Usione nakubembeleza sana ukahisi sina kazi za kufanya, ni mapenzi tu kuna siku nitachoka kuyakumbatia madhaifu yako

covid 19

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2014
Posts
6,967
Reaction score
17,452
Hii ndio kauli niliyoambiwa na wife wangu kipindi hiko nipo moto balaa michepuko kama yote sieliwi nawaza misabwanda tu.

Hii kauli ilibadili maisha yangu sana.
Nikawa mpolee na familia..

Wewe uliambiwa kauli gani na mwenza wako ukabadili maisha yako ya mahusiana?
 
Wanawake Bwana
Anaweza akakusamehe makosa makubwa sanaa
Halafu akakuacha kwa kosa dogo usilodhania

Kuna jamaa alichepuka na mdogo wa mke wake aliyekuwa anakaa naye nyumbani,, mke hata hakuonesha kulalamika alimsamehe

Ni miaka mitano imepita sahv wanamigogoro kibao isiyo na sababu
 
Wewe uliambiwa kauli gani na mwenza wako ukabadili maisha yako ya mahusiana?
Mimi aliniambia β€œ kuna wanawake wengi wazuri zaidi yako wanatamani kuwa na mimi, kwahiyo usijione bora sana.” Hii siku nilibadili maisha yangu ya kimahusiano kwa kumlima kibuti akawe na hao warembo zaidi yangu. Alilia yule mwanaume kama jinga.
 
Hivyo mkaamini alisamehe sababu hakuonyesha kulalamika..??
bado hamuwajui wanawake, karibuni duniani..!!πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Baada ya kulia alikubali matokeo?
 
Sio kama jinga ni jinga hasaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…