Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Alidhani wewe Nani?.

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
Ulizidi kukonda na kuchakaa...kuna mdada mmoja mkenya wanaishi Germany sasa ukimuona utazani beki tatu hana alama ya kutoka ulaya...amechakaa m
Hadi kero....ndio umenikumbusha huyu ndugu yetu mkenya.
Wakenya hata nuru huwa hawana halafu kuvaa hawajui, muonekano hawana wengi wao.
 
Mimi hata omba omba wanao kaa barabaran siwachukuli Poa , Una mdharau kumbe aingiza kipato kuliko wewe unaempa 500
Namjua omba omba flani alikua anapga mishe zake za omba omba POSTA lakini anakaa MBEZI MWISHO.

Nilimjulia ofisini kwangu alikua akipenda kuja na kibaiskeli chake cha walemavu kunywa SUPU kila asubuhi.

Trela linaanza kifungua kinywa chake ni kila siku bili ni 15,000 hiyo no yangu Jikoni. Asipopiga mchemsho wa samaki,ujue atapga mchemsho wa kuku.

Au lah atakupigia SPECIAL ya UTUMBO,sio poa huyu mjomba.

Hapo ofisini kuna dada alikua akitoka nae kimapenzi,ndie aliekuja vujisha kila kitu.

na huyu omba omba ndie alienifanya Hadi LEO siwezi saidia OMBA OMBA wa barabarani.

Omba Omba huyu (mlemavu asie na miguuu)

Kwake sio pa kisport sport,anapolala (hilo godoro + kitanda tu) achana na vitu za electronic video niliyoletewa, nilisema Sisaidii omba omba bila kujiridhisha.

Omba Omba ana hadi nguo za kazini,ah weeeeee Mimi kusaidia omba omba NEVER.
 
Dah 😂 sa we umejuaje mpya?
mi mwenyewe nina ID 10 ukiniblock hii,kesho napanda JF na zingine.

nikiwa kwa ID zingine ndio ninapojua huyu Depal id yake ni hiii,huyu kwini id yake hiii... Mambo wazi wazi, Dr kumbuka anakwambia Mambo Open Open,Kimbia toka nnje ya JF kbsa ila uki switch ID tu tunaswichika na wewe.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
dah kuna demu nilipita naye celebrity maarufu nilimpiga sound mimi nina miliki kampuni ya ujenzi na usafirishaji wa mizigo DRC, zambia, SA nk..

Kiukweli amekula kula sana vichenji vyangu huku nikitumia Vogue Vera yakuazima ya mwanangu mmoja + Nissan patrol V8.. demu akaona kapata kidume, nilimla kotekote kupunguza hasara zangu..

Dah alivyojua sina lolote naungaunga tu mjini ila wanangu wengi wako sawa wanachenjichenji hizi bongo hapa akanikimbia na ananichukia balaa... ILA ANA JINA KUBWA SANA MJINI BONGO shida njaa njaa sana hawa celebrity..
 

hujaendana na uzi wenyewe
 
Mpuuz Sana hyu nesi "eti unamuuguza yesu,pumbafu sana

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Duuu [emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
 
Kipindi hicho nmeingia form 1 kuna jamaa alikuwa anaitwa Juma , uniform zake zilikuwa zimechoka choka inaonekana shati alikuwa anatumia darasa la saba au Kuna mtu alimwachia alaf alikuwa sio muongeaji sana tofouti na wanafunzi wengine kila mtu alikuwa anajifanya mjanja

Sasa mimi nikawa na muona Kama boya flani hivi nikajua hata akili atakuwa hana japo nilikuwa simuoneshi kama na mchukulia poa , sasa imefika mitihan ya mwez wa 6 tumefanya tumeenda likizo tumerudi matokeo yamebandikwa sasa nauliza huyu juma ndo nani naoneshwa jamaa na ambiwa jamaa toka primary uwaanaongoza kiwilaya toka siku hiyoo respect akawa na rafiki yangu tunaenda kusoma wote .
 
Hizi dharau mbona kwa Bongo ni kitu cha kawaida kabisa. Hasa wadada ndio maana wanaangukiaga kubaya kwenye mahusiano
 
Hata sio Sifa bali vitu vingine ni aibu kusimulia, yaani muislam wajigamba kwa kutukufahamika dini yako!! Aibu gani hii
Kwani peponi walio watakatifu wataingia kwa kigezo cha dini? Mwenyezi MUNGU ni dini gani?
 
Ishu kama hii nimewahi ishuhudia pia sehemu, kuna siku nilikuwa nimekaa na jamaa yangu mmoja alikuwa na kibanda cha MPESA, ghafla akaja mzee mmoja na Hilux Double cabin la zamani akali-park kando ya barabara then akaja kutoa pesa hapo kwenye kibanda, kumbe jamaa wa wrong parking mbio mbio wakaliwahi gari wakapiga chain...mzee kurudi kwa gari wakaanza mabishano weeeh na mbaya zaidi alikuwa na mtoto mgonjwa kwenye gari ndo anamuwahisha hospitali, jamaa wa wrong parking sijui wanakuwaga na matatizo gani...waligoma kumfungulia yule mzee mpaka akapiga simu mahali, punde si punde wakaja FFU...FFU wameshuka kwa gari lao wanamfuata mzee wanamsalimia 'afande'...eeh bhana eeh I wish mgeona sura za wale jamaa wa wrong parking[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]kumbe mzee ni kamanda mstaafu alikuwa na cheo sana......[emoji28][emoji28] vijana wa wrong parking walibebwa na chain zao...
 

[emoji81][emoji81][emoji81][emoji81][emoji81]
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mtu unayemdharau either Kwa mwonekano au kazi anayofanya .wengi wamebeba vitu unavyohitaji maisha mwako 100%.kama Kuna kitu unakihitaji duniani haijalishi nicha ukubwa kiasi gani basi watu wa Hali hiyo wanajua namna gani ya kukusaidia...

Mimi nilishasaidiwa vitu viwili vikubwa sio vidogo na MUUZA MAJI YA MADUMU anayesambaza kwenye majumba..unaweza kusema mtu huyu atanisaidiaje na Hali yake hii ya chini? Nilidhani mtu anayevaa tai na smart ndio anaweza kunisaidia ..Ukimwona mtu anafanya kazi ya Hali ya chini usimdharau wengi wao huwa pia na michongo mikubwa Sana na wakikupa unatoboa..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…