Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Link story ya Mercy
 
Episode 11


maisha yakaendelea hapo nishabadili na namba za simu nikarudi kazini ila nikawa mlevi sana, kuna siku mpaka director alikua mmama mmoja hivi alinifukuza ofisini akaniambia we nenda kwanza mpaka kesho, barua za onyo nikawa nakutana nazo karibu kila wiki, Maisha yakaendelea nikaja kuona nikiendelea kufanya kazi dar sitapata amani ya moyo, nikaanza mipango ya kutafuta kazi sehemu nyingine kimya kimya nikaja kupata kazi mwanza ila nilitakiwa nisubiri kama miezi miwili ndo niripoti , sasa kuna siku nimekaa Mary akanipigia sijui hata namba zangu alipewa na nani, akanisihi sana tuonane nikamuambia sawa, basi badae tumeonana yupo smart kweli na kazini alirudishwa pale pale, akawa ananiambia twende ukachukue vitu vyako vilivyobaki, tukaenda home tukaishia kusex tu, mazoea yakaanza taratibu nikaona no this is not right nikamwambia tuache tutarudisha matatizo tu, nikaja kuamugaza naenda mwanza nahama huku, akakubali hivo hivo mpaka siku naondoka tulilala wote asubuhi niliondokea kwake



Mary kwa sasa ameshaolewa na ana mtoto mmoja, hua tunawasiliana sana yaani sana ila hatujawahi kuonana tangia hio siku naenda mwanza yaani hata nikiwa dar tulishakubaliana tusije onana kabisa, kuna siku nipo dar ananiita mikocheni huwez kuamini nilienda ila njiani roho iligoma nikarudi, hata leo hii nimetoka kuongea nae tunashauriana mambo mengi ya kimaisha



samirah ye bado hajaolewa na nina mawasiliano yake hua tunaishia kutaniana hapa na pale tu japokua nae sijawahi kumuona toka ile siku tunaachana akiwa bado chuo, 6 years ago!!!


Mimi sasa, mwanza ndo nikakutana na machizi wenzangu kwenye mapenzi nikapigwa matukio mpaka akili ikakaa sawa, ndo lengo la kuleta huu uzi ila muone kua niliacha wanawake wa aina gani na nikaja kutumbukia na kupigwa matukio na wanawake wa aina ipi, wanakuambia mkataa pema pabaya pamuita, hapa ndo sasa story inaanza rasmi wadau
Kudadeq....viatu ni vizito hivyo
 
Very interesting story....but sad at the same time....Every step unajishtukia ukIwa tayari umesha haribu..majuto baada ya majuto.
Maisha yanaweza yakukufanyia drama ukachanganyikiwa🥲
 
images (10).jpeg
FB_IMG_1735543166436.jpg
images (5).jpeg

GRACE kama GRACE
 

Attachments

  • images (9).jpeg
    images (9).jpeg
    8.9 KB · Views: 9
  • images (6).jpeg
    images (6).jpeg
    7.4 KB · Views: 10
  • images (7).jpeg
    images (7).jpeg
    8.4 KB · Views: 6
Nafupisha story, nilibahatika kumpata upendo wa kweli kwa mary na tulishi kama mme na mke kuanzia tukiwa shule hadi tulipoajiliwa, nikiwa kazini nikapata bikra samira akanishobokea nikamplekea mto. Mary alipokuja kungudua alitaka kujiua, mambo yakawa mengi nikaamua kuhama kikazi toka dar to mwanza,.
Nikiwa mza nikakutana na malaya recho tukaaza naye mahusiano na akanizalia mtoto, alipozaa tu akaniacha na kuendelea na umalaya wake, sa mamamkwe alinipenda akanitunuku mtoto bikra grace. Baada ya recho kujua akaamsha timbwili niko hapa tunasubiri kikao cha familia na mama mkwe.
 
Nafupisha story, nilibahatika kumpata upendo wa kweli kwa mary na tulishi kama mme na mke kuanzia tukiwa shule hadi tulipoajiliwa, nikiwa kazini nikapata bikra samira akanishobokea nikamplekea mto. Mary alipokuja kungudua alitaka kujiua, mambo yakawa mengi nikaamua kuhama kikazi toka dar to mwanza,.
Nikiwa mza nikakutana na malaya recho tukaaza naye mahusiano na akanizalia mtoto, alipozaa tu akaniacha na kuendelea na umalaya wake, sa mamamkwe alinipenda akanitunuku mtoto bikra grace. Baada ya recho kujua akaamsha timbwili niko hapa tunasubiri kikao cha familia na mama mkwe.
Somo la ufupisho ulihudhuria 😅upo vZuri kiswahili one
 
Kuna mwamba mmoja nimemsahau jina pia siku hizi sijamwona hapa kitambo sana, hii tabia ya kusuasua kumalizia story ilimfanya ajenge bifu na wasimulia hadithi pamoja na wasomaji... Ilikua ni mwendo wa kumpiga biti msimuliaji huku mashabiki wakimu-attack huyo mwamba ili mwandishi asije akazira kuleta mwendelezo wa story..... Utasikia LEO UMALIZE HADITHI YAKO MAANA WATU WAMEKUA WAKILALAMIKA KUSUASUA KUMALIZIA STORY, UMALIZE LEO KWA SABABU WATU WAMEKUJA KUSHITAKI KWANGU...
Huyu atakuwa ni INSIDER katuweka macho toka mwaka jana aisee
 
Unamjua mtaalam INSIDER MAN mkuu.
Huyu aliisimamisha jf (MMU) kama mwaka na zaidi na story yake ya UBER,aisee ile ilikuwa ni shido.

Sitosahau kuwa na mimi nishawai soma ile story wakati nipo kwenye foleni ,afu nikaweka reverse kikubwa nilishtukia mapema wakati tuna take off laasiivo cjui kingejiri nini🤷🏿‍♂️
Na ametuchinjia baharini hajamalizia kaishia patamu hataki kuleta muendelezo
 
Back
Top Bottom