Usiombe kuacha kazi kisa Forex. Nilivyofilisika na kukimbilia kijijini Tabora

Usiombe kuacha kazi kisa Forex. Nilivyofilisika na kukimbilia kijijini Tabora

Juzi Mimi na rafiki yangu tumeweka $10
Jana asubuhi ikawa $20.50
Nikamwambia withdraw hiyo $10 kwanza tuile Mambo yasiwe mengi
Duu umenichekeshaji lady trader.
Tokea kukuche wewe ndiye umenichekesha. Naomba tuwe na network ya traders wa Tanzania Ila sio kuuziana Ila kubadilishana story Mana trading is so lonely professional
 
Duu umenichekeshaji lady trader.
Tokea kukuche wewe ndiye umenichekesha. Naomba tuwe na network ya traders wa Tanzania Ila sio kuuziana Ila kubadilishana story Mana trading is so lonely professional
Hii haiwezekani.
 
Forex na Digital marketing na The Gwajimaz, The Mwamposaz na wengineo.
Hawa wote Ni walewale kasoro platforms
Screenshot_20231012-145148.png
hapa unasemaje. Akaunti imetoka dola 1000 mpaka $13000+ .

Yaani huwa nafurahi ama naenjoi watu wanavyoiongelea trading nazidi kusoma akili za binadamu pindi zinaposhindwa kitu Basi zitatafuta kila Aina ya sababu.

Sikieni trading unawaza kinyume na tunavyowaza,tulivyolelewa,kufundishwa shuleni kwenye nyumba za ibada na jamii na hata nyumbani.yaani inaenda kinyume na ubinadamu wetu na ndio Mana watu wanadondokea pua.. hii sio kuwa Ni afrika tu hata ulaya wanapoteza ama kuliwa hela. Kuna mchina mmoja hapa akaniambia ana miaka minne haiichungulii Mana alipoteza $60k so anaichana nayo,Kuna dogo mmoja alipoteza dola laki Saba ulaya huko akajiua.
Hii kitu Ni ya Moto ama Ni Vita so usiisngie unadhani Ni game ya kitoto ama kisichana kila mtu anaweza akaicheza.yaani kufundisha Ni rahisi mno kuliko ku participate.
Hii dude sio lelemaa haina tofauti na Vita ama kupigana ngumi unadhani Ni wangapi Sasa watajaribu
Screenshot_20231012-145148.png
 
View attachment 2779944hapa unasemaje. Akaunti imetoka dola 1000 mpaka $13000+ .

Yaani huwa nafurahi ama naenjoi watu wanavyoiongelea trading nazidi kusoma akili za binadamu pindi zinaposhindwa kitu Basi zitatafuta kila Aina ya sababu.

Sikieni trading unawaza kinyume na tunavyowaza,tulivyolelewa,kufundishwa shuleni kwenye nyumba za ibada na jamii na hata nyumbani.yaani inaenda kinyume na ubinadamu wetu na ndio Mana watu wanadondokea pua.. hii sio kuwa Ni afrika tu hata ulaya wanapoteza ama kuliwa hela. Kuna mchina mmoja hapa akaniambia ana miaka minne haiichungulii Mana alipoteza $60k so anaichana nayo,Kuna dogo mmoja alipoteza dola laki Saba ulaya huko akajiua.
Hii kitu Ni ya Moto ama Ni Vita so usiisngie unadhani Ni game ya kitoto ama kisichana kila mtu anaweza akaicheza.yaani kufundisha Ni rahisi mno kuliko ku participate.
Hii dude sio lelemaa haina tofauti na Vita ama kupigana ngumi unadhani Ni wangapi Sasa watajaribuView attachment 2779944
Share hiyo na mfungua uzi. Mimi hizo katuni zenu huwa hata sizisomi. I'm very fine na hustles zangu, silali njaa.
 
Sehemu ya Pili (2)

Nilipoishia

Niliamua kufungua akaunti yangu ya forex na kutumia akiba yangu kama mtaji wa kuanzia. Safari yangu ya kuelekea uhuru wa kifedha ilikuwa imeanza.

Tuendelee..

Nilitafuta eneo bora pa kufanya biashara yangu ya forex. Nilijitahidi kutafuta mahali ambapo ningeweza kujikita na kuzama kwenye biashara yangu bila ya kuingiliwa na mazingira ya nyumbani. Niliamua kutafuta ofisi ya wazi, na mwishowe, nilipata chimbo karibu na Posta, mitaa ya Samora.

Hapo ndo ikageuka kuwa ofisi yangu. Pale, niliweka kompyuta yangu, chati za forex, na kila kitu ambacho ningehitaji kufanya forex yangu. ningeweza kufanya forex bila kuingiliwa na mazingira ya nyumbani.

'''Kabla sijaendelea niseme tu ukweli, pale nilikutana na wadau wengine bana watu wanapambana na hii forex asikwambie mtu, Nnilikutana na mrembo nakumbuka alisema anasoma Udsm,ni mrembo kwelikweli, hii ilinipa moyo na nikajisemea moyoni kumbe forex ndo mpango mzima, nikajipa moyo !hii si ndo biashara sasa, tena iliyokamilika, hakika sikujutia kuacha kazi, Tena nilianza kuiponda huku nikishangaa nilikuwa wapi Mimi mtoto wa Mwanzibo Kitombo..'''

Hii ni kumbukumbu isiyofutika kwenye moyo wangu hadi kesho.

!!Na yule mdada sikumuacha salama, maana nilikuwa naye karibu kama sufuria na mfuniko!!

Tuendelee

Nilianza kujifunza kwa kina kupitia akaunti ya demo, nikiamini kwamba kama ningeweza kufanya vizuri hapo, ningeweza kufanikiwa kwenye akaunti halisi. Kwa miezi kadhaa, nilijitahidi kufanya forex kwa uangalifu na ujuzi wa kujifunzia kupitia akaunti ya mazoezi. Niliona mafanikio kidogo, na hili lilinipa matumaini kwamba naweza kushinda changamoto zote.

Banabana, nilipoamua kuingia kwenye akaunti halisi na kuweka mtaji mkubwa, hali yangu ilibadilika haraka mapigo ya moyo yalianza kwenda mbio kama farasi wa mwisho kwenye mashindano ya mbio. Hofu ilinikumba na jasho baridi lilianza kunitiririka. Nilijisikia kama mtu aliyeingia kwenye uwanja wa vita bila ya silaha, nikiwa mgeni katika ulimwengu huu wa forex. Kutoka kuangalia tu chati za forex kwenye skrini ya kompyuta yangu hadi kuingia kwenye soko halisi, ilikuwa ni tofauti kubwa.

Kila bonyeza la mouse lilikuwa na uzito wa dunia kwenye kidole changu. Niliogopa kufanya uamuzi mbaya na kupoteza pesa yangu yote. Kila wakati nilipotazama bei zikibadilika haraka kwenye skrini yangu, hisia za kutokuwa na uhakika ziliniondoa usingizi.

Kila pair, iwe EUR/USD siyo GBP/JPY ilionekana kama mtihani wa ujasiri wangu na ujuzi wangu. Hofu ya kupoteza ilinifanya nipambane na migogoro ya ndani, nikiwa na shauku ya kufanikiwa lakini pia na wasiwasi wa kushindwa.

Siku ya tatu hofu ilipungua kila kitu kilionekana kama vile nilivyotarajia. Niliweka trade zenye faida, na akaunti yangu ilionekana kuimarika.

Lakini ghafla, soko lilibadilika mwelekeo, hii siku sintoisahau ilikuwa Arusha nimeenda kula bats na Toto za (R chuga), nimetoka zangu pinpoint naelekea Njiro Tanesco, ndani ya chuo cha wasibu Nina appointment bidada mmoja, ilikuwa jionijioni hivi mvua ikiwa inanyesha nilifika mahali sipakumbuki vizuri gari langu lilikwama, eebhana her, basi nikaanza piga gia wapi, furukita huku na kule wapi, hapo kumbuka nilikuwa nimeweka trade kabla sija weka PT na SL ndo kikatokea hiko kisanga. Baada ya kupambana kulitoa gari kwenye matope. Nikasahau kama niliwema trade, Bahati nzuri walitokea vijana na sikusita kuwaomba msaada, tulifanikiwa kulitoa japo kwa jasho Mimi mwenyewe nimelowana mwili mzima. Kuwashukuru wale vijana nikaingia mfukoni na kutoa note za elfu kumikumi tank nikawapa wale vijana wagawane.

Sasa kimbembe Kikaanzia pale niliporudi kwenye gari langu, nilishtuka ghafla. Nilikumbuka kwamba nilikuwa nimesahau kuweka stop loss wala take profit kwenye biashara yangu. Mioyo yetu inaweza kuwa na furaha na kisha kuwa na wasiwasi mkubwa zaidi ya mara moja.

Nilijikuta nimeshikwa na mshtuko huku nikifikiria kuhusu hatari ya kuacha biashara yangu bila ulinzi wowote. Nilipochukua simu yangu na kufungua MT5.


Hee bana hee nilihisi kuchanganyikiwa....

(Sehemu inayofuata itaendelea Husikose...)
Umeongea kweli kabisa hisia za trader anayeanza. Skills za trading Ni to trade without fear Basi ndio skills unazotakiwa kuzitafuta na sio eti kuwa na maarifa mengi mno ama kuwa smart
 
Duu umenichekeshaji lady trader.
Tokea kukuche wewe ndiye umenichekesha. Naomba tuwe na network ya traders wa Tanzania Ila sio kuuziana Ila kubadilishana story Mana trading is so lonely professional
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Nilimwambia itoe hiyo kwanza tuile hiyo ingine ata ikifa itajijua huko
 
Nilikuwa nimechoka na maisha ya kufanya kazi saa nane kwa siku katika ofisi flani hivi pale posta jijini Dar es Salaam. Ndoto yangu ilikuwa kubwa zaidi kuliko kiti changu cha ofisini na mshahara wangu wa kila mwezi. Nilikuwa na hamu kubwa ya kujaribu kitu kipya, kitu ambacho kingenipa uhuru wa kifedha na fursa za kutimiza ndoto zangu.

Nilitambua kwamba kwenye ulimwengu huu wa kisasa, forex ilikuwa njia inayopendelewa zaidi ya kuwekeza na kupata faida kubwa. Nilivutiwa na hadithi za watu waliojikomboa kutoka kwenye mikono ya ajira na kuwa mabosi wa maisha yao wenyewe kupitia biashara ya forex. Hivyo basi, niliamua kuwa mmoja wao.

Nilipofikiria juu ya kuacha kazi yangu na kujitosa kwenye ulimwengu wa forex, moyo wangu ulijaa msisimko na wasiwasi. Nilisoma vitabu vingi na kujiandaa kwa miezi kadhaa kabla ya kufanya uamuzi wa mwisho. Nikaamua kuwa huu ndio wakati wangu wa kujaribu kitu kipya, wa kujiletea mabadiliko kwenye maisha yangu.

Kuacha kazi haikuwa uamuzi rahisi, lakini nilihisi kwamba huu ndio wakati sahihi wa kujitolea kwenye safari ya forex. Nilijiandaa kihisia na kifedha, nikiwa na matumaini kwamba ningeweza kugeuza ndoto zangu kuwa ukweli. Niliamua kufungua akaunti yangu ya forex na kutumia akiba yangu kama mtaji wa kuanzia. Safari yangu ya kuelekea uhuru wa kifedha ilikuwa imeanza.

Husikose sehemu inayofuata ...
kama unaandika HUSIKOSE sehemu inayofuata . una haki ya kuliwa pesa zako
 
Yani unaanza forex baada ya kuacha kazi?

We boya kweli kwelii..

Halafu uliifanya fx kama full time job, wakati huohuo unaendekeza kula bata, mara umepita na kitrader chenzio cha udsm.... mara uko chuga kukesha night clubs..

Meanwhile you are a novice trader...

Wewe jamaa ni boya, narudia tena..
 
Back
Top Bottom