Utabiri: Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, Sugu atavunja record kwa kupata kura ambazo hakuna mgombea mwingine aliwahi kupata

Utabiri: Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, Sugu atavunja record kwa kupata kura ambazo hakuna mgombea mwingine aliwahi kupata

Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza naomba niwaandae kisaikolojia, wale wote ambao wanafikiri kuwa Chadema haitoshiriki katika uchaguzi mkuu wa uraisi, na ubunge.

Utabiri wangu unaonesha kuwa Chadema itashiriki katika chaguzi zote mbili. Yani uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwakani, na ule wa raisi na wabunge utakaofanyika mwaka 2025.

Sasa basi baada ya kukujulisha kuhusu ushiriki wa Chadema katika chaguzi zijazo, naomba nianze sasa kukufafanulia kuhusu utabiri unaoonesha kuwa ndugu Joseph Mbilinyi aka "Sugu" atapata kura nyingi kuliko wagombea wengine wa upinzani ambao waliwahi kugombea huko nyuma kabla yake.

Ni hivi utabiri unaonesha kwamba ndugu Sugu ana nyota kali ya kiuongozi na kukubalika, hivyo nyota hiyo inamsaidia kupata uungwaji mkono kutoka maeneo mbali mbali ya dunia (kama tulivyoona akitembelewa na mabalozi wa nchi zenye uchumi mkubwa duniani), na pia anaheshimiwa na kukubaliwa hata kwenye chama chake, including viongozi wakubwa wa chama (ukimtoa makamu mwenyekiti) ambae ana ubinafsi. Hivyo utabiri unaonesha kuwa ndugu Sugu ndio atakaepitishwa na chama chake kikiongozwa na mwenyekiti wao kuwa mgombea uraisi wa chama hicho ambacho kilianguka vibaya katika uchaguzi mkuu uliyopita kutokana na sababu ambazo hapa sio mahala pake pa kuzitaja.

Nafikiri wengi mnataka kujua kwamba Sugu atagombeaje uraisi kupitia Chadema na wakati nafasi hiyo inaonekana kudhibitiwa na makamu mwenyekiti wa chama ndugu Lisu, na pia wengine wanajiuliza kwamba utabiri unasemaje Sugu atapeperusha bendera ya chama ambacho kimesema hakitasimamisha wagombea kutokana na hitilafu ya katiba na tume ya uchaguzi. Sasa utabiri unaonesha mazingira ya Sugu kugombea yatakuaje.

Utabiri unaonesha kuwa kutakuwa na msuguano mkali kati ya makamu huyo, na viongozi wenzake wa chama kuhusu chama hicho kushiriki katika uchaguzi mkuu. Mwisho utabiri unaonesha kuwa makamu atashindwa na hivyo chama kitadhamiria kusimamisha wagombea wote kuanzia serikali za mitaa na hapo baadae uraisi.

Utabiri unaonesha kuwa katika swala la uraisi makamu hatoshiriki tena kwa hoja ya kujifanya anasimamia kile anachokiamini na kwamba hayuko tayari kuyumbishwa juu ya misimamo yake. Hapo sasa litatokea kundi la wana Mbeya likiongozwa na vijana na wazee waseme kuwa sasa uraisi ni zamu ya nyanda za juu kusini, watamchukulia Sugu tiketi ya kugombea uraisi, Sugu atakubali na hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya kushinda katika kinyang'anyiro cha kupitishwa na chama.

Utabiri unaonesha kuwa, japo kuna wagombea wengine kadhaa watajitokeza kupambana nae katika kinyang'anyiro hicho, lkn Sugu atapita kwa ushindi mnono na hivyo kuwa mgombea uraisi kwa mara ya kwanza kupitia chama chake Chadema.

Katika uchaguzi huo, Sugu atakuwa mgombea wa kwanza uraisi kutoka upinzani kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine wote waliowahi kugombea tangu mfumo wa vyama vingi uanzishwe. Na hii ni kwa sababu ya nyota yake ambayo inamfanya akubalike kwa vijana, wazee, kina mama, kina baba, kina mjomba, kina shangazi, kina babu, kina bibi nk.

Pia atakuwa mgombea wa kwanza kukipa chama chake wabunge wengi zaidi katika uchaguzi huo. Ukiona wazungu wanaingia na kutoka katika ofisi ya mtu, basi ujue kuna kitu fulani wanakiona kinakuja, kama sio sasa hivi basi baadae.

Kwa wale wanaompenda Sugu na kuhitaji awe raisi wao wa Jamhuri (sio Mbeya pekee) basi waongeze maombi ili aje kushinda katika uchaguzi mkuu ujao, maana utabiri haujaonesha kama atamshinda wa chama tawala, bali umeonesha namna atashinda kinyang'anyiro cha kupeperusha bendera ya chama chake na pia kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wa upinzani waliopita.

Team Lisu wajiandae kisaikolojia, kwani mgombea wa Chadema ashajulikana kupitia utabiri huu.
Ukwel mchungu
 
Atakua fala, ni lazima wakubali kuona potential ya each other na strategically waunganishe wananchi na nguvu zao.
Mafarakano sababu ya vyama hayana tija wala afya.
Nakubaliana na wewe mkuu 🤝
 
Tambo za kabla ya chaguzi huwa ni hizihizi miaka yote!

Na lawama za baada ya chaguzi zinafahamika miaka yote.
Shida ni Tume ya Uchaguzi inayoratibiwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Nashauri uzi huu ungeendana na vigezo anazotakiwa kuwa nazo Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, halafu tuangaloe kama Sugu anakidhi vigezo hivyo.
Utabirri usiozingatia vigezo n8 utabiri wa kiajali ajali.
Vigezo ni ushawishi na kukubalika.
 
Ni vigumu mnyarwanda kuelewa kilichoandikwa na mtanzania.

Kama una rafiki yako mtanzania mwambie akutafsirie mkuu. Si unaona watanzania halisi wamenielewa na Ku comment kutokana na kile walichoelewa!!
Akili ndogo sana, unajificha kwenye utabiri uchwara ,stupid
 
Shida ni Tume ya Uchaguzi inayoratibiwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwani Sugu alivyoshinda uchaguzi wa ubunge jimbo la Mbeya mjini, tume ya uchaguzi ilikuwa ipi?Mkishinda all is allright mkishindwa tume ya uchaguzi haitendi haki!!!
You cannnot have both ways.You cannot have your cake and eat it too.
 
Ulichoandika kina ukweli, hata mimi nitakuwa mmoja wa wachangiaji wa ticket yake ya urais.

Wana mbeya, iringa na songwe tupambane kuhakikisha sugu anakua mgombea urais wa chadema mwaka 2025, maana lisu ushawishi wake umeshuka sana na pia hana jipya la kushawishi watu wampigie kura.
 
Back
Top Bottom