Usibishane na anayepinga kuwa Mungu yupo

Usibishane na anayepinga kuwa Mungu yupo

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Hivi ni kweli watu wanaopinga uwepo wa Mungu wanaamini hivyo kwa mioyo yao? Sidhani!

Kama wapo, ni wachache miongoni mwa wengi wanaodai hivyo. Na kama kweli mtu hafahamu kuhusu uwepo wa Mungu na UWEZO Wake, ni sahihi kumwelewesha, lakini kama anapinga kwa lengo la kupinga ni kupoteza muda kujaribu kumweleza.

Nina mashaka kuwa huenda wanaodai Mungu hayupo, hawafanyi hivyo kwa sababu hawajui, bali wameamua kuwa wapinzani wa Mungu. Kwa lugha nyingine, wameamua kwa hiyari yao kumsaidia Shetani kuwapotosha watu wa Mungu.

Na kama mtu kachagua kuwa upande wa Shetani, ni busara kujihadhari unapoamua kumjibu. Labda, anatafuta ama kukukwaza tu au kuidhoofisha imani yako. Usimpe hiyo nafasi.

Shetani hajabadilisha mbinu. Si mbunifu. Mbinu zile zile alizozitumia zamani kuwaangusha watu wa Mungu ndizo anazozitumia hata sasa.

Unakumbuka alivyomdanganya Eva? Alijua fika kuwa Adam na mkewe waliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, lakini bado aliwaambia wakikaidi Maagizo ya Mungu, watafanana na Mungu.

Watafananeje na Mungu na huku walikuwa wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu? Tayari walikuwa wanafanana na Mungu! Shetani alichotaka ni kuwafanya wamkosee Mungu kwa kukaidi Agizo Lake kwao.

Alimwambiaje Yesu? Alifahamu kwa usahihi kabisa kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, lakini bado alijaribu kumtia mashaka kwa namna ile ile aliyowaangusha Adam na Eva. Alimwambia, "Ikiwa Wewe ni Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate"

Hizo kauli zilizotumiwa na Shetani kuwaangusha Adam na Eva dhambini na aliyojaribu kumlaghai nayo Yesu zinatofautianaje na za watu wanaotaka wathibitishiwe kuwa Mungu Yupo?

Shetani alilenga kumfanya mwanadamu wa kwanza asimwamini Mungu, akafanikiwa. Ndicho alichokusudia pia kwa Yesu, lakini akaangikia pua.

Ni bora unapoona watu kama hao wameibua maswali yenye lengo la kukejeli au kubishana, ukakaa kimya, au ikibidi kuwajibu, ukafanya hivyo kwa tahadhari. Labda tu kama itabainika kuwa lengo lao ni kutaka kujua na si vinginevyo. Kinyume na hapo, ni kupoteza muda kubishana nao.

Akikukejeli, usimrudishie. Ukimrudishia kejeli ni sherehe kwa Shetani. Ndicho anachotafuta. Anataka umkasirishe Mungu.

Akikutukana, kaa kimya. Shetani angetamani na wewe ungetukana, tena kwa tusi kubwa kuliko la aliyekutukana.

Chunga usemi wako. Ukiona utakachokisema hakitakuwa na msaada, ni bora ukae kimya. Au umjibu kwa kumkumbusha kuwa Mungu anampenda. Akijibu kwa jazba, endelea kumwambia, "MUNGU ANAKUPENDA", halafu utaona kama ataendelea na kejeli zake au la.

Narudia tena! Wengi wa wanaopinga juu ya uwepo wa Mungu huenda wanafanya hivyo kwa lengo la kupotosha wenye imani haba, na si kwamba hawajui kuwa Mungu Yupo.

Shauku ya Shetani ni kuona kuwa watu wengi wanaamini Shetani hayupo. Anajua akifanikiwa kuwaaminisha kuwa hayupo, ataweza kuwaaminisha pia kuwa Mungu hayupo. Akishindwa kuwaaminisha hivyo, atatafuta mbinu ya kuwafanya watu waamini kuwa ana nguvu sana.

Shetani ni muongo na baba wa uongo. Maisha yake ni uongo. Usiiingie kwenye mtego wake.

Mungu Yupo, tena Yu Hai. Na Shetani naye pia yupo, na anajua kuwa mwisho wake ni mbaya tu, hana namna ya kuukwepa.

Lakini Mungu ni Mzuri na ni Mkuu sana, hana mpinzani.

Ni hayo tu.
 
Hivi ni kweli watu wanaopinga uwepo wa Mungu wanaamini hivyo kwa mioyo yao? Sidhani!

Kama wapo, ni wachache miongoni mwa wengi wanaodai hivyo. Na kama kweli mtu hafahamu kuhusu uwepo wa Mungu
Kitu kilichopo kinathibitishika kuwa kipo.

Kila siku unaambiwa kuthibitisha hilo unashindwa.

Na unadhindwa kwasababu Mungu huyo hayupo.

Mazoea na urithi wa mapokeo kutoka zama za giza na ujinga ndo umetufikisha hapa.

Your psychology is totally corrupted
 
Dogmatically religious people are those who think that they’re right and everyone else is wrong. For them, religion isn’t about self-development or experiencing the transcendent, but about adhering to a set of rigid beliefs and following the rules laid down by religious authorities.

It’s about defending their beliefs against anyone who questions them,
asserting their "truth" over other people’s, and spreading those beliefs to others. For them, the fact that other people have different beliefs is an affront, since it implies the possibility that their own beliefs may not be true. They need to convince other people that they’re wrong to prove to themselves that they’re right.
 
Kitu kilichopo kinathibitishika kuwa kipo.

Kila siku unaambiwa kuthibitisha hilo unashindwa.

Na unadhindwa kwasababu Mungu huyo hayupo.

Mazoea na urithi wa mapokeo kutoka zama za giza na ujinga ndo umetufikisha hapa.

Your psychology is totally corrupted
Lakini Mungu ANAKUPENDA!
 
Suala uwepo/ kutokuwepo kea Mungu limekaa kiimani zaidi.
 
Suala uwepo/ kutokuwepo kea Mungu limekaa kiimani zaidi.
Hata imani pia kuna imani sahihi iliyo katika ukweli, na imani ya uongo.

Tunarudi pale pale.

Kuwepo kwa Mungu ni kweli au si kweli?
 
Haya ni mahubiri ya dini ya kikristo. Hoja ya uwepo wa MUNGU haiwezi thibitishwa kwa kutumia dini sababu dini ni matokeo ya imani ya uwepo wa MUNGU.

Wanaohitimisha kuwa hakuna MUNGU bila kusema kuna nini ni wapumbavu tu. Huwezi kuta samsung galaxy porini uamue tu kusema haikuwekwa na inteligent being kama binadamu bila kusema ni nani aliyeiweka au imefikaje hapo.

Una haki ya kusema hakuna MUNGU iwapo unaijua siri ya uumbaji ila kama hujui siri ya uumbaji ni sahihi kuamini yupo MUNGU aijuaye siri hiyo huku ukiendelea na tafiti za kujua maisha na yote tuyaonayo ni nini siri yake.
 
Hapa duniani unaweza kubishia chochote na ukashinda

Kwa sababu tu swali what is reality?? Lina utata sana

Usibishane na mtu bila kujua foundation yake Ni ipi kwenye mada husika
 
Haya ni mahubiri ya dini ya kikristo. Hoja ya uwepo wa MUNGU haiwezi thibitishwa kwa kutumia dini sababu dini ni matokeo ya imani ya uwepo wa MUNGU.

Wanaohitimisha kuwa hakuna MUNGU bila kusema kuna nini ni wapumbavu tu. Huwezi kuta samsung galaxy porini uamue tu kusema haikuwekwa na inteligent being kama binadamu bila kusema ni nani aliyekiweka au imefikaje hapo.

Una haki ya kusema hakuna MUNGU iwapo unaijua siri ya uumbaji ila kama hujui siri ya uumbaji ni sahihi kuamini yupo MUNGU aijuaye siri hiyo huku ukiendelea na tafiti za kujua maisha na yote tuyaonayo ni nini siri yake.
Safi sana ..
 
Hivi kama kitu kweli hukiamini would you even waste a second debating it?

Sijawahi kuona mtu anashinda mitandaoni miaka nenda rudi kupinga uwepo wa father Christmas!

Kama kweli mtu haamini father Christmas, angeandika rundo la makala na vitabu na kuhubiri na kujadiliana kila siku kuwa father Christmas hayupo?

Ulichosema ni sawa, sio kuwa hawaamini, ni wanamkataa actively yaani wanam reject/ turning against him. When you observe closely, it's usually out of emotional reasons, na wameamua kusambaza uongo kumhusu.

Anyways Mkristo amekatazwa kujadiliana na waliomkataa Mungu.

Zab 53:1 SUV

Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;

Methali 14:7 BHND

Ondoka mahali alipo mpumbavu, maana hapo alipo hamna maneno ya hekima.

Mathayo 7:6 BHN

Msiwape mbwa vitu vitakatifu wasije wakageuka na kuwararua nyinyi; wala msiwatupie nguruwe lulu zenu wasije wakazikanyaga.

Waroma 1:20

Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani uwezo wake wa milele na Uungu wake, umedhihirika wazi wazi kutokana na vitu alivyoviumba. Kwa hiyo watu hawana kisingizio.

Sahivi ukikutana na mkana Mungu akajifanya anakusimulia aliyofanya hakuna kumu acknowledge. Wanataka sifa na utukufu ziende kwao tu eti 😂

Wajameni mmekura? Ni msimu wa MIHOGO, BWANA AMETUPA MIHOGO TURE TUSHIBE!!
 
Hivi kama kitu kweli hukiamini would you even waste a second debating it?

Sijawahi kuona mtu anashinda mitandaoni miaka nenda rudi kupinga uwepo wa father Christmas!

Kama kweli mtu haamini father Christmas, angeandika rundo la makala na vitabu na kuhubiri na kujadiliana kila siku kuwa father Christmas hayupo?

Ulichosema ni sawa, sio kuwa hawaamini, ni wanamkataa actively yaani wanam reject. When you observe closely, it's usually out of emotional reasons.

Anyways Mkristo amekatazwa kujadiliana na waliomkataa.

Zab 53:1 SUV

Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;

Methali 14:7 BHND

Ondoka mahali alipo mpumbavu, maana hapo alipo hamna maneno ya hekima.

Mathayo 7:6 BHN

Msiwape mbwa vitu vitakatifu wasije wakageuka na kuwararua nyinyi; wala msiwatupie nguruwe lulu zenu wasije wakazikanyaga.

Waroma 1:20

Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani uwezo wake wa milele na Uungu wake, umedhihirika wazi wazi kutokana na vitu alivyoviumba. Kwa hiyo watu hawana kisingizio.

Sahivi ukikutana na mkana Mungu akajifanya anakusimulia aliyofanya hakuna ku acknowledge. Wanataka sifa na utukufu ziende kwao eti 😂

Wajameni mmekura? Ni msimu wa MIHOGO, BWANA AMETUPA MIHOGO TURE TUSHIBE!!
🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom