Ushuhuda kutoka kwa wanandoa waliowahi kuachana, hasa mliokuwa na watoto mkaamua kuacha kila kitu na kuanza upya

Ushuhuda kutoka kwa wanandoa waliowahi kuachana, hasa mliokuwa na watoto mkaamua kuacha kila kitu na kuanza upya

Nawasalimu sana ndugu wana JF.
Kwakweli lengo la ndoa ni kuishi pamoja kwa uaminifu na upendo na kulea familia pamoja.

Nafaham humu kuna watu wenye calibre tofauti na uwezo wa hali ya juu kupambanua mambo kutokana na experience...

Naomba experience yenu, je ilikua rahisi kuanza upya? Kwenda mahakamani kutoa talaka rasmi imeshindikana kabisa..ninachotaka ni kutengana kwa muda napo imeshindikana..hapo more than three children kwenye ndoa wapo involved, ten years na wengine below .simchukii kabisa mume lakini forgiving and forgetting what happened nashindwa kabisa..imani haipo Yarabi tena...nimekata tamaa kabisa...

Imefikia kipindi natafuta kazi mikoani ili nipone moyo...jamani wenzangu mliwezaje...sijashare na ndugu yangu hata mmoja....nikiwaeleza kila kitu watamchukia na they will never forgive him...

Nimeamua kumstiri mume wangu..sijaandika kila kitu ila baadhi yenu ni wanaume ila mngeumia sana na kutoa chozi...ndoa yetu ni ya serikali...naomba experience yenu especially kwa nyie mliokua na watoto mkaamua kuacha kila kitu na kuanza upya..
Ni ngumu saana kurudisha imani ila ni ngumu zaidi kuanza upyaaaa hasa kama watoto wako kati yenu, waweza jidanganya mwaka ama miwili ila inafail....sikushauri hata kidogo take ur time, heal and all shall be well, wanaume ni walewale na wanawake ni walewale...kubwa duaaa!!!
Bottom line zimwi likujualo halikuli likakwishaaa.....
 
Huwa napata wakati mgumu sana ninaposikia watu waliooana na kuzaa, halafu mmojawapo anaona kuachana ndiyo jawabu la matatizo yaliyojitokeza kati ya huyo mume na huyo mke. nilitegemea kuwa kama mmezaa basi fikra kubwa ingekuwa kufikiria hatma ya maisha ya hawa mliowazaa bila ridhaa yao. inanipa shida zaidi kama watu hawa wana elimu ya kutosha, wanaenda kanisani au msikitini. Na mwisho huwa nahisi yeyote anayemlalamikia mwenzake aghalabu naye ana ushetani wake ambao unamwongoza kumshambulia mpambe wa shetani wa mwenzie. Elimu, Mungu na wanjamii wakusaidie, utavuka hayo mapito.
Kuliko kupigana vitu vizito kichwani mkaishia kugawana majengo ya serikali mwingine mochwari, mwingine jela au wote mochwari, si ni bora mkaachana tu. Hata mimi nilikuwa na mentality ya kusimama na ndoa no matter what. Ila siku ikafika nikasema enough is enough. Sasa hivi nina furaha na wanangu, hata X mr sina kinyongo nae. Akipiga simu napokea. Yaani ni full amani ya nafsi.
 
Yaliyotokana na tukio yalipelekea tukio la ugomvi mkubwa mkubwa sana kama two weeks ago.. Ndio maana. Naogopa kueleza sana maana mashuhuda iam sure wengi ni jf members kutokana na neighbohood ugomvi uliotokea...wengine wanaweza kuja na hints hapa...mimi nimeamua kujitenga mbali na muhusika ili moyo upone..ila bado imekua ngumu kuna watoto
Hata wakili ili aweze kukusaidia kwenye kesi lazima ajue key problem, otherwise unaweza kutoa ushauri for the wrong problem.
 
watu wanataka tu umbea hawana chochote cha zaidi,ishia hapo hapo kuwa mmeachana inatosha,unachoulizia ni uzoefu wa wengne walioptia njia kama yako kwahyo kausha zako watakuja yaliyowakuta watakusimulia.

hawa wanaotaka usimulie ilikuaje hawana lolote zaidi ya umbea na mwisho wakuvamie wewe wakwambie ndio ulizingua thread nzima igeuke kukuandama wewe.

ila kama utapenda andika yaliyokutokea kama wanavyodai waja,andika ila jua hawatosaidia chochote zaidi ya kukwambia "pole sana"
Sasa wewe hapa umesaidia nini? Umeishia kujaza server na upupu tuu..
 
Kwakweli kuelezea kila kilichotekea nitareaveal identity za watu...ila kikubwa ni usaliti uliovuka mipaka..na yaliyotokana na usaliti ndio mazito zaidi...naombeni msaaada juu ua uzoefu wenu...mimi na mume wangu hatuwezi kurudi kama mwanzo...
Pole sana. Kama hutajali njoo inbox unieleze nikushauri kama unaona huwezi kuweka hapa hadharani.
 
Furaha ndo kila kitu. Mimi mwenyewe ndoa imenishinda. Nimesepa na wanangu na nina furaha acha kabisa. Si kauliza tulio na uzoefu. Ndo nimempa uzoefu.Wanaume wa bongo wenyewe full michepuko,Maugomvi. Bora kuwa mwenyewe kuliko kwenye ndoa iliyojaa masikitiko.
Wanawake wa Bongo nao siyo pasua kichwa mkuu? Ukipiga kimoja cha nguvu tabu kuisimamia kucha nayo tabu [emoji23] [emoji23]
 
Uzito unakujaga pale ambapo hakuna communication kwenye ndoa. If the two of you cannot sit down to talk about your problems then it is very difficult to solve problems in your marriage.
The thing is mume wangu hapendi communication..anakwepa each time
 
Sioni sababu ya kutowaambia ndugu zako machungu unayopitia ndani ya ndoa yako. Kama watamchukia kwa matendo yake mabaya aliyokufanyia hadi kutaka kuikimbia ndoa so be it! Wa kulaumiwa ni yeye na si wewe. Waite ndugu zangu uwaeleze kila kitu na kuwaomba ushauri nini ufanye. Wala usichelewe kuwaambia ndugu zako.
Nashukuru ndugu kwa mchango wako...ila image ambayo nimepaint kwa ndugu zangu watashangaa sana..na wanamuamini na kumuheshimu mnooo.. Sasa nikiwaambia hayo kesho na keshokutwa sijui watamtazama vipi usoni...hajawahi kulalamika kwa ndugu zangu kuhusu mapungufu yangu na mimi ni mwanadamu siko perfect...
 
Nashukuru ndugu kwa mchango wako...ila image ambayo nimepaint kwa ndugu zangu watashangaa sana..na wanamuamini na kumuheshimu mnooo.. Sasa nikiwaambia hayyo kesho na keshokutwa sijui watamtazama vp usoni...hajawahi kulalamika kwa ndugu zangu kuhusu mapungufu yangu na mimi ni mwanadamu siko perfect...
Basi tueleze sisi usiotujua kabisa.,
Japo kwa mafumbo na kuficha ID halisi na maeneo halisi..ili mradi ushushe mzigo.,

Kwani kampa mimba mamamkwe?.lol...kuna mdau kauliza hapo
 
Pole my dear ila you have to be strong Sana Kama umeona haiwezekani Tena beba wanao ondoka pigania furaha Kuna watu wanaishi kwenye magereza si ndoa Mimi kiukweli kitu chochote kitakachotaka kuniharibia furaha yangu nakiondoa haraka Sana kwenye maisha yangu napenda kua happy siwezi kukaa kwenye ndoa ya mateso never
Amesema yeye ni graduate hana kazi, so hiyo option ya kuondoka na watoto haiwezekani.
 
Kama nawe hauko perfect I don’t know not perfect to what extent basi vumilia tu ndoa iendelee huku ndugu zako wakiendelea kuamini hiyo FAKE image ya mume wako unayowaaminisha ndugu zako.

Nashukuru ndugu kwa mchango wako...ila image ambayo nimepaint kwa ndugu zangu watashangaa sana..na wanamuamini na kumuheshimu mnooo.. Sasa nikiwaambia hayyo kesho na keshokutwa sijui watamtazama vp usoni...hajawahi kulalamika kwa ndugu zangu kuhusu mapungufu yangu na mimi ni mwanadamu siko perfect...
 
Back
Top Bottom