Usomaji wa Maandiko ya kidini (Biblia)

Usomaji wa Maandiko ya kidini (Biblia)

Achana na hadithi zisizo na kichwa wala miguu.

Biblia ni sawa na Hekaya za Abunuwasi au riwaya za Alfu Lela ulela.

Unasoma huku unajipa matumaini uchwara na kusema unapata ufunuo kumbe ni Hallucinations tu.

Biblia ni hadithi hadithi zisizo na ufunuo wowote ule zaidi ya hallucinations zinazoitwa imani.

Amka wewe!!
FB_IMG_1691913349934.jpg
 
Kaka yanayokukuta wewe kama yanayonikuta mimi ila kwangu naona ni zaidi.
Yani am not interested anymore kwenye habari za hizi dini.
Nakua napatwa na khofu labda mungu kaondoa imani juu yangu ndo maana niko hivi kama wao wasemavyo.

Yani nikisikiliza mashekhe na mapastor naona nikama mawazo yangu ni makubwa mbele ya wanachokinena, yani naona tu ni upigaji uliowekwa kwa misingi ya kumtisha na kumfubaza kiakili mwanadamu na sio kumjenga.

Naamini mungu yupo but nakua nakosa right connection kwangu na kwake maana uyu wa kwenye izi dini naona sio kabisa au yawezekana ndio ila sio kwa jinsi wanavyomnena.

VITU VINAVYO NIKATISHA TAMAA KWENYE HIZI DINI.

• Story
Izi dini zina story za historia ya mungu na Dunia mpaka kufika leo, kwakweli mwanzo nilikua naamini mambo ya adam na eva, ghalika na n.k ila nilivyokua nimejikuta izo stories haziningii kichwani mwangu naona ni uzushi tuu, maana issue za nuhu kasimulia nuhu mwenyewe unamiinije kama hakuongeza chumvi,
story za sodom na gomora ilikua ni kijiji sio Dunia yawezekana ikiwa ni natural disaster kama inavyotokea ata hiki kipindi kama volkano na kwa miaka iyo waliona ni jambo kubwa kutokana na teknologia yao kua ndogo ndo maana wakalikuza kupita kiasi!

Kuna hadith nyingi za kiislam kwamba kuna mda mungu alituma ndege wamebeba mawe kuua maadui wa mtume yani zinakua haziningii kabisa, habari za maliamu kuona malaika ndo kabisaa, najiuliza kwani shetani hawezi kua mweupe, au mtu akikumbia utazaa mtoto wa mungu na atahimiza kusali ndo inajustfy kua uyo malaika hakua jini wala shetani!! Maana leo hakuna mtu anayemjua jini malaika na shetani katika maumbile, watu wanadefine ivo vitu kwa matendo, ukitokewa na mtu mweupe akakumbia piga goti shika maji uombe mungu unaamini ni malaika, ukitokewa na kitu cheusi kinaogopesha kinataka kukuua unajua ni shetani.

• Dini kutokea sehemu moja.
Dini zote kuu zimetokea eneo moja, wengine tumekuja kupokea, Huwezi sikia kulikua na mtume wala nabii mchina wala nini, wote ni Middle East. Story za kupokea jumbe za mungu na kuona malaika saivi naona kama ni hadidhi za Juma na Uledi, maana kichwani mwangu inakataa kuamini mtu atoke alikotoka aseme kuua ni dhambi mungu atakuchoma moto!! Sababu naamini hata bila huo ujumbe kwa akili za kawaida tu lazima huone kuua sio sawa, kuiba, kuchukua mpenzi wa mtu, kutukana mtu n.k sio mpaka mtu utishiwe moto.

Kunamda nawaza tuu ni vipi kama hao mitume walikua ni watu kwenye koo zao baada ya kuona vita ni vikubwa na manyanyaso wakaamua kusema wamepokea funuo kuhusu habari za mungu ili kufanya hao wafalme wauaji wasiendelee kuua watu hovyo! Au watu kuchukua wanawake zao kibabe ndo waka establish ndoa!! Maana kabla y Dini kila sehemu kulikua kunaendeshwa kwa akili za wafalme na kwa ubabe tuu bila kujal haki za kibinadamu.

Inshort sidhani kama niko sahihi na wala sijui kama nipo wrong ila izo story za watu wa uko Middle East kutumbia kuna shetani na mungu wanakinzana, asee zimekua ngumu kuningia now days nahisi nahitaji maombi labda kweli uyo shetani kaniingia.
Umefika hatua nzuri ya kujikomboa kifikra na kiakili.

Mungu na Shetani ni dhana za kutungwa hazipo katika uhalisia.

Ndio maana watu wanahangaika sana kuelezea na kuzizungumzia dhana hizi kwa vile hazipo na hazijawahi kuwepo kujiongelea zenyewe.
 
Neno la Mungu ni jipya kila siku tunahitaji upatanisho wa roho mtakatifu wakati wote kumbuka binadamu tunatenda dhambi hivyo ukifanya dhambi roho mtakatifu anaondoka yule adui ankuja kukuangamiza
Huyo Roho mtakatifu anashindwa vipi kukuzuia usifanye dhambi?

Yani huyo roho mtakatifu ni mjinga sana, Anakaa ndani yako badala akuwezeshe na akuzuie usitende dhambi anakuacha utende dhambi kisha aondoke!!

Halafu tena wewe uanze kumtafuta arudi kukaa ndani mwako for nothing ilhali hata uwezo wa kukufanya usitende dhambi hana..

Huyo Roho mtakatifu ni mjinga sana.
 
666 ni mwili wako mwanadamu chapa kwenye paji la uso ni nia ovu moyoni na chapa kwenye mikono ni matendo maovu ambayo yote hayo yana tokana na huyo mnyama (mwili) yaani kuzifuata tamaa za mwili ....chapa ya mnyama maana yake ni DHAMBI👉 siyo mtu fulani au kiumbe fulani kijacho au kipitacho kwa sababu imeandikwa wenye chapa ya huyo mnyama ndiyo watakao ingia motoni na tunajua kuwa kitu pekee kinacho mpeleka mtu motoni ni dhambi ....kwenye ufunuo 666 pia maana yake ni moja na na yale maandiko yanayo sema kahaba mkuu ambaye wafalme wamezini naye huyo kahaba ndiyo (666 yaani mwili wako ) na (wafalme ni nafsi inayo utawala mwili) kahaba kulewa kwa maombi ya watakatifu ni wachamungu kuzishinda tamaa za mwili ambao ndiyo huyo kahaba .....hivyo hizo funuo mbili maana yake ni moja .....huyo kahaba na 666 maana yake ni moja tu kuzini na huyo kahaba ni kufuata tamaa za mwili kwa sababu nguvu ya dhambi ipo kwenye miili yetu.👉kuhusu kuuza wala kununua isipokuwa watakuwa na chapa ya mnyama) hapo nadhani umesha jua maana maana yake kuwa chapa ya mnyama ni DHAMBI hivyo maana yake ni kuwa kila kitu atendacho mwadadamu kitakua kiovu chenye kutawaliwa na dhambi itokanayo na tamaa za mwili ...sasa ikiwa huyo mnyama ni papa je waliokufa kabla ya kuwako papa wataingia peponi ? Je ikiwa huyo mnyama ni kiumbe kijacho je walio kufa kabla ya hicho kiumbe wataingia peponi wote ? Kwa vyovyote vile nilazima huyo mnyama yupo sikuzote za mwanadamu duniani....maana imeandikwa wenye chapa yake ndiyo watakao tupwa motoni je chapa ni nini kama siyo dhambi maana ni dhambi tu itakayo mpeleka mtu motoni .
sawa mkuu, vipi abaout illuminates or freemasons , i think ni kama wameelezewa katika kitabu cha ufunuo, maana huwa na relate hicho chama na kilichopo now kinachonendesha dunia, kwa kujiita 666 na nembo zao.
 
Mkuu vitu usivyokua na ufahamu/hujavi-experience maishani mwako usivizungumzie kabisa hadharani... Kuna watu wanakuamini na kwa namna moja ama nyingine wanapotoka.
Huyo Roho mtakatifu anashindwa vipi kukuzuia usifanye dhambi?

Yani huyo roho mtakatifu ni mjinga sana, Anakaa ndani yako badala akuwezeshe na akuzuie usitende dhambi anakuacha utende dhambi kisha aondoke!!

Halafu tena wewe uanze kumtafuta arudi kukaa ndani mwako for nothing ilhali hata uwezo wa kukufanya usitende dhambi hana..

Huyo Roho mtakatifu ni mjinga sana.

Ivi we unafikili watu ni wajinga kiasi hicho... Kuna level wamefikia katika upande wa pili wa Shilingi ambao wewe hujafika na inawezekana wewe umekwamia kwenye upande mwingine (elimu dunia(science)) ukaona umamaliza, mkuu nikuambie tu kua safari bado.

Kama una miaka chini ya 30 basi usifikie hitimisho kwa jambo lolote kwani kuna mengi ya kujifunza bado... , sayansi yenyewe ni inabadilika(dynamic) na elimu ya ulimwengu huu ni pana sana, (wahenga wanakwambia elimu haina mwisho).
Achana na hadithi zisizo na kichwa wala miguu.

Biblia ni sawa na Hekaya za Abunuwasi au riwaya za Alfu Lela ulela.

Unasoma huku unajipa matumaini uchwara na kusema unapata ufunuo kumbe ni Hallucinations tu.

Biblia ni hadithi hadithi zisizo na ufunuo wowote ule zaidi ya hallucinations zinazoitwa imani.

Amka wewe!!View attachment 3033026
Kuna vitu huwezi kuelewa /huwezi kupata taswira halisi bila kuviishi/kivi-experience... Ni kama vile mtoto anavyokanywa na kuadhibiwa na wazazi wake kwa level ya uelewa wake a naona anaonewa ananyanyaswa lakini akikua anaelewa nini wazazi wake walikikusudia juu yake.
 
Mkuu vitu usivyokua na ufahamu/hujavi-experience maishani mwako usivizungumzie kabisa hadharani... Kuna watu wanakuamini na kwa namna moja ama nyingine wanapotoka.
Ufahamu ni nini?

Umeshawahi ku experience vitu vya kwenye biblia zaidi ya hadithi hadithi tu zisizo na uthibitisho wala uhalisia wowote ule?
Ivi we unafikili watu ni wajinga kiasi hicho... Kuna level wamefikia katika upande wa pili wa Shilingi ambao wewe hujafika na inawezekana wewe umekwamia kwenye upande mwingine (elimu dunia(science)) ukaona umamaliza, mkuu nikuambie tu kua safari bado.
Watu wengi kuamini kitu fulani haina maana kwamba kitu hicho ni cha ukweli kama hakina uthibitisho.

Uwingi wa watu kuamini kitu fulani sio uthibitisho wa ukweli wa hicho kitu.
Kama una miaka chini ya 30 basi usifikie hitimisho kwa jambo lolote kwani kuna mengi ya kujifunza bado... , sayansi yenyewe ni inabadilika(dynamic) na elimu ya ulimwengu huu ni pana sana, (wahenga wanakwambia elimu haina mwisho).

Kuna vitu huwezi kuelewa /huwezi kupata taswira halisi bila kuviishi/kivi-experience... Ni kama vile mtoto anavyokanywa na kuadhibiwa na wazazi wake kwa level ya uelewa wake a naona anaonewa ananyanyaswa lakini akikua anaelewa nini wazazi wake walikikusudia juu yake.
Msingi wa imani ni kutokuwa na uhakika.

Ukweli hauendani na imani, ukweli unaendana na uwepo wa uthibitisho
 
sawa mkuu, vipi abaout illuminates or freemasons , i think ni kama wameelezewa katika kitabu cha ufunuo, maana huwa na relate hicho chama na kilichopo now kinachonendesha dunia, kwa kujiita 666 na nembo zao.
Nimekuambia 666 ni mwili wako wewe mwenyewe ...afataye tamaa za mwili uzaa dhambi ambayo ndiyo chapa ya huyo mnyama. Dhambi ndiyo neno pekee duniani la kuchukua Tahadhari siyo habari ya freemasoni maana hao freemason wasingekuwa tatizo kama dhambi isingekuwepo
 
Kaka yanayokukuta wewe kama yanayonikuta mimi ila kwangu naona ni zaidi.
Yani am not interested anymore kwenye habari za hizi dini.
Nakua napatwa na khofu labda mungu kaondoa imani juu yangu ndo maana niko hivi kama wao wasemavyo.

Yani nikisikiliza mashekhe na mapastor naona nikama mawazo yangu ni makubwa mbele ya wanachokinena, yani naona tu ni upigaji uliowekwa kwa misingi ya kumtisha na kumfubaza kiakili mwanadamu na sio kumjenga.

Naamini mungu yupo but nakua nakosa right connection kwangu na kwake maana uyu wa kwenye izi dini naona sio kabisa au yawezekana ndio ila sio kwa jinsi wanavyomnena.

VITU VINAVYO NIKATISHA TAMAA KWENYE HIZI DINI.

• Story
Izi dini zina story za historia ya mungu na Dunia mpaka kufika leo, kwakweli mwanzo nilikua naamini mambo ya adam na eva, ghalika na n.k ila nilivyokua nimejikuta izo stories haziningii kichwani mwangu naona ni uzushi tuu, maana issue za nuhu kasimulia nuhu mwenyewe unamiinije kama hakuongeza chumvi,
story za sodom na gomora ilikua ni kijiji sio Dunia yawezekana ikiwa ni natural disaster kama inavyotokea ata hiki kipindi kama volkano na kwa miaka iyo waliona ni jambo kubwa kutokana na teknologia yao kua ndogo ndo maana wakalikuza kupita kiasi!

Kuna hadith nyingi za kiislam kwamba kuna mda mungu alituma ndege wamebeba mawe kuua maadui wa mtume yani zinakua haziningii kabisa, habari za maliamu kuona malaika ndo kabisaa, najiuliza kwani shetani hawezi kua mweupe, au mtu akikumbia utazaa mtoto wa mungu na atahimiza kusali ndo inajustfy kua uyo malaika hakua jini wala shetani!! Maana leo hakuna mtu anayemjua jini malaika na shetani katika maumbile, watu wanadefine ivo vitu kwa matendo, ukitokewa na mtu mweupe akakumbia piga goti shika maji uombe mungu unaamini ni malaika, ukitokewa na kitu cheusi kinaogopesha kinataka kukuua unajua ni shetani.

• Dini kutokea sehemu moja.
Dini zote kuu zimetokea eneo moja, wengine tumekuja kupokea, Huwezi sikia kulikua na mtume wala nabii mchina wala nini, wote ni Middle East. Story za kupokea jumbe za mungu na kuona malaika saivi naona kama ni hadidhi za Juma na Uledi, maana kichwani mwangu inakataa kuamini mtu atoke alikotoka aseme kuua ni dhambi mungu atakuchoma moto!! Sababu naamini hata bila huo ujumbe kwa akili za kawaida tu lazima huone kuua sio sawa, kuiba, kuchukua mpenzi wa mtu, kutukana mtu n.k sio mpaka mtu utishiwe moto.

Kunamda nawaza tuu ni vipi kama hao mitume walikua ni watu kwenye koo zao baada ya kuona vita ni vikubwa na manyanyaso wakaamua kusema wamepokea funuo kuhusu habari za mungu ili kufanya hao wafalme wauaji wasiendelee kuua watu hovyo! Au watu kuchukua wanawake zao kibabe ndo waka establish ndoa!! Maana kabla y Dini kila sehemu kulikua kunaendeshwa kwa akili za wafalme na kwa ubabe tuu bila kujal haki za kibinadamu.

Inshort sidhani kama niko sahihi na wala sijui kama nipo wrong ila izo story za watu wa uko Middle East kutumbia kuna shetani na mungu wanakinzana, asee zimekua ngumu kuningia now days nahisi nahitaji maombi labda kweli uyo shetani kaniingia.
Maswali ni mengi sana ila majibu ni machache mnoooo.
 
Aisee Asante sana mleta mada,
Hili suala mimi nilishawahi kujiuliza miaka mingi iliyopita,
1. Kanisani nimehudhuria mwaka mzima na nimefundishwa mafundisho lukuki, lakini je yamenifaidia wapi? Nimeyatendea kazi mangapi? Mbona mahubiri ni yaleyale tu yakijibadili kidogo tu?
  • Utoaji
  • Nguvu ya maombi
  • Jinsi ya kukua kiroho
N.k
2. Ndipo nilikuja kupata majibu kuwa kumbe neno la Bwana linatafsiri zaidi ya 70, kuna nyakati nilikuwa nikipitia nyakati za shida chaajabu nikishika biblia tu kusoma nakutana na andiko ambalo limebeba majibu ya shida zangu, au neno hilo linanitia nguvu ya kusonga mbele. Lakini neno hilo siyo kwamba linakuwa geni kwangu hapana nilishalisoma siku nyingi tu na mara nyingi tu, lakini huwa linajifunua kwa namna ya pekee kulingana na nyakati

USIACHE KUSOMA NENO WALA KUACHA KUHUDHURIA IBADA
Be blessed brother.
 
Ufahamu ni nini?

Umeshawahi ku experience vitu vya kwenye biblia zaidi ya hadithi hadithi tu zisizo na uthibitisho wala uhalisia wowote ule?

Watu wengi kuamini kitu fulani haina maana kwamba kitu hicho ni cha ukweli kama hakina uthibitisho.

Uwingi wa watu kuamini kitu fulani sio uthibitisho wa ukweli wa hicho kitu.

Msingi wa imani ni kutokuwa na uhakika.

Ukweli hauendani na imani, ukweli unaendana na uwepo wa uthibitisho

Nina uhakika wewe ni open minded person, kwa msingi huo huo wa kufikiri nje ya boksi, ukiwa katika huu ulimwengu unaonekana kwa kutumia milango mitano ya fahamu, jishughulishe katika kufahamu je? kuna ulimwenguni usioonekana na usiokua percieved na our 5sense organ.

Huu mwili tulionao ni kama body tu ambayo imefungwa senser kuu 5(5sense organ) ili kutusaidia katika mazingira ya hapa duniani. Sasa fikilia vipi kungekua na senser zaidi ya tano kunauwezekano tungeweza ku-detect mambo mengine pengine kwa usalama wetu na afya ya Akili yetu isingeweza kuhimili hivyo ni hekima/busara tu imetumika.

Sasa fanya u-dig more deeper kuhusu sixth sense (jicho la tatu)) . Kwanini ni kwasababu huo ulimwengu upo!

Na unapokua unahitaji uthibitisho huku ukiwa katika ulimwengu ambao sense organ za mwili wako zipo adaptable na zina access only na physical world, hazina access ya ku-recieve/detect taarifa yoyote kutoka ulimwengu mwingine pasipo kua na connection yoyote ambayo kwa maumbile yetu hatujaumbiwa nayo.

We huoni unatupatia changamoto!!! chukulia mfano umekutana na kipofu wa kuzaliwa anakuomba umuelezee/umchanganulie tofauti iliyopo kati ya rangi ya blue na nyekundu utamueleza vipi hadi aelewe somo, ni Ngumu...! labda umponye kwanza apate kuona tena ndio mkae meza moja hapo mtaelewana.

Sikulazimishi uamini ila fanya udadisi(just for curiosity purpose).
 
Neno linasema ktk 1 YOHANA 3:4 'Kila atendaye dhambi afanya uasi,kwakua dhambi ni uasi.
Zingatia kabla ya Bwana Yesu kuja na kuiondoa dhambi,wanadam wote walikua ni wenye dhambi bila kujali umri wao so mtu anakua mwenye dhambi kwasababu amezaliwa ana dhambi sio kutenda.
Tazama WARUMI 5:12-14 Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;
13 maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria;
14 walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, NAYO ILIWATAWALA HATA WAO WASIOFANYA DHAMBI IFANANAYO NA KOSA LA ADAMU, aliye mfano wake yeye atakayekuja.
Pia tunajua kua mshahara wa dhambi ni mauti (WARUMI 6:23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.)hivyo basi watoto wadogo wanakufa kwasabab ya dhambi! Dhambi inayowaua sio walioifanya maana kuna vichanga kuna vinavyokufa kabla ya kuzaliwa pia bali ni ile waliyoirithi kupitia Adamu na asili yake ya dhambi toka eden ambayo ipo ndani yao!
Lakini Mungu apewe sifa kwakumleta mwanawe mpendwa duniani kutukomboa na dhambi na ktk hali ya uasi.YOHANA 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Uzima unakujaje bila dhambi kuondolewa kutokana na YOHANA 3:16 hapo?
Dhambi na asili yake imeondolewa milele na Bwana Yesu WAEBRANIA 10:10 Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.
12 Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;
14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.
17 Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.
18 Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.

Cheki WARUMI 5:8-10 Basi Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, TULIPOKUWA TUNGALI WENYE DHAMBI.
9.Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye.
10 Kwa maana ikiwa TULIPOKUWA ADUI TULIPATANISHWA NA MUNGU KWA MAUTI YA MWANA WAKE; zaidi sana BAADA YA KUPATANISHWA tutaokolewa katika uzima wake.
Yesu hakutufia tukiwa watakatifu wenye matendo mema bali tukiwa waasi na sio wakristo tu bali ulimwengu mzima!
Hatupatanishwi na Mungu kwa matendo mazuri ya kila siku.

Mtu aliezaliwa mara ya pili ni mwenye haki sio mdhambi tena.2 WAKORINTHO 5:21 Yeye[YESU] asiyejua dhambi ALIMFANYA KUWA DHAMBI KWA AJILI YETU, ILI SISI TUPATE KUWA HAKI YA MUNGU KATIKA YEYE[YESU].
1 WAKORINTHO 6:17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.
So kama umeokoka dhambi huna,coz kama ndani ya Mungu hakuna dhambi nami sina sababu tumekua kitu kimoja naye.
1 YOHANA 3:9-10 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.
10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.

uthibitisho mwingine ni 1 YOHANA 2:1-2 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,
2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.
Hivyo jua kwamba ondoleo la dhambi huja kwa kuliamini jina la Yesu Kristo(MATENDO YA MITUME 10:43)
Kwa maana pia dhambi ni kutokumuamini Yesu(YOHANA 16:8-9)

Yani unamuamini Yesu ila kazi yake ya pale msalabani kumwaga damu yake kwa ajili ya ondoleo la dhambi ya ulimwengu huiamini! Na amesema yeye mwenyewe sehemu nyingi tu ila unachagua kujiita mwenye dhambi,dhaifu,usiefaa,usie kitu na kukiri ungamo kila jumapili kanisani ilhali umekua kiumbe kipya mwenye haki,utakatifu na ukombozi wa Mungu baba!
Kiukweli inashangaza mno wakristo waliokoka wanavyoshikilia dhambi ambayo ilishafutwa milele!

Ktk MATHAYO 5:17-48 Bwana Yesu anaelezea amekuja kuitimiliza yani kuitimiza na kuirekebisha sababu yeye ameleta neema na kweli.maana yake ni kua torati yote ya musa na manabii inatimia katika yeye.so ukiwa ndani yake basi torati yote na manabii inakamilika ndani yako.
Na ndio maana unaona kwanzia mstari ya 21 Bwana Yesu anazinukuu baadhi ya sheria za torati zilivyosema na yeye anaziongezea kua yote hayo ni upendo tu ndio amri kuu(kumpenda Mungu na jirani yako basi)
😁
 
Nina uhakika wewe ni open minded person, kwa msingi huo huo wa kufikiri nje ya boksi, ukiwa katika huu ulimwengu unaonekana kwa kutumia milango mitano ya fahamu, jishughulishe katika kufahamu je? kuna ulimwenguni usioonekana na usiokua percieved na our 5sense organ.

Huu mwili tulionao ni kama body tu ambayo imefungwa senser kuu 5(5sense organ) ili kutusaidia katika mazingira ya hapa duniani. Sasa fikilia vipi kungekua na senser zaidi ya tano kunauwezekano tungeweza ku-detect mambo mengine pengine kwa usalama wetu na afya ya Akili yetu isingeweza kuhimili hivyo ni hekima/busara tu imetumika.

Sasa fanya u-dig more deeper kuhusu sixth sense (jicho la tatu)) . Kwanini ni kwasababu huo ulimwengu upo!

Na unapokua unahitaji uthibitisho huku ukiwa katika ulimwengu ambao sense organ za mwili wako zipo adaptable na zina access only na physical world, hazina access ya ku-recieve/detect taarifa yoyote kutoka ulimwengu mwingine pasipo kua na connection yoyote ambayo kwa maumbile yetu hatujaumbiwa nayo.

We huoni unatupatia changamoto!!! chukulia mfano umekutana na kipofu wa kuzaliwa anakuomba umuelezee/umchanganulie tofauti iliyopo kati ya rangi ya blue na nyekundu utamueleza vipi hadi aelewe somo, ni Ngumu...! labda umponye kwanza apate kuona tena ndio mkae meza moja hapo mtaelewana.

Sikulazimishi uamini ila fanya udadisi(just for curiosity purpose).
Jicho la tatu ni nini?

Unathibitishaje jicho la tatu lipo?

Wewe mwenyewe upo kwenye
huu huu ulimwengu ambao ni physical kwa sense organs 5,

Sasa unajuaje na unathibitishaje kwamba kuna ulimwengu usio onekana upo, ilihali wewe mwenyewe unadai ulimwengu huo hauwezi kuwa accessed kwa sense organs zetu.

Wewe umetumia nini ku access huo ulimwengu usio onekana?
 
Uebert Angel aliyenaswa na camera za Aljazeera akifanya biashara ya magendo ya dhahabu kutoka Zimbabwe?

Baada ya hiyo documentary waliyo tengeneza nini kimefatia? Ulijipa muda wa kusikiliza upande wa pili uliotuhumiwa? Ulisikiliza maelezo yaliyo tolewa na serikali ya Zimbabwe kuhusu hizo tuhuma?

Biblia inasema, “It’s only a fool who judges a matter after hearing only one voice”
 
Neno la Mungu ni lile linalokuwa moyoni mwako.

Biblia huna haja ya kuisoma mara nyingi ikiwa tayari unaijua.

Soma vitabu vingine hasa vile walivyovitoa, soma Quran, ongeza ujuzi na maarifa

Hata Kanisani sio pakwenda kama tayari umefika level fulani ya ufahamu.
Labda upeleke watoto nao wakajifunze.
Vinginevyo utaona uko bored ukifika Kanisani kwa sababu mambo mengi 99% ni marudio na unayajua
Unapotosha
 
HAYA NI MAFUNDISHO YA INJILI FEKI ZA MADHEHEBU YA DINI ...NENO DHEHEBU MAANA YAKE NI HEKATU LA SHETANI
Ili ujue ni kwamba Muumba hana DINI wala Dhehebu, ni mmoja tu na hagawanyiki.sio wa kabila, lugha wala jamaa maana wote tumetoka kwake.

Warumi 11:36
Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.

Ila dunia ilitengeneza mfumo kila kabila lilikuwa na Mungu wake, kila taifa lilikuwa na Mungu wake na kila jamaa ilikuwa na Mungu wake ndio mfumo uliokuwepo.

Ni ufinyu wa uelewa na ufahamu ndo mana unasema ivyo ungejua usiyoyaona ungeelewa.
 
Jicho la tatu ni nini?

Unathibitishaje jicho la tatu lipo?

Wewe mwenyewe upo kwenye
huu huu ulimwengu ambao ni physical kwa sense organs 5,

Sasa unajuaje na unathibitishaje kwamba kuna ulimwengu usio onekana upo, ilihali wewe mwenyewe unadai ulimwengu huo hauwezi kuwa accessed kwa sense organs zetu.

Wewe umetumia nini ku access huo ulimwengu usio onekana?
Majibu yote yapo humo 👆👆👆 moja wapo ni kiunganishi.
connection
Pia
labda umponye kwanza apate kuona tena ndio mkae meza moja hapo mtaelewana.
Kuto kuthibitika kwa haya mambo katika ilimwengu wa kimwili haimaanishi kwamba mambo hayo hayapo..! La! Mambo hayo yapo sema wewe binafsi hujataka kuyafahamu... na uwezo huo umepewa, kila mtu anao ila hatuutumii(hatuamini)

Narudia tena uwezo huo upo na kila mtu anao pasipokujali dini yake, anaendaga ibadani au hua haendi, shida inakuja ni mhusika hajataka kuutumia kwa kufuata kanuni.

Sasa kazi ni kwako kama unataka na wewe kufahamu,,, kwasababu nitakutofautishiaje rangi ya blue na nyekundu ilihali wewe ni kipofu tokea unazaliwa hujawahi ona chochote. Hutanielewa kamwe!. Na kwa kutumia kanuni/ufahamu wa elimu (sayansi) ndio utaona nimechanganyikiwa kabisa.

Sasa nakushauri usifikie hitimisho kwa jambo lolote ambalo Huna uzoefu nalo.
Elimu haina mwisho kila siku tunajifunza vitu vipya unaweza ukajifuza kitu kipya hata ukiwa na miaka 99.

Haya mambo ya imani ya hukulie kama changamoto mpya kwako mwaka huu... uipatie ufumbuzi, kwa lengo la kijifunza zaidi. kama una nia njia huwezi kukosa.
 
Back
Top Bottom