Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

hapana mkuu ,wakati mwingine wakuu zetu katika kazi huwa wanataka kujua kitu flani kupitia njia tofauti tofauti..mf
Mwaka 2013 huko kwetu ( ) kuna kiongozi mkubwa sana wa taifa hili alikuja sehemu kama mwananchi wa kawaida huku akiwa amevaa shuka za kimasai na kofia zile za pama..baadae sana baada ya kuondoka ndio ikajulikana kama ni boss wa taifa kaingia hapa.
Hizo mbinu za mtu mkubwa fulani kuvaa kama mwananchi wa kawaida na kuingia sehemu fulani wakati mwingine utumika kupatia umaarufu tu na hakuna lolote. Mwaka fulani waziri fulani ambaye kwa sasa ni marehemu aliwahi kutinga pale Ubungo bus terminal akiwa kavaa kama mwananchi wa kawaida tena kichwani kavaa pama hilo hilo ulilolitaja. Zaidi ya kusikika kwa tukio hilo hakuna chochote kilichoboreshwa pale stendi. Lakini je, mwananchi wa kawaida uwa hasalimii watu?
 
Wanaume mnaolalamika wanawake wanawadharau, sasa, kama umevaa na kukaa hovyo unategemea nini?
Mbona hamshobokei wanawake walio hovyo kama ni kweli hamtilii maanani outward appearance? Mjitafakari
Kingine, inaonekana tunashida kubwa kwenye maadili yetu. Kwanini tunaambizana ya kuwa tunatakiwa tuheshimu watu wote kwasababu anaweza kuwa na kazi nzuri au unaweza kupata shida akakusaidia nk? Kwanini tusifundishane kuheshimiana kwa upendo kutoka moyoni kuliko kutishana? Hi ndio sababu tunakua wanafiki na chini kwa chini tunachukiana.
Mimi binafsi uwe muokota machupa jalalani au meneja wa wapi, nita watreat sawa bila kujali chochote. Ndio maana kwa watu wenye position kubwa au wanaotegemea special treatment kutoka kwangu wananiona nina dharau, ili hali wale watu wanadharaulika na jamii wananiona sina shida yeyote.
Kuhusu kudharaulika kwasababu ya muonekano wa nje, sijawahi. Sana sana watu wakiniona matarajio yao yanazidi hata uhalisia wangu. Lakini watu wengi, hasa wanaume wananiona nipo shallow kichwani (sexism). Wanahisi siwezi kufanya maamuzi magumu, kuchanganua mambo, kutetea hoja au kuwa na skills kwenye male-dominant fields. Wanahisi nipo kama pambo na nikiwaprove wrong kuna wanaofurahi na kuna wanaonichukia na kunipiga vitu kwa nguvu zao zote.
Kuna shida hapo either unashindana na wanaume uonekane mko sawa. Na ilhali unakojoa umechuchumaaa na mwanaime amesimama. Yaani hautaki kukubali kuwa mwanaume yuko juu yako. Labda ka elimu ulikopata kanakupa ujasiri na unajiona kama laweza kuoa mwanaume.

Yaani sijui kama utadumu na mwanaume .
Labda uoe umuweke mjini ila ukiolewa sidhani
Am sorry ila ni mtizamo wangu.
 
Sisi wengine kumdharau mtu kunakuja Automatic. Sio mpaka uvae vibaya sijui ufanyeje.

Na kumheshimu mtu kunakuja Automatic. Sio mpaka uvae vizuri.

Mimi moyo wangu ukinituma nikudharau nitakudharau bila kujali nafasi yako.


Huwezi heshimu kila mtu, huko ni kujidanganya
Huwezi dharau kila mtu.

Hivyo acheni kutishia watu. Kama unadharaulika kuwa mpole, jua kuna watu wanakuheshimu.

Usitake kila MTU akuheshimu, Wewe nani bhana
 
Kwanza naomba 'nidiclee' kwamba mm ni mmoja wa ME ambae si mtu wa fashion, yani mimi sijui kuvaa kabisa na sina hiyo passion ya pamba pamba. Nishawahi kusemwa sana na ma-ex wangu kuhusu uvaaji wangu lakini haikusaidia kitu.

Sasa weekend iliyopita nilienda sehemu moja flani hivi amazing, chimbo la uhakika haswaa, limejitenga na limetulia kweli. Nilipigilia kipensi changu na ka t-shirt flan hivi local nikachagua sehem nikakaa, kutizama vizuri nikaona kuna meza amekaa mdada mmoja hivi and of coz she is gud looking nikaamua kujitosa angalau kumpa hata hi 'coz tulikuwa wateja 2 tu, nikamfata nikamsalimu.

Yule dada kwanza alinishusha kuanzia juu mpaka chini then akaitikia salamu yangu ki-design kama namsumbua flani hivi. Nikaomba kujumuika nae kama asipojali. Jibu lake ndo lilinitoa confidence kabsa, alinambia: "Kwahiyo kaka unadhani kila msichana akikaa peke yake anahitaji kampani? Hapana sihitaji" Dah, mwanamme nikajizoazoa pale nikarudi nilipokaa. Nilikaa kama masaa ma3 hivi nikaamsha zangu. Sasa kilichotokea jana ndo kimenifanya niandike huu uzi.

Nilipokea maagizo kuanzia J3 ya wiki hii kuwa leo watakuja watu wa Taasisi flani ya kifedha kutoa semina kwa sisi wafanyakazi kwa ajili ya kutushawishi kujiunga na huduma za Taasisi yao, hivyo mimi nikapewa jukumu la kuwakaribisha na kuwapeleka sehemu ambapo semina itafanyika.

Asubuhi mida kama ya saa 3 hv ugeni ukafika, walikuwa watu kama 7 hivi, kati yao alikuwepo yule dada nilieonana naye weekend.

Wakaingia ofisini nikawakaribisha, wakati mkubwa wao anatoa introduction macho nikayakaza kwa yule dada, bahati nzuri tukagonganisha macho, akashtuka flani, nikajua kashanikumbuka.

Baada ya semina kuisha ikafika kipindi cha watu kujiunga sasa kwa walioshawishika. Nikamfata yule dada nikamuomba aje anielekeze namna ya ujazaji fomu. Alivyofika tu, nikamuuliza "Unanikumbuka?" Akachekaaa, akaniambia "Yani wewe, sikutarajia kama unaweza kuwa unafanya kazi huku", nikamuuliza ulitarajia niwe nafanya kazi wapi? Akaishia kucheka tu. Mawasiliano yake kanipa; fresh bila shida kabisa.

Sasa naomba kuuliza wadau, mshawahi kukutana na situation ya namna hii?
Sasa mkuu uko BOT halafu unavaa tshirt chakavu za mtumba na pensi. Lazma uonekane kibaka tu! Dada alihisi utamuibia iphone ake 🤣!!!

Lol...ukiwa mjini hapa jipende. Kuwa smart vaa vizuri, japo sio lazima uwe tozi ila atleast vaa ki bro simple tu! Saa kali, sandals au lightweight shoes outfit bomba tu... Dar kuna maduka mengi mno kiasi kwamba ukishindwa kuwa smart utakuwa na tatizo mahali. Usisahau kunukia
 
Huwezi nilazimisha nikusalimie wakati wa kupokea huduma. Sio lazima kabisa wala haiongezi au kupunguza chochote.
Nikija customer care nahitaji huduma, salamu naweza enda shule ya msingi wakanisalimia watu zaidi ya 1000 na shida yangu isitatuliwe.
Binafsi huwa sipendi MTU anayependekeza salamu. Ujue salamu ni aina ya malipo ama kumnunua MTU moyo wake ili akusaidie kitu Fulani. Ina mana bila ya salamu husaidiwi.
MIE hata ukinipita bila ya salamu afu unarudi umepotea njia nakuelekeza kiroho safi na hata ukinisalimia kama kuninunua ili ndipo nikuelekeze MIE naipotezea salamu yako na kama Nina muda nakupeleka mpaka unakoenda.

Warusi ukiwauliza kitu afu wakakusaidia na ukiwashukuru wanaikataa shukrani yako kwa kuuliza ya nini iyo shukrani. Ina mana wako willing kukusaidia bila hata kuwalipa.

Sasa bongo ndipo utashangaa MTU anakomalia salamu utadhani itamuwekea chakula mezani.

Binafsi sipendi kusalimiwa naonaga kama ni utumwa Fulani yaani ni lazima usalimie kila asubuhi. MIE wangu aishanielewa hakuna salamu hata kama nikitoka kwa wiki nzima. Nikirudi unapita muda kidogo tunaanza story za huku home na huko nilikokuwa.

Wazazi wangu hawakuwa watu wa kudemand salamu kila siku asubuhi. Ilikuwa ni kuamshwa kuwahi shambani basis.
Mpaka umri huu huwa nikienda home salamu ni zile siku za ugeni wiki ikishapita hakuna salamu.

Pia siamini kuwa salamu ndio heshima.

Nina imani masikini anapenda sana salamu mana kwa njia hiyo anajisikia faraja sana anadhani naye anajariwa. Masikini ndiye anayetembelea ndugu zake waliofanikiwa na kuwaongelea na kuringishia watu. Kuwa usinidharau yule karibu mkuu ni mdogo wangu nimemsomesha MIE. Ni kama Mwita weitara akasomeshwa na kaka yake aliyekuwa nauza mayai hapo kipunguni saivi sijui wanakaa kivule.
Ni mfano tu nimetolea hapa kwa karibu mkuu.

Salamu ni muhimu ila isiwe lazima jamani .yaani kuna watu wanaifanya kuwa basic needs kwao.
Binafsi nikiwaga home kwetu huwa siishi kwa furaha mana kila unayepishana naye yabidi u pay attention kwake na umpatie salamu tena usimame mpige story kidogo.sasa ole wako uje upite usalimie ukipunga mkono nakuambia ,Fulani anaringa kisa akasoma ,ama ana Hela.

Ila nikiwa town salamu sio lazima naishi kwa Uhuru hakuna MTU anayejiliza kuwa umetupita bila ya salamu rafiki.

Binafsi kunyenyekea ama kunyenyekewa sipendi.

Haya shikamooni wana jf wote waliozaliwa 65 kurudi nyuma. Wa 66 mpaka 1990 mambo vipi. Waliozaliwa 90 mpaka 2020 mnipe heshima Yangu

Unadhani kwa salamu Umepata nini katika maisha yako hata nisingekusamia si ungebaki na shida zako zilezile ama kuna kitu kimeongezeka.


Binafsi I hate salamu ingawa ni opener ya maongezi. Kuna watu naowakubali sana binafsi unamuuliza MTU kitu anakujibu mwishoni unashukuru na kumpatia salamu yake unasepa. Watu wa ivyo huwa naowanga ni matajiri rohoni kwao ni matajiri rohoni mwao!!!!!
 
100% kila mtu ni muhimu hapa duniani. Hata kama ni mshona viatu inabidi kumheshimu sana
Heshima ni miongoni mwa mahitaji makuu ya mwanadamu..hii ni kulingana na maono ya bwana Abraham Maslow juu ya mahitaji makuu ya binadamu

1.Physiological needs (foods,clothes,shelter)

2. Safety and security needs (kazi,pesa,bima,miliki)

3.Love & belongingess (Upendo wa ndugu,jamaa,marafiki, Mke au GF)

4.Esteem needs (Heshima, kutambulika,wadhifa, kukubalika)

5.Self actualization (kufikia ngazi za juu katika maisha, kuwa na kesho ilio bora zaidi ya leo, kutimiza ndoto zako katika maisha)
 
Binafsi huwa sipendi MTU anayependekeza salamu. Ujue salamu ni aina ya malipo ama kumnunua MTU moyo wake ili akusaidie kitu Fulani. Ina mana bila ya salamu husaidiwi.
MIE hata ukinipita bila ya salamu afu unarudi umepotea njia nakuelekeza kiroho safi na hata ukinisalimia kama kuninunua ili ndipo nikuelekeze MIE naipotezea salamu yako na kama Nina muda nakupeleka mpaka unakoenda.

Warusi ukiwauliza kitu afu wakakusaidia na ukiwashukuru wanaikataa shukrani yako kwa kuuliza ya nini iyo shukrani. Ina mana wako willing kukusaidia bila hata kuwalipa.

Sasa bongo ndipo utashangaa MTU anakomalia salamu utadhani itamuwekea chakula mezani.

Binafsi sipendi kusalimiwa naonaga kama ni utumwa Fulani yaani ni lazima usalimie kila asubuhi. MIE wangu aishanielewa hakuna salamu hata kama nikitoka kwa wiki nzima. Nikirudi unapita muda kidogo tunaanza story za huku home na huko nilikokuwa.

Wazazi wangu hawakuwa watu wa kudemand salamu kila siku asubuhi. Ilikuwa ni kuamshwa kuwahi shambani basis.
Mpaka umri huu huwa nikienda home salamu ni zile siku za ugeni wiki ikishapita hakuna salamu.

Pia siamini kuwa salamu ndio heshima.

Nina imani masikini anapenda sana salamu mana kwa njia hiyo anajisikia faraja sana anadhani naye anajariwa. Masikini ndiye anayetembelea ndugu zake waliofanikiwa na kuwaongelea na kuringishia watu. Kuwa usinidharau yule karibu mkuu ni mdogo wangu nimemsomesha MIE. Ni kama Mwita weitara akasomeshwa na kaka yake aliyekuwa nauza mayai hapo kipunguni saivi sijui wanakaa kivule.
Ni mfano tu nimetolea hapa kwa karibu mkuu.

Salamu ni muhimu ila isiwe lazima jamani .yaani kuna watu wanaifanya kuwa basic needs kwao.
Binafsi nikiwaga home kwetu huwa siishi kwa furaha mana kila unayepishana naye yabidi u pay attention kwake na umpatie salamu tena usimame mpige story kidogo.sasa ole wako uje upite usalimie ukipunga mkono nakuambia ,Fulani anaringa kisa akasoma ,ama ana Hela.

Ila nikiwa town salamu sio lazima naishi kwa Uhuru hakuna MTU anayejiliza kuwa umetupita bila ya salamu rafiki.

Binafsi kunyenyekea ama kunyenyekewa sipendi.

Haya shikamooni wana jf wote waliozaliwa 65 kurudi nyuma. Wa 66 mpaka 1990 mambo vipi. Waliozaliwa 90 mpaka 2020 mnipe heshima Yangu

Unadhani kwa salamu Umepata nini katika maisha yako hata nisingekusamia si ungebaki na shida zako zilezile ama kuna kitu kimeongezeka.


Binafsi I hate salamu ingawa ni opener ya maongezi. Kuna watu naowakubali sana binafsi unamuuliza MTU kitu anakujibu mwishoni unashukuru na kumpatia salamu yake unasepa. Watu wa ivyo huwa naowanga ni matajiri rohoni kwao ni matajiri rohoni mwao!!!!!
Kula like mkuu.
 
Kula like mkuu.
Nye za shto? Hapana ya nini kaka. Napenda tuwe na moyo wa kufanya kitu bila kubembelezwa ama kunyenyekewa sana. Siku ukaniambia nikuyoe ten sio lazima ubadilishe ile sauti iweje. Ongea kawaida tu kama ninakupa nitakupatia sio lazima unyenyekee mpaka ujihisi aibu.
Majuzi hapa nipo NATA nasubiria hiace za igoma. Kuna dogo akanipa salamu nikaichunia kwa kutikisa kichwa akanielezea shida yake kuwa akatokea nyehunge hana nauli anaenda Kishiri nikampatia jero LA hiace kiroho safi alikuwa ni kijana wa kiume kama below 25. Binafsi nimepitia msoto naujua kuna muda Nilikuwa naomba 3000 ya kutuma maombi ya kazi. Ila muda huu Namshukuru sana aliyeniumba amenitendea maajabu hata MIE siwezi kuamini
 
Huyo katibu mkuu nae atakuwa siyo mstaarabu tu. Kusalimia watu kwake ni shida? Ni mmoja wa wale waliolewa madaraka.

Mbona awamu hizi za karibuni ni kawaida tu kwa wateuliwa au mmeshasahau visa vya waziri Ngereja na Mlinzi wa ATM?


tps://www.jamiiforums.com/threads/kisa-cha-waziri-ngeleja-na-mlinzi-kwenye-atm.49162/page-3
 
Kuna mchezaji mmoja wa zamani wa Southampton anaitwa James Beatty alikuwa anataka kununua Porsche 911 akapita kwenye Porsche dealership moja mitaa ya London salesman akamwambia 'you can't afford this' (bei ilikuwa zaidi ya £100,000).
Jamaa akazunguka mitaa miwili mitatu akakuta Porsche dealership ingine akachukua gari kama ile akapita tena pale alipopita mwanzo akampa middle finger yule salesman akaishia. Hapo salesman kapoteza si chini ya £5000 commission.
 
Basi mimi mambo hua ni tofauti kidogo mimi watu hua wananipa heshima ambayo sina sasa kuna situations inakubidi ku maintain hiyo heshima uliyopewa ili usiwadissapoint wale waliokupa hyo heshima na hapo ndipo inabidi kufanya maigizo.

Hata huyu shemeji yenu wa sasa alishaniambia live "yani wewe nilijuaga ni mtu mkubwa (akimaanisha mtu mwenye wadhifa) kumbe huna lolote"

Kwakua nimeshaizoea hyo hali niliishia tu kucheka na kumwambia sasa umeshanijua vizuri unaweza kuamua vinginevyo.

Hua naweza kunyofoa pisi kali baada ya muda nashindwa kufikia matarajio yake basi unakuta imeniacha kiroho safi tu.
 
Mimi ni kati ya wale Washikaji ambao siyo rahisi hata kujua wanafanya nini town, yaani wanapotea unakuja kuwaona weekend, wanazunguka zunguka tu wapo smart
Harakati zangu nafanyia nje kidogo ya mji ambapo jamaa zangu wengi hawafikagi,na harakati yenyewe basi,ya kujua mwenyewe tu
Nina mwanamke mmoja Yeye mtu wa town hapo kati ana Biashara zake,nikiwa town naenda hapo nazugazuga,nikitoka Washikaji wanakuwa wanamuulizia amenipendea nini sasa maana mshikaji niponipo tu na sina mchongo wowote,anaishia kucheka tu maana yeye ndiyo anajua mikakati yangu.
Mwezi March niliugua nikakaa home kama wiki mbili hivi,yule mwanamke wangu akawa anachukua bodaboda kila siku ananiletea vinywaji,matunda na mahitaji mengine maana naishi mwenyewe tu,basi aliokuwa anakuja nao kumleta na kumfuata walistaajabu sana kukuta nimeweka kamjengo ka maana tu huku nina room zangu mbili zimejaa kuku wa kienyeji naokota mayai tu,kifence changu poa kabisa,yaani hatua flani ambayo kila kijana anayeanza maisha anatamani kuikamilisha.
Nimekuja kupona sifa nazikuta mtaani huko,kwamba "jamaa msimchukulie poa,msimuone analandalanda kwake amepiga hatua sana"
Ndiyo hivyo bwana.
 
Back
Top Bottom