Usisite kumsaidia mtu anayeomba umnunulie chakula

Usisite kumsaidia mtu anayeomba umnunulie chakula

King Jody

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2022
Posts
1,834
Reaction score
3,456
Habari za kutwa wana JF

Natambua hali ya maisha ni ngumu kwa ujumla, matapeli ni wengi mno, wengine wanajifanya wagonjwa ili tu wapate msaada, nk,

Lakini ukikutana na mtu hakuombi pesa ila anakwambia ana njaa anaomba umnunulie chakula na ukimwangalia kwa jicho la kawaida anamaanisha anachokisema, usisite kumsaidia, kama unahisi ni tapeli mpeleke kwenye mgahawa mnunulie chakula then uendelee na mambo yako, usimpe pesa mkononi.

Njaa mbaya sana ndugu zangu, siyo kila mtu ana kazi, siyo kila mtu anatafuta kazi akapata kirahisi, maisha ni fumbo, tenda wema nenda zako.

Wengine wamesoma wana ma degree lakini milango bado haijafunguka,kazi zenyewe wanapeana kwa kufahamiana, hawaangalii vigezo, ni mwendo wa kujuana, wanaita connection.

Watu wanapitia magumu yasiyoelezeka hadi wanafikia hatua ya kujinyonga kwa sababu hawaoni thamani yao katika ulimwengu huu.

Ikiwa Mwenyezi Mungu amekujalia unakula vizuri, unalala pazuri, unavaa vizuri wewe na familia yako, Mshukuru sana lakini usisite kuwasaidia wenye uhitaji

Kwa leo ni hayo tu nimeona ni vyema kushare na nyie.
ASANTENI SANA
 
dah asee umeongea mkuu..... hakuna alieniomba chakula nikakosa kumpa sijapitia maisha ya shida ila njaa naijua njaa sio kitu kizuri kabisaaaa

mru akikuomba pesa akasema anaenda kula ww mnunulie chakula ale....
 
Juzi kuna sehemu flan nilikua nimekaa akaja dogo mmoja wa miaka kama 11 kashika unga kwenye hii mifuko midogo , akaniambia naomba nisaidie hela ya mboga nikale na mdogo wangu nikataka kuweka ugumu ili nimuhoji zaidi ila dogo akanikatisha na akaniambia nimebaki mimi na mdogo wangu tu nyumbani hatuna mkaa wala mboga hata huu unga kuna mtu tu kanisaidia.

Ikabidi nitoe chochote, dogo alishukuru na aliondoka haraka sana mwendo wa mtu ambae ni kama vile ana majukumu mengi ya kufanya na muda hautoshi ile kitu kilinigusa sana moyo maisha siyo poa kabisa yani.
 
Mchana jua la utosi wakati naenda matembezi,,napita njia fulani ya vumbi,nikaona mtoto kalala barabaran,nikamuita akaitika akasimama,nkamuulza maswali yangu mwisho akasema ana njaa,

Nkamwambia twende nkakununilie chakula kule ni mazingira ya mbali kidogo na maduka, mtoto akagoma kabisa eti anaogopa,basi nkaishia tu kumwambia aende nyumbani,nisingeweza kumlazimisha mwisho niitwe mtekaji

Ingawa kalionesha kutamani.
 
Juzi kuna sehemu flan nilikua nimekaa akaja dogo mmoja wa miaka kama 11 kashika unga kwenye hii mifuko midogo , akaniambia naomba nisaidie hela ya mboga nikale na mdogo wangu nikataka kuweka ugumu ili nimuhoji zaidi ila dogo akanikatisha na akaniambia nimebaki mimi na mdogo wangu tu nyumbani hatuna mkaa wala mboga hata huu unga kuna mtu tu kanisaidia.

Ikabidi nitoe chochote, dogo alishukuru na aliondoka haraka sana mwendo wa mtu ambae ni kama vile ana majukumu mengi ya kufanya na muda hautoshi ile kitu kilinigusa sana moyo maisha siyo poa kabisa yani.
Ulifanya jambo jema mkuu, ubarikiwe sana
 
Back
Top Bottom