Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Episode 11


maisha yakaendelea hapo nishabadili na namba za simu nikarudi kazini ila nikawa mlevi sana, kuna siku mpaka director alikua mmama mmoja hivi alinifukuza ofisini akaniambia we nenda kwanza mpaka kesho, barua za onyo nikawa nakutana nazo karibu kila wiki, Maisha yakaendelea nikaja kuona nikiendelea kufanya kazi dar sitapata amani ya moyo, nikaanza mipango ya kutafuta kazi sehemu nyingine kimya kimya nikaja kupata kazi mwanza ila nilitakiwa nisubiri kama miezi miwili ndo niripoti , sasa kuna siku nimekaa Mary akanipigia sijui hata namba zangu alipewa na nani, akanisihi sana tuonane nikamuambia sawa, basi badae tumeonana yupo smart kweli na kazini alirudishwa pale pale, akawa ananiambia twende ukachukue vitu vyako vilivyobaki, tukaenda home tukaishia kusex tu, mazoea yakaanza taratibu nikaona no this is not right nikamwambia tuache tutarudisha matatizo tu, nikaja kuamugaza naenda mwanza nahama huku, akakubali hivo hivo mpaka siku naondoka tulilala wote asubuhi niliondokea kwake



Mary kwa sasa ameshaolewa na ana mtoto mmoja, hua tunawasiliana sana yaani sana ila hatujawahi kuonana tangia hio siku naenda mwanza yaani hata nikiwa dar tulishakubaliana tusije onana kabisa, kuna siku nipo dar ananiita mikocheni huwez kuamini nilienda ila njiani roho iligoma nikarudi, hata leo hii nimetoka kuongea nae tunashauriana mambo mengi ya kimaisha



samirah ye bado hajaolewa na nina mawasiliano yake hua tunaishia kutaniana hapa na pale tu japokua nae sijawahi kumuona toka ile siku tunaachana akiwa bado chuo, 6 years ago!!!


Mimi sasa, mwanza ndo nikakutana na machizi wenzangu kwenye mapenzi nikapigwa matukio mpaka akili ikakaa sawa, ndo lengo la kuleta huu uzi ila muone kua niliacha wanawake wa aina gani na nikaja kutumbukia na kupigwa matukio na wanawake wa aina ipi, wanakuambia mkataa pema pabaya pamuita, hapa ndo sasa story inaanza rasmi wadau
Sasa hapo cha ajabu nini??
Wewe na viporo wanakuita upashe, kuna mwenzio huku kashaniitia mpk ukoo wao wote na nimegoma.!

Kawajaza pesa wale maanko jau lakini wapi, kanisusia mpk ofisi tulioanzisha wote na kila kitu labda nitakubali lakini hamna kitu.!!
Na sitegemei kumrudia hata mbwa apige mswaki..!
 
S2 episode 6


Dah nilitafakari sana nikapata mawazo makali sana, nikawaza maisha na Mary kule dar, nikamuwaza Samira, nikawaza nimekuja kuingia kwenye balaa gani tena, uzuri napenda sana kua mtulivu kwenye situation za kupanic mpaka leo ndo niko hivyo, nikawaza sana nikajilaumu nimemtia mimba binti ambae simjui vizuri, mbaya zaidi nishaenda na kujitambulisha kwao, nikawaza sana kuhusu huyu mwanangu tumboni, badae mawazo yanakuja ni wangu kweli au? Yaani nikawa sielewi tu



Nikarudi home usiku kufika napokelewa sina hata furaha, nikampa simu yake akawa kafurahi kweli anasema ngoja nichukue na picha zangu za zamani,mi hapo namchora tu npo zangu kimya, kanipakulia nikamwambia tumbo linauma siwezi kula basi ananibembeleza hapo sina hata hisia wala amani mpaka muda tukaenda kulala, akataka tusex namuambia tu tumbo linasumbua, akaja pitiwa na usingizi, mi hapo siwezi kulala, huwezi kuamini kuanzia hapo nilipatwa na tatizo la kutopata usingizi mpaka leo linanitesa, nikaanza kumuangalia akiwa amelala, ni binti mrembo, nikaanza kuwaza zile sms, natamani hata nimnyonge!! Ila bado nawaza hiki kiumbe tumboni, au nimconvince atoe mimba nimpige chini, ntampa sababu gani, basi tu mawazo hayaishi


Nikatoka nikaenda sebleni nikamimina pombe nikaanza kunywa huko( mpaka leo nina utamaduni huwezi kukosa pombe kwangu hata kama sio za bei lakini lazima niwe na stock ndani)... Mawazo kama yote sielewi cha kufanya, sasa sijui kwanini nikawa namkumbuka sana Mary nikiwa nimelewa, Samira ikawa rahisi kumsahau labda kwa kua hatukua pamoja kwa muda mrefu, nikashika simu nikampigia Mary ikaita weee haikupokelewa, nikaachana nayo, nimekaa sebleni Rachel mara kanifata,
"Mume wangu mbona huku tena usiku na hio pombe na tumbo kulikoni"

Nikamwambia nina kiporo ofisini nataka malizia alafu nakunywa kidogo labda tumbo litakaa sawa, basi akaja pale ananibembeleza na nini hapo nawaza zile sms, nawaza ile clip yaani napata hasira basi tu, badae akarudi kulala nikawaza nikasema ntapata jibu tu hakuna haja ya kupanic


Kesho nikaenda kazini kama kawaida, natoka nikapita pale golini kwake nikampa hi tukawa tunapiga story tu pale, mara mezani nikaona ile simu niliyomrekebeshia nikamuulizia ulipata picha zako za zamani akasema ndio, basi nimekaa pale nikazuga zuga badae nikashika ile simu kuchungulia nakuta sms zote zipo tu kama jana, hajafuta hata kitu, moyoni nikasema huyu binti tofauti na umalaya mbona tena ni kama hamnazo, ni ujinga au kiburi? Yaani ushahidi wote wa ujinga wake anaacha tu na anajua naweza angalia muda wowote..... Nikajisemea moyoni... Karibu uswahilini patrick

Hasira zikapanda pale tena nikaaga nikaondoka zangu, mi huyo mpaka bar nikanywa kidogo nikakumbuka Mary alinichek sikumjibu ikabidi nimpigie, tukapiga story tu pale nikazuga nipo sawa wala hakuna shida yoyote basi badae nikarudi home siku ikaisha


Kumbuka hapo bado nadaiwa laki 3 kwa kina Rachel ambayo sikumalizia, nawaza hapo nipeleke au niachane nayo tu, nikawa najiona mjinga yaani mimi ndo naenda kulipia K ambayo watu washacheza nayo kiasi kile nikasema dah! Si niliacha K za maana dar nikakimbilia huku, acha nikome sasa


Ujinga sasa, badala kipindi cha mwanzo ndo ningeanza kumdadisi Rachel nikajikuta sa ivi ndo naanza kumhoji kuhusu maisha yake, ndo akaniambia baba yao aliwakimbia wakiwa wadogo, na yule mdogo wao wa mwisho ni mtoto wa baba mwingine, anadai baada ya kumaliza la saba hakuendelea na shule, na alipofikisha miaka 16 ndo akahamia kwa yule rafiki yake mwenye mgahawa akaanza kujitegemea, sasa nikawa namuuliza unajitegemea kwa kazi gani sasa akawa anajiuma uma akilini hapo najiambia patrick acha ujinga kwani majibu huna



Mama mkwe nae hapo alishakua free ananipigia simu tu tunawasiliana kama kawaida na nyumbani akawa anakuja freely tu, nikapanga siku nikaenda kumalizia ile laki 3 lakini safari hii nilienda na baba mkubwa(hakuwepo awamu ya kwanza).... Tukafika tukamkuta mama mkwe,Rachel na mzee mmoja safari hii hapakua na maongezi sana tukalipa ile pesa tukala pale maongezi kidogo tukaondoka


Tukapita mahali nikawa nimekaa na baba mkubwa mara from nowhere ananiambia
"Tatizo lenu vijana mnaharibu kwanza ndo mnakuja kutushirikisha, yule binti kama angekua hana mimba ningekushauri uachane nae tu"
Baba mkubwa alishaona pale hamna mtu
 
S2 episode 7


Nikawa nazidi kupata mawazo tu maisha yakaendelea na Rachel ila nikawa sina furaha kama zamani hata sex nikawa kuna muda nafanya basi tu, ila huyu binti bana sijui alikua na shida gani kuna siku nakumbuka sijui nilikua nimekunywa nini maana nikaanza tu kua mnywaji, hio siku tulisex muda mrefu sana nakumbuka baada ya kumaliza akaniambia "patrick, katika wanaume wangu wote sijawahi kupata mwanaume ananitia hivi"

Dah imagine unaambiwa hivo na mke wako, nilitamani nimnase hata vibao ila nikasema hapa hakuna mwanamke hapa nianze kuangalia tu namna ya kujichomoa pindi mtoto akizaliwa, kuna siku nikashika simu anayotumia maana nikawa simuamini sana yaani wale mabwana zake maana majina yalinasa kichwani kwangu wengi tu bado alikua anachat nao, wengi wanamlaumu kwanini ameamua kuolewa, na yeye ana wa entertain tu yani anakua kama anataka hataki kuwapa tena utamu, na sms hizo hafuti anaziacha tu imagine, basi bana mi nikakata shauri hapa mwanamke hakuna, na mahari siwezi kutoa tena



Kuna siku mama akanitumia sms "naona mmeenda kuoa huko kimya kimya na baba zako yatayokukuta mmalize wenyewe" basi nikaona haina maana nikaipotezea tu, maisha yakaendelea nashukuru Mungu mama yake Rachel alikua ni mama flani mpole ivi na ana hekima sana, hapo nilikua na uhuru naweza kupata muda nawatembelea, sikua na roho ya kwanini nilimsaidia kila nachoweza hata wadogo zake Rachel walikua wananipenda sana maana niliwapa chochote kila napopata nafasi.....


Siku zikaenda mimba ikazidi kua kubwa ikabidi nipange sehem nyingine nyumba kubwa zaidi ila hapo katikati nilipigwa matukio na Rachel mpaka akili ikakaa sawa,mara arudi saa 5, mara ukute kafunga tu ofisi hata kama ni mchana na haeleweki yupo wapi, kuna siku nilichukia ikabidi nimchane tu kuhusu hao mabwana zake akaanza kusema hayo yalikua maisha ya nyuma, nikamuuliza sasa mbona bado unawasiliana nao ye akadai wao ndo wanamsumbua, huwezi amini ila nikatokea kumchukia tu tukaanza kulala different rooms, hapo ndani kila mtu anarudi anavyotaka mi hapo wala sijali wala nini nachowaza tu baada ya mtoto kuzaliwa niachane nae


Ikapita muda siku akanifata analia mbona sijui namnyanyasa mi nikamchana tu tuwaze mambo ya mtoto we endelea na wanaume wako, akajibu sawa badae akatoka hio siku hakurudi kabisa na kesho yake, nikafanya udadisi nikagundua hayupo kwao wala kwa rafiki yake nikawa nashangaa tu huyu mwanamke ni jini au sasa na tumbo lote hilo yuko wapi..... Hapo kumbuka Mary naongea nae mara moja moja ila sikuwahi kumwambia kama huku nimeyatimba, na mama mkwe tunawasiliana safi tu wala sikuwahi kumlalamikia kama kuna shida


Muda ukaenda mpaka ikafika siku akajifungua nilimpeleka hospitali moja private alivyojifungua salama nikawachukulia mahitaji alikua na mama yake na mdogo wake wa kike mi nikaenda kazini, jioni narudi nakuta marafiki zake wadada wawili na wakaka watatu wamekuja kumsalimia, katika kutambulishana nikaja gundua kati ya wale wakaka wa3 wawili kati yao wamewahi kua na mahusiano nae kumbuka hapo majina ya kwenye zile sms yaligoma kabisa kutoka kichwani, nikashikwa na hasira tu nikauliza wanaruhusiwa lini wakaniambia kesho mi nikaondoka nikawaacha hospitali


Badae mama mkwe akanipigia anauliza mbona nimeondoka nikawaambia nina presentation ofisini kesho nimekuja iandaa, hapo nina hasira najiuliza huyu mtoto ni wangu kweli, nikaenda sehemu nikapiga mtungi badae nikamtumia rachel sms " kati yangu na hao jamaa zako(nikawataja kwa majina wale washkaji wawili ambao nilikua na uhakika washakua nae) nani baba wa mtoto? Maana naona kama siwaelewi vile??
 
Back
Top Bottom