umasikini' wangu ( kama tuwajuavyo Dada zetu wa Dot Com Generation walivyo )

Baada ya Yule Dada kuanza 'Kuwatukana' wale 'Wajeda' nao sasa wakaamua kuanza kumpa 'Mateso' yao makali ya 'Kijeda' nikaanza Kumsikia Yule akianza 'Kujamba' bila utaratibu 'Maalum' na 'Kutapika' ndipo nami kwa 'Ujasiri' wangu mkubwa 'niliobarikiwa' nao na Mwenyezi Mungu 'Kiustaarabu' kabisa nikawaomba wale 'Wajeda' wasiendelee 'Kumuadhibu' ambapo kwa 'Kuhiheshimu' kweli wakaacha na nikaanza Kuwasomesha.

Sijui nina 'Hirizi' gani ya Asili ambayo hata kama nikikutana na Watu wenye 'Hasira' Kali nikianza 'Kuwaimbisha' tu upesi wanaanza 'Kulegea' kisha tunakuwa 'Marafiki' na Maisha yanasonga mbele. Nilipomaliza tu Kuwaimbisha wale 'Wajeda' nikasikia wanamuambia Yule Dada kuwa ana bahati Mimi nimewaonyesha 'Uungwana' japo ni Raia Mwema tu ila walichokuwa wamepanga Kumfanyia aliyekuwa akijua ni Shetani Lucifa tu pekee.

Cha 'Kushangaza' sasa baada ya Kumalizana tu pale na wale 'Wajeda' na Yule Dada ambaye mara nyingi alikuwa 'akinipuuza' alianza Zoezi la Kutafuta ninapoishi mpaka namba yangu ya Simu na alipofanikiwa akaniambia kwa aina ya 'Ujasiri' ule na 'Kumuokoa' Kwangu kule Siku yoyote ile nikiihitaji 'Mbunye' yake niseme ila nikamwambia ya kwamba huwa simsaidii Mtu kwa Malipo bali ni Utu wangu tu na kama ni 'Umasikini' nimeshauzoea.

Tuacheni 'Kupuuziana' na 'Kudharauliana' tafadhali kwani huwezi jua ni nani 'atakusaidia' au 'kukuokoa' hapa duniani na wengine wameshabarikiwa.
 
Juzi tu NMB Dodoma:

Jamaa flan kavaavaa tu afu na midevudevu hivi

Kaenda NMB ATM kakuta na wadada wa benki wameweka meza ya kutoa huduma kwa wateja pemben hapo. Akafika tu kauliza (bila hata kusalimia).....kwanini kadi yangu inakataa kuniunganisha NMB mkononi

Dada kamjia juu...."kwanza salimia;...vipi habari za huko,...haya tukusaidie nini??"

Jamaa hakupokea. Mie nawaangalia tu.

Dada karudia tena ...."vipi mzima mwenzetu?? Za ulikotoka??!.....mbona umekuja kasi sana??!"....

Jamaa anaeaangalia tu. Mara akauliza...."ivi ni lazima kusalimia/ au kupokea salam ya mhudumu ili nipewe huduma NMB???...

Wakaanza kumshangaa ..."unatokea wapi wewe, yani unakuja kuvamia tu bila kusalimia..." ....wamamzodoa flan.

Jamaa akaingia Benki ndani. Straight kwa Meneja. Nafkiri hakueleza shida aliyopata nje. Alimueleza tu kama kutaka kusaidiwa shida yake. Sijui ndani waliongea nini??

Wametoka na meneja...hadi pale ATM kwenye meza ya wale wadada....meneja akiwa kashika mkononi kadi ya yule mshua....akawambia wale wadada mmoja wao (sikumbuki jina)...

Meneja: .....hebu msaidie Katibu Mkuu hapa kumuunganisha na NMB Mkononi...(Meneja akaongeza:....mkuu hapa utahudumiwa)...mara meneja katuomba wote wa kwenye foleni ya ATM..."naomba ndugu tumpishe kiongozi anajambo kidogo kwenye ATM ...samahani"...wakaingia ATM meneja, mshua na yule dada.

Wakafanya mambo humo ...kidogo wakatoka. Tukaendelea.

Meneja akamsindikiza yule mshua hadi kwenye gari akaondoka meneja anapunga mkono.

Niliwaangalia wale akina dada mavi yalivyowagonga chupi. Walitoa macho sana wakawa na wasiwasi mkubwa....

Walimchukulia poa
Hahahahah nimecheka kweli

Ila wanawake huwa wadhaifu sana na first appearance wanaleta madharau San

Hata Mimi ushawahi nitokea sana

Baadae huwa wanakuja kuwa washkaji[emoji1787]
 
Hahahahah nimecheka kweli

Ila wanawake huwa wadhaifu sana na first appearance wanaleta madharau San

Hata Mimi ushawahi nitokea sana

Baadae huwa wanakuja kuwa washkaji[emoji1787]
Heheh kwako ilikuaje mkuu?
 
hapana mkuu ,wakati mwingine wakuu zetu katika kazi huwa wanataka kujua kitu flani kupitia njia tofauti tofauti..mf
Mwaka 2013 huko kwetu ( ) kuna kiongozi mkubwa sana wa taifa hili alikuja sehemu kama mwananchi wa kawaida huku akiwa amevaa shuka za kimasai na kofia zile za pama..baadae sana baada ya kuondoka ndio ikajulikana kama ni boss wa taifa kaingia hapa.
Jamaa ilikuwa ndio zake anaibuka ghafla tu nyie hamjui

Halafu baadae ndio mnashtuka

Huya wa Sasa Hana hizo guts
 
Wanaume mnaolalamika wanawake wanawadharau, sasa, kama umevaa na kukaa hovyo unategemea nini?
Mbona hamshobokei wanawake walio hovyo kama ni kweli hamtilii maanani outward appearance? Mjitafakari
Kingine, inaonekana tunashida kubwa kwenye maadili yetu. Kwanini tunaambizana ya kuwa tunatakiwa tuheshimu watu wote kwasababu anaweza kuwa na kazi nzuri au unaweza kupata shida akakusaidia nk? Kwanini tusifundishane kuheshimiana kwa upendo kutoka moyoni kuliko kutishana? Hi ndio sababu tunakua wanafiki na chini kwa chini tunachukiana.
Mimi binafsi uwe muokota machupa jalalani au meneja wa wapi, nita watreat sawa bila kujali chochote. Ndio maana kwa watu wenye position kubwa au wanaotegemea special treatment kutoka kwangu wananiona nina dharau, ili hali wale watu wanadharaulika na jamii wananiona sina shida yeyote.
Kuhusu kudharaulika kwasababu ya muonekano wa nje, sijawahi. Sana sana watu wakiniona matarajio yao yanazidi hata uhalisia wangu. Lakini watu wengi, hasa wanaume wananiona nipo shallow kichwani (sexism). Wanahisi siwezi kufanya maamuzi magumu, kuchanganua mambo, kutetea hoja au kuwa na skills kwenye male-dominant fields. Wanahisi nipo kama pambo na nikiwaprove wrong kuna wanaofurahi na kuna wanaonichukia na kunipiga vitu kwa nguvu zao zote.
 
Kuna manager wa hotel fulani kubwa tu. Alitusimulia kuwa siku moja akiwa ndio manager wa zamu akaitwa na muhudumu wa mapokezi shida ikiwa kuna mgeni kachoka choka hivi lakini anahitaji room ya bei mbaya pale hotelini.
Sasa muhudumu wa mapokezi akamwambia mgeni mchovu angoje kidogo akamuonyesha na pa kupumzikia ili amuandalie hiyo room uku ikiwa ni kupata muda ili amwambie manager kuhusu kumpa chumba cha bei mbaya jamaa.
Manager kumuona mgeni alivyo ikabidi aende kuongea nae.mshtuko ukampata baada ya mager kujitambulisha jamaa nae akajitambulisha jina ndipo akajuwa jamaa ni footballer mkubwa tu duniani na jezi aliyovaa juu ni ya timu yake ya taifa.mara moja akapewa room bila hata maswali mengi.
 
nakumbuka kuna kidemu kilikua kinanidharau sana enzi hizo bush, basi nilivyomaliza shule pale kijijini nikaondoka kwenda Dar ikapitwa miaka 4 nikasikia kapewa mimba na aliyempa mimba nimshikaji niliesoma naye na alipewa mimba akiwa bado anasoma, basi kwakuwa jamaa nayeye alikua na ndg Dar ikabidi wakimbilie Dar es salaam kwa ndg wa mshikaji baada ya mwaka mmoja kupita ndipo wakashauriwa waende hospital kwa ajili ya kufanya uzazi wa mpango na hospital ilikua maeneo ninayoishi basi mshikaji ndg yake akamwambia nenda utamkuta rafiki yako uliesoma naye akuelekeze bwana weee

si wakaja mpaka home yule demu hakuamin kama ndiyo mimi aliekuwa ananidharau kule bush basi nikawasindikiza mpaka hospitalini kisha tukarudi nikawapeleka mpaka stendi yule demu nafsi ilimsuta sana mpaka aliamua kunitumia sms akisema kweli nimeamini usimdharau mtu ktk hii Dunia nilikuwa nakuchukulia poa poa kijijini leo unaijua mitaa ya Dar kiasi hiki na umetupeleka mpaka hospitali

aliishia kusema nisamehe, nami sikumjibu maskini.
 
Huyo katibu mkuu nae atakuwa siyo mstaarabu tu. Kusalimia watu kwake ni shida? Ni mmoja wa wale waliolewa madaraka.
Huwezi nilazimisha nikusalimie wakati wa kupokea huduma. Sio lazima kabisa wala haiongezi au kupunguza chochote.
Nikija customer care nahitaji huduma, salamu naweza enda shule ya msingi wakanisalimia watu zaidi ya 1000 na shida yangu isitatuliwe.
 
Huwezi nilazimisha nikusalimie wakati wa kupokea huduma. Sio lazima kabisa wala haiongezi au kupunguza chochote.
Nikija customer care nahitaji huduma, salamu naweza enda shule ya msingi wakanisalimia watu zaidi ya 1000 na shida yangu isitatuliwe.
Hakuna anaekulazimisha kusalimia. Lakini ustaarabu wa mtu uanzia hapo kwenye salaam. Ukisalimia utapoteza nini na utatumia masaa mangapi?
 
Back
Top Bottom