Usipotoshwe na watu wasioelewa maana na utaratibu wa kuwa na raia pacha. Angalia hapa maelezo ya uraia pacha na niulize swali lolote nitakujibu

Hapo ndipo unapokosea. Tunaposema uraia pacha sio kwa Watanzania pekee, bali ni kwa Watanzania kuwa na uraia pacha na nchi nyingine na wasio raia wa Tanzania kuwa na uraia pacha na Tanzania. Haiwezi ikaa suala la upande mmoja kama unavyosema
Mimi najikita kuongelea uraia pacha wa upande wa mtanzania wa country of origin Tanzania kuwa hauna faida yeyote lakini pia uraia pacha wa mtu wa taifa lingine mfano mchina, mhindi na mwarabu una faida gani kubwa wakati kazi yao kubwa inakuwa ku import tu bidhaa toka Nchi zao kuja kuuza kwetu? Na ku drain pesa zetu za kigeni tu? Inasaidia Nini? Hata hao wa Nchi zingine haisaidii
 
Na swalijingine

Tanzania ikiruhusu uraia pacha, ni kwa ajili ya Watanzania pekee?

Hapana. Unaporuhusu uraia pacha inakuwa ni kwa ajili ya Watanzania wanaotaka kuchukua uraia wa nchi nyingine, na watu wa nchi nyingine wanaotaka kuchukua uraia wa Tanzania. Ni lazima Tanzania na nchi hiyo nyingine zote ziwe zinaruhusu uraia pacha.
 
Mkuu Yehodaya, nadhani kuna point hapa unagusia, kwamba Watanzania wakiruhusiwa kuwa na uraia pacha kutakuwa na negative effect kwamba watatoa capital Tanzania kwenda nchi nyingine?

Inawezekana, lakini sidhani kama effect itakuwa kubwa kiasi hicho. Watanzania watakaoingiza capital nchini ni wengi kuliko watakaotoa capital nchini.

Na upande wa pili ni wale watakaopewa uraia wa Tanzania kuingiza capital nchini. Lazima haya mambo yaende pamoja kwa kuwa hatuwezi kuwa na uraia pacha unaoruhusu raia wa nchi nyingine kuwa na uraia pacha na Tanzania lakini raia wa Tanzania wasiwe na uraia pacha na nchi nyingine
 
Kwa miaka kibao uzoefu uko wazi watanzania walioko nje hawasaidii viwanda vya Tanzania kuuza bidhaa za Tanzania kwenye nchi zao Kama wahindi na waarabu .kikubwa Ni kuangalia faida ya diaspora kwenye uchumi mkubwa wa movement of goods kwenda soko kule aliko sio vihela vidovidogo vya remmittance vya pesa za rambi rambi na michango ya harusi

Wahindi na waarabu tunao miaka nenda Rudi lakini wanachofanya Ni kutuletea tu bidhaa zao .Sisi soko lao la bidhaa zao tu kwa asilimia kubwa.miaka nenda Rudi.Mchina kaja ndio kabisa katufanya gulio la bidhaa zake.Ukimpa uraia pacha ana kipi kikubwa kwa Nchi.? Ni Ku drain tu our forex kununua bidhaa kutoka his country of origin at our forex expense Wahindi,waarabu,wachina etc hutoa uraia pacha wakijua what will happen kwa viwanda vyao na bidhaa zao.
 
Kwa ninavyowaona wageni wakipata uraia wa Tanzania hamna maajabu watafanya. Yani Mhindi umpe uraia wa Tanzania akiwa katoka India unadhani atafanya nini, ataleta mapikipiki yao auze achukue hela arudishe kwao India. Ukimleta Mfaransa hivo hivo atafanya. Hawa wataondoa nafasi za wabongo wanao-import bidhaa za nje, watakuwa export houses za makampuni ya kwao

Wabongo walioko nje ni wachache na wana hela kidogo tu za kupandia ndege. Ukiwaambia watoe mitaji walete uku haiwezi fidia hela inayochotwa kwenye mzunguko wetu kwenda nje. Kwa mtazamo wa kiuchumi

Umeeleza mengi ambayo sikuyafahamu. Asante
 
Ikiwa Watanzania wazawa tu tena mpaka wamepewa hatamu serikalini, Wanauza Taifa kwa vipande vya fedha, Itakuwaje kwa mzaliwa wa UK aliyepewa haki yavkuitumikia Tz sambamba na UK yake moyoni?

Sisi nje waliopo nje wengi wamejiendea wenyewe, lakini wageni wengi toka nje WAMETUMWA(hata tudhaniao kuwa ni watalii) Wanakuja with missions, sisi tunawaza njaa zetu binafsi.

Tujenge uwezo kwanza, Uwezo was Kutuma watu nje, sio Uhuru wa kila ajisikiaye kwenda sense tu.
 
Eti utaratibu wa raia pacha, nani kauweka,si binadamu tuu,tena kwa interests hasi.Achaneni na kusombwa na ideas fake zenye nia ovu,be pragmatic,that is deal with things sensibly and realistically in a way that is based on practice rather than theoretical considerations.
 
Mkuu Yehodaya acha hizo. Watanzania wa diaspora watasaidia viwanda vya Tanzania kuuza bidhaa za Tanzania kwenye nchi zao kwa msingi gani, kwa framework gani hasa? Yaani bado uko kwenye mfumo wa uzalendo wa kuwa na viwanda vya serikali kwa hiyo kwa uzalendo watangaze bidhaa za serikali?

Yaani wewe leo uende USA, utazipigia debe bidhaa za juice za Azam kwa kuwa tu ni za Tanzania? Kwa gharama ya nani? Na kwa nini uwalaumu hao Watanzania badala ya kumlaumu Azam kuwa ameshindwa kutumia Diaspora ku-promote bidhaa katika nchi wanazoishi?

Kwani Azam akisema nataka Watanzania mlioko nje muwe ma-agent wangu wa Azam Juice, na awaandalie mazingira ya kuwa agents, nani atakataa fursa kama hiyo?

Na labda pia usisahau chema chajiuza kibaya chajitembeza. Bidhaa za Tanzania zikiwa na viwango bora kuliko hizo za huko wanakoishi Diaspora, zitauzika tu. Lakini Azam akitengeneza juice ambazo baada ya wiki mbili ya shelf life unakuta juice imegawanyika unga chini maji juu, nani atanunua hizo juice huko majuu?

Na usisahau suala la kuwa na competitive advantages. Tanzania tunaweza kuwa na juice bora za machungwa kuliko zilizoko USA, lakini unajua cost za kuzalisha na machungwa kati ya Tanzania na USA? Unaweza kukuta hadi uifikishe orange juice ya Azam USA, itabidi uuze dola 5 kwa kopo la 500ml, wakati juice za USA zinauzwa dola moja kwa kopo la ml 500.

Kwa hiyo mambo sio rahisi kama unavyofikiria, na tusiwalaumu Diaspora kwa mambo ambayo yako nje ya uwezo wao. Jambo rahisi ni Diaspora kuleta capital Tanzania ili kuinua kiwango cha maisha ya Watanzania kwa kutengeneza nafasi za kazi nk. Hata Diaspora kuleta tu fedha za kujengea nyumba ni jambo kubwa sana, na ujue Diaspora ambaye amechukua uraia wa nje anaweza kusita hata kujenga nyumba moja tu Tanzania, wakati ana uwezo wa kujenga nyumba hata kumi akazipangisha. Kwa hiyo tunapoongelea Diaspora kuleta capital Tanzania, usifikirie mambo makubwa sana. Ni katika economies of scale, kwamba kile kidogo kidogo wanacholeta, kwa sababu wako wengi, kinaishia kuwa kikubwa sana.
 
Wewe umesoma sana hadithi za Musiba, vitabu vya Kufa na Kupona, nk. Kwa nini uwe na mawazo negative sana? Kwani nchi ngapi zinaruhusu dual citizeship, na hayo unayosema yameshafanyika katika nchi ngapi unazoweza kuzitolea mfano?

Kwani pia Tanzania tumelala kiasi hicho hadi watu wawe wanajifanyia hujuma wanavyotaka?

Na uraia pacha hauna maana tunatuma watu nje, hiyo ni wrong perception.
 
Inabidi usikilkize ushauri wako mwenyewe - be pragmatic.
 
Kwani nchi ni mali ya nani mpaka muwaombe uraia? Kama makaburi ya babu na bibi zako yako hapa, babu na bibi zako waliishi hapa kabla hata ya nchi kupata uhuru, kwa nini unabembeleza serikali ikupe haki yako ya kuishi hapa kama mzawa?
 
Umeongea vitu vingi sana ohhh Azam aandae mazingira atafute Diaspora wawe agent wake.Mmmmmmm

Wahindi , waarabu na wachina walioko Tanzania hatuna mtu Wala kampuni yeyote huwatongoza kuwa wawe agents wao wa Nchi walikotoka !!!!

Diaspora ya watanzania iliyo nje Ni hopeless na malofa wa kutupwa

Ohh yaandaliwe mazingira Wahindi,waarabu wamekuwa matajiri toka kipindi Cha ukoloni na kipindi Cha Nyerere cha ujamaa wa kikomunisti wakiwa importers was bidhaa toka Nchi zao

Ndio maana nasema kumpa uraia pacha mtanzania wa country of origin Tanzania Ni ujinnga tu ana Nini Cha maana wengi malofa tu hata wakifiwa huko nje hulia michango ya kusafirisha tuchange tulioko Tanzania pia
 
Hili swala la uraia pacha huwa linapotea na kurudi kama homa ya vipindi.....
kamwe hamtofanikiwa
 
Una safari ndefu ya kujifunza. Katika Maisha mengi udhaniayo kuwa rahisi ndiyo yabebayo Uzito, na yale uyaonayo kuwa magumu ndiyo yajaayo Viini Macho.

Uraia pacha ni Fursa, hasa kwenye Ujasusi was Kiuchumi. Ukichagua kutokuona hayo, ni hiyari yako.
 
Naomba unifafanulie namba 10 na 14 kuna sehemu umesema kama utafanya uhalifu nchi uliopewa uraia wanaweza kukunyanganya uraia wao. Suali langu sasa hawa wanakurudisha nchi gani wakati ushaukana uTanzania wako?Ikiwa mzaliwa wa Tanzania wamfanyie update tu ya uraia pacha kwasababu Tanzania ni mama kwake na mama hamkatai mwana. Kwanini aombe tena uraia wa Tanzania? Uraia wa kuzaliwa na wa kuomba upi una nguvu zaidi? Mfano baba Mzaramu mama Mmakonde mtoto akienda umamani hutambulika mtoto wao lakini kabila yake ipo palepale ya kizaramu. Sasa kwanini mzawa wa Tanzania asiwe mtanzania wakati hakiharibu ulaya au America atarudishwa Tanzania tu.
 
Hili swala la uraia pacha huwa linapotea na kurudi kama homa ya vipindi.....
kamwe hamtofanikiwa
Diaspora huwa wanadhani wao huko waliko wana akili sana waliobaki Tanzania Ni wajinga wajinga .Wapeleke mswada bungeni ndio watajua walioko Tanzania akili zimo au la.Tunawaangalia tu .They think we are stupid.
 
Una safari ndefu ya kujifunza. Katika Maisha mengi udhaniayo kuwa rahisi ndiyo yabebayo Uzito, na yale uyaonayo kuwa magumu ndiyo yajaayo Viini Macho.

Uraia pacha ni Fursa, hasa kwenye Ujasusi was Kiuchumi. Ukichagua kutokuona hayo, ni hiyari yako.
Yaani wewe katika kufikiri kwako na conspiracy theory zako, katika ncho zoote Africa zinazoruhusu uraia pacha hilo hawajaliona ila wewe tu ndio una busara ya kuliona? Angalia ramani hapa chini hadi sasa ni nchi ngapi Afrika zimebaki madungaembe ya uraia pacha kwa kuwa zina mawazo kama unayosema. Yaani hawa wote ni wajinga wa kuuza nchi zao ila sisi ndio tunajua.

Unajua, siku ikitokea Watanzania wote wakapoteza pua zao na kutokuwa na pua, na wewe peke yako ndio ukabaki na pua, basi wewe ndio utakaekuwa mwenye ulemavu wa pua. Fikiria hilo kwa makini.

 
Reactions: CES
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…