Ushawahi kukatazwa kula chakula ugenini Hadi baba/mama mwenye mji afike?

Ushawahi kukatazwa kula chakula ugenini Hadi baba/mama mwenye mji afike?

Taratibu zao sasa utalazimisha,wabadilishe kisa unanjaa kapike kwako au kale viepe
Duuuh sawaa aiseew, kama kwa namna hii nawe ndivyo ulivyo sidhani kama unapataga wagen kwako [emoji28][emoji28]
 
Wewe Kama NI mtoto wa kishua,mboga 7 draft.hauwezi kuelewa haya malezi.
Yaani wakati tunakuwa ukitaka kumtibua mama nenda mezani kapakue chakula wakati dingi hajala.
Chukulia kesi ya mgeni mkuu, mbona sie Mzee anatengewa pemben sie twala kulalaa
 
Ingekua vizuri kama mshua anatengewa chake pembeni mliopo pigeni msosi, sisi kwetu utaratibu ulikua huo mshua au maza chakula chake kinakaa pembeni mana hii ya kungojea mtu nyie mna njaa kumbe mwenzenu ukute ashakula zake huko wa home mnataabika sio poa kabisa.
Yeaah ni kweli
 
ni kweli.tatizo hauwezi kumpangia mama jinsi ya kufanya.kipindi hicho una miaka 10+ .lakini nidhamu hyo imetufundusha kuwa na adabu.
sio watoto wa Sasa hivi akiona tu hotpot anapakua.
Mimi hata niende kwa ndugu siwezi kukimbilia mezani kama mkuu wa kaya hayupo.
Daaah aiseeee
 
Kwanza kipi kinakupeleka kwa watu ikiwa mwenye nyumba akiwa hayupo?Ukiwa umealikwa basi mwenye nyumba atakuwepo muda aliokualika.Kukimbilia vyakula vya cross ball ndio matatizo yake itabidi usubiri mpaka mwenye cross ball afike.Vingivevyo kula kwako.Ukiwa mgeni kula kabisa njiani.
 
Chukulia kesi ya mgeni mkuu, mbona sie Mzee anatengewa pemben sie twala kulalaa
Wamama wetu wanaogopa unaweza ukapakua vibaya,au kuchukua chakula kingi n.k
Yaani sio uchoyo Ila NI ile hali ya kumpa baba heshima
mgeni una njaa vumilia au kale kwako.
na Raha ya kula ugenini ule pamoja na wenyeji wako.
 
Duuuh sawaa aiseew, kama kwa namna hii nawe ndivyo ulivyo sidhani kama unapataga wagen kwako [emoji28][emoji28]
Sipatagi hata nanikiwakuta vitimbi watakavyo vipata aisee hawatorudi sijui kwanini ninao marafiki wazuri wamenizoea hawaachi kunisaidia naroho yangu ilivyombaya.
 
Naaga naondoka.

Hata wabembelezaje ili nibaki nakataa

Au la nitaomba wanionyeshe kibanda cha chips nawanunulia nyumba nzima nakaa nakula zangu nasepa.
 
Kwanza kipi kinakupeleka kwa watu ikiwa mwenye nyumba akiwa hayupo?Ukiwa umealikwa basi mwenye nyumba atakuwepo muda aliokualika.Kukimbilia vyakula vya cross ball ndio matatizo yake itabidi usubiri mpaka mwenye cross ball afike.Vingivevyo kula kwako.Ukiwa mgeni kula kabisa njiani.
Mkuu mfano umepita mtaa anaokaa ndugu yako au rafiki yako, hivi huwez kwenda msalimia kwasabab ya kuogopa kusubirishwa msosi???

Hujawahi sikia ile, fulan kapita hapa hata kuja kutusalimia hakuna
 
wamama wetu wanaogopa unaweza ukapakua vibaya,au kuchukua chakula kingi n.k
Yaani sio uchoyo Ila NI ile hali ya kumpa baba heshima
mgeni una njaa vumilia au kale kwako.
na Raha ya kula ugenini ule pamoja na wenyeji wako.
Duuuh aiseee hizi falsafa kwangu hazi apply yaan nikalishe njaa watu SITA sababu ya mmoja[emoji28]
 
Sipatagi hata nanikiwakuta vitimbi watakavyo vipata aisee hawatorudi sijui kwanini ninao marafiki wazuri wamenizoea hawaachi kunisaidia naroho yangu ilivyombaya.
Anyway ndege mfananao huruka pamojaa,
 
Naaga naondoka.

Hata wabembelezaje ili nibaki nakataa


Au la nitaomba wanionyeshe kibanda cha chips nawanunulia nyumba nzima nakaa nakula zangu nasepa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji120][emoji120]
Case closed
 
Mkuu mfano umepita mtaa anaokaa ndugu yako au rafiki yako, hivi huwez kwenda msalimia kwasabab ya kuogopa kusubirishwa msosi???

Hujawahi sikia ile, fulan kapita hapa hata kuja kutusalimia hakuna
Huwa siendi kwa watu bila taarifa au kualikwa.Na ili kuthibitisha napiga simu kabla.Kama mwenye nyumba hayupo siendi.
 
Utamaduni gan hebu nielezee vizur,utamaduni wa kusubir sijui nani aje ndo chakula kiliwe??
Eti unakuta wageni wanakaa na watoto hadi wanasinzia kisa eti tumsubiri baba arudi ndio wote mle chakula utasema huyo baba kawabebea matumbo Mimi sipendi kabisa watu wenye hii tabia.
 
Eti unakuta wageni wanakaa na watoto hadi wanasinzia kisa eti tumsubiri baba arudi ndio wote mle chakula utasema huyo baba kawabebea matumbo Mimi sipendi kabisa watu wenye hii tabia.

Yaan ni ushamba wa hali ya juu tena mnaonekana ni watu wenye kuhusudu chakula na ni aibu sana waache watu wale wajiachie
 
Huwa siendi kwa watu bila taarifa au kualikwa.Na ili kuthibitisha napiga simu kabla.Kama mwenye nyumba hayupo siendi.
Unaposema mwenye nyumba unamaanisha Nan, baba au mama, vp kama mama yupo ila baba hayupo
 
Eti unakuta wageni wanakaa na watoto hadi wanasinzia kisa eti tumsubiri baba arudi ndio wote mle chakula utasema huyo baba kawabebea matumbo Mimi sipendi kabisa watu wenye hii tabia.
Wengi hatupendi sema ndotaratibu za wenyej wetu
 
Back
Top Bottom