Utabiri: Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, Sugu atavunja record kwa kupata kura ambazo hakuna mgombea mwingine aliwahi kupata

Utabiri: Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, Sugu atavunja record kwa kupata kura ambazo hakuna mgombea mwingine aliwahi kupata

Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza naomba niwaandae kisaikolojia, wale wote ambao wanafikiri kuwa Chadema haitoshiriki katika uchaguzi mkuu wa uraisi, na ubunge.

Utabiri wangu unaonesha kuwa Chadema itashiriki katika chaguzi zote mbili. Yani uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwakani, na ule wa raisi na wabunge utakaofanyika mwaka 2025.

Sasa basi baada ya kukujulisha kuhusu ushiriki wa Chadema katika chaguzi zijazo, naomba nianze sasa kukufafanulia kuhusu utabiri unaoonesha kuwa ndugu Joseph Mbilinyi aka "Sugu" atapata kura nyingi kuliko wagombea wengine wa upinzani ambao waliwahi kugombea huko nyuma kabla yake.

Ni hivi utabiri unaonesha kwamba ndugu Sugu ana nyota kali ya kiuongozi na kukubalika, hivyo nyota hiyo inamsaidia kupata uungwaji mkono kutoka maeneo mbali mbali ya dunia (kama tulivyoona akitembelewa na mabalozi wa nchi zenye uchumi mkubwa duniani), na pia anaheshimiwa na kukubaliwa hata kwenye chama chake, including viongozi wakubwa wa chama (ukimtoa makamu mwenyekiti) ambae ana ubinafsi. Hivyo utabiri unaonesha kuwa ndugu Sugu ndio atakaepitishwa na chama chake kikiongozwa na mwenyekiti wao kuwa mgombea uraisi wa chama hicho ambacho kilianguka vibaya katika uchaguzi mkuu uliyopita kutokana na sababu ambazo hapa sio mahala pake pa kuzitaja.

Nafikiri wengi mnataka kujua kwamba Sugu atagombeaje uraisi kupitia Chadema na wakati nafasi hiyo inaonekana kudhibitiwa na makamu mwenyekiti wa chama ndugu Lisu, na pia wengine wanajiuliza kwamba utabiri unasemaje Sugu atapeperusha bendera ya chama ambacho kimesema hakitasimamisha wagombea kutokana na hitilafu ya katiba na tume ya uchaguzi. Sasa utabiri unaonesha mazingira ya Sugu kugombea yatakuaje.

Utabiri unaonesha kuwa kutakuwa na msuguano mkali kati ya makamu huyo, na viongozi wenzake wa chama kuhusu chama hicho kushiriki katika uchaguzi mkuu. Mwisho utabiri unaonesha kuwa makamu atashindwa na hivyo chama kitadhamiria kusimamisha wagombea wote kuanzia serikali za mitaa na hapo baadae uraisi.

Utabiri unaonesha kuwa katika swala la uraisi makamu hatoshiriki tena kwa hoja ya kujifanya anasimamia kile anachokiamini na kwamba hayuko tayari kuyumbishwa juu ya misimamo yake. Hapo sasa litatokea kundi la wana Mbeya likiongozwa na vijana na wazee waseme kuwa sasa uraisi ni zamu ya nyanda za juu kusini, watamchukulia Sugu tiketi ya kugombea uraisi, Sugu atakubali na hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya kushinda katika kinyang'anyiro cha kupitishwa na chama.

Utabiri unaonesha kuwa, japo kuna wagombea wengine kadhaa watajitokeza kupambana nae katika kinyang'anyiro hicho, lkn Sugu atapita kwa ushindi mnono na hivyo kuwa mgombea uraisi kwa mara ya kwanza kupitia chama chake Chadema.

Katika uchaguzi huo, Sugu atakuwa mgombea wa kwanza uraisi kutoka upinzani kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine wote waliowahi kugombea tangu mfumo wa vyama vingi uanzishwe. Na hii ni kwa sababu ya nyota yake ambayo inamfanya akubalike kwa vijana, wazee, kina mama, kina baba, kina mjomba, kina shangazi, kina babu, kina bibi nk.

Pia atakuwa mgombea wa kwanza kukipa chama chake wabunge wengi zaidi katika uchaguzi huo. Ukiona wazungu wanaingia na kutoka katika ofisi ya mtu, basi ujue kuna kitu fulani wanakiona kinakuja, kama sio sasa hivi basi baadae.

Kwa wale wanaompenda Sugu na kuhitaji awe raisi wao wa Jamhuri (sio Mbeya pekee) basi waongeze maombi ili aje kushinda katika uchaguzi mkuu ujao, maana utabiri haujaonesha kama atamshinda wa chama tawala, bali umeonesha namna atashinda kinyang'anyiro cha kupeperusha bendera ya chama chake na pia kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wa upinzani waliopita.

Team Lisu wajiandae kisaikolojia, kwani mgombea wa Chadema ashajulikana kupitia utabiri huu.
Huu si utabiri,hili jambo liko wazi kabisa.
 
Naomba uniwekee baadhi ya tabiri zako zilizo materialize, usiku hii ya Sugu kugombea urais ni gia tuu ya kumkimbia Betina!.
P
Mimi sio mtaalam sana wa tabiri, lkn huu utabiri wa Sugu umenijia ndotoni ghafla nikaona nije niwashirikishe watu hapa JF, ili likitokea niseme kumbe nilichokiona ndotoni ndio kilichotokea.
 
Mimi sio mtaalam sana wa tabiri, lkn huu utabiri wa Sugu umenijia ndotoni ghafla nikaona nije niwashirikishe watu hapa JF, ili likitokea niseme kumbe nilichokiona ndotoni ndio kilichotokea.
Usisahau pia kurudi hapa na kukiri kwamba ulikula sana ukalala na kuota kisichowezekana.Time will tell ingawa najua visingizio havitakosekana.
 
Usisahau pia kurudi hapa na kukiri kwamba ulikula sana ukalala na kuota kisichowezekana.Time will tell ingawa najua visingizio havitakosekana.
Na utabiri wangu ukiwezekana, utarudi kunipongeza mkuu?
 
Sugu atapita kwa ushindi mnono na hivyo kuwa mgombea uraisi kwa mara ya kwanza kupitia chama chake Chadema.

Katika uchaguzi huo, Sugu atakuwa mgombea wa kwanza uraisi kutoka upinzani kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine wote waliowahi kugombea tangu mfumo wa vyama vingi uanzishwe.
Nashauri uzi huu ungeendana na vigezo anazotakiwa kuwa nazo Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, halafu tuangaloe kama Sugu anakidhi vigezo hivyo.
Utabirri usiozingatia vigezo n8 utabiri wa kiajali ajali.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza naomba niwaandae kisaikolojia, wale wote ambao wanafikiri kuwa Chadema haitoshiriki katika uchaguzi mkuu wa uraisi, na ubunge.

Utabiri wangu unaonesha kuwa Chadema itashiriki katika chaguzi zote mbili. Yani uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwakani, na ule wa raisi na wabunge utakaofanyika mwaka 2025.

Sasa basi baada ya kukujulisha kuhusu ushiriki wa Chadema katika chaguzi zijazo, naomba nianze sasa kukufafanulia kuhusu utabiri unaoonesha kuwa ndugu Joseph Mbilinyi aka "Sugu" atapata kura nyingi kuliko wagombea wengine wa upinzani ambao waliwahi kugombea huko nyuma kabla yake.

Ni hivi utabiri unaonesha kwamba ndugu Sugu ana nyota kali ya kiuongozi na kukubalika, hivyo nyota hiyo inamsaidia kupata uungwaji mkono kutoka maeneo mbali mbali ya dunia (kama tulivyoona akitembelewa na mabalozi wa nchi zenye uchumi mkubwa duniani), na pia anaheshimiwa na kukubaliwa hata kwenye chama chake, including viongozi wakubwa wa chama (ukimtoa makamu mwenyekiti) ambae ana ubinafsi. Hivyo utabiri unaonesha kuwa ndugu Sugu ndio atakaepitishwa na chama chake kikiongozwa na mwenyekiti wao kuwa mgombea uraisi wa chama hicho ambacho kilianguka vibaya katika uchaguzi mkuu uliyopita kutokana na sababu ambazo hapa sio mahala pake pa kuzitaja.

Nafikiri wengi mnataka kujua kwamba Sugu atagombeaje uraisi kupitia Chadema na wakati nafasi hiyo inaonekana kudhibitiwa na makamu mwenyekiti wa chama ndugu Lisu, na pia wengine wanajiuliza kwamba utabiri unasemaje Sugu atapeperusha bendera ya chama ambacho kimesema hakitasimamisha wagombea kutokana na hitilafu ya katiba na tume ya uchaguzi. Sasa utabiri unaonesha mazingira ya Sugu kugombea yatakuaje.

Utabiri unaonesha kuwa kutakuwa na msuguano mkali kati ya makamu huyo, na viongozi wenzake wa chama kuhusu chama hicho kushiriki katika uchaguzi mkuu. Mwisho utabiri unaonesha kuwa makamu atashindwa na hivyo chama kitadhamiria kusimamisha wagombea wote kuanzia serikali za mitaa na hapo baadae uraisi.

Utabiri unaonesha kuwa katika swala la uraisi makamu hatoshiriki tena kwa hoja ya kujifanya anasimamia kile anachokiamini na kwamba hayuko tayari kuyumbishwa juu ya misimamo yake. Hapo sasa litatokea kundi la wana Mbeya likiongozwa na vijana na wazee waseme kuwa sasa uraisi ni zamu ya nyanda za juu kusini, watamchukulia Sugu tiketi ya kugombea uraisi, Sugu atakubali na hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya kushinda katika kinyang'anyiro cha kupitishwa na chama.

Utabiri unaonesha kuwa, japo kuna wagombea wengine kadhaa watajitokeza kupambana nae katika kinyang'anyiro hicho, lkn Sugu atapita kwa ushindi mnono na hivyo kuwa mgombea uraisi kwa mara ya kwanza kupitia chama chake Chadema.

Katika uchaguzi huo, Sugu atakuwa mgombea wa kwanza uraisi kutoka upinzani kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine wote waliowahi kugombea tangu mfumo wa vyama vingi uanzishwe. Na hii ni kwa sababu ya nyota yake ambayo inamfanya akubalike kwa vijana, wazee, kina mama, kina baba, kina mjomba, kina shangazi, kina babu, kina bibi nk.

Pia atakuwa mgombea wa kwanza kukipa chama chake wabunge wengi zaidi katika uchaguzi huo. Ukiona wazungu wanaingia na kutoka katika ofisi ya mtu, basi ujue kuna kitu fulani wanakiona kinakuja, kama sio sasa hivi basi baadae.

Kwa wale wanaompenda Sugu na kuhitaji awe raisi wao wa Jamhuri (sio Mbeya pekee) basi waongeze maombi ili aje kushinda katika uchaguzi mkuu ujao, maana utabiri haujaonesha kama atamshinda wa chama tawala, bali umeonesha namna atashinda kinyang'anyiro cha kupeperusha bendera ya chama chake na pia kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wa upinzani waliopita.

Team Lisu wajiandae kisaikolojia, kwani mgombea wa Chadema ashajulikana kupitia utabiri huu.
Sijui umeandika nini,
 
Kuna vitu viwili mkuu. Kuwa makini

1. Kupata kura nyingi
2. Kutangazwa mshindi

Hivi vitu havichangamani na havitegemeani kwa Tz. Be careful
Ndio maana kama ulisoma vizuri hapo chini niliandika kwamba utabiri wangu hauzungumzii wala kuona kwamba Sugu atamshinda mgombea wa chama tawala, iwe kihalali au kiwizi.

Utabiri unanionesha tu kwamba ataibuka kidedea katika kinyang'anyiro cha kupitishwa na chama chake, pia atapata kura nyingi (huenda sio kuzidi za mgombea uraisi wa chama tawala) kuliko wagombea wengine waliowahi kugombea kupitia upinzani kama vile Mrema 1995, Lipumba 2000 - 2005, Dr Slaa 2010, Lowasa, Lisu nk.
 
Back
Top Bottom