Usibishane na anayepinga kuwa Mungu yupo

Usibishane na anayepinga kuwa Mungu yupo

Hawa wafia dini hawana hoja za kuwajibu Atheists

Wana ishia kuzunguka zunguka na kukutishia hofu zao za kidini za Jehanamu na moto wa milele pasipo kutoa majibu.
Wafia dini wengi ni wanafiki wanachokisema sicho wanachokiishi.
 
Ukisaidia maskini unaenda mbinguni , kwa nini wewe usiwe maskini mimi nikikusaidie niende mbinguni?

Kwa hyo Mungu kaumba kilema ili wewe upate chance ya kuwasaidia ili uende mbinguni! Kwa nini wewe usiwe kilema ili mimi niende?

Kwa akili ya kawaida tu hakuna usawa na haki.
 
Zaidi ya asilimia 99% huwa ni mawakala wa shetani. Usione hivyo muda wanapokuwa wanapinga, nao wanakuwa wako kwenye mavuno kama ambavyo wewe huwa unafanya mikutano ya injili ili kuokoa roho za watu
Mnafanya mikutano kwa ajili ya kutapeli watu hela zao kwa jina la sadaka. Kama mnataka kuokoa roho za watu simuende mahospitalin huko watu wanakufa Kila sekunde mkaziokoe hizo roho
 
_20230721_153132.JPG
 
Acha uongo mkuu.
Hii tabia ya kumwita shetani mwongo wakat ninyi ndo waongo ni unafiki wa hali ya juu.

Mosi, Shetani hakumdanganya Eva ila shetani alimwambia Eva ukweli ambao Mungu hakutaka waujue.

Shetani alimwambia Eva kuwa wakila matunda ya mti huo watafumbuliwa macho na watakuwa kama Mungu kwa kujua mema na mabaya. Baada ya Eva na Adam kula matunda kweli walifumbuliwa macho yao na wakatambua kuwa wako uchi na wakajificha Mungu asiwaone(mwa 3:1-11)

Pili, Shetani alimwambia Eva wakila matunda waliyokatazwa hawatakufa. Na hii haikuwa uongo ilikuwa ni kweli mana hata Mungu mwenyewe anakili hapa (mwa 3:22-24). Baada ya Mungu kujua Adam na Eva wamekuwa kama yeye kwa kujua mema na mabaya akaamua kuwafukuza katika bustani ya Eden ili wasije kuchukua matunda ya mti wa uzima wakala ili wakaishi milele. Kwa hiyo wangefanikiwa kula hilo tunda basi wasingekufa.

Naomba niishie hapa maana mpaka hapa sijaona uongo wa shetani isipokuwa wewe na Eva ndo waongo kwa kutaka kugeuza ukweli kuwa uongo.
 
Back
Top Bottom