Usimshauri ndugu au rafiki asomee uandishi wa habari: ni sekta ambayo inaenda kufa na atateseka sana

Usimshauri ndugu au rafiki asomee uandishi wa habari: ni sekta ambayo inaenda kufa na atateseka sana

Kuna mdau humu ameposti juu ya changamoto zinazowakumba waandishi wa Azam Mikoani eti wameshushiwa ujira kutokea tshs 500,000 mpaka 300,000 kwanza nikagutuka kwamba wanalalamika kwa kulipwa 300,000?!!

Kama Azam waandishi mikoani wanalipwa 300,000 basi ITV hali ikoje? Je, hizi media ndogondogo za dini mambo yakoje? Kusema kweli hamna tasnia inazaa watu wenye "low self esteem" kama journalism maana ili waishi ni lazima walambe miguu ya watu wengi ili maisha yaende; mnaonaga vile vipaza sauti (mic) vinavyojaa katika press conference za kina Haji Manara na Mwijaku? Basi usishangae kila "mwandishi" aliyetokea kapoteza siku nzima ili akapewe tshs 10,000 tu siku iende

Kwa wanawake hali ndio mbaya zaidi katika kutafuta namna ya kujiongezea kipato

Pia soma:DOKEZO - Waandishi wa Habari Azam wanataabika Mikoani, wanahitaji msaada kulipwa stahiki zao
Jifunze kuwa content creator, ingia YouTube anza kutengeneza content, utapata matangazo mengi tu.

Ni maajabu unawapa habari Azam TV, badala wewe uwe na online tv yako
 
Hamna kazi ya uandishi ina vilaza wengi sana naweza kuwa smart katika kuendesha kipindi kuliko waliosomea
yap, vishoka wengi. imagine baba levo, mwijaku, masanja, joyce kiria na wengine nao ni waandishi. kwahiyo imekuwa tasnia ya machawa? hivi hawanaga control mechanism?
 
Waandishi wengi ni watu ambao shuleni walikuwa vilaza mno. Wengi wao kidato cha nne walifeli au kupata div IV ya mwisho. Hawakuwa na option zaidi ya kwenda kwenye uandishi. Pia wengi wao walipenda umaarufu zaidi kuliko hela. Media houses kwa sasa hazina uwezo wa kulipa mishahara. Makampuni yanaona ni heri yawekeze kwa Diamond kama mtu binafsi kuliko yaweke hela kwenye Wasafi TV/Fm ya Diamond. Waandishi watumie kujulikana kwao kutafuta kazi nyingine ya kufanya.
 
Shida waandishi waliosomea hawa ajiriwi wanapewa kazi kina dokta kumbuka....

Hiyo sio bongo tu. Hata kenya wanalalamika, nigeria wanalalamika, ghana wanalalamika.

Kwamba media zao siku hizi zinaajiri comedians, actors na tik tokers.. wenye degree za uandishi wa habari wanakosa kazi
 
Elimu yetu hii hii ya kukaririshwa unategemea mtu aibuke na practical experience?
Yes,
tena wanafanya practical jobs vizuri sana, mathalan,
hivi sasa nchi yetu ina mpaka mawaziri wakuu ambao walikua walimu tu, na kuna mawaziri na wakuu wa idara madaktari.

hata huyu muungwana Pascal Mayalla ni muandishi wa habari lakini pia ni mwalimu wa sheria na mfanyabiashara muandishi.

unaweza kusomea na ukafanya practical jobs ya kitu kingine kisichokua taaluma yako...

kwani wao waweze wana nini hata wewe ushindwe una nini gentleman? 🐒
 
Waandishi wengi ni watu ambao shuleni walikuwa vilaza mno. Wengi wao kidato cha nne walifeli au kupata div IV ya mwisho. Hawakuwa na option zaidi ya kwenda kwenye uandishi. Pia wengi wao walipenda umaarufu zaidi kuliko hela. Media houses kwa sasa hazina uwezo wa kulipa mishahara. Makampuni yanaona ni heri yawekeze kwa Diamond kama mtu binafsi kuliko yaweke hela kwenye Wasafi TV/Fm ya Diamond. Waandishi watumie kujulikana kwao kutafuta kazi nyingine ya kufanya.
Kwahiyo.the great.mzee wa DP World.alikuwa.sahihi
 
Kuna mdau humu ameposti juu ya changamoto zinazowakumba waandishi wa Azam Mikoani eti wameshushiwa ujira kutokea tshs 500,000 mpaka 300,000 kwanza nikagutuka kwamba wanalalamika kwa kulipwa 300,000?!!

Kama Azam waandishi mikoani wanalipwa 300,000 basi ITV hali ikoje? Je, hizi media ndogondogo za dini mambo yakoje? Kusema kweli hamna tasnia inazaa watu wenye "low self esteem" kama journalism maana ili waishi ni lazima walambe miguu ya watu wengi ili maisha yaende; mnaonaga vile vipaza sauti (mic) vinavyojaa katika press conference za kina Haji Manara na Mwijaku? Basi usishangae kila "mwandishi" aliyetokea kapoteza siku nzima ili akapewe tshs 10,000 tu siku iende

Kwa wanawake hali ndio mbaya zaidi katika kutafuta namna ya kujiongezea kipato

Pia soma:DOKEZO - Waandishi wa Habari Azam wanataabika Mikoani, wanahitaji msaada kulipwa stahiki zao

Trust, wale wenye akili zao na uelewa, hii mbele yao ni fursa. Wana nafasi adimu ya kujitofautisha, kwa kuandika habari zenye utafiti, balanced, zisizo na uchawa wala vinasaba vyake, na zenye nia ya kuelimisha na kuifahamisha jamii.

Copy and paste journalists wajue hawataweza kupambana na Zembela, Baba Levo au Mzee wa Minyama, ambaop habari zao ziko shallow na zenye mbwembwe nyingi ili kuwaonyesha vijana wanajua wanachofanya. Wale ni wachekeshaji. Vijana wakizeeka wataelewa. Watajuta wakati wamashapigwa.
 
mwajiriwa hupaswi kuwa tajiri ndugu, unapaswa kujikimu pekee yani unyonywe kisha upate ujira mdogo usife njaa
 
Sio Leo Toka kipindi hicho uandishi,utangazaji ni umaskini tu unless uwe na akili nyingi kama Millard ayo otherwise ukisomea journalism umaskini unakumaliza
 
Kuna mdau humu ameposti juu ya changamoto zinazowakumba waandishi wa Azam Mikoani eti wameshushiwa ujira kutokea tshs 500,000 mpaka 300,000 kwanza nikagutuka kwamba wanalalamika kwa kulipwa 300,000?!!

Kama Azam waandishi mikoani wanalipwa 300,000 basi ITV hali ikoje? Je, hizi media ndogondogo za dini mambo yakoje? Kusema kweli hamna tasnia inazaa watu wenye "low self esteem" kama journalism maana ili waishi ni lazima walambe miguu ya watu wengi ili maisha yaende; mnaonaga vile vipaza sauti (mic) vinavyojaa katika press conference za kina Haji Manara na Mwijaku? Basi usishangae kila "mwandishi" aliyetokea kapoteza siku nzima ili akapewe tshs 10,000 tu siku iende

Kwa wanawake hali ndio mbaya zaidi katika kutafuta namna ya kujiongezea kipato

Pia soma:DOKEZO - Waandishi wa Habari Azam wanataabika Mikoani, wanahitaji msaada kulipwa stahiki zao
Azam hawezi shindwa Lipa hizo laki 5-3. UKWAJU tu peke yake unaweza Lipa wa andishi wote tz.
 
Back
Top Bottom